Huyu mzee ni fisadi wa kukubuhu na ndio maana alifukuzwa uwaziri wa viwanda kwa sababu ya kula magendo ya vibari vya sukali. Ufisadi uko ndani ya damu yake na ndio maana akiwa Mwenyekiti wa UDA akishirikiana na meya wa jiji mwizi wakaihujumu kampuni ya uma na fedha zikawekwa kwenye account ya Simba kama vile ilikuwa mali yake!! Sio hivyo tu huyu mzee anahusika pia na kubaka ardhi ya watu huko Katavi [ akishirikiana na Pinda] na kuiuzia kampuni ya kutoka IOWA marekani maelfu ya ekari za ardhi. Sio muadilifu hata chembe na hafai kusikilizwa na wazalendo wa nchi hii.
paka, suala si mbunge kuchukua fedha na kuwapa wapiga kura, kama kila mtu akizihitaji atazitoa wapi? wananchi wenye matatizo ni wengi sana, ni wazi iwapo ukihalalisha hoja eti tunawagawia wapiga kura wetu wanaotusubiri nje ya mjengo....PINDA, ni mawazo mfu.
kazi za wabunge ni hizi
(a) kuandaa mazingira mazuri ya kila mwenye uwezo wa kufanya kazi kufanya kazi ajipatie kipato chake cha halali.
(b) kusimamia miradi ya wananchi ili ifanikiwe kwa kiwango cha juu sana
(c) kuisimamia serikali kama taasisi ili iwajibike kwa wananchi.
wabunge wetu wamjichagulia kazi ya kutoa misaada midogomidogo hali inayopelekea kujenga utegemezi miongoni mwa wanajamii.
wameshindwa kujenga mazingira bora ya kumwezesha kila mwenye uwezo wa kufanya kazi kujitafutia kipato.
(a) wamegawa aridhi bure kwa wawekezaji na kumnyang'anya mwananchi sehemu ya kuzalishia.
(b) wametunga sheria kandamizi za kodi, ambapo mzawa analipa zaidi ya mgeni
na mengine kibao
"Ninachosema ni hivi, kwa mbunge wa kweli ambaye anasimamia maslahi ya wananchi wake, hizo fedha si nyingi. Kwa sababu mbunge makini anahitaji kutoa misaada, kuona malengo ya wapiga kura wake yametimia na mambo mengi angependa kufanya,
Nilipokuwa mbunge niliandamwa sana na wananchi na nilikuwa nawasaidia kila wanapohitaji msaada kutoka kwangu,
Hii ni kauli ya Idd Simba.
Source: Mwananchi 20/12/2011
Hivi ni kweli hizi ndio kazi za Mbunge Jimboni kwake?
mwenzagu umetua lini kutoka sayari mpya kwa maana anachosema idd simba ni ukweli mtupu tena "from the horse's mouth". hujawai kuwa mwakilishi wa wananchi katika nchi hii wala mtoto pekee uliye na mshahara kutoka ukoo maskini. jamani penye ukweli na uhalisia tuseme na tukubali ili tutafute ufumbuzi.Mimi huwa ninajiuliza hivi ukiwa mwana CCM, hata uwezo wa kawaida tu wa kujenga hoja unapunguwa? Kama ni hivyo basi CCM is a mental disease. Hivi kazi za mbunge ni kugawa hela kwa wapiga kura wake? Huyu Idd Simba kweli hakupewa job description ya mbunge wakati alipokuwa mbunge.
Afterall wabunge siku hizi wana mfuko wa jimbo. Kwanini basi wasitumie mfuko huo jimbo kufanya maendelea katika majimbo yao? Idd Simba, FYI mbunge makini ni yule ayeisimamia serikali barabara ktk kutekeleza majukumu yake ya kuwaletea wananchi maendeleo. Mbunge makini si yule anayelilia kuongezewa posho ili apate pesa nyingi za kuwagawia wapiga kura wake, get real dude.
Kama wabunge wetu ndiyo hivi wanavyojenga hoja, basi huko kwenye mabunge ya EA, AU, Madola we are a laughing stock!
mwenzagu umetua lini kutoka sayari mpya kwa maana anachosema idd simba ni ukweli mtupu tena "from the horse's mouth". hujawai kuwa mwakilishi wa wananchi katika nchi hii wala mtoto pekee uliye na mshahara kutoka ukoo maskini. jamani penye ukweli na uhalisia tuseme na tukubali ili tutafute ufumbuzi.
hata huo mfuko wa jimbo wanaharakati waliupinga nao pia si wa mda mrefu kiasi kwamba haujabadilisha tabia iliyozoeleka ya mda mrefu ya wananchi kuwaomba wawakilishi wao misaada ya maendelo yao kama jamii au wao binafsi.
