Ilikuwaje baada ya kupata mpenzi mtandaoni?

Ilikuwaje baada ya kupata mpenzi mtandaoni?

Tulianzana FB, I never imagine kama tungeonanaga, kipindi hicho alikua huko nchi ya watu

Mawasiliano mdogo mdogo inaweza pita mamiezi hatujawasiliana, kisha tukapeana namba

Akanirushia wavu ila sikumuelewa kutokana na kwamba alikua mbali

Ikapita muda bila mawasiliano, siku ya siku napokea simu simu no ngeni kupokea ni yeye ananiambia amerudi bongo. Sahiyo yuko Dom mimi Arusha

Chatting za hapa na pale nikampotezea tena, miezi kadhaa kupita ananiambia amehamia Arusha kikazi

Japo tulikua mkoa mmoja ila miezi miwili baadae ndipo tukaonana kwa mara ya kwanza

Akaingiza ngonjera tena kiasi nikawa nimekubali kama sijakubali hivi

Kaka wawatu alikua mstaarabu na mtu poa sana ila kwa ubwege wangu sikumrudishia upendo alionionyesha nikaishia kutesa hisia zake

Sasa ameoa mimi nipo tu nazurura kama mbuzi aliekosa mchunga[emoji86]

Sent from my vivo 1906 using JamiiForums mobile app
😥😥😭 Valentina wangu..
Endelea kupumzika kwa amani mke mwenza..!!
 
Back
Top Bottom