Hili jambo linamsikitisha kila Mtanzania mwenye akili timamu.Kuna kamatakamata kila kona ya nchi hii. Nyingi ni za kisiasa, na hii inatokana na Tamko la Raisi la kupiga marufuku mikutano ya vyama vya siasa.
Sasa kwa kuwa Nina imani IGP ni mtu anayeijua sheria vizuri, kwanini asimshauri Rais atengue hilo Tamko kwa sababu kwa mujibu wa katiba ya jamhuri ya Muungano wa Tanzania Raisi tayari amevunja katiba.
Kitendo cha Rais kwenda kinyume na katiba aliyoapa kuilinda, kinatoa taswira mbaya sana. Matokeo yake yameanza kuonekana ni usumbufu usio na lazima kwa Jeshi la polisi.
Nina imani polisi na wao wanajua kuwa wanachokifanya ni makosa na ni kupoteza muda wao ambao wangeutumia kwa mambo ya maana zaidi, ni dhahiri pasi na Shaka kuwa polisi wanajua hizi kesi zikifika mahakamani serikali utashindwa.
Nina imani Rais ni mtu msikivu, nami pia Kama raia mwema namshauri, Aongoze nchi kwa mujibu wa katiba aliyoapa kuilinda.Vinginevyo atajikuta anapambana na wanasiasa badala ya kupambana kuletea wananchi maendeleo.
Mwaka wa kwanza ndiyo huo unakatika. Kuna mengi umeahidi wananchi.sasa hivi hali za wananchi ni mbaya Mara 2 zaidi ya tulikotoka. Watu wameanza kuchoka utawala huu mpya.
Kila siku ni matamko tu. Hakuna hata moja linalotekelezeka, viongozi wasipokuwa makini, watashangaa miaka mitano waliyopewa inakatika na hakuna walichokifanya zaidi ya kamata kamata.
God bless us.
Sasa kwa kuwa Nina imani IGP ni mtu anayeijua sheria vizuri, kwanini asimshauri Rais atengue hilo Tamko kwa sababu kwa mujibu wa katiba ya jamhuri ya Muungano wa Tanzania Raisi tayari amevunja katiba.
Kitendo cha Rais kwenda kinyume na katiba aliyoapa kuilinda, kinatoa taswira mbaya sana. Matokeo yake yameanza kuonekana ni usumbufu usio na lazima kwa Jeshi la polisi.
Nina imani polisi na wao wanajua kuwa wanachokifanya ni makosa na ni kupoteza muda wao ambao wangeutumia kwa mambo ya maana zaidi, ni dhahiri pasi na Shaka kuwa polisi wanajua hizi kesi zikifika mahakamani serikali utashindwa.
Nina imani Rais ni mtu msikivu, nami pia Kama raia mwema namshauri, Aongoze nchi kwa mujibu wa katiba aliyoapa kuilinda.Vinginevyo atajikuta anapambana na wanasiasa badala ya kupambana kuletea wananchi maendeleo.
Mwaka wa kwanza ndiyo huo unakatika. Kuna mengi umeahidi wananchi.sasa hivi hali za wananchi ni mbaya Mara 2 zaidi ya tulikotoka. Watu wameanza kuchoka utawala huu mpya.
Kila siku ni matamko tu. Hakuna hata moja linalotekelezeka, viongozi wasipokuwa makini, watashangaa miaka mitano waliyopewa inakatika na hakuna walichokifanya zaidi ya kamata kamata.
God bless us.