Inawezekana Polisi hawahusiki na utekaji!

Inawezekana Polisi hawahusiki na utekaji!

GoldDhahabu

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2023
Posts
7,648
Reaction score
10,843
Baada ya kuunganisha nukta, nimepata jibu kuwa huenda Polisi hawahusiki na utekaji nchini
1. Hawahusiki kuteka lakini wanajua utekaji upo!

2. Wanajua mtoa maagizo ya utekaji hivyo hawawezi kuingilia!

3. Wengine wanaumia kwa yanayoendelea lakini hawana la kufanya isipokuwa kuwatii wakubwa!
 
Ni jukumu la Polisi Kulinda Raia na mali zao.
Kama watu wanatekwa kama kuku bila polisi kujua na kuchukua hatua, basi jeshi hilo limeshindwa kazi lifutwe liundwe jingine
 
Baada ya kuunganisha nukta, nimepata jibu kuwa huenda Polisi hawahusiki na utekaji nchini
1. Hawahusiki kuteka lakini wanajua utekaji upo!

2. Wanajua mtoa maagizo ya utekaji hivyo hawawezi kuingilia!

3. Wengine wanaumia kwa yanayoendelea lakini hawana la kufanya isipokuwa kuwatii wakubwa!
Mafwele siyo polisi?

Pia kina Mdude na Sativa si waliwekwa kwenye selo maalum ambazo zipo kwenye vituo vya polisi?

Kwenye ile kesi Mbowe aliyopewa ya ugaidi, wale wanajeshi ambao walikuwa walinzi wa Mbowe, walielezea kupitishwa kwenye vituo vya polisi na kuteswa. Walielezea walivyokuwa wanapigwa haswa kwenye miguu…

Kama Mkenya ambaye naye alikamatwa, ambapo alipigwa sana kwenye nyayo za miguu nk.

Hizo kauli za kutaka kuwasafisha polisi ni mkakati maalum tu. Kama uwajibishwaji ukifanyika, hawana njia wala utetezi hautawasaidia mbele ya ushahidi wa wazi kabisa dhidi yao.

Tena kuna ambao wako on record wakisema wazi kuwa wao ni kijani.
 
Baada ya kuunganisha nukta, nimepata jibu kuwa huenda Polisi hawahusiki na utekaji nchini
1. Hawahusiki kuteka lakini wanajua utekaji upo!

2. Wanajua mtoa maagizo ya utekaji hivyo hawawezi kuingilia!

3. Wengine wanaumia kwa yanayoendelea lakini hawana la kufanya isipokuwa kuwatii wakubwa!
Kifupi ni kwamba polisi kama jeshi hawahusiki na utekaji na ndiyo maan amara zote wanatoa taarifa zinazokinzana... Ila Wapo maafisa wa polisi waliojumuishwa kwenye kikosi kazi cha kuteka, kutesa na kuua!
Lakini... jambo moja ninaloliamini... Watateka, kutesa na kuua wengi mwisho wa siku watawageukia waliokuwa wanawatuma!
Yaendayo, yanarudi!
 
Polisi wanahusika na USHAHIDI ni huu hapa.


Vg47I7HR9FK68INB.jpg

mdude.jpg

soka-e1724250077267-1024x968.jpg
 
Back
Top Bottom