Ipi dhima ya miundombinu

Ipi dhima ya miundombinu

Mkandara

Platinum Member
Joined
Mar 3, 2006
Posts
15,961
Reaction score
9,345
Nina shaka na maono ya viongozi wa sasa kuhusiana na dhima ya ujenzi mkubwa wa Miundombinu nchini kama kwamba inarudisha kwenye zama za Utumwa na kutawaliwa.

Nakumbuka maono (Vision) ya rais Marehemu Magufuli aliweka juhudi kubwa katika Ujenzi wa Miundombinu hii sambamba na ujenzi wa Viwanda nchi kiasi kwamba aliwaalika hata matajiri wakubwa wa ndani kina Dangote, Bakhresa, Rostam, Aboud na wengineo katika mazao ya kilimo na madini kuwekeza katika viwanda ili kukuza uchumi wa ndani wakati Serikali yake imejikita katika kuboresha miundombinu nchini.

Hoja yangu ipo hapa – Viongozi wa leo wote toka rais aliyepo madarakani mpaka kina Kitila, Zitto na wachumi wataalam wengine wanazungumzia ujenzi huu mkubwa wa Bandari zetu na reli (Ushoroba) kwenda nchi jirani za DRC, Burundi na Rwanda kana kwamba haya ni Maendeleo tunayoyahitaji lakini deep down najiuliza sisi (Tanzania) tutasafirisha nini ikiwa dhima yake ni Usafiri wa bidhaa za nchi jirani kwankutegemea kodi na Ushuru?

Hivi, wafaidika wa uwekezaji huu mkubwa watakuwa kina nani? Je, haitakuwa nchi hizo na makampuni ya nje wakichukua nafasi ya utawala wa zama za Utumwa na hawa viongozi wetu watatumiwa kama Machief wa zamani enzi za Ukoloni. Tegemeo lao (Machief) na letu ni kutoza Kodi na Ushuru exactly kama walivyofanya kina Mtemi Mirambo!

Wakati ule wa Utumwa Bandari zetu za Mombasa, Bagamoyo, Zanzibar na Kilwa zilukuwa ngome za Wakoloni zikitumiwa kuchukua bidhaa toka Bara ikiwa ni pamoja na Watumwa, Pembe za ndofu dhahabu na kadhalika, wao wakituletea sisi shanga, nguo na viatu.

Hata Utawala wa Mjarumani na Muingereza nao walidai Pwani ya Afrika Mashariki kutoka kwa Sultan wa Zanzibar wakajenga miundombinu ya bandari na reli ili waweze kusafirisha bidhaa za ndani kutoka tawala zao kwenda makwao kwa maendeleo ya nchi zao.

Mjarumani hakujenga reli mpaka DRC, Burundi na Rwanda kwa sababu hayakuwa makoloni yake ategemee kodi na Ushuru.

Muingereza vile vile japokuwa tulikuwa na EAC alijenga miundombinu Kenya na Uganda zaidi zikiwa ndani ya koloni lake kwa sababu lengo ni kuvuna walichopanda sio kunufaisha nchi nyinginezo kwa kukusanya kodi na Ushuru.

Maoni hata ya viongozi wangu yanafikiriaha san, mimi nilitegemea uwekezaji huu mkubwa ni kwa ajili yetu sisi ili kukuza Uchumi wetu wa viwanda vya ndani tupate kuuza bidhaa zetu nje, lakini naona kama tuna facilitate control na mahitaji ya nchi jirani na za Magharibi?

Matajiri wakubwa wanatukimbia, wanawekeza nchi jirani kwa sababu mikataba yao ina nafuu kuliko sisi. Dangote, Rostam na wengine wanazitazama nchi jirani kama bora na nafuu kwao katika uwekezaji wa viwanda kuliko Tanzania. Tumefikaje hapa!

Hii itakuwa Biashara ya kuwafadhili kina Tippu Tip.
 
Mkuu Mkandara
Kwanza, hoja ya biashara ya utumwa si sahihi kwa nyakati zetu. Wakoloni walipeleka faida ya biashara ya utumwa Ulaya na Uarabuni. Kwetu sisi faida za bandari zinabaki nchini unless zichepushwe uswiss na wahalifu wetu.

Pili, kuna nchi zinajenga uchumi kwa huduma ''services'' na si uzalishaji. Mifano ni utalii wa Asia na Seychelles na Mauritius hata Afrika kusini. Tanzania, Utalii unaingiza pato la Taifa kuliko Kilimo. Kuna Nchi zina GDP kwa remittance kama Nicaragua, Nepal n.k.

Kutengeneza reli ya kutoa huduma kwa nchi jirani na kuchukua ushuru kuna tatizo gani ikiwa inachangia GDP?
Tazama kodi za Bandari peke yake zinavyochangia hazina. Kuna shida gani kufanya bandari kama kitega uchumi.

Tatu, ujenzi wa reli una stimulate economy. Mfano, tangu kujengwa daraja la Mkapa na barabara ya kusini, mikoa ya kusini imepanda skiuchumi. Infrastracture zinategemea matumizi na matunzo! ni vyanzo vizuri vya mapato

Natamani kungekuwa na reli ya Mtwara -Mbambabay au Arusha-Musoma.
Ukitaka kuendelea hutakiwi kuweka viwanda au mashamba! tengeneza miundo mbinu tu, kila kitu kitafuata chenyewe.
 
Mkuu Mkandara
Kwanza, hoja ya biashara ya utumwa si sahihi kwa nyakati zetu. Wakoloni walipeleka faida ya biashara ya utumwa Ulaya na Uarabuni. Kwetu sisi faida za bandari zinabaki nchini unless zichepushwe uswiss na wahalifu wetu.

Pili, kuna nchi zinajenga uchumi kwa huduma ''services'' na si uzalishaji. Mifano ni utalii wa Asia na Seychelles na Mauritius hata Afrika kusini. Tanzania, Utalii unaingiza pato la Taifa kuliko Kilimo. Kuna Nchi zina GDP kwa remittance kama Nicaragua, Nepal n.k.

Kutengeneza reli ya kutoa huduma kwa nchi jirani na kuchukua ushuru kuna tatizo gani ikiwa inachangia GDP?
Tazama kodi za Bandari peke yake zinavyochangia hazina. Kuna shida gani kufanya bandari kama kitega uchumi.

Tatu, ujenzi wa reli una stimulate economy. Mfano, tangu kujengwa daraja la Mkapa na barabara ya kusini, mikoa ya kusini imepanda skiuchumi. Infrastracture zinategemea matumizi na matunzo! ni vyanzo vizuri vya mapato

Natamani kungekuwa na reli ya Mtwara -Mbambabay au Arusha-Musoma.
Ukitaka kuendelea hutakiwi kuweka viwanda au mashamba! tengeneza miundo mbinu tu, kila kitu kitafuata chenyewe.
Nadhani hujanisoma vizuri kuelewa hoja yangu kwa sababu Bandari haizalishi kitu bali hutoza tozo mbali mbali ya meli zinapo pakia ama kupakua mizigo. Hizi ni huduma ndio maana ikaitwa Miundombinu iwe reli, barabara, viwanja vya ndege, maghala n.k sio biashara yenyewe na huwa havina faida kubwa bali hufanisi shughili nyingine za Kiuchumi. Kule kwenye kuuza Bidhaa zenu nje na mzunguko wa fedha ndiko hukuza GDP halisi ya nchi.

Utalii ni Biashara kama nilivyosema viwanda, hii sio Miundombinu. Hata wao huko Seychelles na Mauritius walijenga miundombinu ili kuboreza Utalii wao na Waka facilitate. Sasa wewe nambie kulingana na.maono ya Viongozi wetu, sisi tinajenga hizi Bandari na reli kwa ajili gani haswa?

Tunaboreshaje huduma zipi nchini ikiwa hatuna ongezeko la uzalishaji wa bidhaa za ndani, hatuna viwanda, kilimo bado hakipewi Kipaumbele na ukiwasikia viongozi wetu leo wanazungumzia usafiri wa bidhaa za DRC, Burundi, Rwanda, Uganda n.k. hutasikia nguvu yote hii na uwekezaji huu mkubwa utasaidia sisi ongezeko la usafirishaji wa bidhaa zetu kadhaa wa kadhaa kwenda nje? That's where the money is! Mbali kabisa ukiacha ongezeko la ajira nchini.

