DOKEZO IGP Wambura tunaomba ingilia Kati hili linaloendelea kwenye hiki Kituo cha Polisi Tabata Relini

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'

Master Legendary

JF-Expert Member
Apr 28, 2013
549
785
Tuma timu yako kwa namna inayofaa leo tarehe 01.10.2023 wakajiridhishe namna Trafic wanavyokomoa Madereva hasa wa Bajaji katika eneo hilo.

Leo nimepita Mandela Road Dar es Salaam nimeona operesheni kali madereva wa Gari wanakamatwa na wengine watu wazima wanafokewa na kujibiwa vibaya kwa kiburi, Dharau na udhalilishaji kama watoto wadogo katika kituo cha Polisi Tabata Relini, usimamizi wa sheria umegeuka Vita pale.

Makosa yenyewe nimeyaangalia mengi yanahitaji Elimu tu lakini watu wanakomolewa wanaandikiwa tu notification kama watu wametumwa kufikia Target flani ya Makusanyo bila kuangalia chochote.

Upokeaji wa Rushwa eneo lile ni wa kiwango cha kutisha,Trafic anaongea waziwazi kwa Dereva kwamba chini ya Elfu 10 hapokei hata kabla Dereva hajamwambia habari za Rushwa hii ni hatari.

Kuna Trafic mmoja mwanamke namba zake zina 88 mbili mkononi kavaa Smart Watch na Bracelet ni hatari kwa Rushwa,kukomoa na Majibu ya hovyo kwa Madereva, anafanya kazi kwa vitisho na vurugu kama mtu ambaye ameshatumia kilevi au kisaikolojia ana matatizo makubwa.

Naona huyu Dada anatumia sana Sticker ya Nenda kwa Usalama kama kosa kubwa sana,kwanini Polisi wasiweke Sheria vizuri kama hilo ni kosa kubwa kiasi hicho zikapatikana palepale kituoni gari ikakaguliwa hapohapo mtu akalipia akapewa badala ya kutumia Rungu la Faini tu kwa kila kitu,rungu la Elimu na Uhamasishaji liko wapi?

Ieleweke hali ya Maisha ni ngumu kumlipisha Dereva wa Bajaji Faini makosa mawili au matatu kwa pamoja asubuhiasubuhi ambayo ukiyaangalia ni makosa ambayo yanahitaji tu Elimu, tukumbuke kumfanyia hivyo umefanya siku nzima afanye kazi bure umemuumiza yeye umeumiza hadi Familia yake ,hii siyo nzuri inazidisha sana Chuki ya Raia kwa Jeshi la Polisi.

Kwa nia njema IGP liangalie hili.
 
Rushwa na Polisi ni jambo la kawaida sana hasa Trafik wapo tayari kwa lolote mradi wachukue Rushwa. Juzi nilikamatwa pale Salenda na Trafik mmoja mwanamama kala mkorogo wa haja, nikaongea nae vizuri sana gari halikuwa na tatizo kbs lakini cha ajabu akalazimisha kosa. IGP Wambura ni lazima atengeneze mfumo wa kukamata hawa Trafik wala rushwa. Kimara stopova ukipita tu taa wapo mtu unajiuliza wanafanya nini? Hawa wa hapa Ova ni walarushwa hatari.
 
Hizo sadaka wanazo kusanya hao omba omba na wakubwa zao Wana mgao wao na hua wanapewa malengo ya kiasi kinacho hitajika Kila siku, ndio maana hua hawana woga wakiwa wanafanya huo upuuzi, haya malalamiko yako kwao ni kama kilio cha samaki machozi yanakwenda na maji
 
Tuma timu yako kwa namna inayofaa leo tarehe 01.10.2023 wakajiridhishe namna Trafic wanavyokomoa Madereva hasa wa Bajaji katika eneo hilo.

Leo nimepita Mandela Road Dar es Salaam nimeona operesheni kali madereva wa Gari wanakamatwa na wengine watu wazima wanafokewa na kujibiwa vibaya kwa kiburi, Dharau na udhalilishaji kama watoto wadogo katika kituo cha Polisi Tabata Relini, usimamizi wa sheria umegeuka Vita pale.

Makosa yenyewe nimeyaangalia mengi yanahitaji Elimu tu lakini watu wanakomolewa wanaandikiwa tu notification kama watu wametumwa kufikia Target flani ya Makusanyo bila kuangalia chochote.

Upokeaji wa Rushwa eneo lile ni wa kiwango cha kutisha,Trafic anaongea waziwazi kwa Dereva kwamba chini ya Elfu 10 hapokei hata kabla Dereva hajamwambia habari za Rushwa hii ni hatari.

Kuna Trafic mmoja mwanamke namba zake zina 88 mbili mkononi kavaa Smart Watch na Bracelet ni hatari kwa Rushwa,kukomoa na Majibu ya hovyo kwa Madereva, anafanya kazi kwa vitisho na vurugu kama mtu ambaye ameshatumia kilevi au kisaikolojia ana matatizo makubwa.

Naona huyu Dada anatumia sana Sticker ya Nenda kwa Usalama kama kosa kubwa sana,kwanini Polisi wasiweke Sheria vizuri kama hilo ni kosa kubwa kiasi hicho zikapatikana palepale kituoni gari ikakaguliwa hapohapo mtu akalipia akapewa badala ya kutumia Rungu la Faini tu kwa kila kitu,rungu la Elimu na Uhamasishaji liko wapi?

Ieleweke hali ya Maisha ni ngumu kumlipisha Dereva wa Bajaji Faini makosa mawili au matatu kwa pamoja asubuhiasubuhi ambayo ukiyaangalia ni makosa ambayo yanahitaji tu Elimu, tukumbuke kumfanyia hivyo umefanya siku nzima afanye kazi bure umemuumiza yeye umeumiza hadi Familia yake ,hii siyo nzuri inazidisha sana Chuki ya Raia kwa Jeshi la Polisi.

Kwa nia njema IGP liangalie hili.
Hao police hawawezi kupambana na Rushwa hizo, unafikiri hawajui wana jua sana ila wana lindana sana.
 
Ila ni kwa sababu labda maumivu au malalamiko ya watu hayana madhara kwa binadamu wengine Ila angekuwa na madhara Kuna trafiki mmoja wa moshi yule jamaa Kila uchwao namuomba Mungu anilipize tu asee. Yule jamaa alinidai rushwa ya shilingi za kitanzania milioni 3 wakati Gari yangu Imeungua ili aniandikie ripoti, Tena waziwazi na akagoma Gari haivutwi haiguswi hadi apewe milioni 3. Sina hamu asee, fikiria Gari Imeungua baada ya nusu saa trafiki anakwambia kama huna milioni 3 usimsumbue hapo hapo mtoto kakimbizwa hosp kapata majeraha ya moto
 
Ila ni kwa sababu labda maumivu au malalamiko ya watu hayana madhara kwa binadamu wengine Ila angekuwa na madhara Kuna trafiki mmoja wa moshi yule jamaa Kila uchwao namuomba Mungu anilipize tu asee. Yule jamaa alinidai rushwa ya shilingi za kitanzania milioni 3 wakati Gari yangu Imeungua ili aniandikie ripoti, Tena waziwazi na akagoma Gari haivutwi haiguswi hadi apewe milioni 3. Sina hamu asee, fikiria Gari Imeungua baada ya nusu saa trafiki anakwambia kama huna milioni 3 usimsumbue hapo hapo mtoto kakimbizwa hosp kapata majeraha ya moto
Ndo mtajifunzà kujua kwamba kupigia kura kwa sera ni muhimu kiliko kushabikia vyama tu........
 
Ndo mtajifunzà kujua kwamba kupigia kura kwa sera ni muhimu kiliko kushabikia vyama tu........
Kwa mazingira ya Sasa ukipiga kura kwa sera au kwa chama au kwa vyovyote vile kitakachotangazwa ni ccm. Kwa Sasa ishu sio sera ni kubebwa na tume ya uchaguzi
 
Kwa mazingira ya Sasa ukipiga kura kwa sera au kwa chama au kwa vyovyote vile kitakachotangazwa ni ccm. Kwa Sasa ishu sio sera ni kubebwa na tume ya uchaguzi
Wote mimi na wewe tu kihoji sera zao ata tume itashindwa, nchi nyingi zimepitia kwenye hali kama hi ya Tanzania ila wana nchi wao wameweza kukikomboa, na wamepata viongozi wanao tekeleza matakua ya wananchi kabisa.......ila raia wa tanzania tuna kasoro fulani ya uoga na unyonge.
 
Hizo sadaka wanazo kusanya hao omba omba na wakubwa zao Wana mgao wao na hua wanapewa malengo ya kiasi kinacho hitajika Kila siku, ndio maana hua hawana woga wakiwa wanafanya huo upuuzi, haya malalamiko yako kwao ni kama kilio cha samaki machozi yanakwenda na maji
Atafutwe mkubwa wao? Atapatikanaje sasa
 
Makosa yenyewe nimeyaangalia mengi yanahitaji Elimu tu lakini watu wanakomolewa wanaandikiwa tu notification ambayo ukiyaangalia ni makosa ambayo yanahitaji tu Elimu.
HATUTAKI KUPEWA ELIMU na polisi, of all the people. Tunajua haki zetu, tunajua sheria za baranatani na nchi at large. Nimekosa niandikie penalty niondoke.

Kama huna elimu, unasubiri hekima za polisi, hukwenda shule at all, you dont know nothing, then speak for your goddamn self.

Wamuite IGP Wambura? Unajuaje Wambura yuko upande wa Wananchi? Wambura amewekwa pale kwa sababu alikuwa ni enforcer mzuri wa sera za police statehood defined by unaccountable abuse of power and brutality. Toka lini nchi hii polisi akam repremand polisi mwenzie? Tunataka inteligent civilians. Hatutaki raia wanaoomba elimu kwa polisi. Mabuti ya polisi yamekanyaga koromea zetu, tunawaombaje elimu?
 
Kwakuwa lengo la uwepo wa sticker wa nenda kwa Usalama ulibuniwa kwa ajili ya mapato basi Police wamefanikiwa kwenye hilo, kama anaekagua gari anadai sticker hambacho hana yeye mwenyewe sijui kila mtu afanye kuifuata huko walikozipeleka kwa Gia ya kusababisha wananchi wasizipate ki urahisi.

Mwisho ila siyo kwa umuhimu, IGP kumbuka sticker hizi zikatwe zilizo/walipo traffic wanapozikagua kama kweli lengo siyo kukomoa wananchi.

Upumbavu imewajaa Trafic huko barabarani, mimi nilishasema sitakuja kutoa rushwa ata seti 1 kumpatia traffic kisa anadai nimefanya kosa.

Kwanza mimi wakinisimamisha huwa siwaongeleshi wanachodai wanawapatia kama anapenda kuandika adhabu yeye anaandika then naondoka zangu, kubishana na mpumbavu naona kama ndiyo upumbavu yenyewe.
 
Ila ni kwa sababu labda maumivu au malalamiko ya watu hayana madhara kwa binadamu wengine Ila angekuwa na madhara Kuna trafiki mmoja wa moshi yule jamaa Kila uchwao namuomba Mungu anilipize tu asee. Yule jamaa alinidai rushwa ya shilingi za kitanzania milioni 3 wakati Gari yangu Imeungua ili aniandikie ripoti, Tena waziwazi na akagoma Gari haivutwi haiguswi hadi apewe milioni 3. Sina hamu asee, fikiria Gari Imeungua baada ya nusu saa trafiki anakwambia kama huna milioni 3 usimsumbue hapo hapo mtoto kakimbizwa hosp kapata majeraha ya moto
Yan hapo ilikuwa unamconnect na takukuru tu
 
Kwakuwa lengo la uwepo wa sticker wa nenda kwa Usalama ulibuniwa kwa ajili ya mapato basi Police wamefanikiwa kwenye hilo, kama anaekagua gari anadai sticker hambacho hana yeye mwenyewe sijui kila mtu afanye kuifuata huko walikozipeleka kwa Gia ya kusababisha wananchi wasizipate ki urahisi.

Mwisho ila siyo kwa umuhimu, IGP kumbuka sticker hizi zikatwe zilizo/walipo traffic wanapozikagua kama kweli lengo siyo kukomoa wananchi.
Upumbavu imewajaa Trafic huko barabarani, mimi nilishasema sitakuja kutoa rushwa ata seti 1 kumpatia traffic kisa anadai nimefanya kosa.

Kwanza mimi wakinisimamisha huwa siwaongeleshi wanachodai wanawapatia kama anapenda kuandika adhabu yeye anaandika then naondoka zangu, kubishana na mpumbavu naona kama ndiyo upumbavu yenyewe.
Polisi imeoza kabisa haifai
 
Kwakuwa lengo la uwepo wa sticker wa nenda kwa Usalama ulibuniwa kwa ajili ya mapato basi Police wamefanikiwa kwenye hilo, kama anaekagua gari anadai sticker hambacho hana yeye mwenyewe sijui kila mtu afanye kuifuata huko walikozipeleka kwa Gia ya kusababisha wananchi wasizipate ki urahisi.

Mwisho ila siyo kwa umuhimu, IGP kumbuka sticker hizi zikatwe zilizo/walipo traffic wanapozikagua kama kweli lengo siyo kukomoa wananchi.
Upumbavu imewajaa Trafic huko barabarani, mimi nilishasema sitakuja kutoa rushwa ata seti 1 kumpatia traffic kisa anadai nimefanya kosa.

Kwanza mimi wakinisimamisha huwa siwaongeleshi wanachodai wanawapatia kama anapenda kuandika adhabu yeye anaandika then naondoka zangu, kubishana na mpumbavu naona kama ndiyo upumbavu yenyewe.
Sio kwamba tuna penda kubishana na hao wapuuzi ila wana uudhi kweli kweli mpaka utawajibu, trafiki kaniomba leseni ni kampa, kaingiza namba ya gari kwenye machine akaona haidaiwi, sasa kanibunia kosa jipya kwa nini nimeva sandals jpili af naendesha gari kwenye main road anataka kunitolea mkeka nilipe fine ya 30k, kweli nikae kimya, hapana
 
Back
Top Bottom