Inafaa kuomba kuongezewa mshahara?

Inafaa kuomba kuongezewa mshahara?

SECRET AGENT

JF-Expert Member
Joined
Jan 4, 2019
Posts
254
Reaction score
499
Nimeajiriwa katika kampuni (private sector), Nafanya kazi kwa bidii sana mpaka boss mwenyewe anaona kwamba kweli napiga kazi na kazi nazofanya zinaingiza pesa na kusifiwa na wateja pia lakini tangu niajiriwe mshahara haupandi na naona ni mdogo sana ukilinganisha na kipato kinachoingia kupitia bidii zangu, muda mwingine natoka kazini usiku nikimalizia kazi za wateja, lakini Bado boss hagusii kabisa suala la kuongeza mshahara. Mbali na hapo elimu yangu ni level ya shahada, ingekua nina elimu ndogo labda ningesema kwa sababu ya kiwango changu cha elimu ndiyo sababu.
Nimekuwa na mawazo ya kujibana nifungue business yangu kwani Nafanya kazi nikiwa na hasira moyoni mwangu. Hasira hiyo inakuja pale ambapo waajiriwa wengine ambao nawazidi mbali kiujuzi na kitaaluma tupo level moja ya mshahara na wengine wamenizidi. Nina bidii na heshima sijawahi kukwazana na boss.

Je ni busara kuomba kuongezewa mshahara au laa naomba ushauri wenu
 
Jaribu kuomba kuongezewa
Kwanjia ya oral/verbal Kama ina ruhusiwa na inawezekana

Officially
Andika hata barua convicing one kwa director wako mshawishi juu ya nyongeza

All d best
 
tafta msaada kwa wasomi wanaohusika na kusimamia wafanyakaz na stahiki zao..Humu utapata majibu ila sio majib sahihi..
 
Jaribu kuomba kuongezewa
Kwanjia ya oral/verbal Kama ina ruhusiwa na inawezekana

Officially
Andika hata barua convicing one kwa director wako mshawishi juu ya nyongeza

All d best
Thanks kwa ushauri wako wenye manufaa
 
tafta msaada kwa wasomi wanaohusika na kusimamia wafanyakaz na stahiki zao..Humu utapata majibu ila sio majib sahihi..
Asante mkuu kwa ushauri, na je hapo boss hawezi kuona kama umemuwajibisha hivi au umemshitaki
 
Nilitumia hicho kigezo ili kuachana nao

wakaniambia hawawezi

ikawa ndio mwisho ya wao kuniajiri

Nipo zangu naingiza miziki huku kwenye memory card
Hahahah, Mkuu uliomba ongezeko kubwa ili uachane nao
 
Nakumbuka miaka 37 iliyopita nilikuwa nafanya kazi kwenye kampuni moja ya wazungu
Baada ya miaka 5 nikiwa nachapa kazi nikaongea na mmoja wa directors na kuhusu mshahara
Akaniambia bila kuuliza hutapandishiwa
Ndipo nikamwendea MD mwenyewe na alikubali kuniongezea
Kuna makampuni wanafurahi hata ukifanya bure ili wao wafaidike

Pia kufungua biashara yako mwenyewe sio wazo baya ila uwe makini sana na sheria
Ingawa kuna wengine huwa wanafanikiwa na wengine kufeli
Nakuombea kila la kheri
Ila ni haki yako kuuliza kupandishiwa mshahara na sio dhambi
Kama anakuhitaji atakuongezea
 
Nakumbuka miaka 37 iliyopita nilikuwa nafanya kazi kwenye kampuni moja ya wazungu
Baada ya miaka 5 nikiwa nachapa kazi nikaongea na mmoja wa directors na kuhusu mshahara
Akaniambia bila kuuliza hutapandishiwa
Ndipo nikamwendea MD mwenyewe na alikubali kuniongezea
Kuna makampuni wanafurahi hata ukifanya bure ili wao wafaidike

Pia kufungua biashara yako mwenyewe sio wazo baya ila uwe makini sana na sheria
Ingawa kuna wengine huwa wanafanikiwa na wengine kufeli
Nakuombea kila la kheri
Ila ni haki yako kuuliza kupandishiwa mshahara na sio dhambi
Kama anakuhitaji atakuongezea
Asante mkuu kwa ushauri wako
 
Nilipitia same situation, nikaomba waongeze wakagoma. Nikatafuta kazi nyingine kimya kimya, nilivyopata nikawapa resignation letter. Wakasema tukae mezani tujadili waongeze kiasi gani, nikawaambia Asanteni Ninashukuru.
 
Pole mkuu, kumbuka si wewe, mimi nafanya kazi na kampuni moja, kibaya zaidi nalipwa pesa ndogo sana (300k) kwa mwezi na bado kuna makato, nimewaomba waongeze naona wapo kimya hivi natafuta mbinu za kukimbia ndani ya mwezi ujao tu. Hakika nitaondoka maana nafanya kazi kwa shida yaani mtu unakuta kuna kipindi hata hela ya kula inakata!
 
Haya yalinishinda kiukweli ulicho andika nikama nimeandika Mimi yaan ukiomba kuongezewa mshahara wanaanza kukujaji vibaya kikubwa jibane hapo hapo kwa hicho kidogo ila uweke lengo angalau ukusanye japo kimtaji cha kujiajili afu uwaachie likazi lao hapo
Nimeajiriwa katika kampuni (private sector), Nafanya kazi kwa bidii sana mpaka boss mwenyewe anaona kwamba kweli napiga kazi na kazi nazofanya zinaingiza pesa na kusifiwa na wateja pia lakini tangu niajiriwe mshahara haupandi na naona ni mdogo sana ukilinganisha na kipato kinachoingia kupitia bidii zangu, muda mwingine natoka kazini usiku nikimalizia kazi za wateja, lakini Bado boss hagusii kabisa suala la kuongeza mshahara. Mbali na hapo elimu yangu ni level ya shahada, ingekua nina elimu ndogo labda ningesema kwa sababu ya kiwango changu cha elimu ndiyo sababu.
Nimekuwa na mawazo ya kujibana nifungue business yangu kwani Nafanya kazi nikiwa na hasira moyoni mwangu. Hasira hiyo inakuja pale ambapo waajiriwa wengine ambao nawazidi mbali kiujuzi na kitaaluma tupo level moja ya mshahara na wengine wamenizidi. Nina bidii na heshima sijawahi kukwazana na boss.

Je ni busara kuomba kuongezewa mshahara au laa naomba ushauri wenu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nimeajiriwa katika kampuni (private sector), Nafanya kazi kwa bidii sana mpaka boss mwenyewe anaona kwamba kweli napiga kazi na kazi nazofanya zinaingiza pesa na kusifiwa na wateja pia lakini tangu niajiriwe mshahara haupandi na naona ni mdogo sana ukilinganisha na kipato kinachoingia kupitia bidii zangu, muda mwingine natoka kazini usiku nikimalizia kazi za wateja, lakini Bado boss hagusii kabisa suala la kuongeza mshahara. Mbali na hapo elimu yangu ni level ya shahada, ingekua nina elimu ndogo labda ningesema kwa sababu ya kiwango changu cha elimu ndiyo sababu.
Nimekuwa na mawazo ya kujibana nifungue business yangu kwani Nafanya kazi nikiwa na hasira moyoni mwangu. Hasira hiyo inakuja pale ambapo waajiriwa wengine ambao nawazidi mbali kiujuzi na kitaaluma tupo level moja ya mshahara na wengine wamenizidi. Nina bidii na heshima sijawahi kukwazana na boss.

Je ni busara kuomba kuongezewa mshahara au laa naomba ushauri wenu
Hili pia lilinikuta Mimi kwenye kampuni fulani,

Nilikua napiga sana kazi na matunda yanaonekana,

Lakini mshahara kukua na kuongezeka ilikua tabu sana

Baada ya kufanya tathmini kua ninacholipwa na pia kulinganisha na makampuni mengine jinsi wanavyolipwa, nikagundua kuwa ninalipwa kiwango cha chini sana

Lakini pia nilikua nikishangaa wafanyakazi wapya waliokuwa wakiajiriwa pale, walikua wanaanza na mshahara mkubwa zaidi ya mimi ingawa wote tulikuwa ni level ya Bachelor Degree

Nikasoma kuwa huyu muajiri wangu ana ni "under value" kwa hiyo nikaandikia barua ya kuacha kazi moja kwa moja bila vya kuomba kuongezewa mshahara

Alivyoipata ile barua, akaniita na kuniuliza shida ni nini??, nikamueleza maslahi ya kazi ni madogo, akanijibu hawawezi kuongeza mshahara, ok nikwamwambia mimi pia siwezi kuendelea kufanya kazi kwa maslahi haya

Nikaacha kazi, hivi sasa nasajili laini kwa alama za vidole mtaani

Kikubwa ni kuwa angalau kazi unayofanya hata ni kwenye mazingira magumu angalau ikuhakikishie uhakika wa chakula mwezi mzima

Sio ati unafanya kazi hata pesa ya kununua chakula na kujikimu tu kwa mwezi mzima haifiki, ila unawaingizia pesa ya kutosha wanahisa na wakurugenzi wa hiyo kampuni, hapo sasa inakuwa haina maana sasa ni bora uje kusajili laini kwa alama za vidole huku mtaani

Ushauri wangu ni kua jiamini na kaonane na muajiri wako na umuombe akuongezee mshahara, hiyo ni haki yako ya kimsingi kabisa, maana unafanya kazi ili ulipwe na si vinginevyo

Ahsante

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Pole mkuu, kumbuka si wewe, mimi nafanya kazi na kampuni moja, kibaya zaidi nalipwa pesa ndogo sana (300k) kwa mwezi na bado kuna makato, nimewaomba waongeze naona wapo kimya hivi natafuta mbinu za kukimbia ndani ya mwezi ujao tu. Hakika nitaondoka maana nafanya kazi kwa shida yaani mtu unakuta kuna kipindi hata hela ya kula inakata!
ahhhaaa...!!!,kumbe ndio weweeee!!!-sasa ngoja nikufate officen kwako nimeshakujua

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nimeajiriwa katika kampuni (private sector), Nafanya kazi kwa bidii sana mpaka boss mwenyewe anaona kwamba kweli napiga kazi na kazi nazofanya zinaingiza pesa na kusifiwa na wateja pia lakini tangu niajiriwe mshahara haupandi na naona ni mdogo sana ukilinganisha na kipato kinachoingia kupitia bidii zangu, muda mwingine natoka kazini usiku nikimalizia kazi za wateja, lakini Bado boss hagusii kabisa suala la kuongeza mshahara. Mbali na hapo elimu yangu ni level ya shahada, ingekua nina elimu ndogo labda ningesema kwa sababu ya kiwango changu cha elimu ndiyo sababu.
Nimekuwa na mawazo ya kujibana nifungue business yangu kwani Nafanya kazi nikiwa na hasira moyoni mwangu. Hasira hiyo inakuja pale ambapo waajiriwa wengine ambao nawazidi mbali kiujuzi na kitaaluma tupo level moja ya mshahara na wengine wamenizidi. Nina bidii na heshima sijawahi kukwazana na boss.

Je ni busara kuomba kuongezewa mshahara au laa naomba ushauri wenu
Ugonjwa wa private sector huo unanitesa sana,dawa ni kutia bidii tafuta kwingine. Waajiri wengi hupenda watu wenye juhudi lakini wao kumjali maslahi hawana....

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nilipitia same situation, nikaomba waongeze wakagoma. Nikatafuta kazi nyingine kimya kimya, nilivyopata nikawapa resignation letter. Wakasema tukae mezani tujadili waongeze kiasi gani, nikawaambia Asanteni Ninashukuru.
Hii ndio njia sahihi ya kufanya.
Kama mtu umezoea kuingiziwa mshahara kila mwezi ni ngumu Sana kuacha ghafla ujiingize kwenye biashara na kufanikiwa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nimeajiriwa katika kampuni (private sector), Nafanya kazi kwa bidii sana mpaka boss mwenyewe anaona kwamba kweli napiga kazi na kazi nazofanya zinaingiza pesa na kusifiwa na wateja pia lakini tangu niajiriwe mshahara haupandi na naona ni mdogo sana ukilinganisha na kipato kinachoingia kupitia bidii zangu, muda mwingine natoka kazini usiku nikimalizia kazi za wateja, lakini Bado boss hagusii kabisa suala la kuongeza mshahara. Mbali na hapo elimu yangu ni level ya shahada, ingekua nina elimu ndogo labda ningesema kwa sababu ya kiwango changu cha elimu ndiyo sababu.
Nimekuwa na mawazo ya kujibana nifungue business yangu kwani Nafanya kazi nikiwa na hasira moyoni mwangu. Hasira hiyo inakuja pale ambapo waajiriwa wengine ambao nawazidi mbali kiujuzi na kitaaluma tupo level moja ya mshahara na wengine wamenizidi. Nina bidii na heshima sijawahi kukwazana na boss.

Je ni busara kuomba kuongezewa mshahara au laa naomba ushauri wenu
Utatupatia mrejesho mkuu,
Baada ya kumuona bosi wako

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom