Ukinisoma vizuri sibishi kuwa Muhimbili ina matatizo
na mengine ya mda mrefu
mimi ninachopinga ni watu waliotuambia sasa Muhimbili mambo safi
baada ya ziara ya kwanza ya Magufuli...na vile vitanda vilivyo changishwa wabunge....
napinga hii hali kuonekana mpya wakati hii hali ipo kila siku
kwa kweli watu watano na watoto wanalalaje hizi ni chumvi tuuHii habari ni kweli AU mna pass time????
Je kungekuwa hakuna mgonjwa mashuhuri wa kwenda kumjulia hali hapo hospital pangeendelea kubaki hivyohivyo bila kumulikwa?
Mkuu uliona habari vema ama unakurupuka tu. Nafasi ilikuwa ya kutosha sana ila vitanda havikuwepo vya kutosha na hoja yao haikuwa kuongenzwa kwa jengo bali upungufu wa vijana.Vitanda siyo tatizo tena hilo lilishatatuliwa na viko vya kutosha tu ila tatizo ni nafasi utaviweka wapi?
Sehemu kubwa ya Wagonjwa wanaokuja Muhimbili hawakupaswa hata kuja Muhimbili bali kwa hali ya kawaida walipaswa waende kwenye Hospitali zao za Wilaya kama M'mala, Amana, Temeke na zinginezo lkn hizi zote zimetelekezwa kwa miaka mingi sasa huwezi kutegemea miujiza leo hii, hii sekta ya Afya ina changamoto kubwa sana na ndiyo wengine tunapinga kutumia fedha nyingi kujenga daraja la Kigamboni ambao halina umuhimu mkubwa kwa wakazi wa Dar badala hizi fedha zingeelekezwa kwenye mambo ya jamii kama Afya nina Imani Kigamboni wangepata Hospitali ya hadhi ya Amana, Tegeta wangepata, Tabata wangepata hii ingesaidia sana lkn Watz wenyewe wanataka Daraja Kigamboni wakapige picha!
Mkuu uliona habari vema ama unakurupuka tu. Nafasi ilikuwa ya kutosha sana ila vitanda havikuwepo vya kutosha na hoja yao haikuwa kuongenzwa kwa jengo bali upungufu wa vijana.
Ha haaa km watu wanaomsifia magufuli ni wa aina yako,nna uhakika tumepoteza tena fursa ya kuwa na kiongozi bora kwa miaka mingine 5. Yaani hata picha za jana unapingana nazo?? Yaani nyie mkwere ndiyo aliwaombea mfikiriwe??Wewe hauna akili kwanza hiyo picha ni ya lini? Hiyo picha ni kabla ya Utawala wa Raisi Magufuli, sasa nakupa changamoto kapige picha kama hiyo kwenye Hospitali hapa Dar halafu ulete tena!
Fahamu kuwa vitanda katika hospitali zetu sio vya kulalia kama tunavyofanya sehemu nyingine, bali ni kujipumzisha au kukalia na mgonjwa akichoka analala chini.Nimeona Azam two tv Magufuli mwenyewe kauliza kwa mshangao watu watano?
wakamjibu ndio
Mimi kwa kweli sijawahi kuona serikali au viongozi wetu wanatatua tatizo likaisha sijui tatizo ni nini. Hata vitu vidogo vinawashinda uchafu tu unawashinda kusimamia.watajifanya wakali na vifaini siku mbili tatu uchafu upo palepale hakuna anayejali nao wanapita kila siku na wanaona.ukienda kwenye elimu shida watoto bado wana kaa chini hadi leo kuna shule za serikali mikoani hazina hata paa. Ukija ktk afya matatizo ni yale yale maisha yote.foleni maji ujambazi ufisadi hakuna kitu tunaweza kusema jamani hiki serikali imebadilisha na si tatizo tena.
Sasa ni nini kila kitu hawajawahi kuweza.
Matatizo katika sekta ya afya hayataisha kwa "ziara za kushtukiza" na maagizo au matamko ya wanasiasa hata siku moja!! Kama kweli tunataka mabadiliko yenye tija na ya kudumu katika hii sekta, kuna vitu vingi sana tunatakiwa kufanya!!
Haya mambo ya maagizo na ziara za ghafla zita achieve only a partial and superficial effect. Na muhimbili specifically, matatizo yake ni deep-seated. Tatizo sasa hivi ukiongea katika muktadha huo unaonekana mchawi tuu, kila mtu yuko "super-excited"The Boss
Labda mambo safi kwa kutegemea hali ilivyokuwa awali. Mimi ninaamini kuwa matatizo ya Muhimbili hayawezi kutatuliwa 'overnight', ni juhudi shirikishi zinahitajika kutoka kila pembe. Waandishi/media wawe wanajiongeza kwa kurudi eneo la tukio kutupa habari za yanayojiri bila kuongozana na hao viongozi.
Unacheza na maneno. Hayo uliyoandika ni sawa na kuwaambia matatizo yametatuliwa. Ukisoma taarifa zinazotolewa mwelekeo ni huo wa kuwaaminisha hivyo. Soma uhuru na habarileo la leo utaona ilivyoripotiwa ziara ya Mh Rais jana wodi ya wazazi utajua ninalolisema.Ni nani amewaambia wananchi kwamba matatizo yametauliwa? Sijawahi kusikia mahali popote tangu Raisi magufuli aingie madarakani akisema kwamba matatizo ya Muhimbili au afya yametatuliwa hilo nalisikia kwako, nilichosikia ni kwamba hali imeboreshwa kulinganisha na ilivyokuwa hapo mwanzo kama ununuzi wa vitanda, mashine na upatikanaji wa dawa ktk MSD, lkn siyo kutatuliwa hilo sijawahi kulisikia!