Katika maono haya tulonayo ya Ushorobo tunategemea mapato gani kama sii tozo za kodi na Ushuru. Bidhaa zote ni za nje wala hatutaongia Ubia kama bomba la mafuta kutoka Uganda!

Kuna tofauti gani na enzi za Utumwa wakati ambao Kilwa, Bagamoyo na Zanzibar zilitumiwa kwa usafiri wa bidhaa zao wakineemesha nchi zao.

Narudia kusema, hata Wajarumani walijenga reli ya kati mwisho Kigoma nanya Tanga ili kusafirisha bidhaa zinazozalishwa ndani iwe mawese, Chai, Mpira, Pamba, Magogo, Katani, Kahawa, Pembe za ndovu na dhahabu. Na ndovyo nchi zote duniani zinajitazama mahitaji yao kwanza katikamkukuza Uchumi wao.

Kwa mtazamo wangu kama sisi hatuna maono juu ya kukuza Uzalishaji wa bidhaa zetu wenyewe, kuwekeza katika ujenzi wa viwanda sambamba na ujenzi wa miundombinu ya Bandari, SGR na Umeme. Tutakuwa tumerudi nyuma sana. Tusidanganywe na Hormuz Strait ya Iran kama njia kuunya mapato, pale ugonvi mkubwa na Marekani sio ushorobo huo bali pato la mafuta (oli) ya Iran.
 
Nadhani hujanisoma vizuri kuelewa hoja yangu kwa sababu Bandari haizalishi kitu bali hutoza tozo mbali mbali ya meli zinapo pakia ama kupakua mizigo. Hizi ni huduma ndio maana ikaitwa Miundombinu iwe reli, barabara, viwanja vya ndege, maghala n.k sio biasjara yenyewe na huwa havina faida kubwa bali hufanisi shughili nyingine za Kiuchumi. Kule kwenye kuuza Bidhaa zenu nje ndiko hukuza GDP halisi ya nchi.
Hauko sahihi. Singapore na Dubai ni nchi ambazo maendeleo yao yamechangiwa sana na bandari zao. Bandari ya Singapore inachangia 7% ya GDP ya Singapore. Bandari ya Jebel Ali Free Zone inachangia 23-33% ya uchumi wa Dubai. Bandari ya Rotterdam inazalisha Euro bilioni 45.6 na inachangia 6.2% ya uchumi wa Netherlands. Biashara kubwa ni kupakua na kupakua mizigo kupeleka nchi nyingine. Biashara ya huduma sasa hivi inachindana na uzalishaji wa bidhaa. Nchi nyingi zilizoendelea zimejitoa katika uzalishaji wa bidhaa kubwa kwa sababu 1.profit margin yake ni ndogo, 2. ushindani mkubwa na uchafuzi wa mazingira. Aidha, sehemu kubwa ya uzalishaji mwingi sasa hivi unaelekea katika matumizi makubwa ya robots na AI. Baada ya muda cheap labour haitakuwa kigezo cha kujenga kiwanda.
Utalii ni Biashara kama nilivyosema viwanda, hii sio Miundombinu. Hata wao huko Seychelles na Mauritius walijenga miundombinu ili kuboreza Utalii wao na Waka facilitate. Sasa wewe nambie kulingana na.maono ya Viongozi wetu, sisi tinajenga hizi Bandari na reli kwa ajili gani haswa?
Inategemea aina ya utalii unaotaka. Kama utalii wako ni watu kutembelea mbuga uboreshaji wa miundo mbinu sio mpango sahihi. Ili kuhakikisha mbuga zinadumu ni muhimu ku control idadi ya watu wanaotembelea. Ndio maana hali inayoendelea Ngorongoro sio sustainable. Kuhusu maono ya viongozi wetu sijui kama kuna mpango mahsusi wa matumizi ya bandari na reli katika kuboresha maisha ya watanzania wa kawaida. Wangekuwa na maono wasingezungumzia ujenzi wa reli kati ya Arusha na Musoma ambayo itaathiri sana mbuga ya Serengeti.
Tunaboresha huduma zipi nchini ikiwa hatuna uongezeko na uzaliahaji wa bidhaa za ndani, hatuna viwanda, kilimo bado hakipewi Kipaumbele na ukiwasikia viongozi wetu leo wanazungumzia usafiri wa bidhaa za DRC, Burundi, Rwanda, Uganda n.k. hutasikia nguvu yote hii na uwekezaji huu mkubwa utasaidia sisi ongezeko la usafirishaji wa bidhaa kadhaa wa kadhaa kwenda nje? That's where the money is! Mbali kabisa ukiacha ongezeko la ajira nchini.
Mimi nadhani kuliko kuwekeza katika uzalishaji wa bidhaa, tungewekeza katika uboreshaji wa elimu ya msingi ili iendane na aina ya uzalishaji unaotakiwa katika huu wakati tunaoishi. Aidha, tunatakiwa kuwekeza katika matumizi ya kiswahili katika nyanja za tamaduni na burdani.
Katika maono haya tulonayo ya Ushorobo tunategemea mapato gani kama sii tozo za kodi na Ushuru. Bidhaa zote ni za nje wala hatutaongia Ubia kama bomba la mafuta kutoka Uganda!
Hakuna ulazima wa kutengeneza kila kitu. Kama kuna nchi ambayo ni bora katika uzalishaji wa bidhaa fulani tuachane nayo. Ni ujinga kukazania kutengeneza magari yetu, simu zetu, majokofu yetu n.k. kwa sababu soko lake litakuwa limited sana. Tutapata shida sana kuuza magari yanayoitwa Nyumbu sio tu kwa kukosa ubora bali pia kutokuwa na uwezo wa kuyatangaza ipasavyo katika masoko ya nchi nyingine. Hata wachina walipata shida sana kushindana na Apple katika mauzo ya simu janja nchini mwao. Kimbilio lao lilikuwa ni nchi kama zetu ambako bei ni kigezo kikubwa. Sasa hivi, ingawa simu zao kama za One Plus zimeboreshwa sana lakini bado watu wanapendelea zaidi I Phone.
Kuna tofauti gani na enzi za Utumwa wakati ambao Kilwa, Bagamoyo na Zanzibar zilitumiwa kwa usafiri wa bidhaa zao wakineemesha nchi zao.

Narudia kusema, hata Wajarumani walijenga reli ya kati mwisho Kigoma nanya Tanga ili kusafirisha bidhaa zinazozalishwa ndani iwe mawese, Chai, Mpira, Pamba, Magogo, Katani, Kahawa, Pembe za ndovu na dhahabu. Na ndovyo nchi zote duniani zinajitazama mahitaji yao kwanza katikamkukuza Uchumi wao.
Sio dhambi nchi kutaka kujineemesha. Wajibu wetu ni sisi kuangalia namna gani tunaweza kujineemesha kupitia wao. Kampuni ya Bajaj ilianza kutengeneza pikipiki za Vespa underlicence. Baada ya muda wakaachana na Vespa na kushindana nao kiasi ya sasa wao kuwazidi katika uzalishaji wa pikipiki. Kutegemea fadhila ndio kumetufikisha hapa tulipo. Tunapaswa kuwavuta, halafu wakiwa hapa kujifunza kutoka kwao ili baadae tuachane nao. Na yote haya hayatafanywa na serikali. Serikali wajibu wake sio kuzalisha bali kuweka mazingira yatakayowezesha uzalishaji.
Kwa mtazamo wangu kama sisi hatuna maono juu ya kukuza Uzalishaji wa bidhaa zetu wenyewe, kuwekeza katika ujenzi wa viwanda sambamba na ujenzi wa miundombinu ya Bandari, SGR na Umeme. Tutakuwa tumerudi nyuma sana. Tusidanganywe na Hormuz Strait ya Iran kama njia kuunya mapato, pale ugonvi mkubwa na Marekani sio ushorobo huo bali pato la mafuta (oli) ya Iran.
Hapa sijakuelewa.

Amandla...
 
