Ijue sheria ya viboko mashuleni

moyafricatz

JF-Expert Member
Nov 27, 2015
2,900
4,865
Kifungu cha 61(1)(v) Cha Sheria ya Elimu Sura ya 353 marejeo ya mwaka 2002, kinampa mamlaka waziri wa Elimu kutunga kanuni za masuala mbalimbali zitakayokidhi utekelezaji wa masuala ya sheria hiyo.

Mojawapo ya kanuni zilizotungwa ni The Education (Corporal Punishmemt ) Regulation G.N.294 ya mwaka 2002.

Kanuni hizi zinatoa mwongozo ni wakati gani adhabu ya viboko inatakiwa kutolewa na kwa kiwango gani kanuni ya 3(1) inasema athabu ya viboko itatolewa iwapo patatokea utovu mkubwa wa nidhabu au kosa kubwa litakalofanywa ndani au nje ya shule amabalo litailetea litaishushia shule heshima.

Kanuni ndogo ya (2) inasema adhabu ya viboko itolewa kwa kuzingatia umri, jinsia na afya ya mwanafunzi na isizidi viboko 4 kwa tukio lolote.

Nani Ana mamlaka ya kumchapa mwafunzi.

Sheria inamtaka mwalimu mkuu wa shule husika kutoa adhabu ya viboko au kukasimisha mamlaka yake kwa umakini mkubwa kwa mwalimu yeyote kutoa adhabu hiyo.Mwalimu anayechaguliwa kutoa adhabu atakuwa na mamlaka ya kutoa adhabu pale tu atakapopata idhini ya mwalimu mkuu katika tukio husika.

Kanuni ya (5) inataka kila adhabu ya viboko inapotolewa kwa mwanafunzi kumbukumbu ya kutolewa kwa adhabu hiyo sharti iwekwe kwenye kitabu, ikitaja jina la mwanafunzi,kosa alilolifanya,idadi ya viboko na jina la mwalimu aliyetoa adhabu. Na kumbukumbu hizo lazima zisainiwe na Mkuu wa shule.

MY TAKE :
Walimu tusiongozwe na hasira katika kuadhibu watoto kwa makosa ambayo pengine hayahitaji adhabu ya viboko.
 
Tulikua na mwalim akiitwa moja kubwa
Yaani yeye adhabu yake ni fimbo moja tu lakini hasira,jazba na nguvu zote anamalizia akiivutia fimbo kasi ya kukuchapa
 
Hapo kwenye kurekodi sijui idadi ya fimbo alizochapwa,jina la mwalimu aliyemchapa na hilo la idadi ya fimbo 4 hayafanyikagi hayo
 
Walimu wengi Wa sasa wanaijua sana hiyo sheria ndo maana siku hizi wanafunzi wanafanya watakavyo mbele ya Mwalimu na Mwalimu anawachekea tu na wala hawana muda kabisa Wa kukimbizana na mtoto Wa MTU. Utaanza kusema walimu Wa siku hizo bwana wana urafiki sana na wanafunzi sasa unataka wafanyeje? Sasa hivi Mwanafunzi kama akupendi anaweza kukusingizia chochote hadi ukaozea jera.
Walimu endeleeni kufanya mambo yenu nyinyi Wa kwenu pelekeni Private penye Elimu bora na waache maskini mnaotaka kusaidia watoto waendelee kufuata hizi sheria.

Mtoto Wa siku hizi kwa sheria hizi ni uchawi bora kwake.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Walimu wengi Wa sasa wanaijua sana hiyo sheria ndo maana siku hizi wanafunzi wanafanya watakavyo mbele ya Mwalimu na Mwalimu anawachekea tu na wala hawana muda kabisa Wa kukimbizana na mtoto Wa MTU. Utaanza kusema walimu Wa siku hizo bwana wana urafiki sana na wanafunzi sasa unataka wafanyeje? Sasa hivi Mwanafunzi kama akupendi anaweza kukusingizia chochote hadi ukaozea jera.
Walimu endeleeni kufanya mambo yenu nyinyi Wa kwenu pelekeni Private penye Elimu bora na waache maskini mnaotaka kusaidia watoto waendelee kufuata hizi sheria.

Mtoto Wa siku hizi kwa sheria hizi ni uchawi bora kwake.

Sent using Jamii Forums mobile app
Sheria zimewekwa ili zifuatwe kuvunja sheria ndo kunasababisha hata kuua wanafunzi kwa viboko

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sheria Bongo...... Mtasubiri sana, mwanao atachapwa hadi atasahau jina lake

Sent using Jamii Forums mobile app
Ni kama ile sheria inayodai kuwa askari polisi kabla ya kukukamata kwa kosa lolote ni sharti ajitambulishe majina yake kamili, namba yake na cheo chake na sababu yakukukamata. Na ukifikishwa jituoni unawezajidhamini mwenyewe kulingana na kosa na pia ufikishwe mahakamani ndani ya 24h

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkiua mnasema "bahati mbaya" ????

Sent using Jamii Forums mobile app
acheni uoga.....kupigwa na kufa au kuua sio mpango wa mwalim.....anyway ...ambaye ni mwalim wa shule ya secondary au ya msingi ajibu hapa : lengo kuu la adhabu ni nini? unajua wengi wenu mko nje ya field ya ualim....ngoja niwatolee mfano mmoja....mwaka 2016 nilkuwa field ya ualim shule flan ya sekondar DSM ...mara kaletwa bint wa f4 aliyemgomea mwalm kutoka darasan katika kipindi cha commerce na wakati yeye hasomi. katika kumuhoji akadai " mimi sioni kama ni kosa kumgomea mwalim kutoka darasani hata kama sisomi kipindi hicho" basi tulimchapa bakola 100++ mpaka akakiri kua n kosa na kuomba radhi ...heshima ikarudi.... msikopi Ulaya kila kitu.!!!! hii ni Afrika
 
acheni uoga.....kupigwa na kufa au kuua sio mpango wa mwalim.....anyway ...ambaye ni mwalim wa shule ya secondary au ya msingi ajibu hapa : lengo kuu la adhabu ni nini? unajua wengi wenu mko nje ya field ya ualim....ngoja niwatolee mfano mmoja....mwaka 2016 nilkuwa field ya ualim shule flan ya sekondar DSM ...mara kaletwa bint wa f4 aliyemgomea mwalm kutoka darasan katika kipindi cha commerce na wakati yeye hasomi. katika kumuhoji akadai " mimi sioni kama ni kosa kumgomea mwalim kutoka darasani hata kama sisomi kipindi hicho" basi tulimchapa bakola 100++ mpaka akakiri kua n kosa na kuomba radhi ...heshima ikarudi.... msikopi Ulaya kila kitu.!!!! hii ni Afrika
STUPID.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom