Inatosha - Lowassa Jiuzulu!

Lakini hapa kuna mtego ambao Mkakati wa kina Lowassa utakwama. Kama mnakumbuka Mwakyembe alitoa wito kwa "mtu yeyote" mwenye maelezo kuhusu Richmond ajitokeze na kuonana na Kamati. Kwenye ripoti hiyo anasema hakuna mtu aliyejitokeza kwa hiari yake (hapa anawabana kina Karamagi, et al).


HIvyo wakija na "hatukupewa nafasi ya kusikilizwa" Mwakyemba atawaambia.. "tarehe... nilizungumza na vyombo vya habari na kutoa wito kwa "mtu yeyote"... hapo ndipo watakapojua kuwa mtego umetegwa aidha watautegua, ama watanaswa!

Nadhani ushauri huu uuende Dodoma mara moja!!!
 
Hii hadithi ya kutokupewa nafasi ya kujitetea ni kinyesi cha fahali. Ikumbukwe kuwa wito wa Kamati Teule kuhusu kusema lolote (chini ya kiapo au la) kuhusiana na skendo hii, ulikuwa kwa wananchi wote na last time I checked, Lowassa, Karamagi na RA wote ni wananchi wa Tanzania. Sasa walitaka wapewe special treatment?

They can say whatever they want, lakini hizo zote ni excuses. EL mwenyewe amechanganyikiwa na akawakoromea mawaziri waitee serikali badala ya kushabikia ripoti. Hivi alikuwa amelewa au amelogwa? Who in their right mind atapingana na ripoti iliyodhihirisha kulikuwa na ukaidi na ukiukwaji wa sheria, kanuni na hata maagizo la baraza la mawaziri? Tena vyote hivi viko kwenye Hansard!

Lowassa aache kuwa mbinafsi, akiri makosa, atubu na kujutia, kisha atumikie hukumu. Anazidi kujiaibisha na hususan familia yake (yule mtoto mdogo, sijui aitwa Richard)ukiachilia wale waliohusika na upuuzi huu.
 
Remarks;

It is true that we hava long way to go... hata Kijiji na Mzee Mwanakijiji walivyotangaziwa na Mwakyembe kwenda kutoa ushahidi... hakuweza hata kupiga zile simu zake...

Even our heroes... kweli, kweli ... kazi ipo...

Hata Wabunge wa Upinzani? Na heros wetu... Dr. Slaa na Zitto Kabwe achilia mbali Kijana Mnyika...
 
kuna news zinatoka DOM na si za reliable source..inasemekana Msabaha amebeba msalaba na kujiuluzu amekubali full responsibility...na Lowasa majibu yake ni "nilimwamini waziri Msabaha na ametuangusha"....tungojee full report asubuhi....
i hope haitakuwa hivyo MUNGU tusaidie

Deja Vu!!! Sound like the story of Meghji and Ballali!!! Blame it on someone else!
 
Wakuu naomba kujua kama hii Bunge session huko bongo inaoneshwa live kwenye TV kama walivyoonesha sakata la Zitto

Mkuu Kithuku

Sijui kama umeisha jibiwa hili, kama kuna siku watu walikunywa bia ni jana.

Unaambiwa ITV ilirudia kila kitu(marudio-usiku) kwa sasa hata hawa jamaa wakifanya nini watanzania kuanzia watoto wadogo wameisha hukumu kabisa.

Discussion hata watoto wa darasa la kwanza(siku hizi miaka 5) tayari wameisha jua MAFISADI wa nchi ni akina nani, hata EL, Karamagi na group lao wakifikiria watakufa kiume hakuna hili.

TUnataka akina MWakyembe, Manyanya na wengineo wengi kuokoa Tanzania.

Nina uhakika kama CCM itakinga kifua utakuwa mwisho wa hiki chama.

Pia leo watu hawabanduki kwenye TV hata maofisini, watu watatumia technology kuweza kupata watu wanaotetea MAFISADI.

Katika list waliobaki, Chenge no.1, asifikiri watanzania hatujui kuwa bado yeye.
 
Ewe mola twakuomba umpe hekima na busara raisi wetu ili aweze fanya maamuzi ya busara kwa maufaa ya Taifa la Tanzania
 
Suala lililopo mbele yetu ni pana, linagusa uadilifu wa viongozi wote katika taifa hili.Wananchi ni lazima tuamke tukatae hali hii ya kuwa na watu wanaoiba katika taasisi za umma na kisha kugombea uwakilishi wa wananchi.Kwa kuwa kipindi cha uchaguzi bado itabidi tujipange ili tuweze kutoa elimu kwa wenzetu ili makosa haya yasiendelee kutugharimu.Kwa sasa tuombe Waziri Mkuu ajiuzulu ili kutoa nafasi ya Baraza jipya kuundwa na baada ya hapo wahusika wa kashfa mbalimbali wafikishwe mahakamani. Iwapo Waziri Mkuu hatajiuzulu naomba Wananchi kupitia maandamano ya amani tumshinikize hadi aachie ngazi.
 
So far, sioni njia nyingine yoyote isipokuwa kuvunja baraza na kuliunda upya na hivyo kuwatosa waliokuwamo na wasiokuwamo. Upande mwingine ni Waziri Mkuu awashawishi mawaziri wenzake wajiuzulu kuonesha mshikamano naye (siyo kuonesha kuwajibika) ili wampe Rais nafasi ya kutengeneza upya serikali yake. Hapa ndipo suala la ubia linapojitokeza..
 
Pamoja na semina elekezi zote zile bado mambo yameenda hovyo namna hii? Kulikoni?
Mimi napata kigugumizi kwamba kama mwanasheria mkuu wa serikali naye amehusika katika ufisadi huo, hivi kuna mantiki gani ya yeye kuendelea kwake kuwa katika kamati ya kuchunguza BOT? Si atavuga mambo huyu?
 
Mngoja ametajwa kuwa katika dirty scandal nyingi sana za mabillioni ya pesa. is time for JK to take him out of the ofisi
 
Naona tunapotezeana muda na Taifa letu haliwezi kujifunga katika nyuzi za kashfa miezi nenda miezi rudi. Haiwezekani watu wale wale waendelee kutuumiza vichwa kana kwamba katika Jamhuri mzima wenye akili timamu ni wao tu!

Binafsi siyo tu nimechoka na kuandika kuhusu kashfa lakini nimechoka na majina yale yale hadi inakuwa kama uchuro!

Mgonja
Chenge
Rostam
Lowassa

Wanatoka sayari gani hawa kiasi kwamba kuwaondoa hadi tuliite Bunge la Mbinguni? Wana maslahi gani kwenye ofisi za serikali kiasi kwamba wanaweza kuendelea kuendeshwa katika magari ya serikali kama vile malaika wa kheri?

Mhe. Rais, sijakuomba vitu vingi muda mrefu ila sasa naomba nilete ombi rasmi, vunja baraza unda jipya. Jipya siyo kwa sababu ya uundwaji wake bali jipya kwa watu watakaokuwemo, majukumu yatakayosimamiwa nayo, na uwazi na uwajibikaji wa wananchi hao.

Kwa miaka nenda rudi tumekuwa na wanaume kama mawaziri wakuu, inatosha majaribio hayo, naamini Taifa letu liko tayari kuwa na mama ambaye anaweza kusimama na kufanya kweli maana inawezekana kwa kuwaangalia kina baba zaidi tumefunga macho kuona vipaji vingine!

Tengeza Baraza ambalo siyo tu litakuwa ni msaada kwako, bali litakuwa na lengo moja kubwa nalo ni kupiga vita ufisadi katika kila nyanja na sekta. Kupiga vita upotevu (isomeke ukwapuaji) wa fedha za serikali na matumizi mabaya ya ofisi na madaraka.

Mhe. Rais unasimama katika wakati wa pekee wa historia yetu, Watanzania hata wasiokubaliana na wewe au wasiokipenda chama chako kilichogubikwa na kashfa hizi nyingi ndani ya serikali yake, bado wanakuangalia wewe kama kiongozi wa Taifa lao.

Wakati huu wa pekee na ambao bila ya shaka ni wa tunu, unakutaka wewe kusimama hata ikibidi peke yako kufanya maamuzi machungu kama vile Rambo alivyojishona kidonde chake baada ya kuanguka toka kwenye genge (Kwenye First Blood - I hope you saw the movie.. )na wewe ushone kidonda cha kujitakia na ambacho kinazidi kujeruhiwa kwa mlundikano wa kashfa!

