Idadi ya sayari zinazolizunguka Jua

Idadi ya sayari zinazolizunguka Jua

Ningemwita Mgalanjuka, ila kwa namna ulivyouliza napata picha ya ufahamu wako na sidhani kama utamwelewa, tena kwa kiswahili hiki hiki.
Manake nondo zake huwa nasoma, sielewi, hadi namwita mtu mwengine anisomee kwa sauti lakini natoka mweupe.
Tafadhali Monstgala unahitajika huku.

Mkuu Mkiu nimeitikia wito,

Sayari katika mfumo wa Jua ziko nane. Baada ya kukua kwa teknolojia katika upande wa uchunguzi wa anga basi tukapata kuangalia vizuri mfumo huu na hapo ndipo Pluto ilipoonekana kuwa haikidhi vigezo vya kuwa Sayari. Ikaondolewa na kuwekwa kama mojawapo ya vidude vidogo kuliko zilivyo Sayari nyingine (Dwarf planet) kama alivyojibu mkuu apakak.

Mtoa mada kasema "sayari zilizopo Duniani", hakuna Sayari Duniani, ni kosa la muundo wa swali ambalo wadau wameliona lakini kichwa cha mada kimekaa vizuri na kinaeleweka. Hivyo katika mfumo wa Jua ni Sayari nane (8) lakini kama swali lako lililenga nje ya mfumo wa Jua basi yafuatayo ndio makadirio yake.

Sayari zinazoendelea kugunduliwa na kuhakikiwa ziko nje ya mfumo wa Jua. Kuiona sayari iliyo mbali si rahisi kabisa kutokana na ukweli kwamba sayari nyingi hazitoi mwanga kama zilivyo nyota. Hii inapelekea mwanga wa nyota kuzifanya zisionekane lakini kwa mbinu za kisasa sayari hizi zinafuatiliwa katika mifumo ya nyota nyingine na kuhakikiwa. Mpaka sasa zaidi ya sayari 1800 nje ya mfumo wa Jua zimehakikiwa na zimepewa majina.

Makadirio ya wingi wa sayari katika observable universe ni kwamba sayari ziko nyingi sawa na idadi ya nyota. Uwiano wa sayari na nyota ni kwa kila nyota moja kuna sayari moja. nyota 1:sayari 1 . Ni kwamba si rahisi kuziona ila nyota nyingi zinazungukwa na sayari na vitu vingine. Pia kuna baadhi ya sayari zisizozunguka nyota ziko kivyao-vyao. Katika ulimwengu unaoonekana kuna galaxi zaidi ya bilioni 100. Kila galaxi ina nyota kuanzia 10,000 (dwarf galaxies) mpaka trillioni 200( super massive galaxies) Sasa kama nyota katika ulimwengu tunaoweza kuuona ziko zaidi ya mchanga wa beach zote Duniani, ambao unakadiliwa kuwa Quintilion 7.5., basi sayari pia ni lukuki. Nyingi zaidi ya akili inavyoweza kuhesabu labda kukadiria.

Ukitaka majina ya Sayari katika solar system unaweza ku-google tu. Ukitaka kusoma zaidi pia google.

Cheers.
 
Wakuu kwa sasa dunia ina sayari ngapi maana nasikia kuna ugunduzi wa sayari nyingine zaidi ila sijajua ni ngapi. Kwa anayefahamu atupie na majina yake.

Haya Mgalanjuka ameshakuja, kazi kwako kumwelewa.
 
Unazidi kukoroga. Unadhani kuna jua moja? Pengine ungeweka sawa kwa kusema 'hili jua' tunaloliona na kupata mwanga wake.

Jua liko moja tu ila ni mojawapo ya nyota ambazo ziko nyingi. Pia kuna nyota zinazofanana na Jua. Jua ni jina la nyota iliyo karibu yetu (our host star).
 
Wakuu kwa sasa dunia ina sayari ngapi maana nasikia kuna ugunduzi wa sayari nyingine zaidi ila sijajua ni ngapi. Kwa anayefahamu atupie na majina yake.

sidhani kama ulisikia vizuri. dunia yenyewe ni sayari alafu iwe na sayari tena? au imezaa?
 
kwani heading haijabadilika au huoni nini mkuu na kwa kukujulisha tu kuna jua moja tu hakuna jua zaidi ya moja na kama una ushahidi wa kua na zaidi ya jua moja weka hapa.

wewe kweli kichwa chako ni kizito-katika galaxy yetu-milk way galaxy ambayo ni ndogo sana tena sana ndo kuna jua moja. lakini katika galaxy nyingine kuna jua zaidi ya moja. kwa ufupi all the stars you see during the night are suns of other galaxies. they are seen small because they are billions of miles from where we are. pitia Google/vitabu/journals za astronomical studies.
 
Unazidi kukoroga. Unadhani kuna jua moja? Pengine ungeweka sawa kwa kusema 'hili jua' tunaloliona na kupata mwanga wake.
acha uongo.... Jua ni moja tu na ndilo lina angaza sayari zote...

