mbandeon
JF-Expert Member
- Aug 27, 2014
- 1,540
- 639
Magufuli na CCM yake ndio wamepewa ridhaa na dhamana ya kukusanya kodi na kusimamia rasili mali zetu wewe kapuku panya mpunga kauze chai huna unalojua zaidi ya kutujazidia server zetu hapa JF.Turufu kubwa inayotumiwa na wanaCCM, ili Rais Magufuli apewe tena miaka mingine 5 ya kutawala nchi hii, ni kuwa Rais huyo amejenga reli ya SGR, amejenga mafly overs, amejenga mabarabara ya lami, anajenga bwawa la umeme katika mto wa Rufiji
Nimekuwa nikijiuliza ni kwanini juhudi zinazofanywa na watanzania wote, bila kujali itikadi zetu za kisiasa, sifa zote achukue mtu mmoja, ambaye ni Mwenyekiti wa CCM, ambaye pia ndiye Rais wetu Magufuli?
Kwa kuwa siyo siri tena, kuwa turufu kubwa wanayotumia wanaccm kuelekea uchaguzi mkuu mwishoni mwa mwaka huu, ni ujenzi wa miundo mbinu mbalimbali inayoendelea nchini, utadhani kuwa pesa ya kugharimia miundo mbinu hiyo, anatoa toka mifukoni mwake, yeye Rais Magufuli!
Hata serikali ya makaburu wa Afrika Kusini, walijenga miundo mbinu ambayo ndiyo inayongoza kwa ubora wake humu barani Afrika. Hata hivyo wananchi wa nchi hiyo, waliamua kumchagua mzalendo mweusi, Shujaa Nelson Mandela kuwa Rais wao na kuwapiga chini makaburu weupe ambao ndiyo waliokuwa wakijidai kuwa miundo mbinu hiyo imejengwa na wao.
Vile vile inajulikana kuwa pesa yote ya walipa kodi wa nchi hii, ya wanaccm na wanaChadema, zinakusanywa kwa pamoja na kuwekwa kwenye Hazina ya Taifa na ndiyo hizo zinazojenga, hiyo miundo mbinu, ambayo wanaccm "wanajimwambafai" kuwa wamejenga wao!
Wakati tunaelekea kwenye uchaguzi mkuu mwishoni mwa mwaka huu ni lazima watanzania tusikubali kulaghaiwa kwa hizo propaganda nyepesi kuwa eti miundo mbinu yote nchi hii imejengwa na wanaccm!
Hebu tusikilize sera za kila mgombea na wananchi tuchague kiongozi ambaye tunaamini ndiye atakayetuvusha kama Taifa, katika umoja wetu na kudumisha utulivu wa nchi hii.
Tusichague kiongozi ambaye tunamuona dhahiri kuwa analibomoa kwa kasi kubwa Taifa hili umoja wetu na kuleta chuki ndani ya jamii ya watanzania.
Mungu ibariki Tanzania.