Elections 2010 Igunga: Mbunge kunywa sumu CCM ikishindwa

jamani living stone lusinde babo ana fikra za zamani..!

Kampeni za uchaguzi mdogo katika jimbo la igunga, zimezidi kupamba moto baada ya mbunge wa mtera, livingstone lusinde (ccm), kujiapiza mbele ya wananchi kuwa atakunywa sumu iwapo chama hicho kitashindwa kwenye uchaguzi huo.

Akizungumza na wanakijiji wa ugaka kwenye kata ya nkinga wilayani hapa wakati akimwombea kura mgombea wa ccm, dk. Peter kafumu, lusinde alisema kutokana na mwenendo mzuri wa kampeni za ccm na jinsi wanavyowafikia wananchi, haoni sababu za kushindwa kwenye uchaguzi huo.

“hapa nimewaona waandishi wa gazeti la mbowe (mwenyekiti wa taifa wa chadema); nataka mkaandike kwa namna ambavyo tumezunguka, ccm tukishindwa nakunywa sumu,” alisema na kuongeza:

“nataka tuwaambie, tutawapiga bao la mbali kabisa na huyo dk. Slaa sisi tunammudu ndiyo maana tukamwambia mzee kikwete, endelea kuongoza nchi atuache vijana tumkabe koo maana yule mzee ni mnafiki mkubwa,” alisema lusinde.

“kale kazee kagonjwa kale, ndiyo maana nimekuja kuwaambia inawezekana viongozi wa chadema wanavuta bangi, zile bangi zile, haiwezekani unatembea nchi nzima unahamasisha vurugu, unatangaza vita,” alisema lusinde mjumbe wa halmashauri kuu (nec) ya ccm.

Kwa upande wake mratibu wa kampeni hizo, mwigulu mchemba, aliwataka wananchi hao kumchagua dk. Kafumu na kusema wanasiasa wa upinzani wanasema tangu uhuru serikali ya ccm haijafanya kitu kabisa, igunga haijapata maendeleo wakati si kweli.

“wenzetu wanapandikiza chuki kwa vijana wa vyuo vikuu nao wanakubali kupotoshwa na wanasema serikali ya ccm haijafanya kitu si kweli. Kwanza idadi ya wanafunzi wa vyuo vikuu imeongezeka halafu wanasema rais huyu hajafanya kitu, kama si kulaaniwa ni nini?” alihoji.

Alisema wapinzani wanatumia umaskini wa wananchi kama mtaji wa kisiasa, wamelalamikia kupandishwa kwa bei ya pamba ili watu wakasirike na kutoichagua ccm.

“wacha niwaambie wakati wa ukame serikali ya ccm iligawa chakula jimbo lilipokuwa wazi wakasema tusigawe chakula eti hiyo ni rushwa sasa tusipogawa chakula mtatuchagua? Hivi njaa ina likizo? Kwa nini serikali ipeleke chakula mpaka somalia lakini igunga ibaki na njaa hivi mtapiga kura mkiwa na njaa?” alihoji mwigulu.

kweli hii ni nchi ya wadanganyika kama hizi hoja ndiyo za kushinda uchaguzi.
 
tunepewa macho mawili, ili tuone sana,
tumepewa masikio mawili, ili tusikie sana
tumepewa matundu mawili ya pua, ili tunuse sana,
tumepewa vidole kumi, ili tuguse na kutambua tushikasho
tumepewa mdomo mmoja ili tunachoona, tunachosikia, tunachonusa na kushika tusikiseme sana.


asije akajutia aliyoyasema
 
Mhe. Lusinde, chondechonde, ulimi ni kiungo kidogo lakini mambo yake ni makubwa! Wewe ni Mbunge, na tunategemea wananchi waliokuchagua wanakutegemea kwa uwakilishi zaidi, na kujenga hoja za maendeleo kwa wao waliokuchagua lakini zaidi kwa watanzania wote, kwani kuuingia pale Bungeni, tayari unakura nzito ktk masuala yote ya mustakabali wa sheria za nchi hii. Sasa hayo maneno unayoongea unavuka mipaka na kutaka kumjaribu Muumba (MUNGU), si busara kabisa kwa Mhe Mbunge kuonyesha kutofahamu ukomo wa meneno yako, MUNGU hajaribiwi na kwa MUNGU kaauli huumba. Hembu omba sala ya toba kabla ya Uchaguzi, kwani unaweza kuyapata ya ajabu kwa kauli yako hiyo na tena si lazima iwe mara baada ya uchaguzi huu, kwani MUNGU hutenda kwa muda wake. Take Care!
 
