Tipstipstor
JF-Expert Member
- Nov 29, 2021
- 1,531
- 3,331
Ahlan wa sahlan
Wakati ulimwengu ukifurahia kuwaona wachezaji magwiji wawili walioitikisa dunia ,namaanisha Mreno Sir Cristiano Ronaldo na Sir Lionel Messi, tunasahau kuwa hakuna kocha aliyewahi kufundisha mpira wa burudani na wa ushindi kama Mhispania Sir Pep Guardiola.
Sir Guardiola hapewi heshima inayostahili kutokana na umahiri wake ,kila timu anayohamia huwa anahama na mpira wake, wakati anaondoka Barcelona,wengi walimbeza kuwa alikuwa akibebwa na umahiri wa kina messi,iniesta na xavi. Aliwathibitishia kuwa si kama wanavyodhani wakosoaji wake, alikwenda kuibadilisha bayern Munich kutoka ktk mpira wao wa kupiga mashuti mpk kutandaza pasi safi. Vivyo hivyo alipofika Man city aliweza kuvunja utawala wa klabu pinzani kama watani wao wa jadi Man utd ambao hivi punde wametoka kubugizwa na kushindiliwa bakora nne, chelsea na liverpool.
Itoshe kusema kuwa unaweza kumdhibiti Sir Guardiola katika mechi moja ila huwezi kumzuia katika ligi. Licha ya ushindi wanaoupata Man city bado wanapata na burudani safi ya kushuhudia timu yao ikiwadhalilisha wapinzani mpira huu naufananisha na mpira wanaoucheza mabingwa wa soka la Tanzania Simba Sc ambao wanafundishwa na mrithi wa Guardiola , Sir Pablo Franco Martin ambae pia anatokea Hispania.
Naamini Sir Pep hatakama utampeleka katika klabu ya wanalizombe,Maji maji ya Songea bado ataweza kuibadilisha na kuwa tishio sio tu Tanzania bali Africa nzima.
Sir Guardiola umezidi kuwaonea Manchester United, mechi ya kwanza msimu huu walicheza dk 25 za mwisho padi na kugusa mpira ,leo umeamua kuwachezesha dk 45 zote za kipindi cha pili pasi na kugusa mpira.
Wakati ulimwengu ukifurahia kuwaona wachezaji magwiji wawili walioitikisa dunia ,namaanisha Mreno Sir Cristiano Ronaldo na Sir Lionel Messi, tunasahau kuwa hakuna kocha aliyewahi kufundisha mpira wa burudani na wa ushindi kama Mhispania Sir Pep Guardiola.
Sir Guardiola hapewi heshima inayostahili kutokana na umahiri wake ,kila timu anayohamia huwa anahama na mpira wake, wakati anaondoka Barcelona,wengi walimbeza kuwa alikuwa akibebwa na umahiri wa kina messi,iniesta na xavi. Aliwathibitishia kuwa si kama wanavyodhani wakosoaji wake, alikwenda kuibadilisha bayern Munich kutoka ktk mpira wao wa kupiga mashuti mpk kutandaza pasi safi. Vivyo hivyo alipofika Man city aliweza kuvunja utawala wa klabu pinzani kama watani wao wa jadi Man utd ambao hivi punde wametoka kubugizwa na kushindiliwa bakora nne, chelsea na liverpool.
Itoshe kusema kuwa unaweza kumdhibiti Sir Guardiola katika mechi moja ila huwezi kumzuia katika ligi. Licha ya ushindi wanaoupata Man city bado wanapata na burudani safi ya kushuhudia timu yao ikiwadhalilisha wapinzani mpira huu naufananisha na mpira wanaoucheza mabingwa wa soka la Tanzania Simba Sc ambao wanafundishwa na mrithi wa Guardiola , Sir Pablo Franco Martin ambae pia anatokea Hispania.
Naamini Sir Pep hatakama utampeleka katika klabu ya wanalizombe,Maji maji ya Songea bado ataweza kuibadilisha na kuwa tishio sio tu Tanzania bali Africa nzima.
Sir Guardiola umezidi kuwaonea Manchester United, mechi ya kwanza msimu huu walicheza dk 25 za mwisho padi na kugusa mpira ,leo umeamua kuwachezesha dk 45 zote za kipindi cha pili pasi na kugusa mpira.