jayspol malika
Member
- Jan 19, 2017
- 14
- 28
Kwa wengi msioifahamu Mwanza jiji ( Mwanza city) au The Rock City , ni jiji la pili Tanzania baada ya jiji la Dar es salaam.
Jiji hili lilipewa hadhi ya kuwa Manispaa mwaka 1978 na mwaka 2002 tarehe 07 mwezi wa 07 likapandishwa hadhi ya kuwa jiji la Mwanza , lenye wilaya mbili za Ilemela na Nyamagana na jumla ya kata 20, 9 Ilemela na 11 Nyamagana . Nyamagana ndio yalipo makao makuu ya jiji la Mwanza.
UTAWALA
Baada ya jiji la Mwanza kupanuka , liligawanywa sehemu mbili yaani halmashauri ya jiji la Mwanza yenye wilaya moja ya nyamagana, hapo kuna mkurugenzi wa halmashauri ya jiji la Mwanza, mkuu wa wilaya ya Nyamagana pia halmashauri ya Manispaa ya Ilemela yenye wilaya ya Ilemela , Kuna mkurugenzi wa halmashauri ya manispaa ya Ilemela, mkuu wa wilaya wa wilaya ya Mwanza.
Hapo Ni kiutawala tu lakini huwezi kuitenganisha Mwanza ( Ilemela na Nyamagana) zilizokuwa tarafa za halmashauri ya manispaa ya Mwanza hadi mwaka 2002.
IDADI YA WATU
Kwa sasa tunasubiri takwimu za watu na makazi za mwaka 2022, hata hivyo inakadiriwa kuwa na watu milioni tatu hadi sasa.
VYANZO VYA MAPATO
Biashara, kilimo na ufugaji, kwa takwimu za mwaka huu hadi kufikia mwezi wa 6 mwaka huu halmashauri ya jiji imeweza kuchangia Tsh bilioni 17 Kama pato la ndani huku halmashauri ya Manispaa ya Ilemela ikichangia Tsh bilioni 10 na kufanya Mwanza jiji kuchangia Tsh bilioni 27 kwa mujibu wa TAMISEMI.
ELIMU
Jiji la Mwanza lina vyuo vikuu kamili viwili , vyenye makao yake makuu jijini Mwanza yaani SAINT AUGUSTINE UNIVERSITY OF TANZANIA ( SAUT) na CATHOLIC UNIVERSITY OF HEALTH AND ALLIEND SCIENCE ( CUHAS) zamani au maarufu Weill Bugando University vyote vinamilikiwa na kanisa katoliki Tanzania kupitia TEC ( Tanzania Episcopal Conference) , hakuna chuo kikuu cha serikali jijini Mwanza ( Serikali Sasa ione umuhimu kujenga chuo kikuu Mwanza, University of Mwanza, ( UoM) kiweze kushinda na UdSm, UDOM, na Nelson Mandela.
WENYEJI
Wenyeji wa jiji la Mwanza ni kabila la Wasukuma ( Wang'weri) , yaani wasukuma wa magharibi .
Karibuni jijini Mwanza kwa fursa mbalimbali.
Imeandikwa na mimi Malika.
Kwa maoni ushauri, karibuni kwenye uzi.
Jiji hili lilipewa hadhi ya kuwa Manispaa mwaka 1978 na mwaka 2002 tarehe 07 mwezi wa 07 likapandishwa hadhi ya kuwa jiji la Mwanza , lenye wilaya mbili za Ilemela na Nyamagana na jumla ya kata 20, 9 Ilemela na 11 Nyamagana . Nyamagana ndio yalipo makao makuu ya jiji la Mwanza.
UTAWALA
Baada ya jiji la Mwanza kupanuka , liligawanywa sehemu mbili yaani halmashauri ya jiji la Mwanza yenye wilaya moja ya nyamagana, hapo kuna mkurugenzi wa halmashauri ya jiji la Mwanza, mkuu wa wilaya ya Nyamagana pia halmashauri ya Manispaa ya Ilemela yenye wilaya ya Ilemela , Kuna mkurugenzi wa halmashauri ya manispaa ya Ilemela, mkuu wa wilaya wa wilaya ya Mwanza.
Hapo Ni kiutawala tu lakini huwezi kuitenganisha Mwanza ( Ilemela na Nyamagana) zilizokuwa tarafa za halmashauri ya manispaa ya Mwanza hadi mwaka 2002.
IDADI YA WATU
Kwa sasa tunasubiri takwimu za watu na makazi za mwaka 2022, hata hivyo inakadiriwa kuwa na watu milioni tatu hadi sasa.
VYANZO VYA MAPATO
Biashara, kilimo na ufugaji, kwa takwimu za mwaka huu hadi kufikia mwezi wa 6 mwaka huu halmashauri ya jiji imeweza kuchangia Tsh bilioni 17 Kama pato la ndani huku halmashauri ya Manispaa ya Ilemela ikichangia Tsh bilioni 10 na kufanya Mwanza jiji kuchangia Tsh bilioni 27 kwa mujibu wa TAMISEMI.
ELIMU
Jiji la Mwanza lina vyuo vikuu kamili viwili , vyenye makao yake makuu jijini Mwanza yaani SAINT AUGUSTINE UNIVERSITY OF TANZANIA ( SAUT) na CATHOLIC UNIVERSITY OF HEALTH AND ALLIEND SCIENCE ( CUHAS) zamani au maarufu Weill Bugando University vyote vinamilikiwa na kanisa katoliki Tanzania kupitia TEC ( Tanzania Episcopal Conference) , hakuna chuo kikuu cha serikali jijini Mwanza ( Serikali Sasa ione umuhimu kujenga chuo kikuu Mwanza, University of Mwanza, ( UoM) kiweze kushinda na UdSm, UDOM, na Nelson Mandela.
WENYEJI
Wenyeji wa jiji la Mwanza ni kabila la Wasukuma ( Wang'weri) , yaani wasukuma wa magharibi .
Karibuni jijini Mwanza kwa fursa mbalimbali.
Imeandikwa na mimi Malika.
Kwa maoni ushauri, karibuni kwenye uzi.