Mwigulu anathibitisha kuwa CCM haina mvuto tena kwa wasomi,anasema CDM inawadanganya na kuwatumia vijana wa vyuo vikuu!hivi kweli mwingine akiwa na wafuasi wa vyuo vikuu na mwingine akawa na wafuasi kijijini ni nani anaweza kuwa amewapata wafuasi wake kwa kuwadanganya kwa chumvi?na hili la CCM kutokuwa na mvuto vyuo vikuu ni kweli kabisa!wakati ule wa mdahalo wa katiba mpya UDOM CCM iliweka ghiriba wanachuo kutoingia lakini yaliyotokea ya maelfu ya wana chuo kuvamia ukumbi na kuziba barabara ikafahamika LEMA alionekana UDOM siku moja kabla nae alikiri kuwa nao wanastahili.SLAA alifanya mkutano mmoja kwa ajili ya ufunguzi wa Tawi la MABIBO HOSTEL zinazo tumiwa na wanachuo wa UDSM vijana walifurika sanaaaaa!Lakini CCM leo hawawezi kufanya mkutano chuo kikuu chochote maana wanajua watavuna aibu.UVCCM walijaribu kuandaa maandamano ya wanavyuo eti bodi ya mikopo ivunjwe waliachana na mpango huo baada ya watu wao kurudisha ripoti kuwa watavuna aibu.So ni swala la muda tu hawa vijana wa vyuo watakapomaliza kuwaelimisha baba zao,vijana wenzao,mama zao hakika CCM itaondoshwa.NAPE KAMA HAYA NI UONGO ANDAA MKUTANO UDSM,UDOM
 
Huyu alifaha kuwa na kundi la kina masanja TBC1, au waunde bunge komed jamaa anafaa.
 
khaa! CCM wameishiwa hadi kumkodi huyu Lusinde? Angalia aliyoyasema sasa. Kwa wenye akili timamu watajua hafai na hivyo anapunguza kura za dr. Kafumu badala ya kuziongeza.
Poleni CCM

Tatizo lao walidhani kwa kuwa kamng'oa Tingatinga, basi anaweza kubeba mikoba yake, kumbe anachemsha. Ningewashauri wakamwangukie mzee malecela kama walivyofanya kwa Rostam ili aje aokoe jahazi
 
Mungu alimwumba mwanadamu kwa mfano wake..akasema enenda ukaijaze nchi na kutawala vilivyomo...naacha huu ujumbe kwa Lusinde..kunywa sumu ni kutawala??????? Mbona ccm mazezeta hivi???
 
mimi watu kama hawa huwa siwajadiri bila kujua level yao ya elimu,so mwanaJF yeyote alie na CV yake au anaejua level ya elimu yake basi anitumie kwenye email hii: paulchengula@gmail.com, coz unaweza ukamtoa kasoro kwa pumba zake kumbe unamuonea,ila nadhani atakua ni darasa la pili B,coz simuelewi kabisa.............................!
 
Naona hapa CCM kupitia kwa Lusinde wanatia presha kwa msimamizi wa uchaguzi kuhakikisha kuwa CCM inashinda Igunga. Guess what, wana Igunga wanaamini HAKI yao ina thamani kuliko UHAI wa Lusinde.
Lusinde naona naye anatumia masaburi kwenye spichi zake, yaani yeye anafikiri wana Igunga wanamthamini Lusinde kuliko maisha na haki zao. Huu ni UZOBA mwingine wa Magamba.
 
Wapi mesie, wapi jibarati, wapi mwita25.. meenda wapi nyinyi??.. naacha kazi ya kurukiarukia threads.. au "wakubwa" wamegoma kuwapa posho!! manake sijaowaona katika thread hii.. Unajua nini, Nyie mlikuwa malimbukeni, mlilipwa kwa ajili ya kudandia na kukoroga kila thread ya Igunga, naskia Juzi Bosi wenu kaitwa "Ofisi kuu" ametukanwa huyo kama mtoto mdogo na "wazee".. kisa kwanini alikwenda Igunga bila ruksa.. kitendo kilichomghadhibisha mzee mkapa.. baada tu ya kufungua kampeni akatimka zake.. nani aiibike. naskia Bosi wenu kenda zake Nairobi akatulize kichwa.. mna kazi nyie.. mie niliwaambia acheni mambo hayo.. ooo mkaniona nawazibia rizki.. sasa kiko wapi? aibu.. na Tukikasirika zaidi tunawataja kwa majina na FB zenu..

Chama hakiongozwi na Posho na vibahasha.. vina mwisho.. vikiisha unachanganyikiwa na kuwa muasi wa kutisha. halafu unajua nini, nyie mlikurupukia threads, mkazijibu bila hoja.. haipendeeeeezi.. Kweli kama chama kilikuwa na Mbinu hiyo basi kingewatafuta wajenga hoja na kuwamwaga JF.. Ila wenye hoja wote hawanunuliki.. ni wazalendo halisia.