Hauko sahihi. Singapore na Dubai ni nchi ambazo maendeleo yao yamechangiwa sana na bandari zao. Bandari ya Singapore inachangia 7% ya GDP ya Singapore. Bandari ya Jebel Ali Free Zone inachangia 23-33% ya uchumi wa Dubai. Bandari ya Rotterdam inazalisha Euro bilioni 45.6 na inachangia 6.2% ya uchumi wa Netherlands. Biashara kubwa ni kupakua na kupakua mizigo kupeleka nchi nyingine. Biashara ya huduma sasa hivi inachindana na uzalishaji wa bidhaa. Nchi nyingi zilizoendelea zimejitoa katika uzalishaji wa bidhaa kubwa kwa sababu 1.profit margin yake ni ndogo, 2. ushindani mkubwa na uchafuzi wa mazingira. Aidha, sehemu kubwa ya uzalishaji mwingi sasa hivi unaelekea katika matumizi makubwa ya robots na AI. Baada ya muda cheap labour haitakuwa kigezo cha kujenga kiwanda.

Inategemea aina ya utalii unaotaka. Kama utalii wako ni watu kutembelea mbuga uboreshaji wa miundo mbinu sio mpango sahihi. Ili kuhakikisha mbuga zinadumu ni muhimu ku control idadi ya watu wanaotembelea. Ndio maana hali inayoendelea Ngorongoro sio sustainable. Kuhusu maono ya viongozi wetu sijui kama kuna mpango mahsusi wa matumizi ya bandari na reli katika kuboresha maisha ya watanzania wa kawaida. Wangekuwa na maono wasingezungumzia ujenzi wa reli kati ya Arusha na Musoma ambayo itaathiri sana mbuga ya Serengeti.

Mimi nadhani kuliko kuwekeza katika uzalishaji wa bidhaa, tungewekeza katika uboreshaji wa elimu ya msingi ili iendane na aina ya uzalishaji unaotakiwa katika huu wakati tunaoishi. Aidha, tunatakiwa kuwekeza katika matumizi ya kiswahili katika nyanja za tamaduni na burdani.

Hakuna ulazima wa kutengeneza kila kitu. Kama kuna nchi ambayo ni bora katika uzalishaji wa bidhaa fulani tuachane nayo. Ni ujinga kukazania kutengeneza magari yetu, simu zetu, majokofu yetu n.k. kwa sababu soko lake litakuwa limited sana. Tutapata shida sana kuuza magari yanayoitwa Nyumbu sio tu kwa kukosa ubora bali pia kutokuwa na uwezo wa kuyatangaza ipasavyo katika masoko ya nchi nyingine. Hata wachina walipata shida sana kushindana na Apple katika mauzo ya simu janja nchini mwao. Kimbilio lao lilikuwa ni nchi kama zetu ambako bei ni kigezo kikubwa. Sasa hivi, ingawa simu zao kama za One Plus zimeboreshwa sana lakini bado watu wanapendelea zaidi I Phone.

Sio dhambi nchi kutaka kujineemesha. Wajibu wetu ni sisi kuangalia namna gani tunaweza kujineemesha kupitia wao. Kampuni ya Bajaj ilianza kutengeneza pikipiki za Vespa underlicence. Baada ya muda wakaachana na Vespa na kushindana nao kiasi ya sasa wao kuwazidi katika uzalishaji wa pikipiki. Kutegemea fadhila ndio kumetufikisha hapa tulipo. Tunapaswa kuwavuta, halafu wakiwa hapa kujifunza kutoka kwao ili baadae tuachane nao. Na yote haya hayatafanywa na serikali. Serikali wajibu wake sio kuzalisha bali kuweka mazingira yatakayowezesha uzalishaji.

Hapa sijakuelewa.

Amandla...
Nimekusoma vizuri lakini bado huelewi undani wa hoja yangu. Isitoshe pato la bandari pekee iwe ya Dubai au popote kwa kupakia na kushusha mizigo ya nje ni asilimia ndogo. Kumbuka kuwa Dubai ina mafuta (Oil) meli zinapangana kwenda chukua mafuta. Tanker zinaingia kna kutoka kila saa. It's what's on their market ndio inayoipa nguvu port of Dubai

Pili, Dubai ni maarufu duniani kama kitovu cha Bashara, kila mtu anaenda shopping Dubai na ndio kiamsho cha biashara na nguvu ya bandari ya Dubai. meli nyingi zinazoenda pale kushusha mizigo, hiyo.mizigo haiendi popote nje, budhaa zote zinauzwa pale Dubai, wageni njooni mnunue hapa! hii imeongeza thamani ya bandari yake. Hakuna reli ya kwenda sijui wapi!

Kama ingekuwa kusafirisha bidhaa ipite tu pale kwenda nchi jirani, Dubai isingekuwa ilivyo leo, isitoshe nchi jirani yake zote wanazo Bandari zao. Kuwait, Qatar, Oman, Abu dhabi n.k. so nini kimefanyika Dubai? Na nashukuru umetoa mifano ya bandari hizo ambazo ukitazama utagundua hazipakani na nchi ambazo hazina Bahari (Land locked) Kwa hiyo Bandari zao ni kwa maslahi ya nchi zao sio nchi jirani

Singapole, ile ni nchi ya viwanda, sehemu kubwa ya mapato yao ni mauzo ya bidhaa zao, they are industrialised, hawategemei mapato ya Bandari kwa malengo kama sisi, Bandari zao zinatumiwa na meli nyingi kusimama pale (service) sio kushusha mizigo sijui ya nchi jirani. Nchi jirani zipi? kiuhalisia nchi zote zina Bandari zake pia. Swali liwe Kwa nini meli nyingi hazisimami Bandari za majirani isipokuwa Singapole? wao wanasafirisha bidhaa zaidi ya nchi jirani.

Kwa hiyo, bado yale mawazo ya Kujenga Bandari na reli kwa ajili ya mizigo ya nchi jirani ni Kosa kubwa sana la Kiuchumi kwetu, kinachotakiwa ni sisi kujenga Bandari na reli kwa ajili ya sisi wenyewe kuwauzia hizo nchi.

Waje Tanzania kununua mali hapa.au sisi tusafirishe bidhaa zetu kwenda kwao. Hii habari ya njia ya kupitia itawafaidisha nchi jirani zaidi kuliko sisi. Na yawezekana sisi ndio tukawa mateja tukaanza kununu bidhaa zao wao.

Narudia kusema, ujenzi wa Bandari, reli na Umeme ulenge kukuza Uzalishaji wa bidhaa za ndani sio kusafirisha mizigo ya nchi nyingine.
 
Nimekusoma vizuri lakini bado huelewi undani wa hoja yangu. Isitoshe pato la bandari pekee iwe ya Dubai au popote kwa kupakia na kushusha mizigo ya nje ni asilimia ndogo. Kumbuka kuwa Dubai ina mafuta (Oil) meli zinapangana kwenda chukua mafuta. Tanker zinaingia kna kutoka kila saa. It's what's on their market ndio inayoipa nguvu port of Dubai
Nimekusoma vizuri. Dubai haina mafuta kama Abu Dhabi. Kinachokipa utajiri Dubai sio mafuta bali location yake kama kiungo cha biashara kati ya mabara tofauti. Na hii isingewezekana kama wasingewekeza kwenye bandari. Uwepo wa bandari hiyo ndio ulio ipa uwezo wa kusafirisha bidhaa zake nyingine.
Pili, Dubai ni maarufu duniani kama kitovu cha Bashara, kila mtu anaenda shopping Dubai na ndio kiamsho cha biashara na nguvu ya bandari ya Dubai. meli nyingi zinazoenda pale kushusha mizigo, hiyo.mizigo haiendi popote nje, budhaa zote zinauzwa pale Dubai, wageni njooni mnunue hapa! hii imeongeza thamani ya bandari yake. Hakuna reli ya kwenda sijui wapi!
Imekuwa kitovu cha biashara kwa sababu ya bandari yake, sio mafuta yake. Hata kabla ya kupatikana ilikuwa kitovu cha biashara kupitia mashua zake. Bidhaa zinazouzwa na kutumika Dubai ni chache sana ukilinganisha na zinazo safirishwa kwenda nchi nyingine. Ingekuwa vinginevyo, bandari yao ingekufa zamani sana.
Kama ingekuwa kusafirisha bidhaa ipite tu pale kwenda nchi jirani, Dubai isingekuwa ilivyo leo, isitoshe nchi jirani yake zote wanazo Bandari zao. Kuwait, Qatar, Oman, Abu dhabi n.k. so nini kimefanyika Dubai?
Bila ile bandari Dubai isingekuwa kama ilivyo sasa maana haijajaliwa utajiri wa asili kama hizo nchi ulizotaja. Dubai sio tu iliwekeza kwenye bandari bali iliboresha sana ufanisi na connections kiasi kuwa nchi nyingine zinapendelea zaidi kupitisha bidhaa zao Dubai kuliko kwenye bandari zao. Zile nchi zilibweteka na utajiri wa asili waliokuwa nao.
Singapole, ile ni nchi ya viwanda, sehemu kubwa ya mapato yao ni mauzo ya bidhaa zao, they are industrialised, hawategemei Bandari kwa malengo kama sisi, Bandari zao zinatumiwa na meli nyingi kusimama pale (service) sio kushusha mizigo sijui ya nchi jirani. Nchi jirani zipi? kiuhalisia zote zina Bandari pia. Swali liwe Kwa nini meli nyingi hazisimami Bandari za majirani isipokuwa Singapole?
Singapore isingekuwa na viwanda kama isingekuwa na bandari bora. Asilimia 80 ya biashara ya bandari ya Singapore ni transshipment. Hii ni kupakua mizigo kutoka meli moja kuingiza kwenye meli nyingine. Inafanya hivyo kwa mizigo inayoenda nchi zilizopo jirani yake. Meli zinasimama Singapore kwa sababu ya connections zake na ufanisi wake. Meli inaweza kushusha mizigo Singapore inayoenda nchi zaidi kuliko kama ingesimama kwenye Port Kelang Malaysia. Ni suala pia la economies of scale. Nchi nyingi za Europe zina bandari lakini zinapendelea kupitisha mizigo yao Rotterdam. Kwa kufanya hivyo inawaondolea ulazima wa kuwekeza kwenye bandari kubwa kwa sababu wanajua mzigo ukifika Rotterdam unaweza kwenda sehemu yeyote duniani kwa urahisi na mapema. Hii imerahisishwa sana siku hizi kutokana na matumizi makubwa ya containers.
Kwa hiyo, bado yale mawazo ya Kujenga Bandari na reli kwa ajili ya mizigo ya nchi jirani ni Kosa kubwa sana la Kiuchumi kwetu, kinachotakiwa ni sisi kujenga Bandari na reli kwa ajili ya sisi wenyewe kuwauzia hizo nchi.
Hayo ni mawazo ya kinyerere. Hatuzalishi bidhaa za kutosha kujustify uwekekezaji mkubwa kama huo. Njia pekee ya kufanya mradi huo uwe economically feasible ni kuwa na bandari inayoweza kupokea na kusafirisha mizigo inayoenda sio tu DRC, Rwanda, Burundi n.k. bali pia Comoro na visiwa vingine. Tukiwekeza vizuri, bandari hiyo inaweza ku feed pia bandari za Mombasa, Beira n.k. Ni kujipanga tu.

Mfano mwingine ni kiwanja cha ndege. Abiria wengi wanaotumia airport ya Addis ni wanaounganisha kwenda kungine. Ethiopia wangelenga abiria wa kiethiopia peke yake ingekula kwao.
Waje Tanzania kununua mali hapa.au sisi tusafirishe bidhaa zetu kwenda kwao. Hii habari ya njia ya kupitia itawafaidisha nchi jirani zaidi kuliko sisi. Na yawezekana sisi ndio tukawa mateja tukaanza kununu bidhaa zao wao.
Hauwezi kumlazimisha mtu aje kununua kitu Tanzania. Ila kama una bandari na connections nzuri watengenezaji wa vifaa wanaweza kujenga viwanda na ma godown Tanzania ili bidhaa zao zitakazo tengenezwa Tanzania ziweze kusafirishwa kwa gharama ndogo kwenda nchi nyingine.

Wataweza kwa mfano kusafirisha components za malori kutoka China mpaka Tanzania ambako watazi assemble na kusafirisha malori kwenda nchi jirani. Hii ni afadhali kwao kuliko kusafirisha lori zima kutoka China kwenda nchi za jirani.
Narudia kusema, ujenzi wa Bandari, reli na Umeme ulenge kukuza Uzalishaji wa bidhaa za ndani sio kusafirisha mizigo ya nchi nyingine.
Hauko sahihi kwenye hilo. Uzalishaji wa bidhaa nchini una challenge nyingi ikiwa pamoja na ukubwa wa soko. Ukiwa na bandari bora, uwigo wa soko unapanuka na hivyo kuwavutia watengenezaji wa bidhaa. Hata makampuni kama Amazon watavutiwa kujenga logistics centre zao Tanzania tukiwa na bandari na usafiri bora.

Kujenga viwanda bila kuwa na uhakika wa soko au uwezo wa kusafirisha bidhaa hakutatusaidia sana.

Amandla...
 
Nitajaribu kukujibu taratibu hoja moja baada ya nyingine. Unaposema Location yake una maana gani? Kama ni mkondo wa Harmuz Strait, Muscat, Oman ipo sehemu nzuri kuliko Dubai! Kuunganisha mabara matatu. Dubai lazima uingie ndani ya Hormuz Strait, Unaingia kule kufanya nini ikiwa hakuna Biashara?


Naona bado unatoka nje ya mjadala, sijasema tusijenge Bandari au kwamba Bandari haina umuhimu isipokuwa nachosema unajenga Bandari na reli kwa ajili gani? Unalenga kukuza biashara zako au za nchi jirani. Hapa ndipo napokosana na wewe. Bandari tujenge kubwa East Africa haina tatizo lakini unatarajia kufanya biashara gani itakayo ongeza pato la Taifa.

Kama ni kupokea mizigo ya nchi jirani na kuzisafirisha hii sio sababu ya kuwepo Bandari za Dubai, Singapole na hata Rotterdam! Nchi jirani zote zina Bandari zake wala sio land locked. So kwa nini Bandari hizo zimekuwa maarufu kibiashara? ni Free Port and Free Trade Zone.

Kenya wana Bandari kama sisi lakini Kenya ndio tunafanya nao biashara kubwa kuliko nchi jirani nyinginezo kwa sababu Kenya wana viwanda na wanapata mali ghafi kutoka kwetu. Tunauziana wenyewe mazao, na Bishara nyinginezo.

Naamini kabisa Magufuli alitaka kujenga Bandari, reli na Bwawa la Nyeeere ili kukuza Uchumi wetu wa ndani (Uzalishaji) kwanhiyo Viwanda vingeenda sambamba na ujenzi wa reli na kuboresha uwezo wa Bandari zetu, hii ya kupeleka nchi jirani ni kibwagizo baada ya makubaliano na nchi hizo. Tunajenga kwetu kwa ajili ya matumizi yetu na wao wataunganisha kwao kwanajili yao. Sasa isije kuwa tunajenga reli na Bandari ili kuhudumia nchi jirani tukaishia hapo.

Dubai hawakufikiri hivyo, Singapole hawakufikiri hivyo na kwingineko iwe Amerika, China au South Africa.
 
Nitajaribu kukujibu taratibu hoja moja baada ya nyingine. Unaposema Location yake una maana gani? Kama ni mkondo wa Harmuz Strait, Muscat, Oman ipo sehemu nzuri kuliko Dubai! Kuunganisha mabara matatu. Dubai lazima uingie ndani ya Hormuz Strait, Unaingia kule kufanya nini ikiwa hakuna Biashara?
Suala sio tu kuwa kwenye mkondo wa Hormuz bali uamuzi wa ku take advantage na location hiyo. Dubai waliamua mapema sana kuwekeza kwenye bandari na logistics zake kabla ya Oman na nchi nyingine za jirani. Inawezekana pia location yake mwanzoni tu wa Hormuz strait uliikinga na madhoruba ya gulf of Oman na hivyo kuweza kuhudumia meli kwa urahisi zaidi. Na wao kuwa sehemu ya UAE iliwawezesha kuwa bandari kuu yao. Kutokana na umuhimu wa bandari kwa uchumi wao sasa wanajenga terminal nyingine nje ya Furaijah ili kuwa na alternative Hormuz ikifungwa.

