Ingependeza kila ukanda ugekuwa na chuo kikuu cha serikali, mgawanyo wa vyuo vikuu bado ni kikwazo kwa baadhi ya kanda

Ingependeza kila ukanda ugekuwa na chuo kikuu cha serikali, mgawanyo wa vyuo vikuu bado ni kikwazo kwa baadhi ya kanda

mkata uzi

JF-Expert Member
Joined
Aug 3, 2025
Posts
1,910
Reaction score
5,451
Naomba tuelewane ni chuo kikuu kilichojitosheleza chenye vitivo mbali mbali vya Uhandisi, Sheria, Ualimu, Biashara, Udaktari, n.k.

Sio kampasi ya chuo kikuu au institute au college ambayo inatoa fani chache.

Kila ukanda sikuhizi una toa wahitimu wengi sana wa form 4 na form 6, ni haki yao kufikiwa na huduma ya kijamii ya vyuo kwa urahisi.

1. Ukanda wa Kaskazini - MUCO

Arusha
Kilimanjaro
Manyara

2. Ukanda wa Ziwa - HAKUNA

Mwanza
Mara
Kagera
Geita
Simiyu

3. Ukanda wa Mashariki - MZUMBE, UDSM, SUA, n.k.

Dar es Salaam
Pwani (Coast)
Morogoro
Tanga

4. Ukanda wa Kati - UDOM

Dodoma
Singida
Shinyanga

5. Ukanda wa Kusini - HAKUNA

Lindi
Mtwara
Ruvuma

6. Ukanda wa Nyanda za Juu Kusini - MUST

Mbeya
Songwe
Njombe
Iringa
Rukwa

7. Ukanda wa Magharibi - Hakuna

Tabora
Kigoma
Katavi
 
1. Ukanda wa Kaskazini

Arusha
Kilimanjaro
Manyara

2. Ukanda wa Ziwa

Mwanza
Mara
Kagera
Geita
Simiyu

3. Ukanda wa Mashariki

Dar es Salaam
Pwani (Coast)
Morogoro

Tanga

4. Ukanda wa Kati

Dodoma
Singida
Shinyanga

5. Ukanda wa Kusini

Lindi
Mtwara
Ruvuma

6. Ukanda wa Nyanda za Juu Kusini

Mbeya
Songwe
Njombe
Iringa
Rukwa

7. Ukanda wa Magharibi

Tabora
Kigoma
Katavi
Hizo university Kwa sasa zinatosha tunahitaji vyuo vingi vya ufundi ili kuweze kunusuru wimbi kubwa la vijana wasio na ajira
 
Hizo university Kwa sasa zinatosha tunahitaji vyuo vingi vya ufundi ili kuweze kunusuru wimbi kubwa la vijana wasio na ajira
Nani kakwambia zinatosha, hivi unajua kuna watu wanatumia zaidi ya laki 3 kwa usafiri tu kila mwaka kwasababu hakuna vyuo vikuu mikoa yao wala mikoa ya karibu ?

Unajua kuna vijana wangapi waliokatisha ndoto zao za kusoma vyuo kwa kukosekana vyuo vikuu ndani ya mikoa yao au mikoa ya karibu ?
 
Baada ya hapo wanakwenda wapi? Wanafanya Nini? Hizi universe degree zetu zimetosha tunahitaji technical zaidi mkuu kuweza kuwakomboa vijana, yaani hadi wapakistan wanatushinda!
Nani kakwambia zinatosha, hivi unajua kuna watu wanatumia zaidi ya laki 3 kwa usafiri tu kila mwaka kwasababu hakuna vyuo vikuu mikoa yao waka kanda zilizopo ?
 
Baada ya hapo wanakwenda wapi? Wanafanya Nini? Hizi universe degree zetu zimetosha tunahitaji technical zaidi mkuu kuweza kuwakomboa vijana, yaani hadi wapakistan wanatushinda!
Engineers, Lecturers, Doctors, Wahasibu, Majaji, n.k. kila mwaka wanahitajika kujaza nafasi za wastaafu na wengine hujiajiri, hizi ni kazi za kusomea vyuoni sio Veta. kama mtu ana aspirations za kuwa Lawyer aweze kupata access ya chuo ndani ya mkoa au ndani ya ukanda,
 
