Natafuta Ajira
JF-Expert Member
- Mar 25, 2020
- 4,425
- 9,823
Nina shida ya kusikia vizuri. Nilianza kuona effects za tatizo nikiwa form 3. Nimejitahiri kusaka matibabu mara kadha, mara ya mwisho kwenda hospital pale CCBRT niliambiwa ngoma ipo fresh shida ipo kwenye nerves hazina muunganiko mzuri na ubongo. Kwa sasa hakuna matibabu hata oparesheni haiwezi ikasaidia. Dokta aliniambia kuna hearing device naweza kutumia ila inawezekana zisisaidie pia na kuna uwezekano wa kuongeza ukubwa wa tatizo ikapelekea kuwa kiziwi kabisa. Nikaona acha tu nijikubali ivyo ivyo sijawahi kusaka tena matibabu kuanzia hapo.
Nikiongea na mtu face to face tunaweza tukaelewana ingawa sometimes inakua kwa ugumu kidogo kama tupo sehemu yenye makelele, ninaeongea nae akiwa na kigugumizi au akiongea kwa sauti ya chini sana tatizo kubwa kuongea na mtu kwenye simu ndio simuelewi kabisa. Sauti naisikia ila haiji kimpangilio kuweza kujua mwenzangu anaongea nini.
Nakumbana na changamoto nyingi sana. Sana sana kwenye suala la zima la mishe za kujitafutia kipato. Kwenye oral interview sometimes kusikia shida, mishe ambazo zinahitaji kuwasiliana na watu mara kwa mara mfano udalali siwezi kufanya kabisa hata kwenye CV imenilazimu kuandika namba ya ndugu maana nikiweka namba yangu naweza kupigiwa na muajiri nisimsikie vizuri. Mawasiliano yangu ni kwa njia ya sms tu.
Nahitaji kujua kama kuna hearphone ninazoweza kutumia kutatuta changamoto ya kuwasiliana na mtu kwenye simu. Na pia kwenye mishe za kujitafutia nitilie mkazo kwenye career ipi ambayo tatizo langu halitakua kikwazo.
Nikiongea na mtu face to face tunaweza tukaelewana ingawa sometimes inakua kwa ugumu kidogo kama tupo sehemu yenye makelele, ninaeongea nae akiwa na kigugumizi au akiongea kwa sauti ya chini sana tatizo kubwa kuongea na mtu kwenye simu ndio simuelewi kabisa. Sauti naisikia ila haiji kimpangilio kuweza kujua mwenzangu anaongea nini.
Nakumbana na changamoto nyingi sana. Sana sana kwenye suala la zima la mishe za kujitafutia kipato. Kwenye oral interview sometimes kusikia shida, mishe ambazo zinahitaji kuwasiliana na watu mara kwa mara mfano udalali siwezi kufanya kabisa hata kwenye CV imenilazimu kuandika namba ya ndugu maana nikiweka namba yangu naweza kupigiwa na muajiri nisimsikie vizuri. Mawasiliano yangu ni kwa njia ya sms tu.
Nahitaji kujua kama kuna hearphone ninazoweza kutumia kutatuta changamoto ya kuwasiliana na mtu kwenye simu. Na pia kwenye mishe za kujitafutia nitilie mkazo kwenye career ipi ambayo tatizo langu halitakua kikwazo.