Muscat pia imezungukwa na milima, hivyo inakuwa ngumu kuwa na maeneo makubwa ya kuhudumia containers. Mwisho, kiongozi wa Dubai alitaka iwe international hivyo ali relax tamaduni yake za eneo hilo kuvutia zaidi wawekezaji na watu kutoka nchi nyingine nje ya uarabuni. Muscat iliamua kulinda utamadunu wake na kujikita katika utalii wa kitamaduni na kihistoria.
Naona bado unatoka nje ya mjadala, sijasema tusijenge Bandari au kwamba Bandari haina umuhimu isipokuwa nachosema unajenga Bandari na reli kwa ajili gani? Unalenga kukuza biashara zako au za nchi jirani. Hapa ndipo napokosana na wewe. Bandari tujenge kubwa East Africa haina tatizo lakini unatarajia kufanya biashara gani itakayo ongeza pato la Taifa.
Naona unataka kuhamisha magoli. Utaulizaje sababu ya kujenga bandari kama hauoni umuhimu wake?

Tunatofautiana katika definition ya biashara. Kuwepo kwq bandari kunaongeza pato la taifa kwa kuwa mlango mkubwa wa bidhaa zinazotoka na kwenda katika nchi nyingine. Nchi nyingi zilizowekeza sana katika bandari hazikufanya hivyo kwa ajili ya bidhaa zake wenyewe bali kuwa hub ya usafirishaji wa bidhaa kutoka nchi nyingine.

Ndio maana nikakutolea mfano wa Airport ya Addis ambayo inategemea wasafiri wanaopita Addis kuliko wanaoenda na kutoka Ethiopia. Uwepo wa Airport imewezesha biashara nyingi za sekta ya aviation.
Kama ni kupokea mizigo ya nchi jirani na kuzisafirisha hii sio sababu ya kuwepo Bandari za Dubai, Singapole na hata Rotterdam! Nchi jirani zote zina Bandari zake wala sio land locked. So kwa nini Bandari hizo zimekuwa maarufu kibiashara? ni Free Port and Free Trade Zone.
Tunarudi pale pale. Ingawa nchi jirani zina bandari zake, bandari hizo hazina uwezo wa Dubai, Singapore au Rotterdam. Bandari zao zinatumika zaidi kusafirisha bidhaa kwenda na kutoka katika bandari hizo kuu ambako kuna mameli makubwa yanayoenda katika mabara mengine. Hilo la Free port limetokana na uwekekezaji mkubwa katika bandari zao. Bila bandari bora hazina mantik. Ndio maana duty free zone zetu hazina mvuto wa maana. Haina maana kutengeneza bidhaa ambazo utashindwa kuzisafirisha kwa urahisi.
Kenya wana Bandari kama sisi lakini Kenya ndio tunafanya nao biashara kubwa kuliko nchi jirani nyinginezo kwa sababu Kenya wana viwanda na wanapata mali ghafi kutoka kwetu. Tunauziana wenyewe mazao, na Bishara nyinginezo.
Biashara yetu yote na Kenya haipitii kwenye bandari. Sidhani kama Kenya inatoa mali ghafi za viwanda vyake kutoka Tanzania peke yake. Aidha, wao nao wanaona fursa ya bandari ndio maana wanawekeza ili watoe huduma bora zaidi kwa nchi kama Uganda, Rwanda na hata Tanzania. Ni washindani wetu.
Naamini kabisa Magufuli alitaka kujenga Bandari, reli na Bwawa la Nyeeere ili kukuza Uchumi wetu wa ndani (Uzalishaji) kwanhiyo Viwanda vingeenda sambamba na ujenzi wa reli na kuboresha uwezo wa Bandari zetu, hii ya kupeleka nchi jirani ni kibwagizo baada ya makubaliano na nchi hizo. Tunajenga kwetu kwa ajili ya matumizi yetu na wao wataunganisha kwao kwanajili yao. Sasa isije kuwa tunajenga reli na Bandari ili kuhudumia nchi jirani tukaishia hapo.
Haya ni mawazo ya kijamaa yaliyotufanya tupoteze muda kuwekeza kwenye viwanda vya kubuni na kuunda magari ( Nyumbu), baiskeli, korosho n.k. Badala ya kuwekeza kwenye mazingira yatakayo wavutia wawekezaji sisi tulikimbilia kujenga viwanda. Badala ya viwanda hivyo tungewekeza kwenye miundo mbinu ya usafiri, maji safi, usafirishaji, elimu bora na sheria bora, wawekezaji wangejenga hivyo viwanda na kuhakikisha kuwa bidhaa zake zina soko. Wewe unataka tufanye opposite. Mimi ninachosema ni kuwa tukiwa na mazingira rafiki na mazuri, serikali haitakuwa na sababu ya kujenga viwanda vya magari bali kampuni zinazotengeneza magari zitavutiwa kujenga viwanda Tanzania kwa sababu soko la bidhaa zao litakuwa zaidi ya Tanzania. Unacho shauri wewe ni kutufanya tuwe kama Korea ya Kaskazini.
Dubai hawakufikiri hivyo, Singapole hawakufikiri hivyo na kwingineko iwe Amerika, China au South Africa.
Sio kweli. Udogo wa nchi za Dubai, Singapore na Netherlands ndio sababu ziliwafanya wawekeze katika kuwa hub za usafirishaji wa nchi za jirani. Nchi kama China, Marekani zina advantage ya ukubwa wa masoko yao ya ndani. Lakini hata wao wamekuwa wakihamishia viwanda vyao nje ya nchi zao. China Vietnam, Cambodia n.k. na Marekani Mexico. Pamoja na juhudi zake, Trump ameshindwa kuvirudisha viwanda vingi Marekani. Na tariff alizoweka ndio zina muharibia kabisa.

Dunia ya leo ni ya kujua strength na weakness zako na kuzitumia kikamilifu.
Mimi naona niishie hapa maana nimeanza kujirudia na sitaki huu mjadala ugeuke kuwa wa mabishano. Naona tukubali tu kutofautiana.

Amandla...
 
Suala sio tu kuwa kwenye mkondo wa Hormuz bali uamuzi wa ku take advantage na location hiyo. Dubai waliamua mapema sana kuwekeza kwenye bandari na logistics zake kabla ya Oman na nchi nyingine za jirani. Inawezekana pia location yake mwanzoni tu wa Hormuz strait uliikinga na madhoruba ya gulf of Oman na hivyo kuweza kuhudumia meli kwa urahisi zaidi. Na wao kuwa sehemu ya UAE iliwawezesha kuwa bandari kuu yao. Kutokana na umuhimu wa bandari kwa uchumi wao sasa wanajenga terminal nyingine nje ya Furaijah ili kuwa na alternative Hormuz ikifungwa.

Muscat pia imezungukwa na milima, hivyo inakuwa ngumu kuwa na maeneo makubwa ya kuhudumia containers. Mwisho, kiongozi wa Dubai alitaka iwe international hivyo ali relax tamaduni yake za eneo hilo kuvutia zaidi wawekezaji na watu kutoka nchi nyingine nje ya uarabuni. Muscat iliamua kulinda utamadunu wake na kujikita katika utalii wa kitamaduni na kihistoria.

Naona unataka kuhamisha magoli. Utaulizaje sababu ya kujenga bandari kama hauoni umuhimu wake?

Tunatofautiana katika definition ya biashara. Kuwepo kwq bandari kunaongeza pato la taifa kwa kuwa mlango mkubwa wa bidhaa zinazotoka na kwenda katika nchi nyingine. Nchi nyingi zilizowekeza sana katika bandari hazikufanya hivyo kwa ajili ya bidhaa zake wenyewe bali kuwa hub ya usafirishaji wa bidhaa kutoka nchi nyingine.

Ndio maana nikakutolea mfano wa Airport ya Addis ambayo inategemea wasafiri wanaopita Addis kuliko wanaoenda na kutoka Ethiopia. Uwepo wa Airport imewezesha biashara nyingi za sekta ya aviation.

Tunarudi pale pale. Ingawa nchi jirani zina bandari zake, bandari hizo hazina uwezo wa Dubai, Singapore au Rotterdam. Bandari zao zinatumika zaidi kusafirisha bidhaa kwenda na kutoka katika bandari hizo kuu ambako kuna mameli makubwa yanayoenda katika mabara mengine. Hilo la Free port limetokana na uwekekezaji mkubwa katika bandari zao. Bila bandari bora hazina mantik. Ndio maana duty free zone zetu hazina mvuto wa maana. Haina maana kutengeneza bidhaa ambazo utashindwa kuzisafirisha kwa urahisi.