Bado ninaamini kuwa ukitaka kusafisha serikali yetu unaweza. Hauhitaji kibali cha kiumbe mwingine yoyote yule duniani, na hauhitaji kusikiliza ushauri wa mizimu na mapepo!

Katika hili lazima ujisikie mpweke na peke. Ujisikie kama mtu aliyeachwa nyikani na rafiki zake, wakati huu ni lazima ubakiwe na machozi ya uchungu kwani uliyekula naye chakula, ndiye amekuinulia kisigino!!

Mhe. Rais ongoza Taifa katika vita vya ufisadi, vita ambavyo maadui wako ndani ya serikali yako! Ni wewe uliye Amiri wa majeshi yetu yote! Pigana mwana wa Tanzania, na ufanya kama alivyofanya Wallace kwenye "Braveheart"! Pambana usirudi nyuma.

Vinginevyo, nafasi hii ikipotea, siyo tu wataanguka wasaidizi wako, bali na wewe mwenyewe utaanguka kama gunia la lumbesa kwenye kona za Tandale! Utabwaga chini kama manyanga ya wazaramo!

Jifunge kibwewe Kikwete, uliomba kazi, ifanye!

Umewasahau Mramba, Karamagi na maswahiba. Ushindi ni lazima

JJ
 
Keiawa ni kweli hatuna huo utamaduni lakini this time sio swala la utamaduni tena THEY MUST GO FOR SURE ENOUGH IS ENOUGH.

Mwanakiji tuko pamoja mimi pia naona kuna watu wanajirudia kwenye kila scandal lakini bado wapo napata taabu kulielewa hili kwa kweli. Me nadhani wasipojiuzuru this time TUTAWAFUATA HUKO HUKO OFISINI NA KUWATOA KWA VIBOKO.
 
Shame,shame, shame,
Yaani jana nilipokuwa naangalia tv report ikisomwa nilikuwa nasikia baridi. Aibu gani hii, lowasa katoa macho hana aibu kama kibaki.Yani asipojiuzulu sijui ni bora mtu ajilipue tu karibu na yeye tumsahau.Jk kibarua kigumu hiki sasa, n its time to show us that you are the real man. WAENDEE
 
Mheshimiwa Rais Kikwete wakati wa kampeni ya kuwania Urais ulikuwa ukimuomba sana Mungu ili akujalie uupate uraisi mpaka ikapelekea kuanguka pale jangwani kwa sababu ya swaumu kali. Nia yako ilikuwa njema kabisa ili uwatumikie waTanzania kufikia ktk maisha bora kwa kila mtu.

Swali, Je siku hizi unaomba kama ulivyokuwa unomba wakati wa kampeni? au ndiyo umeacha kabisa?

Maana kwa sasa ulitakiwa umuombe Mungu kwa nguvu zaidi ya kipindi cha kampeni. Kuonguza taifa si mchezo mzee unahitaji uwezo wa Mungu akupe busara na mamlaka binafsi juu kuongoza nchi. Sisi raia tutakuombea lakini wewe ndiyo iwe zaidi.

Huu ni ushauri wa kiroho mzee endelea kuchapa kazi. Nchi hii inahitaji uwepo wa Mungu ktk kuiendesha maana inamianya mingi sana ya adui shetani kuichezea. Ombea baraza lako la mawaziri mzee
 
Mheshimiwa Rais Kikwete wakati wa kampeni ya kuwania Urais ulikuwa ukimuomba sana Mungu ili akujalie uupate uraisi mpaka ikapelekea kuanguka pale jangwani kwa sababu ya swaumu kali. Nia yako ilikuwa njema kabisa ili uwatumikie waTanzania kufikia ktk maisha bora kwa kila mtu.

Swali, Je siku hizi unaomba kama ulivyokuwa unomba wakati wa kampeni? au ndiyo umeacha kabisa?

Maana kwa sasa ulitakiwa umuombe Mungu kwa nguvu zaidi ya kipindi cha kampeni. Kuonguza taifa si mchezo mzee unahitaji uwezo wa Mungu akupe busara na mamlaka binafsi juu kuongoza nchi. Sisi raia tutakuombea lakini wewe ndiyo iwe zaidi.

Huu ni ushauri wa kiroho mzee endelea kuchapa kazi. Nchi hii inahitaji uwepo wa Mungu ktk kuiendesha maana inamianya mingi sana ya adui shetani kuichezea. Ombea baraza lako la mawaziri mzee
 
Nasubiria kwa hamu taarifa za leo kutoka dodoma!!!!

Lowassa by no means ni jina lilitajwa sana mpaka sasa kwa mwaka 2008.... naomba atumie tu busara zake kufanya maamuzi stahili
 
JF ni kiboko kwa haraka haraka tu watu walijiunga Wed Feb 2008 ni wengi sana

Hii riport imepandisha hadhi ya JF as well. Maana karibu kila kitu kilichopo kwenye ripoti kilikuwa kimesemwa JF
 
Ripoti ya tume kutangazwa bungeni na kurushwa hewani na vyombo vya habari mubashara ni tukio la kihistoria katika nchi yetu tangu tulipopata uhuru 1961.Msisimko umetukumba wale tuliokuwa tunaisikiliza ripoti ya Dr.Harrison Mwakyembe na sasa tunasubiri wakulu waliotajwa wawajibishwe na kurudisha fedha walizokomba,kuanzia EL hadi mtu wa mwisho katika ile chain.Kwa sasa tunainua mikono juu na kumwombea JK achukue hatua dhidi ya hawa majambazi na kurudisha heshima ya uongozi wa nchi yetu.Nategemea katika masaa 24 yajayo kutatokea mabadiliko makubwa katika baraza la mawaziri na makatibu wakuu wwa wizara zilizotajwa katika ripoti hii.Mungu ibariki Tanzania.
 
Grey Mgonja anakuwa "featuring" kwenye kila ripoti ya ubadhirifu, hivi ni kitu gani kinamfanya asiwajibishwe mpaka sasa? Hivi hili la BOT yeye limempitia kando kweli?
Naomba kueleweshwa, kwa nini ako kazini hadi leo wakati madudu waliyofanya na Balali yanatosha kabisa kumnyang'anya kazi?

HUENDA HUYU BWANA NI MTU ANAYEJUA KULA KIUSTAARABU,MAANA HAPA NASOMEKA AKIWA ANATOA ALERTS KILA KONA KAMA ALIVYOMFANYIA MAMA MEGHJI.

TUOMBEANE MUNGU TUJAALIWE HEKIMA NA AMANI.

JAMANI HUYU JAMAA JK NA ILE SMILE YAKE SI MCHEZO BWANA.

SASA NAJARIBU KUMKUMBUKA NDG.RIZIWAN TULIPOKUTANA UWANJA WA TAIFA 1994 SIKU SIMBA SPORT CLUB NA EL HARRACH YA ALGERIA. KIJANA TULIKUWA NAYE UPANDE ULE MALOFA,NIKATAMBULISHWA NA JAMAA YANGU MMOJA WA SIMBA WHO WAS RELATED TO KAKA DITO,JAMAA AKAMUULIZA MBONA UKO HUKU,AKAJIBU ,UNAJUA KUJA KWENYEWE HUKU NI KWA UJANJA HIVYO NI VEMA NIKATULIA UPANDE HUU NIANGALIE MPIRA,STORY ZIKASONGA MBELE TUKISUBIRI SOKA LA CAF,BY THEN NILIKUWA 7YRS OLDER THAN RIZIWAN, MARA GHAFLA MVUA KALI IKADONDOKA PALE,TULIOLOWANA KAMA MBUZI.

SASA MZAZI WA AINA HII ANAONEKANA WAZI NI MWANANCHI,SASA KTK JAMBO HILI NAAMINI KABISA KUWA ATAONYESHA WAZI YEYE NI MWANANCHI NA MZAZI ANAYEPENDA SIFA NJEMA KWA VIJANA WAKE.

KUNA KUUA CARRIER YA SIASA ZA WATU HAPA LAKINI PIA KUNA KUIJENGA JAMII NJEMA PIA.

MH.RAIS ATANGULIWE NA HEKIMA KTK JAMBO HILI NA UZURI YEYE SASA KESHAFANYA ALWAYS HAKI ITANDEKA KWA MUJIBU WA SHERIA.

YUKO DODOMA KIKAZI,NA NINAKUMBUKA KUNA SIKU NILIMUULIZA FMES,KUWA HIVI BUNGE LINAKETI LINI?

MPENI NAFASI ATENDE KAZI.
 
Back
Top Bottom