Hadi sasa kuna sayari Tisa zilizothibitishwa japo zipo kma mbili zilogunduliwa lakn bado zpo ktk kufanyiwa utafiti.... Ukitaka ntakutajia sayari zote na ukubwa wa jua na sayari
 
wewe kweli kichwa chako ni kizito-katika galaxy yetu-milk way galaxy ambayo ni ndogo sana tena sana ndo kuna jua moja. lakini katika galaxy nyingine kuna jua zaidi ya moja. kwa ufupi all the stars you see during the night are suns of other galaxies. they are seen small because they are billions of miles from where we are. pitia Google/vitabu/journals za astronomical studies.

Mkuu rolla unamaanisha nini unaposema katika Milky way ndio kuna Jua moja? Milkyway hakika si ndogo ni moja ya galaxi kubwa sana ingawa pia zipo kubwa zaidi. Jua ni jina la nyota yetu tunayoizunguka, kuna nyota nyingine zinazofanana na Jua na zenye mifumo yenye sayari. Hizi ni host stars kwa sayari hizo na pale lugha ya "their suns" inapotumika ni katika kujenga logic ya hizi host stars zenye planetary systems. Kuibeba lugha hii ya "their suns" na kuhitimisha kuwa kuna "majua" mengi ni sawa na kusema kuna "Dunia" nyingi badala ya kusema kuna sayari nyingi. Hata kama tutakapogundua sayari nyingine yenye kufanana kabisa na Dunia yetu, hiyo sayari haiwezi kuwa Dunia nyingine bali sayari nyingine kama Dunia.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu rolla unamaanisha nini unaposema katika Milky way ndio kuna Jua moja? Milkyway hakika si ndogo ni moja ya galaxi kubwa sana ingawa pia zipo kubwa zaidi. Jua ni jina la nyota yetu tunayoizunguka, kuna nyota nyingine zinazofanana na Jua na zenye mifumo yenye sayari. Hizi ni host stars kwa sayari hizo na pale lugha ya "their suns" inapotumika ni katika kujenga logic ya hizi host stars zenye planetary systems. Kuibeba lugha hii ya "their suns" na kuhitimisha kuwa kuna "majua" mengi ni sawa na kusema kuna "Dunia" nyingi badala ya kusema kuna sayari nyingi. Hata kama tutakapogundua sayari nyingine yenye kufanana kabisa na Dunia yetu, hiyo sayari haiwezi kuwa Dunia nyingine bali sayari nyingine kama Dunia.

i am sorry bro: huu mchanyato wako siuwezi, maana inaonekana we are tuning at different frequencies kwa maana hiyo hatuwezi sikilizana, kwa kuwa hatufahamiani: kwa hoja zako nashawishika kuamini kwamba uelewa wako juu ya elimu ya nyota na anga za juu/mbali ni very elementary. nisipoteze mda wangu na wewe usinipotezee wangu. naomba nitembelee forums nyingine time is not on my side.
 
Last edited by a moderator:
i am sorry bro: huu mchanyato wako siuwezi, maana inaonekana we are tuning at different frequencies kwa maana hiyo hatuwezi sikilizana, kwa kuwa hatufahamiani: kwa hoja zako nashawishika kuamini kwamba uelewa wako juu ya elimu ya nyota na anga za juu/mbali ni very elementary. nisipoteze mda wangu na wewe usinipotezee wangu. naomba nitembelee forums nyingine time is not on my side.

Shukrani, all the best.
 
mercury
venus
earth
mars
jupiter
saturn
uranus
neptune
pluto

kumbukumbu za std 5 vingine ni vimondo na satelites tu..
 
Sayari ziko nyingi sana hazina idadi na kila siku wanazidi kugundua. Only Allah knows
 
wewe kweli kichwa chako ni kizito-katika galaxy yetu-milk way galaxy ambayo ni ndogo sana tena sana ndo kuna jua moja. lakini katika galaxy nyingine kuna jua zaidi ya moja. kwa ufupi all the stars you see during the night are suns of other galaxies. they are seen small because they are billions of miles from where we are. pitia Google/vitabu/journals za astronomical studies.

Rolla kwa taarifa tu The Milky way galaxy ni moja ya galaxies kubwa na kwa kiwango cha chini kuna zaidi ya stars 200 bils (Kumbuka Jua letu ni moja ya stars kwenye galaxy yetu-The Milky way, kwa maana nyingine Jua ndo nyota yetu tunayoizunguka ikiwa na hizo sayari 8). Most of the stars you see at night are within the Milky way galaxy. Kumbuka kwa muda wa usiku hata sayari tunaziona kwa sababu zina reflect mwanga wa star yetu (JUA), mfano wa karibu ni Mwezi tunauona kwa sababu una reflect mwanga wa Jua.
 
