Ifahamu kamandi ya jeshi la Anga

Ifahamu kamandi ya jeshi la Anga

Mshana Jr

Platinum Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
359,898
Reaction score
828,493
Kamandi ya Jeshi la Anga ni moja ya Kamandi muhimu zinazounda Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania kiutendaji, kivita na kiutawala. Kamandi ya Jeshi la Anga inayo majukumu ya ziada ya msingi katika kutimiza wajibu wake wa ulinzi wa Anga la Tanzania. Kamandi hiyo inao uzoefu wa kusafirisha maafisa na askari wakati wa amani na dharura, pia husaidia mamlaka za kiraia katika kutimiza wajibu wake na kusafirisha mizigo.

Juhudi za awali za kuunda nguvu za Jeshi la Anga ndani ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania zilianza mapema mwaka 1964 pale ambapo kikundi cha maafisa kadhaa walipelekwa nchini Israeli na Ujerumani ya Magharibi wakati huo kusomea urubani.

Hata hivyo, wanafunzi waliokwenda kujifunza urubani katika nchi ya Ujerumani ya Magharibi hawakuweza kumaliza mafunzo ya urubani kutokana na kuvunjika kwa uhusiano wa kibalozi baina ya Ujerumani Mashariki na Ujerumani Magharibi mwaka 1965.

Baada ya jitihada za muda, hatimae kikosi cha usafirishaji wa anga kilianza operesheni mwaka 1969 kikiwa na ndege mbalimbali, ikiwa ni pamoja na ndege nne aina ya OTTER na zilizosalia za CARRIBOU. Wakati wote wa chimbuko la nguvu za anga shughuli zote za kioperesheni zilizohusu vikosi na vitengo vya ulinzi wa anga viliongozwa na Tawi la Operesheni na Mafunzo (COT) la Makao Makuu ya Jeshi.

Mwaka 1971 kilianzishwa kikosi maalum cha mizinga ya kutungulia ndege kikiongozwa na Kapteni Abdallah, makao yake yakiwepo Mgulani. Maafisa wa mwanzo walipelekwa Pakistan na India kwa mafunzo ya mizinga hiyo. Mwaka huohuo Rais na Amiri Jeshi Mkuu (mstaafu) Mwl. Julius K. Nyerere aliagiza Jeshi lipatiwe ndegevita.

Mwaka 1973 timu ya marubani wanafunzi 48 wakiongozwa na Meja JE Luhanga(alistaafu akiwa Meja Jenerali) walihitimu mafunzo yao nchini China na wakaanzisha kikosi cha kwanza cha ndegevita

Maendeleo makubwa yalifanyika katika kipindi cha miaka mitano ambapo idadi ya vikosi na zana za Ulinzi wa Anga viliongezeka. Mwaka 1975 vikosi vya Rada vilianzishwa na kugawiwa kanda za uchunguzi wa Anga, kipindi hichohicho vikosi vya makombora matiifu ya kutungulia ndege (SAM) vilianzishwa katika miji mbalimbali.

Utaratibu wa utendaji kivita na mafunzo wa vikosi vyote vya ulinzi wa anga toka 1974 hadi 1982 ulifanywa na Tawi la Makao Makuu ya Jeshi (MMJ) la Chief of Air Defence (CAD) chini ya Kanali SA Hemedi, ambaye baadae alipandishwa cheo kuwa Brigedia Jenerali.

Majukumu ya Kamandi ya Anga.

a. Kutoa ulinzi wa Anga kwa maeneo muhimu ya kitaifa, kisiasa, kiuchumi na kwa Wananchi,

b. Kutoa ulinzi wa Anga kwa maeneo na vituo muhimu vya kijeshi na mkusanyiko wa Majeshi,

c. Kutoa msaada wa kimapigano kwa operesheni za Majeshi ya Nchi Kavu na Wanamaji,

d. Kutoa msaada kwa mamlaka za kiraia hasa nyakati za maafa ya kitaifa na kusindikiza ndege za viongozi pia hukusanya taarifa za kiusalama,

e. Kuendeleza juhudi za mahusiano ya kijeshi na nchi nyingine kwa njia ya mazoezi ya pamoja.

f. Kushiriki katika operesheni za kulinda amani za Umoja wa Mataifa.

Chanzo: TPDF

1759606317697.jpg
 
KAPTENI AKISEMA INA MAANA GANI HASA?

Baada ya Capt. John Charles Tesha kutoa sauti ya video yenye maneno mazito mitandaoni, hali ya taharuki imetanda jijini Dar es Salaam huku watu wakiuliza kulikoni. Wakati watu wengine wakihangaika kutaka kujua, Capt. Tesha ni nani hasa, sisi tunaona ni vizuri tukakielezea cheo cha Captain. Yeye mwenyewe alijitambulisha kama Capt. Tesha, lakini baadaye, mitandaoni watu wanamtaja kwa jina la Capt. John Charles Tesha.

Captain kama cheo cha kijeshi, kinamaanisha afisa wa jeshi aliye chini ya Meja (Major) lakini juu ya Luteni (Lieutenant). Kwa ujumla, Captain ndiye anayeelezwa kuwa ni "great soldier, strategist and experienced commandor' yaani askari mwenye mikakati na mwenye uzoefu wa kupigana.

Katika mfumo wa majeshi ya nchi za magharibi kama Marekani na Uingereza, Captain ni afisa mwenye uwezo wa kuongoza kikosi cha askari wapiganaji kuanzia 60 hadi 200 kulingana na mazingira. Kwa hiyo, Capt. Tesha anaweza pia kuwa na kikosi cha watu wasiozidi 200 chini yake na ambao wanaweza kupokea amri yake moja kwa moja bila kuhoji na kutilia shaka na kisha kuitekeleza.

Katika nchi zilizotawaliwa na Ufaransa, hasa za Afrika Magharibi, mapinduzi mengi ya kijeshi yaliyongozwa au yanaongozwa na askari walio na cheo cha Captain. Hii ni kutokana na ukweli kuwa kiuhalisia, Captain ndiye askari ambaye anaweza kuongoza watu wengi zaidi. Maafisa wengine, huongoza vikosi ambavyo ndani yake kuna watu wenye vyeo wa Captain na hivyo, ili afisa wa juu amri yake itekelezwe ni lazima pia ipite kwa afisa mwengine hadi imfikie Captain ambaye huamrisha askari wapiganaji ambao wako chini yake.

Hata askari waliokuwa wamemuasi Nyerere mwaka 1964 hawakuwa askari wa vyeo vya juu, bali walikuwa hawa hawa wapiganaji. Kikosi kikiasi, hakuna cha Jenerali, Luteni Jenerali, Meja Jenerali, Brigadia Jenerali wala Kanali; wote hao watajificha wakisubiri ujasiri wa hao 'makapiteni' wanaowatii kama watapokea amri zao kupambana na kikosi kilichoasi.

Kwa ujumla, hakuna mtu yeyote mwenye akili timamu na mwenye uelewe wa mambo ya jeshi ambaye atafurahia maasi ya jeshi. Ukilisikiliza kwa umakini kauli ya Capt. Tesha, utabaini ya kuwa Captain akichukua nchi wakubwa wote watapata kibano.

Katika historia ya Tanzania, haijawahi kutokea Captain wa Jeshi akatoka hadharani kusema au kutoa tahadhari kwa Jenerali au Mkuu wa Majeshi. Tuichukulie kauli ya Capt. Tesha kama ishara muhimu kwetu sote kama taifa na hivyo tukae chini kutafakari kwa kina maneno yake. Badala ya kumjadili Capt. Tesha, tujikite katika kujadili ukweli na uhalisia wa maneno yake!

Kukanusha juu ya uwepo wa mtu mwenye jina la Capt. Tesha Jeshini au la hakutasadia sana hasa kama maneno aliyosema yana ukweli! Kama maneno hayo ni ya uwongo basi pia hata kukanusha hakuna maana kwani uwongo pia hauna utamaduni wa kujitetea, ukasimama!
Je, nini kimekushangaza? Je, nini maoni yako?

Mwana Kondoo Ameshinda! Tumfuate!
Askofu Emmaus Bandekile Mwamakula
Itunge, Dar es Salaam; 4 Oktoba 2025; Saa 2:20 usiku.
1759606582378.jpg
 
Jamaa ni kitengo cha midege yani muda wote anacheza na mawingu tu.

Sasa wakijidai wanataka kukimbia nchi, wakumbuke jamaa yetu Tesha mambo ya anga ndio idara yake chocho zote jamaa anazijua.

Wakijaribu kupanda pipa wasepe sidhani kama hata kwenye mataa ya hapo Nairobi watafika maana umegusa department yake.

Au waseme wachukue Air Tanzania watorokee upande wa Uganda napo sidhani kama watafika mbali kwani kona za pale Mombasa ni kali sana afu pia route hii ina mlima sana so itawapa ugumu kukimbia kwasababu ya uzito wa engine ya ndege ya abiria ila yeye kwasababu anatumia fighter jet ni simple tu.
 
Katika historia ya Tanzania, haijawahi kutokea Captain wa Jeshi akatoka hadharani kusema au kutoa tahadhari kwa Jenerali au Mkuu wa Majeshi. Tuichukulie kauli ya Capt. Tesha kama ishara muhimu kwetu sote kama taifa na hivyo tukae chini kutafakari kwa kina maneno yake. Badala ya kumjadili Capt. Tesha, tujikite katika kujadili ukweli na uhalisia wa maneno yake!JE, JWTZ LIMEJIBU HOJA YA CAPT. TESHA?

Baada ya Capt Tesha kutoa hotuba kwa njia ya video, Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) limetoa kauli kwa njia ya waraka. Hata hivyo, waraka huo unafichua ya kuwa baadhi ya hoja hizo hutolewa na:

1. Watu walio katika mazingira ya kijeshi.

2. Watu wanaojinasibisha na Jeshi.

3. Watu walioachishwa Jeshi kwa tabia mbaya

4. Watu walioachishwa Jeshi kwa kujihusisha na siasa na wanaharakati.

Waraka huo haujakanusha ukweli wa maudhui yaliyomo katika hotuba ya Capt. Tesha. Lakini pia, waraka huo umekwepa kumzungumzia mtu aliyejitambulisha kama Capt. Tesha, hivyo Jeshi halijasema kama Capt. Tesha ni askari aliye kazini au la, na pia kama ni askari au mtu anayeangukia katika aina kundi lipi kati ya hayo manne hapo juu, Jeshi halijasema.

Kwa ujumla, kauli ya Jeshi haijajibu maswali bali imezidi kuongeza maswali na hivyo kuzidi kuwafanya watu wazidi kusikiliza hotuba ya Capt. Tesha kuliko kuipuuza. Ni wazi kabisa ya kuwa Capt. Tesha ni phenomona iliyoibuka kwa ghafla bila ya kutegemewa. Kwa sababu hiyo, ili kuikabili phenomona kama hiyo huhita tafakuri nzito na hekima ya hali ya juu.

Ukurasa wa askofu unawaalika watu kujadili na kutafakari juu ya ukweli au uwongo ulio katika hoja za Capt. Tesha badala ya kujadili, kutaka kujua kikosi chake au hata hali yake ya ajira ya jeshini kama ni hai au mfu. Tukiazima kauli ya Kikwete, "hoja haipigwi rungu'! Kwa hiyo tujadili au kujibu au tukanushe hoja ya Capt. Tesha.
Je, nini kimekushangaza? Je, nini maoni yako?

Mwana Kondoo Ameshinda! Tumfuate!
Askofu Emmaus Bandekile Mwamakula
Itunge, Dar es Salaam; 4 Oktoba 2025; Saa 4:00 usiku
 
Well explanations
Tukiachana na vyeo vya juu hapa tunapata picha kwamba wanaopigana ni ma captain na sio ma major wala ma brigedia kwanza wale ni wazee na wana vitambi ata kukimbia hawawezi
Nasimama na captains wote wa kamandi mbali mbali
 
Jamaa ni kitengo cha midege yani muda wote anacheza na mawingu tu.

Sasa wakijidai wanataka kukimbia nchi, wakumbuke jamaa yetu Tesha mambo ya anga ndio idara yake chocho zote jamaa anazijua.

Wakijaribu kupanda pipa wasepe sidhani kama hata kwenye mataa ya hapo Nairobi watafika maana umegusa department yake.