amini nakwambia hiyo posho itapitishwa hasira zenu mtazimalizia kwenye kura 2015 mtakaowachagua nao watazila na kamchezo kataendelea millele na milele sema amina.
bobuk-inaelekea hujui vitu vingi kwani ni kama mtu aliyepandia gari njiani tena karibu na mwisho wa safari.
kwanza utopia halistahili kuwepo kabisa katika mchango wako ulivyolitumia linakurudi wewe. utopia ni kichume cha uhalisia, sasa uhalisia ni nini na ni upi. tiba ya autopia ni sayansi na sayansi inasisitiza kufuata ukweli. ukweli tunaupata watu? kwa wahusuka. katika hili wewe sa idd simba nani unatupatia uhakika?
sayansi pia inaamini katika kile watu wanachoona, kwa maneno yako mwenyewe umesema mind set za watu wengi wanawaomba wabunge misaada na hii itaendelea mpaka hiyo mind set itakapobadilirika.
ni utopia kujaribu kufikiria kuwa mtu anaweza kuchaguliwa bila kutumia pesa- atawafikiaje wapiga kura.
aidha ni aibu kumuita wenje fresh from SAUT. KUMBUKA SIYO KILA MBICHI NI FRESH.
bado ninaamini umefika hivi karibuni kutoka sayari mpya iliyogunduliwa
naunga mkono hoja jakoMimi huwa ninajiuliza hivi ukiwa mwana CCM, hata uwezo wa kawaida tu wa kujenga hoja unapunguwa? Kama ni hivyo basi CCM is a mental disease. Hivi kazi za mbunge ni kugawa hela kwa wapiga kura wake? Huyu Idd Simba kweli hakupewa job description ya mbunge wakati alipokuwa mbunge.
Afterall wabunge siku hizi wana mfuko wa jimbo. Kwanini basi wasitumie mfuko huo jimbo kufanya maendelea katika majimbo yao? Idd Simba, FYI mbunge makini ni yule ayeisimamia serikali barabara ktk kutekeleza majukumu yake ya kuwaletea wananchi maendeleo. Mbunge makini si yule anayelilia kuongezewa posho ili apate pesa nyingi za kuwagawia wapiga kura wake, get real dude.
Kama wabunge wetu ndiyo hivi wanavyojenga hoja, basi huko kwenye mabunge ya EA, AU, Madola we are a laughing stock!
babuk,
unajadili jinsi mambo yanavyopaswa kuwa huku ukikwepa mambo jinsi yalivyo. hayo ndiyo matokeo ya elimu ya darasani -IDEAL TYPE, UTOPIA. na hapo ndipo tunapopishana.
wapo watumishi wengi wa serikali wanaopata kipato kikubwa ima kama mshahara au kama posho kuzidi hata wabunge. lakini wabunge kama wawakilishi wa watu wanafatwa na watu mbalimabali kwa ajili ya kuomba misaada- unahiari ya kukataa au kukubali lakini hali halisi ndo ilivyo. hii huwezi kuikuta kwenye kitabu chochote hata tovuti ya bunge.
babuk,
sasa inaelekea unaanza kuelewa kidogo kumbe wako watu mitaani wanaoomba wanzao, ambao wanadhani wanahaki ya kuomba na kupewa bila kujali kama wanaowaomba wanauwezo wa kuwasaidia. kwa jinsi tulivyolelewa ni wachache sana wanauwezo wa kukataa kutoa chochote wanapombwa kwani wakati mwingine gharama za kukataa ni kubwa kuliko za kutoa. hebu fikiria kaja mtu kutoka kijijini kwenu anataka msaada wa shillingi 20000. unaamua kutompa lakini huwezi kumwambia aondoke kwako na wewe unachumba kimoja kwa ajili yako na mkeo. kwa hakika gharama za kumuweka hapo zitazidi hicho anachokuomba.hivyo ukiendelea kumuamnyima inakula kwako.
babuk matokeo ya mfumo huu wa wachache kuombwa na wengi ndo maana watumishi wote wamebuni PERSONAL ECONOMIC SURVIVAL ACTIVITIES (PESA)-WIZI, RUSHWA SEMINA WASHA AU KUTOKUWEPO KAZINI HUKU WAKILIPWA MISHAHARA NK. ndo maana mashirika 420 aliyoazisha nyerere yamekufa
babuk kumbuka kipato katika afrika kipato chako si chako peke yako ni cha wote wanaokufahamu na wasio kufahamu. sas chukua picha hiyona muuangalie diwani au mbunge- ombaomba wake wantoka kata nzima na jimbo zima.
bado naamini wewe umefika hivi punde kutoka sayari mpya. achana na vitabu maadishi yako ubaoni.