Inakatisha tamaa

Inakatisha tamaa

Fundi mahiri wa Ujenzi

JF-Expert Member
Joined
Dec 10, 2012
Posts
4,717
Reaction score
3,680
Salaaaaaaaaaaaaaaaaaam kwa wote.
Bila shaka lunch ilikuwa mrwaaaaaaaaaaaaaaa!!!!!!!!!!!!!!!!!!!

Mwenzenu yamenikuta!

Mke wangu ana ujauzito wa miezi mitano. Namtakia afya njema na mungu atusaidie tupate mzaliwa wa kwanza.
Lkn nina miezi kama mitatu hivi...jamani niko kwenye shida

Kinachonipa shida ni Hiki:-

Kila ninachokifanya kwake ni kero mfano:

1. Anaweza akaninunia. Basi akinuna nami simuongeleshi lkn cha ajabu kukaa kwangu kimya linakuwa kosa na unakuwa ugomvi mkubwa sana kwanini simuongeleshi!
2. Hataki kuniona. Nikiona hivyo najichanganya kitaa na wadau mpaka mida ya saa nne usiku lengolangu likiwa nikifika home nioge nikalale kimya kimya lkn cha ajabu nikifanya hivyo bonge la ugomvi eti nilikuwa wapi. hataki nitoke
3. kiufupi ni migogoro daily ndugu zangu

Sasa imefikia point naanza kupoteza upendo kwake

Sina raha kwakweli. Naanza kupata fikra za kutafuta mrembo mwingine anipe japo faraja

Ungekuwa ni wewe ungechukua uamuzi gani?
 
We mimba huwa zina makorokocho yake... Wapo wanaofichiwa funguo za magari, wapo wanaobamiziwa simu ukutani, wapo wasiopenda kukuona na ukitoka kesi... yaani we acha tu..... Suluhisho ni kuivumilia hali hiyo hadi atakapojifungua. Ukitafuta kimwana, naye ukimtia mimba si yatakuwa hayohayo? Mwisho wa siku utajaza mtaa watoto wanaofanana umri
 
pole na hongera kwa kuwa wajawazito... kwa maana watarajiwa baba na mama! mungu awajaalie mtoto mwema na mwenye afya.

Sasa jamaa hayo yote ni mambo ya mapito, huna haja ya kutafuta mpangokando...wa nini? vipi kwani huli cha usiku kwa mwenzio?

Pia jitahidi kutekeleza mwenzio anachohitaji, usimkimbie na wala usimnunie akiwa amenuna... fanya nae utani!
 
Uamuzi wa kutafuta mrembo ni kukimbia majukumu....Bora umesema ni mtoto wa 1 maana ningekutafuta halafu ningeishia kwa wajeda. Hiyo ni hali ya kawaida sio kwamba anapenda yeye la hasha ila ni kiumbe kilicho tumboni kinamsukuma kufanya hivyo ila moyo wake unakupenda sana ndio maana anataka uwe naye karibu na pia usimchunie hata kama kiumbe kimekuchunia. Napenda kukunong'oneza ikiwezekana uanze kununua nguo za awali ila nyingi ziwe za mtoto wa kiume tehe teheeeeeeeeeeeeee.
 
We mimba huwa zina makorokocho yake... Wapo wanaofichiwa funguo za magari, wapo wanaobamiziwa simu ukutani, wapo wasiopenda kukuona na ukitoka kesi... yaani we acha tu..... Suluhisho ni kuivumilia hali hiyo hadi atakapojifungua. Ukitafuta kimwana, naye ukimtia mimba si yatakuwa hayohayo? Mwisho wa siku utajaza mtaa watoto wanaofanana umri

Asante kwa ushauri
 
pole na hongera kwa kuwa wajawazito... kwa maana watarajiwa baba na mama! mungu awajaalie mtoto mwema na mwenye afya.

Sasa jamaa hayo yote ni mambo ya mapito, huna haja ya kutafuta mpangokando...wa nini? vipi kwani huli cha usiku kwa mwenzio?

Pia jitahidi kutekeleza mwenzio anachohitaji, usimkimbie na wala usimnunie akiwa amenuna... fanya nae utani!

Mkuu hali ni mbaya hata ukijishusha hapakaliki. Mfano anakuambia kwa ukali sitaki kukuona umenikera sana ukiangalia ulichomkera haukioni. Ok unaamua umpishe ili aridhike na nafsi yake inakuwa shida tena.
 
Uamuzi wa kutafuta mrembo ni kukimbia majukumu....Bora umesema ni mtoto wa 1 maana ningekutafuta halafu ningeishia kwa wajeda. Hiyo ni hali ya kawaida sio kwamba anapenda yeye la hasha ila ni kiumbe kilicho tumboni kinamsukuma kufanya hivyo ila moyo wake unakupenda sana ndio maana anataka uwe na karibu na pia usimchunie hata kama kiumbe kumichuna. Napenda kukunong'oneza ikiwezekana uanze kununua nguo za awali ila nyingi ziwe za mtoto wa kiume tehe teheeeeeeeeeeeeee.

Nahisi una kauzoefu flani juu ya hili
 
Sina raha kwakweli. Naanza kupata fikra za kutafuta mrembo mwingine anipe japo faraja

Usingeweka hiyo sentensi, maelezo yako yangekuwa na mantiki kubwa sana na yenye manufaa. Wewe sio wa kwanza kupatwa na shida hiyo, ambayo ni kawaida sana kwenye kipindi kama alicho nacho mkeo. Badala ya kujipendekezea kumiliki nyumba ndogo ungeomba kwanza ushauri kwa walioishi na wake wa namna hiyo.
 
Mchukue yule Mrembo uliyemuajiri kama Meneja wa Pub...au sio wewe Mkuu?
 
Usingeweka hiyo sentensi, maelezo yako yangekuwa na mantiki kubwa sana na yenye manufaa. Wewe sio wa kwanza kupatwa na shida hiyo, ambayo ni kawaida sana kwenye kipindi kama alicho nacho mkeo. Badala ya kujipendekezea kumiliki nyumba ndogo ungeomba kwanza ushauri kwa walioishi na wake wa namna hiyo.

Fanya kama hako kasentesi hakapo then nishauri mkuu. Ushauri wako kwangu ni mhimu sana
 
Pole,lakini vumilia sababu kila mimba iko kivyake na wazimu wake,mie mwenzio nikiwa na mimba huka kizingitini hapiti mtu wandani wandani wa nje wanje,mara nataka kusafiri nikifika nnakokwenda hata siku2 sikai nataka kurudi yani ilimradi tafran,
mie nakua usingizi sipati mumewangua akiweka kichwa anakoroma,namuamsha mara nataka maji mara nataka tende mbichi hata kama sio msimu staki kujua nataka nataka sasa jaribu kumchukulia,na zowea hali ya mwenzio itafika mda atawacha..
 
Binafsi sijawahi kukumbana na hali hii lakini kutokana na uzoefu kwa wengine nadhani ni kitu cha kupita tu..Kikubwa uwe 'mvumilivu' sana kwa sababu ukitafuta fairness hutaipata..Kubali vile anataka yeye umfanyie..Miezi tisa sio mingi ya kukufanya uteseke kiivyo...Geuza hizo karaha ziwe 'upendo' kwa sababu she is carrying your baby in her womb..kwa hiyo wewe pia ni sehemu ya 'tatizo' kama ambavyo wewe waliona..mengine ngoja waje wanawake wenyewe wakusaidie!................
 
Hebu rudia kale kausemi ulikosema pale kanisani kama ni mkristu " ninakupokea mwenzangu ......kwa mema na mabaya...."
 
huyo mwanamke anajiendekeza tu kwani yeye ni wakwanza kuzaaa???siamini mimba yaweza mfanya eti amchukie mtu kha siamini haya wanajijengea tu kma defence mechanism fulani unakut eti mama anamchukia mtoto wake wakumzaa is it coming kisa ana mimba nyingine???????mwanamke mpumbavu huibomoa nyumba yake kwa mikono yake mwenyewe .mimba yaweza kukufanya uchukie vyakula na sio watu hilo ni pepo chafu
 
Moses hiyo ni hali ya kawaida, na huwa haidumu sana, huwa ni ya kipindi tu, na pale anapokwambia hataki kukuona si kama hakupendi ila inamjia hasira tu pale anapokuona, lakini ukiondoka tu, roho inaanza kuuma kuwa amekufukuza.Kwa kweli Mimba zina makorokocho sana.
Mimi nikiwa hivyo sipendi mume wangu atafune nimuone, nasikia kinyaa, nahisi anatafuna vibaya, na pia akioga mwenyewe naona ananuka, So ni lazima nikamuogeshe na nimsugue ninavyotaka mm , ndipo atapanda kitandani alale, akigoma tu mm naenda kulala Sitting room, na kilio juu! ila nikijifungua tu ajue kazi imekweisha kwake .Kwa hiyo VUMILIA NI UPEPO TU"
 
My friend! Hiki ni kipindi kigumu sana kwa mke wako, imagine kutembea na kiumbe kingine tumboni kinachopumua kama wewe na yeye, I wish wanaume tungeonjeshwa hiyo experience pia.

Sasa yeye anaona unainjoi maisha huku yeye anateseka, lakini baadae mtoto atakuwa wenu nyote, hii lazima impe hasira.

Siri ya kum-win ni kukaa naye bega kwa bega, akikutuma kitu tekeleza haraka sana, kama vihela vipo unamtoa mara kwa mara kubadili mlo. Onyesha uko karibu naye na wewe unaguswa sana na hiyo hali yake, ataanza kukuhurumia na kukupenda.

Ukiweza kufanikiwa kuiteka akili yake ktk hiki kipindi uta-score maksi nyingi sana, kwa sababu inajulikana kwamba kipindi hiki lazima mwanaume atafute nyumba ndogo ya kusapoti, na hii ndiyo huingezaga hasira hata kama hajaprove, ila tu akiona haupo anajua ndiko ulikokuwa.

Sasa jipe muda wa kuwa naye karibu sana, atakupenda sana na utashangaa, tena akikukubali hata ile mambo yetu utainjoi maana atakuwa anakupa bila shida, inabaki ni kutafuta mikao laini. Hautawaza tena kutafuta kidumu.

Jaribu hii halafu utaona majibu.
 
Back
Top Bottom