Idadi ya nondo katika floor ya ghorofa

Idadi ya nondo katika floor ya ghorofa

Memory

Senior Member
Joined
Jun 29, 2011
Posts
106
Reaction score
37
Naomba nifahamu ghorofa standard yenye urefu wa mita 20 na upana wa mita 10 inahitaji nondo za aina ngapi na kwa idadi ipi ili kukamilisha ile level ya kwanza tu bila kuhusisha zile zilizoko katika foundation na beam. Hapa nataka nifahamu idadi ya nondo kwa kila 10 or 20square meters ya 1st, 2nd....n floors.
 
Kwanii usiwasiliane na wakandarasi mbali mbali ili kulinganisha ujuzi?
 
Kwanii usiwasiliane na wakandarasi mbali mbali ili kulinganisha ujuzi?

Heshima mbele mkuu,
Majibu ya humu huwa yanafaida kwa wengi sio kwa muulizaji tu
kuna watu wako mbali na nyumbani(Tanzania) na hawana uwezo wa kuwaona hao makandarasi na wana plan ya kujenga maghorofa mara wafikapo nyumbani,
kama unajua weka wazi tu ili watu wakokotoe gharama
 
Heshima mbele mkuu,
Majibu ya humu huwa yanafaida kwa wengi sio kwa muulizaji tu
kuna watu wako mbali na nyumbani(Tanzania) na hawana uwezo wa kuwaona hao makandarasi na wana plan ya kujenga maghorofa mara wafikapo nyumbani,
kama unajua weka wazi tu ili watu wakokotoe gharama
Mkuu, kuna tatizo gani ukiwasiliana na ndugu, jamaa na marafiki walioko nyumbani ili wakutafutie hizo dataz.
 
Mkuu nakutahadharisha tena nakuomba sana, ujenzi wa ghorofa (gorofa) maswala ya nondo mwachie Engineer si suala la kukisikia au kuulizia mitaani au kwa fundi mzoefu. Nasema hakuna kitu kama hicho, utakuja juta baadae!! Mahesabu ya nondo yanafanywa kwa utaalamu (calculations) kutumia fomula sio kukisia, ukubwa wa eneo/unene wa zege (floor thickness), matumizi ya jengo na pia ratio (vipimo) vya zege. "Foundation" ndio inabeba kila kilicho juu ya ghorofa, kwa hiyo huwezi kubadili juu bila kurekebisha chini au kujua chini kuna uwezo gani.
* Tuache njia za mkato, mme sahau mara hii kilichotokea Changombe/Kariakoo/Kisutu na kwengineko?
 
Mkuu nakutahadharisha tena nakuomba sana, ujenzi wa ghorofa (gorofa) maswala ya nondo mwachie Engineer si suala la kukisikia au kuulizia mitaani au kwa fundi mzoefu. Nasema hakuna kitu kama hicho, utakuja juta baadae!! Mahesabu ya nondo yanafanywa kwa utaalamu (calculations) kutumia fomula sio kukisia, ukubwa wa eneo/unene wa zege (floor thickness), matumizi ya jengo na pia ratio (vipimo) vya zege. "Foundation" ndio inabeba kila kilicho juu ya ghorofa, kwa hiyo huwezi kubadili juu bila kurekebisha chini au kujua chini kuna uwezo gani.
* Tuache njia za mkato, mme sahau mara hii kilichotokea Changombe/Kariakoo/Kisutu na kwengineko?

kwani humu hakuna engineerz?
 
Kila point hapa ni muhimu katika kufanya maamuzi, lakini pia tusisahau kuwa hapa kuna wahandisi wazuri tu ambao wanaweza kutupatia rough estimations ili unapowasililiana na watu wa mbali bado utakuwa na picha ya vitu kadha wa kadha. Tuendelee kuelimishana.
 
Haiwezekani kupata jibu kwa data hizo tu, inategemea na design ya jengo, aina na concrete mix, hizo nondo zitapangwa vipi etc.

