Next Level
JF-Expert Member
- Nov 17, 2008
- 3,153
- 186
Nchi hii siku zote inaangushwa na mikoa ya Mwaza, tabora na Shinyanga. Kuna almost 75% ya wapiga kura halafu hawana uelewa wowote juu ya maswala ya kisiasa, wao bora liende.Mama yangu anamiaka 75 na kajiandikisha kupiga kura yeye naye anadai hata iweje hakuna chama kama CCM anadai je wewe mwanagu unaweza kunikataa mimi kuwa si mamako, kwake yeye CCM ndiye mama wa siasa na vyama vyote kwa hiyo vyama vingine havina nguvu au ubavu wa kushindana na chama mama.
Loh nikaishiwa hamu,nikajaribu kumueleza maovu yote yanayofanywa na CCM kwani hata muda wa kunisikiliza hakuwa nao akaniambia we mwanangu lakini kwa hilo la kuisema CCM unaenda mbali akafunga mazungumzo, kwa hiyo ni kweli hata Chadema wangekuja na ilani ya uchaguzi nzuri kiasi gani bado kuna safari ndefu kwa wananchi walio wengi kujua ilani kwanza nini au ina manufaa gani.
Tukumbuke enzi za Mkapa alisema ilani ya CCM haitekelezeki na bado tukamchagua mgomnea wa CCM kwa kishindo, ingekuwa ni nchi zingine zenye uelewa juu ya Ilani, CCM ingekuwa ishazikwa zamani kwenye kaburi futi sita ardhini.
Ni kweli kabisa MMkj, hebu angalia Majiji kama Dar na Mwanza, kama kwa huo tunaoita uelewa wao wangeonyesha nguvu zao za kura na kuukataa ubabaishaji wa CCM unadhani hali ingekuwaje? Ngome kuu za upinzani zilipaswa kuwa katika miji mikubwa na sio kama ilivyo sasa.Wananiudhi kweli watu wanaodharau "wanakijiji" wenzangu.. wakati wabunge 60 wa CCM na wengine wamebwaga na wanakijiji hao hao; ni wanakijiji hadi hivi sasa ndio wanaongoza Tanzania kwa kuchagua upinzani! Walio mjini ndio wa kulaumiwa kwa kuendelea kwa utawala wa CCM hivi sasa. Msitushakizie.
Nina wasiwasi kuwa Tanzania haina tofauti yoyote na Kenya au Zimbabwe linapokuja swala la uchaguzi. Ni bora kuhakikisha kuwa vyama vyote vinajiimarisha vya kutosha kulinda na kudhibiti na upigaji na uhesabuji wa kura kwa karibu sana.
So TRUE. God help us. But sadly , God helps those who help themselves.Changamoto kubwa ipo kwenye uelewa wa watanzania walio wengi juu ya hayo mambo ya ilani na sera za chama. Wananchi wengi hawajui hizi habari, wanachojali wamepata tshirt, khanga na kofia za kijani basi hicho ndo cha maana kwao. Pamoja na ilani hizo nzuri, hakikisheni kwamba na nyie mwaka huu mnawekeza vya kutosha kwenye mabango, tshirt, kofia na khanga. Hayo ndo mambo ya msingi zaidi kwa wananchi wa vijijini.
Kwa namna moja au nyingine ni vema mkatambua ukweli kwamba mtaji mkubwa wa CCM ni umaskini na ujinga wa watanzania. Ndiyo maana CCM haitakaa ifanye jitihada ya kumaliza umaskini nchini wala jitihada za kupunguza umaskini kwa kuwa hali hiyo ndiyo inayowafanya wao waendelee kutawala. Wanatumia ujinga wa watanzania kuelekeza chuki kwa vyama vya upinzani kwamba ni vyama vya kuleta vita. Wananchi wa kawaida wanaohofia vita hawawezi kukubali kuchagua chama kitakacholeta vita. Kunahitajika elimu na strategy zaidi kuliko sera pekee. Take care.
Mkuu Ilani ndio sababu, nia na kuonyesha uwezo wa kutaka kushika madaraka ya kuongoza nchi..
Hata kama watu wanachagua vichwa safari hii Chadema hawako nyuma sana hivyo ushindani utabakia ktk Ilani za chama. Na kama ujuavyo wananchi wana CHUKI!
Naogopa tu hiyo chuki ya hawa waitwao Wajinga waliolala, isije kuwa ni zaidi ya kura zao ikawa za Wanyamulembe..
Shida yenyewe ipo hapa!
Huwa sishtuliwi na mambo mengi ya kisiasa; lakini kama nilichokiona kwa macho yangu ndicho kitakachokuwepo kwenye Ilani ya Chadema basi naweza kusema tu kuwa ni ya "kuthubutu, inatisha na inawaweka CCM pabaya". Kama ndiyo hiyo, basi itabidi CCM warudi darasani kuandika Ilani yao upya maana kama watu watapigia kura Ilani.. basi mtanange huu wa demokrasia 'UNOGILE". Cheche za Fikra itatoka na exclusive mapema Alhamisi baada ya kuzungumza na baadhi ya viongozi wa juu wa Chadema akiwemo Bw. Freeman Mbowe, Tundu Lissu na wengine..
Mwaka huu watu watapigia kura sura au watapigia sera!
yes.. unaitwa "MTANANGE WA DEMOKRASIA"..!!! quote me!
Mwanakijiji unaenda mbali saana kwa kuwaza Ilani. Kamwe nchi hii, ilani haitaiangusha CCM. Leo hii tuulizane hapa hata kabla yakufika kule vijijini, ni nani aliisoma Ilani ya CCM ya 2005 na nani anaweza kuizungumzia utekelezaji wake! Jibu ni kuwa utashangaa saana. Wengi kati yetu tunapenda kusoma mistari miwili na kufunika na hao ndio tunajiita wasomi. Sasa, vipi kuhusu wanakijiji? Matatizo ni makubwa saana katika kujisomea kwa Taifa letu na ndio maana hata umakini hakuna. Tena basi si kusoma tu hata kuandika. Jipe fursa upitie hata magazeti yetu utashangaa. Kwahiyo binafsi naona CCM itaondoka madarakani kwa njia za kupayuka tu na kuzungumza na wananchi zaidi juu ya haki zao bila hata ya kuwaeleza ilani inasema nini!
Angalizo/Vision
Chadema wamewashinda CCM kwa kupata Kura nyingi za nafasi ya Rais, na wabunge wengi pia;
Habari mpya ni kwamba sio Chadema walioshinda, ni CCM; Kura za Tanga zilikuwa bado kuhesabiwa wakati tunatoa taarifa ya kwanza
Hilo ni Angalizo tu kwa Chadema nikimaanisha kwamba mipango yote mizuri watakayo panga 'haina maana' kama hakuna mkakati Madhubuti wa kulinda Kura, hata kama mkakati huo utawaudhi baadhi ya watu.. especially the so called 'Wanaharakati wa Human rights'
Get prepared
CHADEMA mliomo humu ndani please take this a challenge and work on it. Tengenezeni ilani version ya kuwawezesha wadanganyika wa kule namanyere kuelewa, i am sure you will defeat them. Go Slaa...