Jalalani Lindi campus
Screenshot_20260106-235953_Instagram.jpg
 
Engineers, Lecturers, Doctors, Wahasibu, Majaji, n.k. kila mwaka wanahitajika kujaza nafasi za wastaafu na wengine hujiajiri, hizi ni kazi za kusomea vyuoni sio Veta. kama mtu ana aspirations za kuwa Lawyer aweze kupata access ya chuo ndani ya mkoa au ndani ya ukanda,
Quantity tunawaitaji lakini sio Kwa wingi tunaotaka kuwazalisha, ndio mwisho wa siku wawe bodaboda
 
me naona kila mkoa ungekuwa na chuo chake maan vijan ni weng wanaochipukia, sasa kwakuw vyuo ndo hivyo vichache inabidi kwenye matokeo hasa advance watu kurimwa(kufelishwa)ili waende wachache kulingan na vyuo tulivonavyo
 
Quantity tunawaitaji lakini sio Kwa wingi tunaotaka kuwazalisha, ndio mwisho wa siku wawe bodaboda
Quantity inaweza kuwa controlled, lakini chuo kikuu ni huduma ya kijamii inayopaswa kuwafikia watu kirahisi kwa usawa
 
me naona kila mkoa ungekuwa na chuo chake maan vijan ni weng wanaochipukia, sasa kwakuw vyuo ndo hivyo vichache inabidi kwenye matokeo hasa advance watu kurimwa(kufelishwa)ili waende wachache kulingan na vyuo tulivonavyo
Tatizo ni kwamba hakuna usawa, kuna maeneo yanajengwa sana vyuo lakini kwengine utadhani sio sehemu ya nchi

Na vyuo ni huduma ya kijamii sio biashara,
 
Mkuu neno usawa liondoe kwenye kamusi Yako hakutakuwa na usawa mpaka Dunia itakaporudi kwenye default version yake
Quantity inaweza kuwa controlled, lakini chuo kikuu ni huduma ya kijamii inayopaswa kuwafikia watu kirahisi kwa usawa
 
Hizo university Kwa sasa zinatosha tunahitaji vyuo vingi vya ufundi ili kuweze kunusuru wimbi kubwa la vijana wasio na ajira
Vyuo vikuu vinazalisha wavaa suti jua Kali tu,wanachoweza kubishana wakichanganya lugha
 
Musoma Kuna chuo kikuu chq kilimo, ambacho wanajenga kampasi pale tabora

Vile vile Kuna kampasi kama sio chuo kamili kinajengwa kule buhigwe kigoma.

Vile vile Kuna kampasi nyingi za vyuo mkoa wa mwanza
1. CBE
2. DIT
3. TIA
4. ARU wapo Sengerema
5. Chuo cha Mipango kina kozi zote zinazotolewa na kampasi kuu Dodoma
6. LGTI Wana tawi Shinyanga
7. Chuo cha Ushirika kina tawi shinyanga
8. Mzimbe Wana matawi mbeya. Dsm, Tanga wanaendelea na ujenzi
9. Must Wana kampasi mtwara
10. Udsm Wana kampasi unguja
11. Chuo cha kumbukumbu ya mwalimu nyerere Wana kampasi unguja na pemba
12. Udom Wana kampasi kati ya iringa au njombe
13. Tia au IAA (chuo cha uhasibu arusha Wana kampasi babati
14. TIA Wana kampasi pia singida, mtwara, mbeya, singida nk
15. Chuo kikuu huria kina kampasi mikoa yote ya Tanzania kwa kozi zote zinazotolewa kampasi kuu dsm.

Kagera Kuna kampasi ya UDSM

Rukwa Kuna kampasi ya MUST na Chuo kingine kama sikosei.

Kilimanjaro Kuna kampasi ya Chuo cha kumbukumbu ya mwalimu nyerere

Hizo ni taarifa baadhi

Veta ni kila wilaya, sio tena kila mkoa.... tunapoelekea ni kila tarafa na baadae kila kata na kijiji
 
Vyuo napo vikiwa vingi thaman ya elimu inapotea. Inakua kama shule za kata hivi.
 
Vyuo vikuu vinazalisha wavaa suti jua Kali tu,wanachoweza kubishana wakichanganya lugha
Mtoa mada hajui kuwa tuna graduate wengi ambao mchango wao ni mdogo sana tofauti na elimu zao na wengine wamepata matatizo ya afya ya akili sababu ya elimu zao
 
Back
Top Bottom