Au waseme wachukue Air Tanzania watorokee upande wa Uganda napo sidhani kama watafika mbali kwani kona za pale Mombasa ni kali sana afu pia route hii ina mlima sana so itawapa ugumu kukimbia kwasababu ya uzito wa engine ya ndege ya abiria ila yeye kwasababu anatumia fighter jet ni simple tu.
Umewaza very deep 💪🏿📌🔨
 
Kweli, binafsi natamani maelezo mengi zaidi ya haya
Ni kwasababu kilichoongelewa kina akisi msimamo wa kundi kubwa kama alivyosema Capatin.

Hivi unadhani ingekuwa ni mpotoshaji tu aliyejivalia magwanda ya Kijeshi unadhani wange hesitate kupinga kuwa huyo mtu ni tapeli na hayupo kwenye kitengo?

Hell no.

Wangefanya hivyo tena kwa mbwembwe zote ikiwemo kutoa kauli za kutaka kumtia nguvuni kwa kosa hilo. Lakini kwanini hawajafanya?

Ni kwasababu wanatengeneza backup ya wao kuwa salama siku zijazo mambo yakibadilika.

Yaani kiufupi hii taarifa inawafanya wawe salama iwapo matokeo mawili yote yakatokea.

1. Tukio la maandamano na wananchi kufanikiwa kuuangusha utawala huu.
2. Tukio la maandamano kukwama na watawala kufanikiwa kuendeleza utawala wao.

Maana yake outcome ya hayo mambo mawili inawaweka hao idara ya mawasiliano katika hali ya usalama. Ikitokea wananchi wameangusha utawala, bado watakuwa salama kwasababu hawakupinga kwa kumtaja muhusika (Tesha)

Watawala wakifanikiwa bado hiyo idara ya habari haitobeba lawama kwasababu wataonekana walijaribu kukanusha uvumi uliokuwa unaenea japo hawakuwa too specific.
 
Ni kwasababu kilichoongelewa kina akisi msimamo wa kundi kubwa kama alivyosema Capatin.

Hivi unadhani ingekuwa ni mpotoshaji tu aliyejivalia magwanda ya Kijeshi unadhani wange hesitate kupinga kuwa huyo mtu ni tapeli na hayupo kwenye kitengo?

Hell no.

Wangefanya hivyo tena kwa mbwembwe zote ikiwemo kutoa kauli za kutaka kumtia nguvuni kwa kosa hilo. Lakini kwanini hawajafanya?

Ni kwasababu wanatengeneza backup ya wao kuwa salama siku zijazo mambo yakibadilika.

Yaani kiufupi hii taarifa inawafanya wawe salama iwapo matokeo mawili yote yakatokea.

1. Tukio la maandamano na wananchi kufanikiwa kuuangusha utawala huu.
2. Tukio la maandamano kukwama na watawala kufanikiwa kuendeleza utawala wao.

Maana yake outcome ya hayo mambo mawili inawaweka hao idara ya mawasiliano katika hali ya usalama. Ikitokea wananchi wameangusha utawala, bado watakuwa salama kwasababu hawakupinga kwa kumtaja muhusika (Tesha)

Watawala wakifanikiwa bado hiyo idara ya habari haitobeba lawama kwasababu wataonekana walijaribu kukanusha uvumi uliokuwa unaenea japo hawakuwa too specific.
Sasahivi ndio nimeelewa, naona barua iko peace sana ukilinganisha na mambo ambayo Tesha ameongea. Ni kama huyu jamaa anakubaliana na Tesha ila anaogopa kwenda tofauti na kiapo chake 😅

Hapa kidogo nimeanza kupata matumaini
 
Msigwa ni chawa mbovu sana, yeye, wasanii wa muziki na wengine kina Millard Ayo. Sasa Millard Ayo sijui ni chawa au ni muoga, hata sielewi
 
Kuna watu wanaomba jeshi lichukuwe nchi ili tupate mabadiliko lakini mimi akili yangu ipo kwengine kabisa. Mimi naomba ichukwe nchi na imchukuwe huyu Mbunge wetu nipate nifanye mapinduzi nyumbani kwake mkewe ana mtak..oo wa kunikata kiu yangu😂😂
 
Back
Top Bottom