TANU hawakuwa wabinafsi mission yao ilikuwa moja kudai uhuru, ndo maana hata alipokuja mwalimu watangulizi wake waliona wamwachie bila kumuwekea figisu kulikuwa na Viongozi wenye maono na wasio wabinafsi, CCM ya sasa imejaa Wezi Wabinafsi na wenye tamaa, wana roho ya nkikosa tuharibikiwe wote. Walianza na hoja mkiwachagua wapinzani ni chama changa wakaja Upinzani wa Lipumba una misimamo ya udini wakati huo huo anagombea na kikwete muislam kama yeye Wakaja na hoja ya CHADEMA ni ukanda wa kaskazin chama cha kikabila Wakaja Chama cha mabeberu wakaja chama kinasupport Ushoga, sahivi wanasema Chama cha kikatoliki, na sasa wanawekeza nguvu kubwa kutoa pesa kwa KKKT na bakwata wakidhan wanajenga taasisi imara za kidini kumbe ndo wanavuruga, kirusi kwenye Taifa hili ni mtu yeyote mwenye ukaribu na CCM
Hii ndio HOJA yenyewe. Tatizo ni chama dola - CCM. udini, kanda, uzanzibari, n.k. vinatumika tu kupambana na wanaopinga chama dola na magenge yake kuendelea kuhodhi madaraka na mamlaka kinyume cha katiba ya JMT. Kama kuna malalamiko basi yaelekezwe kwenye kupambana na mfumo wa chama dola unaoendelea kulitesa taifa. Huo mfumo umehodhi rasilimali, mamlaka, fikra na tunu zote za taifa na kuwahamasisha wananchi kufukuzia mizuka (ghosts) ya udini, uzanzibari, mabeberu, wapinzani, wasaliti, vibaraka, n.k. kama ndio sababu za matatizo yao badala ya kupambana na tatizo lenyewe.
Mleta mada, MSA, anachofanya ni kuziba pengo kubwa lililoko kwenye historia ya uhuru wa Tanganyika. Nimesoma baadhi ya maandiko yake na ya waandishi mbalimbali wa nje kuhusu historia ya Nyerere, TANU na Tanganyika ambayo yanathibitisha pengo hilo ambalo ni kama liliwekwa kwa makusudi pengine "kuwarahisishia" Watanzania wasisumbuke sana na historia ya nchi yao bali wazingatie zaidi yajayo - labda kwa lengo maalum alilolijua Nyerere na watu wake.
Sijaona uthibitisho wowote wa MSA kudhamiria kuleta udini kwenye maandiko yake. Maandiko yake ni ya muda mrefu na hayajawahi kuleta shida. Tatizo ni kuwa wengi wa watu muhimu (
notable historical figures) katika pengo lililopo kwenye historia ya nchi hii ni waislamu. Wako wakristo wachache pia ambao vijana wengi hawajahi kuwasikia au kujua habari zao kama kina: J. P. Kasella Bantu, C.K. Tumbo, J. Rupia, Alexander M. Tobias, Dr Michael Lugazia, Denis Phombeah, Z. James, Dome Okochi, C. Ongalo, Patrick Aoko, n.k..
Bahati mbaya yako mengi sana ambayo, kwa bahati mbaya, yamo kwenye vitabu vilivyoandikwa kwa undani kwa kiingereza ambacho hapa kwetu ni ugomvi mwingine. Na kwamba siku hizi vijana wengi hawana muda wa kusoma vitabu bali hutegemea zaidi kupata habari toka JF, Facebook, instagram, X, n.k. ni suala jingine.
Yawezekana MSA kawekeza zaidi katika kuandika yanayohusu "wazee wake" wa Mzizima waliosahaulika au kufutwa kabisa katika historia Tanganyika na hivyo kuonekana "mdini". Na hao Indio walikuwa wengi zaidi na instrumental katika kuanzisha TAA baadaye TANU. (Naongezea pia klabu za Simba na Yanga). Hivyo, naweza kuzielewa hisia hizo za MSA.
Naamini kulikuwa na namna Serikali ingeweza kuweka sawa mambo haya katika mizania ya historia rasmi ya taifa iliyochapishwa badala ya kuyafunikafunika tu. Na ndio hivyo hivyo ilivyofanyika kuhusu masuala ya Mapinduzi ya Zanzibar na Muungano na kuyapelekea kuyafanya NYETI sana hadi yakageuka kuwa moto mkali kuanzia visiwani kwenyewe hadi sasa "Tanganyika". Mhispania George Santayana alisema: "
those who cannot remember the past, are condemned to repeat it".
Ushauri wangu kwa wote, someni maandiko ya MSA kwa akili iliyo wazi (open and critical mind) kama kweli mnataka kuelimika kuhusu historia ya Tanganyika. Tafuteni na mengine yaliyoko ili kujithibitishia na kuelimika zaidi. Ya Sheikh Mwaipopo, machawa wote wa CCM na wajinga wengine (wa dini zote) hayahusiki kabisa Katika msimulizi ya MSA. Sijaona MSA akifanya endorsement yoyote kwa watu hao wala misimamo yao ya kijinga. Mnaweza kumfanyia
critique (uchambuzi yakinifu) lakini si kumpuuza kabisa.