Idd Simba atetea posho za Wabunge


kweli kabisa, alijiuzulu uwaziri kwa ile kashfa ya sukari.
 

Hili naona linafanana sana na shibuda likiona magazeti yamelisahau linakaa kutoa kauli tata
 
Fisadi ndiye aliyesababisha sukari kupanda bei toka sh 450 kwa kilo mpaka leo sh 3000 Kwani alipiga marufuku sukari ya nje halafu yeye akaleta kwa mgongo wa jeshi na kuiuza kwa sh 750 ingekuwa china kisha nyongwa siku nyingi
 
Simba fisadi hata sitaki kusikia harufu yake. Kila analolisema ni wizi mtupu asiaminiwe kabisa.
Uda wizi mtupu kauza na kuweka pesa kwenye akaunti yake binafsi.......
Pride anawaibia maskini wajasiliamali mchana kweupe na kanyamaziwa na wezi wenzie.........!
Alizunguka nchi nzima akipigia kampeni kampuni feki moja inaitwa NICO akishawishi watu wanunue share akishirikiana na yule mchaga wameweka ndani vipesa vyetu tulivyotoa kununua hisa. Hamna lolote linalovunwa. Ni jambazi la kutupwa halifai hata kuzungumza mbele ya watanganyika.
Nikisikia sauti yake nataka kupasuka kwa hasira mwizi huyu.
Hana la kutushauri mjinga huyu.
 
Anachosema Idd Simba nadhani ni kulingana na mazingira tuliyopo, mfumo wa katiba yetu na kwamba majukumu a mbunge ni kupeleka maendeleo kwa wnaanchi sasa iwe kutoka mfukoni mwake ama serikalini lakini kwa ujumla ni kwamba tunawachagua wabung wetu kwa misingi ya nani ataweza kuepelka maendeleo na kusaidia watu..Hadi hapo tutyakaporekebisha mfumo huu ndio tunaweza kusema mengineyo...

Nilikuwa nikisoma report moja inasema ya kwamba kati ya vitu vilivyoangusha uchumi wa Tanzania enzi ya mwalimu ni pamoja na Kudhibiti Ufisadi (economic saboteur) wa mwaka 1973..Hivyo ukitazama juu juu bila kuzingatia kwamba miaka ile ulanguzi ndio ulikuwa ukiendesha uchumi wa nchi unaweza mlaani aloandika...

Na leo hii hata tunapopinga Ufisadi ni muhimu sana kutazama mizizi yake na jinsi ilivyojisimika ktk uchumi wetu kabla hatujaikata laa sivyo inaweza poromosha kila kitu maana investors wote kutoka nje wamepitia njia za Ufisadi je tukiwakamata wote na kutaifisha ama kufunga biashara zao tunaweza jimudu?
 
Sigma shame on you too. Unafiki unaujua au unabwabwaja? Mie namjua Idd Simba akiwa waziri kuliko wewe hasa pale alipowatetea wazawa. Kwa vile wengine mnajiandikia bila kumbukumbu, una haki ya kunena lolote hata kama ni upupu na mpumba kama ulivyofanya kuniita mnafiki wakati wewe ni kihiyo wa kawaida na bendera inayofuata upepo.
 
Alaaaaahhhhhhhhh..kumbe basi waanzishe mfuko mwingine wa SACCOS ya Wabunge au kila mbunge awe na NGO/CBO etc TUJUE MOJA!!
 


ni kweli kabisa hiyo posho ya laki 2 kwa siku kwa mbunge hazitoshi
ila mshahara wa 146000 kwa mwezi ambayo sawa na kama 4800 kwa siku
zinatosha. wabunge ni binadamu jamani kama sisi, tungewaongezea hiyo posho
yao... na kaulimbiu ya maisha bora kwa kila mtanzania kuna haja ya kuiangalia upya
 
Idd Simba angeonyesha mfano kwa kuanza kuwalipa wafanyakazi wake wa PRIDE hata sh 20,000 tu kila wanapoenda kazini, au arudishe pesa za UDA ndo zitumike kulipia posho, af ndo aje azungumzie na posho za ubunge
 
mwenzagu umetua lini kutoka sayari mpya kwa maana anachosema idd simba ni ukweli mtupu tena "from the horse's mouth". hujawai kuwa mwakilishi wa wananchi katika nchi hii wala mtoto pekee uliye na mshahara kutoka ukoo maskini. jamani penye ukweli na uhalisia tuseme na tukubali ili tutafute ufumbuzi.
hata huo mfuko wa jimbo wanaharakati waliupinga nao pia si wa mda mrefu kiasi kwamba haujabadilisha tabia iliyozoeleka ya mda mrefu ya wananchi kuwaomba wawakilishi wao misaada ya maendelo yao kama jamii au wao binafsi.
amini nakwambia hiyo posho itapitishwa hasira zenu mtazimalizia kwenye kura 2015 mtakaowachagua nao watazila na kamchezo kataendelea millele na milele sema amina.
 

Wewe ndiye unaishi kwenye dunia ya UTOPIA ndiyo maana hata hoja zako ziko pogo. Kama mimi ni
mtoto pekee kutoka familia masikini ninayepokea mshahara, mbona sijaomba niongezewe posho ili nipate
pesa nyingi ya kuigawia familia yangu?. Shirikisha akili zako wakati unapoandika.

Aidha I can bet my neck mimi tangu nianze kupiga kura hakuna hata mbunge mmoja aliyewahi kunigawia
pesa pamoja na kwamba mimi ni mpiga kura mzuri.

YES we will keep changing them hadi hii mind set kwamba kazi ya mbunge ni kuwagawia wananachi pesa
itakapobadilika. There is a light at the end of the channel. Waulize wapiga kura wa jimbo la Mwanza mjini.
Boman 1990 aligawa pesa wananchi wakampiga chini wakachagua mwalimu wa school Mabiti. 2010 Masha
amemwaga pesa wananchi wamepiga chini wamechagua a fresh graduate from SAUT Wenje.

Bottomline, hizo posho wanazotaka wabunge wa CCM waongezewe ili wapate ziada ya kuwagawia wananchi
ni HONGO, period. Tunajua Simba anajikomba kwasababu sakata lake la UDA liko bungeni hivyo anatafuta
huruma ya wabunge kwa mgongo huo. That is a child brain.
 
bobuk-inaelekea hujui vitu vingi kwani ni kama mtu aliyepandia gari njiani tena karibu na mwisho wa safari.
kwanza utopia halistahili kuwepo kabisa katika mchango wako ulivyolitumia linakurudi wewe. utopia ni kichume cha uhalisia, sasa uhalisia ni nini na ni upi. tiba ya autopia ni sayansi na sayansi inasisitiza kufuata ukweli. ukweli tunaupata watu? kwa wahusuka. katika hili wewe sa idd simba nani unatupatia uhakika?
sayansi pia inaamini katika kile watu wanachoona, kwa maneno yako mwenyewe umesema mind set za watu wengi wanawaomba wabunge misaada na hii itaendelea mpaka hiyo mind set itakapobadilirika.

ni utopia kujaribu kufikiria kuwa mtu anaweza kuchaguliwa bila kutumia pesa- atawafikiaje wapiga kura.
aidha ni aibu kumuita wenje fresh from SAUT. KUMBUKA SIYO KILA MBICHI NI FRESH.

bado ninaamini umefika hivi karibuni kutoka sayari mpya iliyogunduliwa
 

Sitachoka kukuelimisha maana dunia hii kuna watu na viatu. Nitarudia tena in bold and short.
Hakuna hata nchi moja ambayo katika job description za mbunge inaeleza kuwa kazi mojawapo
ni mbunge ni kugawa pesa kwa wapiga kura wake. Tembelea website ya bunge kama utaikuta hiyo
kazi ya mbunge kugawa pesa. Indeed wanaogawa pesa wanatoa HONGO which is a crime na utakuta
wanagawa hizo pesa hasa wakati wa Kampeini. BTW, wewe tangu umemchagua mbunge wako
ameshakugawia shilingi ngapi? jijibu kimoyomoyo.

Ukinionyesha hata nchi moja under this sun ambayo inasema kazi ya mbunge ni kugawa pesa kwa wapiga
kura wake, Mimi nitakuonesha malaika wa Mungu anayegawa pesa bure kwa binadamu.

The ball is in your coat
 
naunga mkono hoja jako
 
babuk,
unajadili jinsi mambo yanavyopaswa kuwa huku ukikwepa mambo jinsi yalivyo. hayo ndiyo matokeo ya elimu ya darasani -IDEAL TYPE, UTOPIA. na hapo ndipo tunapopishana.
wapo watumishi wengi wa serikali wanaopata kipato kikubwa ima kama mshahara au kama posho kuzidi hata wabunge. lakini wabunge kama wawakilishi wa watu wanafatwa na watu mbalimabali kwa ajili ya kuomba misaada- unahiari ya kukataa au kukubali lakini hali halisi ndo ilivyo. hii huwezi kuikuta kwenye kitabu chochote hata tovuti ya bunge.
 

Ndugu comte Hapa ndiyo tunatofautiana kama mbingu na ardhi. FYI, hata mimi huwa ninafuatwa
na ndugu, jamaa, marafiki, jirani na hata omba omba, wote hao wakiniomba misaada. Lakini
hata siku moja siwezi kwenda kumwambia mwajiri wangu kwamba aniongezee mshahara au
posho ili nipate pesa ya ziada ya kugawa kwa hao niliowataja. Hiyo argument ni mfu na kama
ndiyo uwezo wa wabunge wetu huo kujenga hoja, ndiyo maana nikasema basi huko kwenye
mabunge ya EA, AU, Madola We are a laughing stock.

Pinda PM, Simba wote wanajenga hoja kwa kutumia hiyo twisted argument, na wewe bila
kutafakari una jump to a band wagon.
 
babuk,
sasa inaelekea unaanza kuelewa kidogo kumbe wako watu mitaani wanaoomba wanzao, ambao wanadhani wanahaki ya kuomba na kupewa bila kujali kama wanaowaomba wanauwezo wa kuwasaidia. kwa jinsi tulivyolelewa ni wachache sana wanauwezo wa kukataa kutoa chochote wanapombwa kwani wakati mwingine gharama za kukataa ni kubwa kuliko za kutoa. hebu fikiria kaja mtu kutoka kijijini kwenu anataka msaada wa shillingi 20000. unaamua kutompa lakini huwezi kumwambia aondoke kwako na wewe unachumba kimoja kwa ajili yako na mkeo. kwa hakika gharama za kumuweka hapo zitazidi hicho anachokuomba.hivyo ukiendelea kumuamnyima inakula kwako.
babuk matokeo ya mfumo huu wa wachache kuombwa na wengi ndo maana watumishi wote wamebuni PERSONAL ECONOMIC SURVIVAL ACTIVITIES (PESA)-WIZI, RUSHWA SEMINA WASHA AU KUTOKUWEPO KAZINI HUKU WAKILIPWA MISHAHARA NK. ndo maana mashirika 420 aliyoazisha nyerere yamekufa
babuk kumbuka kipato katika afrika kipato chako si chako peke yako ni cha wote wanaokufahamu na wasio kufahamu. sas chukua picha hiyona muuangalie diwani au mbunge- ombaomba wake wantoka kata nzima na jimbo zima.

bado naamini wewe umefika hivi punde kutoka sayari mpya. achana na vitabu maadishi yako ubaoni.
 

Two wrongs do not make a right. Hatuwezi kuhalalisha wizi kwasababu eti kuna wezi! Mbuge anaweza kumsaidia
mpiga kura wake, kama mimi ninavyoweza kumsaidia ndugu/jamaa yangu kwasababu za kibinadamu na pia kama
uwezo wa kusaidia unaruhusu. Lakini hiyo haifanyi kuwa kigezo cha kuombea kuongezewa mshahara au posho na
mwajiri.

Hayo yote niliyo BOLD yametokea kwasababu ya ulegelege wa akina Idd Simba & Co. wa kushindwa kuisimamia serikali.
Matokeo yake wanahamishia ulegelege wao wa kutowajibika kwenye posho. Eti mbunge makini anahitaji posho kubwa!
I bet my neck mbunge goigoi kama akina Idd Simba & Co. hata akipewa posho ya 1 billioni @ day hataweza kuisamamia
serikali as his/her primary responsibility. I stand to be corrected.
 
Babuk,
unamjua mbuge asiyechukua posho hata mmoja?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…