Biashara yetu yote na Kenya haipitii kwenye bandari. Sidhani kama Kenya inatoa mali ghafi za viwanda vyake kutoka Tanzania peke yake. Aidha, wao nao wanaona fursa ya bandari ndio maana wanawekeza ili watoe huduma bora zaidi kwa nchi kama Uganda, Rwanda na hata Tanzania. Ni washindani wetu.

Haya ni mawazo ya kijamaa yaliyotufanya tupoteze muda kuwekeza kwenye viwanda vya kubuni na kuunda magari ( Nyumbu), baiskeli, korosho n.k. Badala ya kuwekeza kwenye mazingira yatakayo wavutia wawekezaji sisi tulikimbilia kujenga viwanda. Badala ya viwanda hivyo tungewekeza kwenye miundo mbinu ya usafiri, maji safi, usafirishaji, elimu bora na sheria bora, wawekezaji wangejenga hivyo viwanda na kuhakikisha kuwa bidhaa zake zina soko. Wewe unataka tufanye opposite. Mimi ninachosema ni kuwa tukiwa na mazingira rafiki na mazuri, serikali haitakuwa na sababu ya kujenga viwanda vya magari bali kampuni zinazotengeneza magari zitavutiwa kujenga viwanda Tanzania kwa sababu soko la bidhaa zao litakuwa zaidi ya Tanzania. Unacho shauri wewe ni kutufanya tuwe kama Korea ya Kaskazini.

Sio kweli. Udogo wa nchi za Dubai, Singapore na Netherlands ndio sababu ziliwafanya wawekeze katika kuwa hub za usafirishaji wa nchi za jirani. Nchi kama China, Marekani zina advantage ya ukubwa wa masoko yao ya ndani. Lakini hata wao wamekuwa wakihamishia viwanda vyao nje ya nchi zao. China Vietnam, Cambodia n.k. na Marekani Mexico. Pamoja na juhudi zake, Trump ameshindwa kuvirudisha viwanda vingi Marekani. Na tariff alizoweka ndio zina muharibia kabisa.

Dunia ya leo ni ya kujua strength na weakness zako na kuzitumia kikamilifu.
Mimi naona niishie hapa maana nimeanza kujirudia na sitaki huu mjadala ugeuke kuwa wa mabishano. Naona tukubali tu kutofautiana.

Amandla...
Mkuu naona bado unazungumzuia Bandari kama kwamba mimi napinga Ujenzi ama kuwepo kwa Bandari kubwa nchini. Tanzania tunazo 3 kubwa na tunatarajia kujenga nyingine ya Bagamoyo. Ihave no problem with that.

Infact kama unakumbuka miaka ile ya JK 2005 -2010) ni mimi niloweka hapa #Jamiiforums Idea ya ujenzi wa Bandari ya Bagamoyo ili kuachana na Bandari ya Dar es Salaam kutokana na ufinyu wa mkondo wake.

Nikaandika kuwa Bandari ya Dar es Salaaam itumike kwa ajili ya shughuli za mji mkuu wa Biashara. Bandari

Itumike kwa meli za Utalii Cruiser ships, Yatch Clubs na Boat za usafiri wa ndani . Pia zijengwe Hotels, Condo, restaurant, maduka na kadhalika.

Bandari ya Bagamoyo itakayo jengwa muhimu iwe Free Port na Free Trade zone. Laa haiwezekani basi ijengwe Bandari hiyo Zanzibar kwa mpango huo huo, Zanzibar Port iwe free port and free trade zone. Nchi jirani wote waje kufanya shopping zao Tanzania badala ta kwenda China. Sasa mkuu wangu kama hukumbi basi wapo wanaokumbuka! Hiki kichwa kina Idea za kufa mtu.

Labda nifafanue zaidi nachokataa mimi. Ni malengo yanayokusudiwa ni kuhudumia usafiri wa mizigo ya nchi jirani badala ya kuhudumia mizigo yetu sisi – Period. Mtazamo wangu ujenzi wowote wa Miundombinu lazima uhusiane na maonio ama vision ya maendeleo ya Tanzania kwanza.

Umeendelea kutolea mfano wa Dubai, sikatai yote unayosema, lakini Dubai haina nchi jirani zinazohitaji mizogo ipitie hapo. Na ukweli ni kwamba Dubai mchango wa Bandari kwa hizo tozo ni kama asilimia 17, lakini asilimia 70+ ya mapato yake inatokana na biashara za ndani kutokana na Bandari hiyo. Bandari ya Dubai ndio kichocheo cha makiaji ya Biasha na Uchumi wa Dubai.

Hayo ya Muscat, Oman sijui kuna milima au nini sii hoja yangu, bali Dubai walifikiria nini walipojenga Bandari hiyo wakafanya iwe free port na free trade zone kama Singapole, Malaysia na hata UK wanayo! Bandari hizi zimeongeza kwa asilimia kubwa zaidi shughuli za Uzalishaji na Biashara (services).

Naendelea kusema hivi, mipango yote ya maendeleo kujenga Miundombinu lazima kwanza ilenge kukidhi mahitaji ya ndani na ziada kuongeza wimbi la biashara na Uzalishaji nchini.

Changamoto kubwa tulonayo Tanzania bado ni kuendelea kusafirisha MALIGHAFI nje wakati tunaweza kujenga viwanda ndani, tukaongeza thamani ya mbidhaa zetu, ardhi ipo ya kutosha.

Yanisikitisha kusikia kiongozi ninae msikia, anazungumzia DRC, Burundi, Rwanda Uganda kama kwamba tuna Ubia nao!

Hii hainishawishi kabisa kama tuna nia njema na maendeleo ya Tanzania. Bandari, reli na nguvu za Umeme ni kichocheo cha Uchumi wa nchi, focus yetu iwe hapa nyumbani. Bandari na reli zinaweza changia asilia hata ifike 20, lakini kutokana na miundombinu hiyo shughuli za Uchumi nchini zitapanda kiasi kwamba biashara za Kilimo, Uvuvi, Ufugaji, madini na viwanda zitatuletea asilimia zaidi ya 70 kama Dubai. Hapo tutatoka katika Umaskini nasi tutaitwa NCHI YA VIWANDA.

Kama bado hunielewi, sijui niseme nini zaidi. Tanzania kweli ni nchi ya kutegemea Utalii ati ndio tegemeo kubwa la mapato yake? It's shame..
 
Mkuu naona bado unazungumzuia Bandari kama kwamba mimi napinga Ujenzi ama kuwepo kwa Bandari kubwa nchini. Tanzania tunazo 3 kubwa na tunatarajia kujenga nyingine ya Bagamoyo. Ihave no problem with that.

Infact kama unakumbuka miaka ile ya JK 2005 -2010) ni mimi niloweka hapa #Jamiiforums Idea ya ujenzi wa Bandari ya Bagamoyo ili kuachana na Bandari ya Dar es Salaam kutokana na ufinyu wa mkondo wake.

Nikaandika kuwa Bandari ya Dar es Salaaam itumike kwa ajili ya shughuli za mji mkuu wa Biashara. Bandari

Itumike kwa meli za Utalii Cruiser ships, Yatch Clubs na Boat za usafiri wa ndani . Pia zijengwe Hotels, Condo, restaurant, maduka na kadhalika.

Bandari ya Bagamoyo itakayo jengwa muhimu iwe Free Port na Free Trade zone. Laa haiwezekani basi ijengwe Bandari hiyo Zanzibar kwa mpango huo huo, Zanzibar Port iwe free port and free trade zone. Nchi jirani wote waje kufanya shopping zao Tanzania badala ta kwenda China. Sasa mkuu wangu kama hukumbi basi wapo wanaokumbuka! Hiki kichwa kina Idea za kufa mtu.

Labda nifafanue zaidi nachokataa mimi. Ni malengo yanayokusudiwa ni kuhudumia usafiri wa mizigo ya nchi jirani badala ya kuhudumia mizigo yetu sisi – Period. Mtazamo wangu ujenzi wowote wa Miundombinu lazima uhusiane na maonio ama vision ya maendeleo ya Tanzania kwanza.