Mkuu Mkiu nimeitikia wito,

Sayari katika mfumo wa Jua ziko nane. Baada ya kukua kwa teknolojia katika upande wa uchunguzi wa anga basi tukapata kuangalia vizuri mfumo huu na hapo ndipo Pluto ilipoonekana kuwa haikidhi vigezo vya kuwa Sayari. Ikaondolewa na kuwekwa kama mojawapo ya vidude vidogo kuliko zilivyo Sayari nyingine (Dwarf planet) kama alivyojibu mkuu apakak.

Mtoa mada kasema "sayari zilizopo Duniani", hakuna Sayari Duniani, ni kosa la muundo wa swali ambalo wadau wameliona lakini kichwa cha mada kimekaa vizuri na kinaeleweka. Hivyo katika mfumo wa Jua ni Sayari nane (8) lakini kama swali lako lililenga nje ya mfumo wa Jua basi yafuatayo ndio makadirio yake.

Sayari zinazoendelea kugunduliwa na kuhakikiwa ziko nje ya mfumo wa Jua. Kuiona sayari iliyo mbali si rahisi kabisa kutokana na ukweli kwamba sayari nyingi hazitoi mwanga kama zilivyo nyota. Hii inapelekea mwanga wa nyota kuzifanya zisionekane lakini kwa mbinu za kisasa sayari hizi zinafuatiliwa katika mifumo ya nyota nyingine na kuhakikiwa. Mpaka sasa zaidi ya sayari 1800 nje ya mfumo wa Jua zimehakikiwa na zimepewa majina.

Makadirio ya wingi wa sayari katika observable universe ni kwamba sayari ziko nyingi sawa na idadi ya nyota. Uwiano wa sayari na nyota ni kwa kila nyota moja kuna sayari moja. nyota 1:sayari 1 . Ni kwamba si rahisi kuziona ila nyota nyingi zinazungukwa na sayari na vitu vingine. Pia kuna baadhi ya sayari zisizozunguka nyota ziko kivyao-vyao. Katika ulimwengu unaoonekana kuna galaxi zaidi ya bilioni 100. Kila galaxi ina nyota kuanzia 10,000 (dwarf galaxies) mpaka trillioni 200( super massive galaxies) Sasa kama nyota katika ulimwengu tunaoweza kuuona ziko zaidi ya mchanga wa beach zote Duniani, ambao unakadiliwa kuwa Quintilion 7.5., basi sayari pia ni lukuki. Nyingi zaidi ya akili inavyoweza kuhesabu labda kukadiria.

Ukitaka majina ya Sayari katika solar system unaweza ku-google tu. Ukitaka kusoma zaidi pia google.

Cheers.

hapo somo limeeleweka. :A S thumbs_up:
 
Rolla kwa taarifa tu The Milky way galaxy ni moja ya galaxies kubwa na kwa kiwango cha chini kuna zaidi ya stars 200 bils (Kumbuka Jua letu ni moja ya stars kwenye galaxy yetu-The Milky way, kwa maana nyingine Jua ndo nyota yetu tunayoizunguka ikiwa na hizo sayari 8). Most of the stars you see at night are within the Milky way galaxy. Kumbuka kwa muda wa usiku hata sayari tunaziona kwa sababu zina reflect mwanga wa star yetu (JUA), mfano wa karibu ni Mwezi tunauona kwa sababu una reflect mwanga wa Jua.
kama umenielewa vizuri we are on the same boat. but nina wasiwasi na chanzo cha taarifa yako juu ya milky way galaxy
 
acha uongo.... Jua ni moja tu na ndilo lina angaza sayari zote...

Hadi sasa kuna sayari Tisa zilizothibitishwa japo zipo kma mbili zilogunduliwa lakn bado zpo ktk kufanyiwa utafiti.... Ukitaka ntakutajia sayari zote na ukubwa wa jua na sayari

unatuhumu wenzako waongo wakati hakuna ujualo...sayari zipo 8, hiyo ya tisa ambayo ni Pluto haipo katika orodha ya sayari tangu 2006!!
 
kama umenielewa vizuri we are on the same boat. but nina wasiwasi na chanzo cha taarifa yako juu ya milky way galaxy

tuko pamoja kwa upande wa jina la galaxw yetu tu lakini si katika ukubwa wake pamoja na stars zilimo. You cant be serious saying the Milky way is one of the smallest galaxies. Real there is onlw one star in the Milkw way, real!!!!!! and some distant galaxies have two stars!!!!!!????????.
 
Wasi wasi wa kitu gani juu The Milky way; be specific- jina, stars or. Just say what u think is wrong in my comment.

labda wakati mwingine tutaelimishana. mana right now niko bize asubuhi natoa briefing kwa board of directors, na saa 6 tuna ugeni wa kamati ya kudumu ya bunge ya ulinzi na usalama. sorry bro
 
Nyongeza:

........JUA LETU?

Maana kuna mifumo ya jua mingi sana hivi karibuni imegunduliwa mingine mingi na kwa ujumla inakadiriwa kuwa na sayari zaidi ya 700

Sidhani kama kuna jua jingine zaidi ya hili kuna nyota nyingine ambazo zipo kama ulivo mfumo wa jua
 
Back
Top Bottom