Pia unasema ghorofa ya n hauwezi kufanya hesabu kihivyo, construction ya ghrorofa ya n iko effected na ghorofa zilizo juu yake na probably chini yake as well. Kwa kifupi zidhani kama unaweza kupata jibu la maana bila kuconsider design nzima.
 
Haiwezekani kupata jibu kwa data hizo tu, inategemea na design ya jengo, aina na concrete mix, hizo nondo zitapangwa vipi etc.

Pia unasema ghorofa ya n hauwezi kufanya hesabu kihivyo, construction ya ghrorofa ya n iko effected na ghorofa zilizo juu yake na probably chini yake as well. Kwa kifupi zidhani kama unaweza kupata jibu la maana bila kuconsider design nzima.

Heshima Mbele mkuu Kang,
Haya hapa chini ni maelezo muhimu ya jamaa

"Naomba nifahamu ghorofa standard yenye urefu wa mita 20 na upana wa mita 10 inahitaji nondo za aina ngapi na kwa idadi ipi ili kukamilisha ile level ya kwanza tu bila kuhusisha zile zilizoko katika foundation na beam. Hapa nataka nifahamu idadi ya nondo kwa kila 10 or 20square meters ya 1st, 2nd....n floors."
 
kwani humu hakuna engineerz?
Wapo lakini mkuu kuna taaluma zingine zinahitaji face2face consultations, sio rahisi kuomba ushauri wa daktari unapohitaji upasuaji ni lazima daktari afanye mwenyewe. Mgonjwa huwezi chukua kisu ukapasua tumbo. Kadhalika masuala ya nondo kwenye jengo la ghorofa ni mambo ya calculation si ya makisio kama vile unavyofikiria. Kwa maana ingine ni taaluma ya kulipia, ndio maana lazima Engineer uwe legally registered/licensed ili ukiboronga uwajibishwe.
 
Naomba nifahamu ghorofa standard yenye urefu wa mita 20 na upana wa mita 10 inahitaji nondo za aina ngapi na kwa idadi ipi ili kukamilisha ile level ya kwanza tu bila kuhusisha zile zilizoko katika foundation na beam. Hapa nataka nifahamu idadi ya nondo kwa kila 10 or 20square meters ya 1st, 2nd....n floors.

Kinacho determine idadi na aina/ubora wa ndondo sio ukubwa wa eneo peke yake. Designer atatakiwa kujua pia aina ya mzigo inayokusudiwa kubebwa na hiyo floor (dead and live loads) na location zake. Kwa kifupi ni vigumu mno kwa engineer yoyote kuja hapa kusema ni idadi fulani ya nondo utahitaji unless afanye assumption ya hizo factors zote nyingine.
 
Kinacho determine idadi na aina/ubora wa ndondo sio ukubwa wa eneo peke yake. Designer atatakiwa kujua pia aina ya mzigo inayokusudiwa kubebwa na hiyo floor (dead and live loads) na location zake. Kwa kifupi ni vigumu mno kwa engineer yoyote kuja hapa kusema ni idadi fulani ya nondo utahitaji unless afanye assumption ya hizo factors zote nyingine.

hapo kwenye Green ndipo pa muhimu, assumption zikiwa kumi mtu atajua pa kuanzia
 
Heshima Mbele mkuu Kang,
Haya hapa chini ni maelezo muhimu ya jamaa

"Naomba nifahamu ghorofa standard yenye urefu wa mita 20 na upana wa mita 10 inahitaji nondo za aina ngapi na kwa idadi ipi ili kukamilisha ile level ya kwanza tu bila kuhusisha zile zilizoko katika foundation na beam. Hapa nataka nifahamu idadi ya nondo kwa kila 10 or 20square meters ya 1st, 2nd....n floors."
Best option ....chukua ramani zako muone QUALIFIED ENGINEER atakueleza kila utakacho taka kujua. Maelezo utakayopewa hapa sikushauri kuyapokea.
 
Shule tosha kabisa, lakini hawa wajasilimiamali wa kibongo pia hawako serious maana kuna jamaa aliniambia ana mtaalam nikampatia design toa Italy lakini mpaka leo sioni. Lakini nimepata data za kuanzia. Ahsanteni.
 
Naomba nifahamu ghorofa standard yenye urefu wa mita 20 na upana wa mita 10 inahitaji nondo za aina ngapi na kwa idadi ipi ili kukamilisha ile level ya kwanza tu bila kuhusisha zile zilizoko katika foundation na beam. Hapa nataka nifahamu idadi ya nondo kwa kila 10 or 20square meters ya 1st, 2nd....n floors.

Mkuu Urefu wa mita 20 ni average ya ghorafa 5 hadi 6. Mkuu haya mambo hayahitaji blaa blaa. Tafuta Architect akuchoree kwanza kutokana na mahitaji yako then Structural Engineer atamaliza kazi yako

Structural Engineer atakusaidia kujua utakuwa na slabs za unene upi na saizi ya nondo na idadi yake pamoja na kiasi gani utatumia kwenye slab yako. Atakusaidia kujua utaweka beams za saizi ipi kama ni 230*450mm, 230*500, 230*600 nk pamoja na idadi na saizi ya nondo, atakusaidi kujua pia utatumia nguzo(columns) za saizi ipi na nondo za saizi ipi na idadi yako, njia hizo hizo atatumia kwenye ngazi, vitako(pads) nk.
Hayo yote yanahitaji mahesabu wala hamna longo longo, yote haya yanafanyika baada ya architect kuchora michoro yake yenye mpangilio wa vyumba, elevations zake na sections pia.
 
Jaribu nondo mbili halafu tupe jibu...tujifunze toka kwako mkuu itakuwa poa au laah!! Ma injinia wa kariakoo wakiwa kazini kuangalia idadi ya nondo zao hadi raha..sasa kazi hakuna na mtu kachukua tena tayari ya ukandarasi hadi raha....usishangae kuona magorofa ya kko yana ufa kama michoro ya wasanii au ramani ya mito.

from what i think kama unataka kujenga gorofa, idadi ya nondo inaendana na vitu vingi sana... Best luck mkuu
 
Nondo sio lazima

Unaweza kutumia njia kama hii inayotumika makoko Nigeria



teh teh teh
 
Last edited by a moderator:
Hili halihitaji longolongo sana! Mfuate architect na structural eng's wakusaidie vizuri. Kama uko dar au unaifahamu dar vizuri, jaribu kuchunguza magorofa tofauti tofauti kwa umakini kuhusu matumizi yake, halafu jiulize swali lako barabara.
 
Wingi na ukubwa wa nondo hutegemea aina ya Zege, ubora wake na unene wake.

Wanasema ni heri uzidishe Zege kuliko kuzidisha nondo. Jengo lililozidiwa uzito na limejengwa na nondo dhaifu, huwa linaanza kupata mipasuko na hiyo kuwajulisha wakazi kuwa janga linakuja. Jengo lililojengwa na Zege dhaifu na nondo nyingi, hatari yake ni kuwa kuvunjika bila kutowa tahadhari (ghafla).

Kabla hujajua aina ya nondo, kwanza unaangalia upana/urefu wa hizo sakafu zenyewe. Hapo unaanza kupanga zege ya ubora gani itumike. Ukishapata aina ya zege, ndiyo unakuja sasa kupiga mahesabu unene wa nondo, ubora wake, aina na idadi yake. Kumbuka nondo nyingi kwenye jengo ni hatari sana na utakuja kuuwa watu bure.

Zege imara linasababisha ukubwa wa nondo kupungua. Kama una Zege imara kwa mfano lenye glass fibres, huweki nondo. Naungana na wale waliokupa onyo kuwa usijijengee ghorofa bila wataalamu kulipitia. Nasikitika sana kwa hali iliyopo sasa Tanzania kuwa mtu anajijengea tu jengo lake bila usimamizi wowote imara kutoka kwa wataalamu. Kama waipenda familia yako, sikiliza maonyo ya hao jamaa juu.
 
Back
Top Bottom