Amanito
JF-Expert Member
- Nov 20, 2015
- 259
- 551
Shukrani sana Mkuu.. Umeniongezea kitu ambacho nilikuwa sikifahamuNa pia haikuwa Muay Thai ilikuja kuitwa hivyo baada ya wao kuhitaji mchezo kwa ajili ya mashindano na kuondoa kabisa techniques ambazo zilikuwa kwa ajili ya kuua adui vitani awali ilijulikana kama MUAY BORAN.
Hii wa Thailand waliitumia katika vita kupambana na adui na kwa sasa ni vijijini sana ndo kuna mabaki ya wataalamu wake ambayo huyo Tony Jaa baba yake pia aliwahi kuicheza na kumpa vitu yeye pia.
Ukiifuatilia vizuri kuna techniques humo zinahusu wanyama kama Mamba, Nyani, Tembo, Nyati n.k
Bongo hii mtu akikwambia kaicheza na yupo fiti huyo muongo. Hiyo ni Traditional Martial Art ambayo ili uwe fiti ni lazima ufundwe kule kule na wenyewe kwanza siyo kuangalia you tube tu kuna matambiko yake pia.