Interview ya kwenye skype ni balaa!!!

Boutafrica

JF-Expert Member
Dec 11, 2014
953
2,070
Wakuu nina kifahamu kiingereza vizuri tu japo si sana ila nina matatizo kidogo kwenye hii lugha ,matatizo yenyewe ni haya:

(1)Juzi kati nilibahatika kufanya interview katika kampuni flani hivi ya kigeni,ila interview ile iliendeshwa kwa njia ya skype,yaani me nipo dar nimekaa meza moja na watu wawili (interviwers)na wa tatu ni yule mzungu wa kwenye skype.Muuliza maswali mkuu alikuwa ni yule mzungu wa kwenye skype ambaye alikuwa anaongea kutoka denmark,sasa ilikuwa mimi ni lazima nicontact direct kwenye skype,sasa kitu ambacho kilikuwa kinanipa shida ni yule mzungu matamshi yake,yaani kusema ule ukweli nilikuwa siyapati/simuelewi kabisa matamshi yake yani alikuwa anaongea kama "kajaza mlenda kooni" ilikuwa kila akiniuliza swali lazima niwageukie wale wabongo wenzangu ambao nao pia ni interviwers wanifafanulie kilichoulizwa kule kisha ndiyo natoa jibu.Nashuru Mungu nilimaliza vizuri interview ile na nimebakisha hatua chache kupata hiyo kazi,ila changamoto niliyoipata ndiyo hiyo.

(2)Kila nikiongea na mzungu yeyote yule tukiwa face to face huwa naelewa vizuri sana kila anachokitamka ila huwa napata shida sana kumuelewa mzungu akiongea akiwa kwenye tv au radio hasa ninapokuwa najaribu kufuatilia international news kwenye bbc,aljazeera au kwenye movies nk...,yaani napata maneno machache sana ,sesntence yake moja naweza kukakamata neno la mwanzo na la mwisho.Lakini cha ajabu mwarabu,muhindi au muafrica akiongea kwenye tv yan hata nisipomuangalia nisikie tu hata sauti huwa namuelewa vizuri sana,shida ni hawa akina Trump na wenzie hawa....
Sasa tatizo ni nini na nifanye nini ili kumaster hii lugha kwenye mazingira ya aina zote?
 
Kila nikiongea na mzungu yeyote yule tukiwa face to face huwa naelewa vizuri sana kila anachokitamka ila huwa napata shida sana kumuelewa mzungu akiongea akiwa kwenye tv au radio,yaani napata maneno machache sana ,sesntence yake moja naweza kukakamata neno la mwanzo na la mwisho.
Aiseee!!!
 
Hata mimi nilipata changamoto na profesa wa kiingereza ilinichukua siku nzima accent yao kwa kweli ngumu bora wazungu wa mataifa mengine hasa wamarekani
 
Mkuu, wewe wahi tu kwa Rasi Lion.
Hiyo ndiyo suluhisho tu bila hivyo itafikia wakati hadi face to face itakuwa ni mbinde kunasa signal.

Pardon , repeat please zitakuwa nyingi sana.

Yule waziri wa mambo ya mbali wa awamu ile ya katikati aliulizwa ivyo hivyo maswali na mtangazaji wa BBC yule waziri akawa anajibu kwa kubet swali na majibu sasa matokeo yake tuliyaona wenyewe kwenye ngazi ya nchi.

Kwa hiyo, mkuu wahi tu English language course kwa Rasi Lions a k.a Simba hapo Dar utapona ugonjwa wako siyo wa kufa.
 
Asilimia kubwa ya watu ambao English ni first language hawazungumzi kiingereza fasaha, huzungumza kwa kuendana na lahaja ya mahala alipo kulia. Huzungumza kwa lafudhi ngumu sana kwa aliyejifunza kiingereza darasani kumwelewa.
 
ndo mana siwezagi kuangalia MOVIE bila subtitle hata iwe nzuri kiasi gani bila SUBTITLE asilani abadani siwezi kuangalia coz siwaelewi wanachozungumza
mkuu hilo tatizo si wewe tu tupo wengi tu
 
Asilimia kubwa ya watu ambao English ni first language hawazungumzi kiingereza fasaha, huzungumza kwa kuendana na lahaja ya mahala alipo kulia. Huzungumza kwa lafudhi ngumu sana kwa aliyejifunza kiingereza darasani kumwelewa.
Mkuu upo sahihi kabisa,yaani mimi ikitokea muhindi au mwarabu anaongea kiingereza kwenye tv au radio huwa namuelewa maneno/matamshi yake yote ila kwa mzungu huwa siambui chochote,yaani nampata kwa shida sana.
 
Nilikuwa na tatizo kama lako. Kuna mzungu mmoja akanishauri niwe naangalia sana series za kizungu, na kuangalia videos za kizungu hii ilinisaidia kuzoea matamshi yao
kweli kabisa naunga mkono hoja yako ingawa mm bila subtitle huwa ni shida ila zimenisaidia sana kuimprove usikivu wa maneno kutokana na kuzoea vijitamshi vyao
 
hiyo imetokea kwa sababu wewe unajiita no signal, kwa hiyo lazima kwenye electronic device hupati signal
 
Huo ni ugonjwa wa wengi apa Tanzania, ata na wengineo ...
Huo si ugonjwa na wala si tatizo kwa mtanzania asili, bali ni sahihi kwani si lugha yetu na ni lugha ya kujifunza tu, nadhan huyu mleta mada anapaswa kujitahidi kwa kusikiliza kwa umakini, kuangalia mdomo wa mzunguzaji na kufuatilia series za kizungu pia kusoma makala mbalimbali za kiingereza na kufanya mazoez ya kuongea lugha hiyo mara kwa mara inaweza kusaidia.
 
Wazungu wengi ambao sio waingereza/wamarekani kiingereza chao sio kizuri kabisa na wana accent nzito kama haujazoea unaweza usielewe. Hata wamarekani wengine wako ovyo sana kwenye english na accents zisizoeleweka hasa southern USA. So usijilaumu sana.
 
Huo si ugonjwa na wala si tatizo kwa mtanzania asili, bali ni sahihi kwani si lugha yetu na ni lugha ya kujifunza tu, nadhan huyu mleta mada anapaswa kujitahidi kwa kusikiliza kwa umakini, kuangalia mdomo wa mzunguzaji na kufuatilia series za kizungu pia kusoma makala mbalimbali za kiingereza na kufanya mazoez ya kuongea lugha hiyo mara kwa mara inaweza kusaidia.
Iyo option uliyotoa ndio ugonjwa mkubwa kabisa kwa watanzania.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom