Napenda sana na nimefanya sana Kung fu
1. Tambua sababu ya wewe kujifunza mchezo husika. Unataka nini kwenye mchezo huo? Wewe self defense
Binafsi nilitaka kujijengea nidhamu binafsi, kuimarisha afya ya akili na mwili na kujijenga kiroho.
2. Tambua bidii katika kujifunza ndiyo nguzo, usiingie kutaka kujua self defense tu na kutoweka. Kuna makundi ya watu,
Kuna anayejua kucheza kata na anazo technique nyingi ila Hana nguvu ya mwili (ndani na nje) huyu akikutana na mtu mwenye nguvu na imara kimwili hatoboi kabisa. Kuna watu wana mikono mizito yaani wewe kublock tu mkono wake hutakuwa tofauti na mtu aliyepigwa.
Kuna yule mwenye nguvu na uimara wa mwili ila Hana mbinu. Huyu akikutana na mwenye mbinu na yupo imara ni lazima atapigwa.
Binafsi huwa naona ni bora zaidi kuujenga mwili kwa mazoezi imara kisha ndio uanze kujifunza hizo kata na techniques. Ila ukitaka uimara na wakati huo pia wataka master kata, hapa jiandae kwa mazoezi yaliyoshiba ili kuwa vizuri yaani nguvu na techniques.
3. Fanya martial arts yenye manufaa kwako, nidhamu itawale maana ndiyo nguzo kuu katika mchezo wa ngumi.
Mwisho acha kuuliza muda wa kuwa bora kwenye mchezo wa ngumi. Ubora wa karateka haitegemei muda ila ni bidii ya kujifunza. Na hii mchezo jitahidi ukianza usiache yaani endelea kufanya mpaka siku unakufa.
Marial arts ni maisha, hivyo ishi mchezo na uifanye kitu ambacho ni lazima kufanya kila siku ya maisha yako.