JokaKuu,Yericko Nyerere,
..nimesikitishwa na kitendo cha Raisi kuamua kwenda Addis kwenye sherehe, wakati huku nyumbani kuna machafuko na wananchi wamepoteza maisha. je, kwa mtizamo wa Raisi, sherehe za Addis zina umuhimu kuliko haya yanayotokea kusini mwa nchi yetu?
cc: THE BIG SHOW, Mchambuzi, Sikonge, Masanilo, EMT, NasDaz
Kwanza nisingependa kuita hiki kinachotokea hapa nyumbani hivi sasa ni maafa! Maafa ni jambo zito na mungu aipushie mbali manake nchi hii haijapata kuwa tayari kwa maafa tangu nipate akili! Hata hivyo, sina shaka kwamba nchini kwa sasa kuna matatizo, na haya si tu yale ya Mtwara bali sehemu mbalimbali.
Pamoja na yote hayo, bado naona ni namna gani suala la kuadhimisha miaka 50 ya OAU ilivyokuwa na ulazima kwetu hata kama sio muhimu kihivyo! Ulazima ninaouona hapa ni ule ukweli kwamba hasilani hapana yeyote anayeweza kuyataja mafanikio ya OAU pasipo kuitaja Tanzanaia! OAU ni Tanzania na Tanzania ni OAU kutokana na sababu kubwa kwamba, one of the objectives za OAU ilikuwa ni kuhakikisha nchi zote za Africa zinakuwa huru! Wataalamu wa siasa na historia wanaweza kunisahihisha lakini kama kumbukumbu zangu zipo sawa, nazani Makao Makuu ya Kamati ya Ukombozi ya OAU yalikuwa Jijini Dar es salaam chini ya Brigedia Mstaafu Hashim Mbita(ready 2b corrected if am wrong). Kamati Kuu ya Ukombozi ya OAU ndiyo ilikuwa na jukumu la kuhakikisha Afrika yote inakuwa huru! Kama kuna mafanikio kwa 99% ya OAU basi ni hili la kufanikisha uhuru wa nchi zote za Afrika ingawaje bado kuna doa ndani ya Sahara Magharibi ambako Morocco bado hawataki kuondoa ushawishi wao! So, ule ukweli tu kwamba mafanikio makubwa ya OAU ni kufanikisha the main objective ambayo ilisimamiwa vizuri na serikali ya Tanzania; ambapo awamu ya kwanza chini ya Mwalimu ilitumia resources zake nyingi sana kufanikisha main objective inakuwa well attainable; basi bila shaka Rais wa Tanzania alikuwa na sababu za kwenda kushuhudia maadhimisho hayo!
Na jambo lingine ambalo naweza kusema OAU/AU kwa sasa wanatakiwa kujivunia ni hili la kuto-entertain mapinduzi...hakika hili nalo wanapaswa kujivunia kidogo manake nazani hivi sasa wanajeshi popote pale Africa kabla hawajafanya mapinduzi, changamoto ya kwanza wanayokabiliana nayo ni kujiuliza endapo mapinduzi yao yatakubalika! Hili, limesaidia sana kupunguza mapinduzi ya kijeshi Africa!
Last edited by a moderator: