RWANDES
JF-Expert Member
- Jun 12, 2019
- 1,615
- 3,909
Taarifa zilizopo ni kwamba RPC KAGERA ambaye ametoka Pwani na kupelekwa mkoa Kagera ndugu Wankyo nadhani kauli ya jana ya kuhitaji ukuu wa Jeshi la Polisi imemuungiza matatani hii imeonesha hana nidhamu ya hali ya juu ndani ya jeshi hivyo basi staff officer aliyepo mkoa wa Rukwa ameteuliwa kuwa kamanda wa jeshi la polisi mkoa wa Kagera na Wankyo amepelekwa makao makuu ya jeshi mkoani DODOMA ambapo ni mji mkuu wa tanzania.
Ikumbukwe kuwa kauli aliyotoa jana kiutendaji ndani ya jeshi la polisi huku akijuwa mkuu wake wa kazi yupo na anafanya kazi hakustahili kusema kuwa mkuu wake wa kazi anafanya kazi ila yeye akipewa ukuu wa jeshi anaweza kufanya vizuri zaidi hii imeonesha kuwa nafasi aliyeteuliwa na amri jeshi mkuu hatoshi kuliongoza jeshi hivyo basi kwa kuwa jeshi huongozwa kwa nidhamu ya hali ya juu ndiyo maana mabadiliko hayo yamefanyika ili akae makao makuu ajifunze nidhamu pamoja na kuandika vipeperushi mabalimbali vinavyolihusu jeshi la polisi.
Pia soma: Wankyo Nyigesa RPC Kagera: Natamani kuwa IGP, aliyepo hajafanya makosa lakini mimi nitafanya mazuri zaidi
Ikumbukwe kuwa kauli aliyotoa jana kiutendaji ndani ya jeshi la polisi huku akijuwa mkuu wake wa kazi yupo na anafanya kazi hakustahili kusema kuwa mkuu wake wa kazi anafanya kazi ila yeye akipewa ukuu wa jeshi anaweza kufanya vizuri zaidi hii imeonesha kuwa nafasi aliyeteuliwa na amri jeshi mkuu hatoshi kuliongoza jeshi hivyo basi kwa kuwa jeshi huongozwa kwa nidhamu ya hali ya juu ndiyo maana mabadiliko hayo yamefanyika ili akae makao makuu ajifunze nidhamu pamoja na kuandika vipeperushi mabalimbali vinavyolihusu jeshi la polisi.
Pia soma: Wankyo Nyigesa RPC Kagera: Natamani kuwa IGP, aliyepo hajafanya makosa lakini mimi nitafanya mazuri zaidi