Umeendelea kutolea mfano wa Dubai, sikatai yote unayosema, lakini Dubai haina nchi jirani zinazohitaji mizogo ipitie hapo. Na ukweli ni kwamba Dubai mchango wa Bandari kwa hizo tozo ni kama asilimia 17, lakini asilimia 70+ ya mapato yake inatokana na biashara za ndani kutokana na Bandari hiyo. Bandari ya Dubai ndio kichocheo cha makiaji ya Biasha na Uchumi wa Dubai.

Hayo ya Muscat, Oman sijui kuna milima au nini sii hoja yangu, bali Dubai walifikiria nini walipojenga Bandari hiyo wakafanya iwe free port na free trade zone kama Singapole, Malaysia na hata UK wanayo! Bandari hizi zimeongeza kwa asilimia kubwa zaidi shughuli za Uzalishaji na Biashara (services).

Naendelea kusema hivi, mipango yote ya maendeleo kujenga Miundombinu lazima kwanza ilenge kukidhi mahitaji ya ndani na ziada kuongeza wimbi la biashara na Uzalishaji nchini.

Changamoto kubwa tulonayo Tanzania bado ni kuendelea kusafirisha MALIGHAFI nje wakati tunaweza kujenga viwanda ndani, tukaongeza thamani ya mbidhaa zetu, ardhi ipo ya kutosha.

Yanisikitisha kusikia kiongozi ninae msikia, anazungumzia DRC, Burundi, Rwanda Uganda kama kwamba tuna Ubia nao!

Hii hainishawishi kabisa kama tuna nia njema na maendeleo ya Tanzania. Bandari, reli na nguvu za Umeme ni kichocheo cha Uchumi wa nchi, focus yetu iwe hapa nyumbani. Bandari na reli zinaweza changia asilia hata ifike 20, lakini kutokana na miundombinu hiyo shughuli za Uchumi nchini zitapanda kiasi kwamba biashara za Kilimo, Uvuvi, Ufugaji, madini na viwanda zitatuletea asilimia zaidi ya 70 kama Dubai. Hapo tutatoka katika Umaskini nasi tutaitwa NCHI YA VIWANDA.

Kama bado hunielewi, sijui niseme nini zaidi. Tanzania kweli ni nchi ya kutegemea Utalii ati ndio tegemeo kubwa la mapato yake? It's shame..
Sio kwamba sikuelewi. Ninakuelewa sana lakini sikubaliani na wewe.
Ningekujibu hoja zako lakini naona tunarudi pale pale. Mengi uliyozungumzia sikubaliani nayo lakini naona tuishie hapa tulipo kwa kukubaliana kutofautiana.

Amandla....
 
Sio kwamba sikuelewi. Ninakuelewa sana lakini sikubaliani na wewe.
Ningekujibu hoja zako lakini naona tunarudi pale pale. Mengi uliyozungumzia sikubaliani nayo lakini naona tuishie hapa tulipo kwa kukubaliana kutofautiana.

Amandla....
Haina shida kwa sababu nimezoea kutokubaliana na wengi hapa JF toka zamani. Mwisho wa siku huyaona yakatokea mkashindwa kunambia japo Mkandara you were right,!

Isitoshe unasema vitu ambavyo mimi sijasema, kwekeza katika viwanda sijasema wawe Watqnzania tu, nilimtolea mfano Dangote huyu sio Mtanzania. Na yaonyesha alikubali mwanzo sasa amechomoa, kwa nini? Sababu zinazotolewa hazina maana kabisa kuna kitu tunakosea aidha masharti ya Mikataba ni migumu ama hali ya Kisiasa inawaogopesha.

Nimalizie kwa kuuliza hivi: - Tuachane na mawazo yangu, chukua yaliyopo kuwa timesafirisha mpaka Kigoma bidhaa za DRC, hilo trani la mizigo litarudi na nini kutoka Kigoma? Ndio yake ya uwanja wa Ndege wa Chato kumpeleka rais karibu na nyumbani, Sawa na kusema ujenzi wa Uwanja ule kwa sababu hiyo, pasipo hesabu ya abiria na mizigo kwenda na kurudi ni hasara ya Uwekezaji. Haina maana napinga Ujenzi wa Kiwanja cha ndege Chato au popote.

Kama hakuna mpango wa kuongeza Uzalishaji wa kilimo na viwanda, treni litarudi tupu, meli nazo zitaondoka bila mizigo kutoka Tanzania kwenda nje. Na ndio uhalisia wa sasa hivi, hatusafirishi mizigo mingi ya meli kuliko inayoingia..

Dubai walijenga Bandari nanUwanja wa ndege tayari wana vision watazotumiaje hizo Bandari na Uwanja wa ndege kuwanufaisha wao Kibiashara, sio hata Abu dhabi wala Sharja! Abu dhabi nao wana mpango wao wa kiuchumi bila kuitegemea Dubai.

Hawa ndugu zetu wa DRC, Burundi, Rwanda tutawasaidia kusafirisha mizigo yao lakini hii isiwe ndio maono yetu Kiuchumi, lazima tujitazame sisi.

Uwekezaji huu mkuwa wa Bandari na Reli ni kwa ajili ya bidhaa zetu kwanza, wao ni top up- extra. Sioni kitu cha ku trade na nchi hizo, pengine ningesema moango huu utafuatana na trade treat ya kuuziana bidhaa fulani - None zero..

Uwe na siku njema, Maasalaam.
 
Kwa hiyo, bado yale mawazo ya Kujenga Bandari na reli kwa ajili ya mizigo ya nchi jirani ni Kosa kubwa sana la Kiuchumi kwetu, kinachotakiwa ni sisi kujenga Bandari na reli kwa ajili ya sisi wenyewe kuwauzia hizo nchi.

Waje Tanzania kununua mali hapa.au sisi tusafirishe bidhaa zetu kwenda kwao. Hii habari ya njia ya kupitia itawafaidisha nchi jirani zaidi kuliko sisi. Na yawezekana sisi ndio tukawa mateja tukaanza kununu bidhaa zao wao.

Narudia kusema, ujenzi wa Bandari, reli na Umeme ulenge kukuza Uzalishaji wa bidhaa za ndani sio kusafirisha mizigo ya nchi nyingine.
Mkandara hapa kuna kitu hajaelewa. Nani amesema bandari ikijengwa itatumika kwa mizigo ya nje tu!
Miundo mbinu ya reli popote inapopita ina faida kwa Jamii. Nani kasema SGR ya kwenda Burundi haiwezi kuchukua dagaa wa kigoma na mawese au Sangara wa Mwanza na Pamba!

Kuna capacity building! Hivi kuna kosa gani bandari ya Kigoma ikijengwa kusafirisha mawese wakati huo huo kupitisha mizigo ya DRC? Hapa tuna lose nini.

Sielewi kwanini unadhani reli na bandari hazina mchango katika trade, manufacturing and industrialization
Bandari ya Dar peke yake imechangia 6.2 % ya GDP mwaka jana. Kwanini una dogosha kiasi hicho

Ku diversify economy ni jambo zuri. Kila kinachoweza kuchangia GDP kifanyiwe kazi. Iwe madini, Utalii, miundo mbinu n.k Uzalishaji hufuata mazingira mazuri ikiwemo usafirishaji.
 
Haina shida kwa sababu nimezoea kutokubaliana na wengi hapa JF toka zamani. Mwisho wa siku huyaona yakatokea mkashindwa kunambia japo Mkandara you were right,!
Nilidhani tumemaliza mjadala kumbe bado. Sio peke yako ambae mara nyingi hakubaliani na wengi. Ni jambo la kawaida.

Hauwezi kuambiwa uko sahihi wakati hauko sahihi. Huo utakuwa unafik. Kwenye huu mjadala uko wrong sana na nitajaribu tena kukuonyesha kwa nini nasema hivyo. Lakini sidhani kama utanielewa kwa sababu hauamini kuwa unaweza kukosea.
Isitoshe unasema vitu ambavyo mimi sijasema, kwekeza katika viwanda sijasema wawe Watqnzania tu, nilimtolea mfano Dangote huyu sio Mtanzania.
Nionyeshe wapi nimesema hivyo?
Na yaonyesha alikubali mwanzo sasa amechomoa, kwa nini? Sababu zinazotolewa hazina maana kabisa kuna kitu tunakosea aidha masharti ya Mikataba ni migumu ama hali ya Kisiasa inawaogopesha.
Dangote ni mfano mzuri wa mapungufu ya hoja yako. Dangote alijenga kiwanda cha simenti kusini kwa kuamini bandari ya Mtwara itaboreshwa kukidhi mahitaji yake na kutakuwa na connection ya uhakika kwenda Malawi. Alitegemea kutumia bandari hiyo sio tu kusafirisha simenti bali kuingiza makaa ya mawe kutoka Afrika ya Kusini ambayo yatatumika katika uzalishaji wa simenti.

Upanuzi wa bandari ya Mtwara una sua sua hivyo kumfanya kutegemea zaidi malori ambayo pamoja na kuongeza gharama ya usafirishaji lakini pia hali ya barabara inaleta changamoto. Hapo bado hujaweka ajali na udokozi. Ndio maana mpaka sasa hivi kiwanda hakijapanuliwa.

Serikali pia ilimlazimisha atumie makaa ya mawe yanayochimbwa ndani ya nchi ambayo quality yake sio nzuri na uzalishaji wake haukidhi mahitaji ya kiwanda chake.

Yote haya yanaonekana wazi kwa sababu sio tu kiwanda cha Dangote hakijapanuliwa bali hamna kiwanda kingine cha maana kilichojengwa Mtwara na Lindi.

Dangote ameamua kujenga refinery Kenya kwa sababu za kibiashara na sio siasa:
1. Kenya imewekeza sana katika bandari za Lamu na Mombasa hivyo itarahisisha kusafirisha mazao ya mafuta kwenda nchi nyingine kama Ethiopia, South Sudan, n.k.
2. Kenya ina mradi mkubwa wa kujenga bomba la mafuta kutoka South Sudan. South Sudan tayari inazalisha mafuta na inataka kuwa na bandari mbadala wa inazotumia sasa hivi.
3. Kenya ina mafuta yake yenyewe katika jimbo la Turkana.
4. Soko la Kenya ni kubwa kuliko la Tanzania. Na wako karibu sana na Ethiopia na South Sudan, nchi ambazo uchumi wao unakuwa kwa kasi sana.
5. Kenya ina mazingira bora zaidi ya kibiashara. Ni vigumu sana wao kukiuka mikataba na wanasiasa kuwaingilia wafanya biashara. Masharti ya mkataba sio tatizo. Tatizo ni utayari wa kuyatekeleza na haki ya mwekezaji pale ambapo yanakiukwa.
Nimalizie kwa kuuliza hivi: - Tuachane na mawazo yangu, chukua yaliyopo kuwa timesafirisha mpaka Kigoma bidhaa za DRC, hilo trani la mizigo litarudi na nini kutoka Kigoma?
Reli hiyo haitasafirisha tu mizigo ya kwenda DRC peke yake. Itasafirisha pia mizigo kwenda Burundi na ya Kigoma. DRC wanachimba madini mengi sana ambayo yahitaji kusafirishwa kwenda nchi za nje. DRC wana mazao mengi ya porini yenye soko nje ya DRC. Aidha, usafiri wa uhakika utafungua soko la Kigoma na Mpanda. Wakulima na wavuvi wa huko watafaidika. Viwanda vya ku process mazao ya ziwani vitafunguliwa. Na mazao hayo yatauzwa Tanzania na nchi za jirani. Yote haya yatawezekana usafiri wa reli utakapo boreshwa. Uwepo wa bandari ya kuaminika itapanua soko la bidhaa za Kigoma, DRC, Burundi, Tabora kwenda sio tu Ulaya na Asia bali pia nchi kama Comoro na Seychelles. Bila reli na bandari za kiwango cha juu hayatawezekana.
Ndio yake ya uwanja wa Ndege wa Chato kumpeleka rais karibu na nyumbani, Sawa na kusema ujenzi wa Uwanja ule kwa sababu hiyo, pasipo hesabu ya abiria na mizigo kwenda na kurudi ni hasara ya Uwekezaji. Haina maana napinga Ujenzi wa Kiwanja cha ndege Chato au popote.
Una fananisha machungwa na apple. Uwanja huo wa ndege ulijengwa kisiasa. Ni bidhaa chache sana za kiwandani husafirishwa kwa ndege. Ndio maana huu mjadala una husu bandari, sio kiwanja cha ndege. Tofauti na wewe, mimi napinga ujenzi wa kiwanja cha ndege Chato na kwingine kinachojengwa kwa sababu za kisiasa, sio za kiuchumi. Naona una uma na kupuliza.
Kama hakuna mpango wa kuongeza Uzalishaji wa kilimo na viwanda, treni litarudi tupu, meli nazo zitaondoka bila mizigo kutoka Tanzania kwenda nje. Na ndio uhalisia wa sasa hivi, hatusafirishi mizigo mingi ya meli kuliko inayoingia..
Uwepo wa treni utachochea watu kuwekeza kwenye kilimo na ufunguzi wa viwanda. Ni sehemu muhimu ya kuongeza uzalishaji wa kilimo na viwanda. Usafirishaji ukiwa hauamini, wazalishaji watakata tamaa mapema kwa kukosa soko la bidhaa zao. Kitu kinachowarudisha nyuma wakulima wetu ni kukosekana kwa soko. Soko likiwa la uhakika uwekezaji utakuwepo. Reli na bandari zitahakikisha uwepo wa soko la bidhaa.
Dubai walijenga Bandari nanUwanja wa ndege tayari wana vision watazotumiaje hizo Bandari na Uwanja wa ndege kuwanufaisha wao Kibiashara, sio hata Abu dhabi wala Sharja! Abu dhabi nao wana mpango wao wa kiuchumi bila kuitegemea Dubai.
Dubai wana vision ya kuwa kiungo kikubwa cha biashara duniani ili nchi yao ifaidike. Hata Tanzania tunapowekeza kwenye bandari lengo sio kuzifaidisha DRC na Rwanda. Lengo ni ku take advantage udhaifu wa nchi hizo kwa faida ya watanzania. Ada inayotozwa na Dubai kwa wale wote wanaopitisha bidhaa zao katika bandari zao, inachangia kwa kiasi kikubwa maendeleo ya Dubai. Ni dhari kuwa Abu Dhabi na nchi nyingine za jirani nazo zina mipango yake. Ndivyo inavyo paswa kuwa. Sisi vile vile tunapaswa kujipanga dhidi ya ushindani kutoka bandari za Kenya, Msumbiji, Afrika ya Kusini na hata Angola. Na tujiweke katika nafasi ya wawekezaji kutaka kuwekeza Tanzania kuliko nchi jirani.
Hawa ndugu zetu wa DRC, Burundi, Rwanda tutawasaidia kusafirisha mizigo yao lakini hii isiwe ndio maono yetu Kiuchumi, lazima tujitazame sisi.
Hatuwasaidii. Hawasafirishi bure. Wanalipa ada ambayo itatumika nchini mwetu. Tunajitazama kwa kujua kuwa kufanya hivyo, kutatufaidisha sote. Hata sisi tutatumia reli hizo kusafirisha bidhaa zetu kwenda DRC, Burundi na Rwanda. Uwepo wa reli utaturahisisha sisi kuagiza magari yanayoundwa Rwanda kwa bei nafuu. Sote tunafaidika, hamna anayemsaidia mwenzake.
Uwekezaji huu mkuwa wa Bandari na Reli ni kwa ajili ya bidhaa zetu kwanza, wao ni top up- extra. Sioni kitu cha ku trade na nchi hizo, pengine ningesema moango huu utafuatana na trade treat ya kuuziana bidhaa fulani - None zero..
Kama hauoni faida ya kufanya biashara na Rwanda, Burundi na DRC basi tatizo ni kubwa kuliko nilivyo dhani. Trade treaty kati ya nchi hizi ya nini wakati nchi zote hizo ni sehemu ya EAC? Matamshi kama haya ndio yaliyofanya nikuage maana hatuongei lugha moja.

Amandla...
Uwe na siku njema, Maasalaam.
 
Back
Top Bottom