ice-USA, mwenye uelewa, sijaelewa!

ice-USA, mwenye uelewa, sijaelewa!

Kijakazi

Platinum Member
Joined
Jun 26, 2007
Posts
9,351
Reaction score
15,069
bado sijaelewa hivi hawa ice ambao wako kwenye news kila mahali tatizo liko wapi? kwa nini stress hizi zoote na maandamano ya kuwapinga, je, wanaonea watu au tatizo ni nini? nilifikiri labda wanafanya control ya watu ambao wako nchini USA illegally au kwa maneno mengine hawakupswa kuwepo USA, sasa tatizo liko wapi hapo kama kwa mfano wewe ni mgeni na una kila kitu i.e vibali vya kuwepo huko USA kwa nini iwe tabu kuwaonyesha tu vibali vyako na kuendelea na maisha yako au bado watakuonea hata kama una kila kitu? iweje mpaka watu wanauliwa kwa risasi au kuumizwa, je ni vibali tu vya kuishi huko au kuna mengine labda?

i am confused ...
 
Wageni wanaua wakristo U.S

ICE ipo kulinda wakristo,Western Christian system na ku fight against communists.

Tuwaunge mkono ICE mtumishi wanakomesha jihadists na communists
 
ICE wengi ni wapya na proMAGA na tatizo lao kubwa wanalolamikiwa ni kwamba wanafanya kazi za kwa mfumo kama wa policeCCM. Wakiwa wanafanya operations mahali wakikuhisi tu wewe sio raia kwa sababu sio mzungu mweupe mfano ni black, asian, Mwarabu au latina watataka uwape kitambulisho(racial profiling) sasa unaweza kuwa ni raia kabisa wa Marekani tena uliyezaliwa hapo ila wakati huo hauna kitambulisho, unaweza kuwa ni mhamiaji ambaye uko kwenye mchakato wa kupata nyaraka za ukimbizi, green card, uraia au kuongeza muda wa visa hapo ndipo mtiti utakapokuja sasa mpaka wakuelewe wasikutie jela au hata kukufanyia deportation.

Kuna raia wengi tu Wamarekani ambao sio wenye asili ya Wazungu wamejikuta wanashikiliwa mahabusu au wamefanyiwa deportation na ICE ya Trump. Sasa kwa sababu Wamarekani wengi hawajazoea na hawapendi uonevu kama huo ndipo unaona hizo vurugu zote raia wakiliamsha, sio kama bongo mtu atakuja achukuliwe tu kwenye bus, bar, kazini au nyumbani kwake bila utambulisho na maelezo ya kueleweka halafu wanaomzunguka wakae kimya wamejikunyata.
 
bado sijaelewa hivi hawa ice ambao wako kwenye news kila mahali tatizo liko wapi? kwa nini stress hizi zoote na maandamano ya kuwapinga, je, wanaonea watu au tatizo ni nini? nilifikiri labda wanafanya control ya watu ambao wako nchini USA illegally au kwa maneno mengine hawakupswa kuwepo USA, sasa tatizo liko wapi hapo kama kwa mfano wewe ni mgeni na una kila kitu i.e vibali vya kuwepo huko USA kwa nini iwe tabu kuwaonyesha tu vibali vyako na kuendelea na maisha yako au bado watakuonea hata kama una kila kitu? iweje mpaka watu wanauliwa kwa risasi au kuumizwa, je ni vibali tu vya kuishi huko au kuna mengine labda?

i am confused ...
ICE kule Marekani ni kifupi cha U.S. Immigration and Customs Enforcement — yaani Idara ya Utekelezaji wa Sheria za Uhamiaji na Forodha ya Marekani.

Kwa ufupi, ICE hufanya kazi hizi kuu:

  • Kusimamia sheria za uhamiaji: Kuwabaini, kuwakamata, na kuwaondoa (kurejesha) wahamiaji wasio na vibali halali.
  • Kupambana na uhalifu wa kuvuka mipaka: Kama usafirishaji haramu wa binadamu, dawa za kulevya, silaha, na bidhaa bandia.
  • Kulinda usalama wa taifa: Kuchunguza makosa yanayohusiana na ugaidi, fedha haramu, na uhalifu wa kimataifa.
ICE iko chini ya Idara ya Usalama wa Ndani ya Marekani (Department of Homeland Security – DHS).

Kimsingi, ICE sio idara ya kutoa visa au uraia; kazi hizo ziko kwa USCIS. ICE inalenga zaidi utekelezaji wa sheria.
 
ICE wameruhusiwa kumkamata mtu yeyoye wanayehisi ni mhamiaji, kwahiyo hawathibitishi mambo mwisho wa siku makundi yenye sifa mbaya kama weusi, waislamu na wamexico wanakamatwa zaidi.

Watu wameuawa, hadi watoto wamekamatwa bila kupewa nafasi ya kujitetea kisheria.

Trump ameweka lengo la kuondoa wahamiaji 1,000,000 kwa mwaka. Ili kufikia hili lengo mambo yanafanyika kihuni.
 
ICE wengi ni wapya na proMAGA na tatizo lao kubwa wanalolamikiwa ni kwamba wanafanya kazi za kwa mfumo kama wa policeCCM. Wakiwa wanafanya operations mahali wakikuhisi tu wewe sio raia kwa sababu sio mzungu mweupe mfano ni black, asian, Mwarabu au latina watataka uwape kitambulisho(racial profiling) sasa unaweza kuwa ni raia kabisa wa Marekani tena uliyezaliwa hapo ila wakati huo hauna kitambulisho, unaweza kuwa ni mhamiaji ambaye uko kwenye mchakato wa kupata nyaraka za ukimbizi, green card, uraia au kuongeza muda wa visa hapo ndipo mtiti utakapokuja sasa mpaka wakuelewe wasikutie jela au hata kukufanyia deportation.

