Ijue Toyota Coaster new model Fourth Generation

Bujibuji Simba Nyamaume

JF-Expert Member
Feb 4, 2009
74,427
154,271
220px-Toyota_Coaster_EX_XZB70.jpg
The fourth Generation Toyota Coaster ilitambulishwa rasmi mnamo tarehe 22 December 2016 na kuwekwa sikoni Japan kwa ajili ta mauzo tarehe 23 January 2017.
Gari hii inapatikana ikiwa na aina za injini zilezile za matoleo ya machaguo ya model zilizopita ambazo ni 3B,13B,14B,15B-T,1HZ,1HZ-T na 1HD-T.

Coaster ni gari ya kwanza kufanyiwa mabadiliko mazima ya muundo wa bodi ( full redesign ) chini ya shirika jipya la Toyota's Commercial Vehicle (CV) kampuni ambayo Ni mahsusi kwa ajili ya kubuni na kuendeleza magari ya BIASHARA.
The fourth generation Coaster imefungwa vifaa vingi vya teknolojia ya juu vya kiusalama kama standard air-bags kwa ajili ya dereva na abiria wa kiti cha mbele.

Pia gari inakuja na Vehicle Stability Control (VSC), a ringed frame body kwa ajili ya kudhibiti gari isianguke ikikata Kona ikiwa kwenye mwendokasi, pre-tensioners kwa ajili yamikanda kwenye viti na pia zimewekwa force limiters inayopunguza pressure kwenye vifua kwenye vifua vya abiria iwapo itatokea magari kugongana uso kwa uso.

220px-Toyota_Coaster_EX_XZB70_rear.jpg
Urefu wa Kimo umeongezwa kwa mm (2.4 in), Upana umeongezwa kwa 40 mm (1.6 in) na urefu wa kimo cha kioo umeongezwa kwa50 mm (2.0 in) ukilinganisha na model zilizopita.
Pia ngazi za mlangoni zilirefushwa kwa 65 mm (2.6 in) ili kufanya wepesi wakati wa kuingia na wakati wa kutoka.
Viti ndani vimeongezewa shepu na upana wa sehemu ya kukalia na ile sehemu ya kuegemeza mgongo.
Kioo cha mbele kimepanuliwa ili kumuwezesha dereva kuona kwa uzuri.
Coaster imetolewa katika configurations tatu;
  • Standard wheelbase configuration ambayo inabeba abiria 25,
  • The long wheelbase configuration inayokuja na viti vya abiria 24 au 29
  • School BUS configuration ambayo ina seat 3 za watu wazima na 49 vya watoto. The school bus configuration haina kiti Cha mbele cha abiria.
800px-三重客運KKA-8066_桃603_20181104.jpg
 
Bei sh ngapi mkuu
 
Toyota Coaster Bora ni Second Generation(Box Body) na third generation (Coaster Mayai). Unakutana na injini Kama 3B,13B,14B,15B-T,1HZ,1HZ-T na 1HD-T.

Na baadhi zilikuwa na Air suspension hizo box body na Mayai, Bujibuji nakumbuka miaka ya 2000-2008 njia ya Mbeya-Tukuyu-Kyela ilikuwa na Coaster nyingi zenye air suspension zilikuwa zimenyanyuliwa nyuma ilikuwa ni mbio za kutisha na njia ya Tukuyu Ina Kona Kali na ukungu, hizo 1HD-T zilipiga Sana chini hiyo njia kutokana na madereva kukimbia Sana.
 
Toyota Coaster Bora ni Second Generation(Box Body) na third generation (Coaster Mayai). Unakutana na injini Kama 3B,13B,14B,15B-T,1HZ,1HZ-T na 1HD-T.

Na baadhi zilikuwa na Air suspension hizo box body na Mayai, Bujibuji nakumbuka miaka ya 2000-2008 njia ya Mbeya-Tukuyu-Kyela ilikuwa na Coaster nyingi zenye air suspension zilikuwa zimenyanyuliwa nyuma ilikuwa ni mbio za kutisha na njia ya Tukuyu Ina Kona Kali na ukungu, hizo 1HD-T zilipiga Sana chini hiyo njia kutokana na madereva kukimbia Sana.
Kulikuwa na moja inaitwa MV Saratoga, aisee ilikuwa Ni zaidi ya moto
 
Hiyo kama haijanunuliwa haijanunuliwa na Serikali, Basi tutegemee kuiona miaka kumi na tano ijayo, Tena na teknolojia itakuwa imebadilika, maana saa hizi wengi wanahamia kwenye renewable energy vehicles
Huu uthibitisho wa Nissan Civilian ni gari mbovu, au Mitsubishi Rosa sio imara mmeutoa wapi?
 
15 Reactions
Reply
Back
Top Bottom