Adhabu ya viboko ifutwe mashuleni: Madhara yake hayadhibitiki

GODZILLA

JF-Expert Member
Dec 26, 2014
5,902
10,503
Sijui ni mpaka lini tu hizi adhabu za kinyama zitafutwa mashuleni?

Maana ni kama vile hakuna anayeona madhara yake japo kila siku tunashuhudia watoto na wanafunzi wakiuliwa na walimu mashuleni.

Tulishakuwa na sheria inayotoa mwongozo wa utoaji wa viboko lakini haizingatiwi kabisa, kitu ambacho kinaleta hatari kubwa juu ya usalama wa watoto mashuleni.

Hatuwezi kuwa kila mara tunasubiri mwanafunzi auwawe ndipo tuanze kutoa matamko wakati uwezo wa kudhibiti huu unyama dhidi ya watoto tunao.

Ndani ya miezi saba tu tangu mwaka 2023 uanze imeripotiwa kutokea vifo zaidi ya saba vya watoto mashuleni kutokana na vipigo vya walimu.

Hatuwezi kuendelea na huu uhuni. Ni wazi sheria inayotoa mwongozo wa viboko imeshindwa kufanya kazi, hivyo ifutwe moja kwa moja kwa mustakabali wa watoto wetu.

Natoa rai kwa serikali ione ulazima wa haraka wa kufuta viboko na kumaliza mauaji ya watoto mashuleni.

Naambatanisha uthibitisho.
 
.
IMG-20230802-WA0040.jpg
 
Maticha most of them hawajielewi kabisaa

Waendelee kuvaa mikadeti iliopauka pauka
Sijui wana matatizo gani hawa!

Walishaelekezwa na waraka unaotoa mwongozo wa viboko lakini hawaufuati hata kidogo. Matokeo yake ni kuua watoto.

Sheria inasema viboko vitolewe panapotokea KOSA KUBWA LA KINIDHAMU.

Lakini ni nini haswa KOSA KUBWA LA KINIDHAMU? Sheria haisemi, na matokeo yake mtoto hata akiongea darasani anashambuliwa kwa viboko kama mnyama.

Sheria inasema mtu pekee mwenye ruhusa ya kuchapa mtoto ni MWALIMU MKUU, tena kwa vigezo na masharti maalumu.

Kwa kuwa wameshindwa kufuata utaratibu, basi hizi adhabu ziondolewe mara moja.
 
Wangekuwa wanafuata miongozo ya fimbo nne mimi sioni shida, tatizo wanapitiliza mpaka wanafanya mauaji. Na ukifuatilia wengi hata kama hayajatokea mauaji wengi wanapiga kupitiliza....bora fimbo zitolewe kabisa tujue moja, I agree with you mtoa mada.
Vipigo kwa watoto ni vikali sana mashuleni, tena kwa makosa ambayo hata si makosa kiuhalisia.

Hata sheria yenyewe nayo inachangia kuleta matatizo makubwa zaidi.

Sheria inasema, adhabu ya viboko itatolewa na MWALIMU MKUU TU kwa vigezo maalumu endapo mwanafunzi atatenda KOSA KUBWA LA KINIDHAMU.

Lakini KOSA KUBWA LA KINIDHAMU ni LIPI HASWAA? Sheria haisemii.

Matokeo yake mtoto hata akinong'ona darasani anashambuliwa kwa viboko visivyo na idadi.

Walimu hawafuati miongozo, lakini hata sheria nayo ni BUTU na inatoa mianya ya kuleta matatizo. Ifutwe kabisa moja kwa moja.
 
Kiukweli walimu wengi wanafeli kufuata miongozo ya kutoa adhabu kwa wanafunzi,matokeo yake wanaleta madhara kama vifo,majeraha kwa wanafunzi.Naunga mkono hoja.

Japokuwa watoto wa siku hizi wabishi sana haiwapi Walimu ruhusa kuwaadhibu hovyo hovyo na kuleta madhara.
Walimu pia wasilete hasira za nyumbani mashuleni ni hatari.
 
Wangekuwa wanafuata miongozo ya fimbo nne mimi sioni shida, tatizo wanapitiliza mpaka wanafanya mauaji. Na ukifuatilia wengi hata kama hayajatokea mauaji wengi wanapiga kupitiliza....bora fimbo zitolewe kabisa tujue moja, I agree with you mtoa mada.
Tuunge.mkono 100%,inasikitisha sana.Mbona watoto wa kizungu hawapigwi?Na pia nchi za kiarabu hawapigwi wanafunzi.
 
Sijui wana matatizo gani hawa!

Walishaelekezwa na waraka unaotoa mwongozo wa viboko lakini hawaufuati hata kidogo. Matokeo yake ni kuua watoto...
Yule mwalimu James, aliyempiga mtoto wa darasa la kwanza,mtoto wa miaka 7,mimi simjui huyu mtoto,lakini nimeumia sana. Pengine angekuja kuwa Daktari bingwa.

Vipi mwalimu mtu mzima unampiga mtoto wa miaka 7,mpaka unamuua.
 
Back
Top Bottom