Kwa Lusinde, mie nilitegemea watoto hufuata busara za Wakubwa.. balozi wetu mstaafu na mmojawapo wa mawaziri wa iliyokuwa Tanganyika wakati wa Nyerere, Mzee Job Lusinde.. kwenye
(Lusinde: Watuhumiwa ufisadi wafukuzwe) amefafanua kwa Undani uozo ambao kwa sasa umo ndani ya Chama tawala sitaki kuongelea huko sana ila nilitegemea vijana kama kina Livingstone Lusinde, Nappe nauye (Moses Nauye) na wengine waliodumbukia ndani ya chama... wangefuata Nyayo za wazee wao hao, na wangefafanua sababu hasa za mzigo huu wa matatizo ya wananchi sambamba na maadhimisho ya miaka 50 ya uhuru (kama sio wa kiintelijensia), na kuunganisha na Tija ya kuwataka wananchi wamchague mbunge "wake" huko Igunga, zaidi ya Kuropoka matusi tena hadharani..
Mimi simlaumu Sana Lusinde, na si kwamba elimu inamfanya awe mropokaji.. kichwa yake tu mbovu huyo kijana.. sasa kwanini "Chama hicho" wampe posho ya milioni 2,670,000 kwa siku tatu kwenda Igunga kumnadi mgombea wa chama chao, Mtu mwenye kichwa kama hicho.. sisi tuamini vipi basi.. kwamba KK yote ya Chama hicho vichwa vyao ni "Shake before use!!".. in that case then.. kwa kuwa chama hushika hatamu!! basi HATAMU limeshikwa na watu wa aina hiyo.. oooh my goodness Tanzania
 
Sina uhakika sana, maybe i have to conferm with my law knowledge but i think ni kosa kutishia kujiua mbele ya jamii,
I stand to be corrected
 
Sina uhakika sana, maybe i have to comferm with my law knowledge but i think ni kosa kutishia kujiua mbele ya jamii,
I stand to be corrected
 
Jamani Living stone Lusinde Babo ana fikra za zamani..!

KAMPENI za uchaguzi mdogo katika jimbo la Igunga, zimezidi kupamba moto baada ya Mbunge wa Mtera, Livingstone Lusinde (CCM), kujiapiza mbele ya wananchi kuwa atakunywa sumu iwapo chama hicho kitashindwa kwenye uchaguzi huo.

Akizungumza na wanakijiji wa Ugaka kwenye kata ya Nkinga wilayani hapa wakati akimwombea kura mgombea wa CCM, Dk. Peter Kafumu, Lusinde alisema kutokana na mwenendo mzuri wa kampeni za CCM na jinsi wanavyowafikia wananchi, haoni sababu za kushindwa kwenye uchaguzi huo.

“Hapa nimewaona waandishi wa gazeti la Mbowe (Mwenyekiti wa Taifa wa CHADEMA); nataka mkaandike kwa namna ambavyo tumezunguka, CCM tukishindwa nakunywa sumu,” alisema na kuongeza:

“Nataka tuwaambie, tutawapiga bao la mbali kabisa na huyo Dk. Slaa sisi tunammudu ndiyo maana tukamwambia Mzee Kikwete, endelea kuongoza nchi atuache vijana tumkabe koo maana yule mzee ni mnafiki mkubwa,” alisema Lusinde.

“Kale kazee kagonjwa kale, ndiyo maana nimekuja kuwaambia inawezekana viongozi wa CHADEMA wanavuta bangi, zile bangi zile, haiwezekani unatembea nchi nzima unahamasisha vurugu, unatangaza vita,” alisema Lusinde Mjumbe wa Halmashauri Kuu (NEC) ya CCM.

Kwa upande wake mratibu wa kampeni hizo, Mwigulu Mchemba, aliwataka wananchi hao kumchagua Dk. Kafumu na kusema wanasiasa wa upinzani wanasema tangu uhuru serikali ya CCM haijafanya kitu kabisa, Igunga haijapata maendeleo wakati si kweli.

“Wenzetu wanapandikiza chuki kwa vijana wa vyuo vikuu nao wanakubali kupotoshwa na wanasema serikali ya CCM haijafanya kitu si kweli. Kwanza idadi ya wanafunzi wa vyuo vikuu imeongezeka halafu wanasema Rais huyu hajafanya kitu, kama si kulaaniwa ni nini?” alihoji.

Alisema wapinzani wanatumia umaskini wa wananchi kama mtaji wa kisiasa, wamelalamikia kupandishwa kwa bei ya pamba ili watu wakasirike na kutoichagua CCM.

“Wacha niwaambie wakati wa ukame serikali ya CCM iligawa chakula jimbo lilipokuwa wazi wakasema tusigawe chakula eti hiyo ni rushwa sasa tusipogawa chakula mtatuchagua? Hivi njaa ina likizo? Kwa nini serikali ipeleke chakula mpaka Somalia lakini Igunga ibaki na njaa hivi mtapiga kura mkiwa na njaa?” alihoji Mwigulu.

Naomba kujua tu level ya shule ya Lusinde ili tumfahamu mtu tunayemjadili inaweza kuwa ndio uwezo wake wa kufikiri umeishia hapo! Mtu makini hawezi kuanza kujiapiza badala ya kueleza sera za chama chake! Hapa nimeamini CCM hawana hoja wala jipya lolote na imejaa mavuvuzela tu!!!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom