Inakuwaje Upande wa Sekta ya Madini Tanzania tunaambulia 16% kwenye Mikataba na Madini ni Yetu? Naomba nieleweshwe Tafadhali Uenda nikaelewa

Inakuwaje Upande wa Sekta ya Madini Tanzania tunaambulia 16% kwenye Mikataba na Madini ni Yetu? Naomba nieleweshwe Tafadhali Uenda nikaelewa

TUKANA UONE

JF-Expert Member
Joined
Jan 3, 2018
Posts
2,718
Reaction score
8,192
Wakuu naomba mtu mwenye uelewa na mambo ya Madini pamoja na Mikataba anieleweshe ili nami nipate kuelewa !

Tanzania imebarikiwa Kuwa na Madini tofauti tofauti ambayo bila shaka yangetutoa kwenye Umasikini watu wetu wakaishi maisha mazuri na Kuwa na kipato kizuri !

Nimejaribu kudodosa na kupitia machapisho mbalimbali na kugundua kwamba,kwenye Migodi yote ya Madini ya dhahanu ambayo inaendelea kufanya kazi na Ile ambayo haijachimbwa ni kwamba,Wawekezaji wao hupata zaidi ya Asilimia 80% ya Mali yote halafu sisi wenye Mali tunapata Asilimia zisizozidi Asilimia 20 %

Sasa Je,swali langu ni kwamba,ni kwanini sisi wenye Mali tunapata mgao kidogo ilihali mchimbaji (Muwekezaji) anachukua sehemu kubwa ya Madini yetu?

Je nchi yetu Haina uwezo wa kuchimba Madini hadi tutafute watu watuchimbie na bado wanachukua sehemu kubwa ya Madini yetu halafu sisi tunabaki na kidogo?

Je,wakuu hivi ni kweli kabisa au stori tu za vijiweni?,maana binafsi naona kama haingii akilini hata kidogo

Hebu nielewesheni wakuu nami nielewe yawezekana kumbe Mimi ndiye sielewi!

Nipo tayari kueleweshwa na nitakuwa tayari kuelewa !
 
Mainjinia, wanasheria, wataalamu wengineo tunao somesha wanatembea na KADI ZA CHAMA MIFUKONI NA KUWA MACHAWA badala ya kutembea na tafiti, mipango, mbinu na namna bora ya ku utilize resources zetu.

Viongozi wanao simamia hizo sector wanawaza kujenga na kushibisha matumbo kwa ajili ya vizazi vyao kwanza ndipo mengine yafanyike.

Wanasiasa wenye dhamana wanacheza na PERCENTS kwenye mikataba.

Raia wasimamizi namba moja wa nchi zao wapo tayari kwenda AIRPORT KUIPOKEA SIMBA/YANGA KWA MAMIA AU MAELFU ila sio kwenda kuhoji kwanini nchi bado ni.masikini licha ya utajiri wote tulio nao.

TSS
JESHI
VITENGO VINGINE WAPO KIMYA. kwa maksuudi au kwa sababu mfumo umewafunga.
 
Back
Top Bottom