Kuna raia wengi tu Wamarekani ambao sio wenye asili ya Wazungu wamejikuta wanashikiliwa mahabusu au wamefanyiwa deportation na ICE ya Trump. Sasa kwa sababu Wamarekani wengi hawajazoea na hawapendi uonevu kama huo ndipo unaona hizo vurugu zote raia wakiliamsha, sio kama bongo mtu atakuja achukuliwe tu kwenye bus, bar, kazini au nyumbani kwake bila utambulisho na maelezo ya kueleweka halafu wanaomzunguka wakae kimya wamejikunyata.

hilo mbona hata tanzagiza wanafanya mara nyingi nimevuka boda kwa basi na polisi wakisimamisha basi kukagua wa kwanza ni msomali, ethiopia au yoyote ambaye anauonekano ambao siyo wa kibongo, nimeshasafiri na wasomali ambao walikaguliwa na uhamiaji wao tu peke yao isistoshe bado sielewi kuna tatizo gani kama ukiulizwa kitambulisho na kuwaonyesha bado ''watakuonea'' tu? ...
 
Hao wanaokataa ni Pro Democrats


Acha wapelekewe moto

Wasomali wamepiga Hela wanazitakatoshia Eastleigh Kenya
ICE wengi ni wapya na proMAGA na tatizo lao kubwa wanalolamikiwa ni kwamba wanafanya kazi za kwa mfumo kama wa policeCCM. Wakiwa wanafanya operations mahali wakikuhisi tu wewe sio raia kwa sababu sio mzungu mweupe mfano ni black, asian, Mwarabu au latina watataka uwape kitambulisho(racial profiling) sasa unaweza kuwa ni raia kabisa wa Marekani tena uliyezaliwa hapo ila wakati huo hauna kitambulisho, unaweza kuwa ni mhamiaji ambaye uko kwenye mchakato wa kupata nyaraka za ukimbizi, green card, uraia au kuongeza muda wa visa hapo ndipo mtiti utakapokuja sasa mpaka wakuelewe wasikutie jela au hata kukufanyia deportation.

Kuna raia wengi tu Wamarekani ambao sio wenye asili ya Wazungu wamejikuta wanashikiliwa mahabusu au wamefanyiwa deportation na ICE ya Trump. Sasa kwa sababu Wamarekani wengi hawajazoea na hawapendi uonevu kama huo ndipo unaona hizo vurugu zote raia wakiliamsha, sio kama bongo mtu atakuja achukuliwe tu kwenye bus, bar, kazini au nyumbani kwake bila utambulisho na maelezo ya kueleweka halafu wanaomzunguka wakae kimya wamejikunyata
 
ICE kule Marekani ni kifupi cha U.S. Immigration and Customs Enforcement — yaani Idara ya Utekelezaji wa Sheria za Uhamiaji na Forodha ya Marekani.

Kwa ufupi, ICE hufanya kazi hizi kuu:

  • Kusimamia sheria za uhamiaji: Kuwabaini, kuwakamata, na kuwaondoa (kurejesha) wahamiaji wasio na vibali halali.
  • Kupambana na uhalifu wa kuvuka mipaka: Kama usafirishaji haramu wa binadamu, dawa za kulevya, silaha, na bidhaa bandia.
  • Kulinda usalama wa taifa: Kuchunguza makosa yanayohusiana na ugaidi, fedha haramu, na uhalifu wa kimataifa.
ICE iko chini ya Idara ya Usalama wa Ndani ya Marekani (Department of Homeland Security – DHS).

Kimsingi, ICE sio idara ya kutoa visa au uraia; kazi hizo ziko kwa USCIS. ICE inalenga zaidi utekelezaji wa sheria.

asante kwa maelezo mazuri kwa hiyo wako kwa mujibu wa sheria za USA sasa tatizo liko wapi, kwa nini wanwazuiwa wasifanya kazi zao kwa maandamano na fujo za kila aina wakati wako kwa mujibu wa sheria na wanafwata sheria? ...
 
hilo mbona hata tanzagiza wanafanya mara nyingi nimevuka boda kwa basi na polisi wakisimamisha basi kukagua wa kwanza ni msomali, ethiopia au yoyote ambaye siyo mweusi, nimeshasafiri na wasomali ambao walikaguliwa na uhamiaji wao tu peke yao ...
Sasa hilo si bus lilikuwa limevuka boda! Pia Tanzania sio nchi ya Wahamiaji kama Marekani kwa hiyo ukimkuta Mwarabu, Muethihopia au Msomali anazurura huko Sirari unaweza kushituka. Marekani ni nchi ya Wahamiaji na katika majiji yao wamejaa raia wa kila aina wenye uraia, green cards, nyaraka za ukimbizi n.k kutoka kote duniani, hizo operations za ICE ambako unaona vurugu zinazuka zinafanyika mbali kabisa na mipaka ya Marekani zikilenga zaidi Blue states za Democrats kisiasa.
 
Sasa hilo si bus lilikuwa limevuka boda! Pia Tanzania sio nchi ya Wahamiaji kama Marekani kwa hiyo ukimkuta Msomali huko Sirari unaweza kushituka. Marekani ni nchi ya Wahamiaji na katika majiji yao wamejaa raia wa kila aina wenye uraia, green cards, nyaraka za ukimbizi n.k kutoka kote duniani, hizo operations za ICE ambako unaona vurugu zinazuka zinafanyika mbali kabisa na mipaka ya Marekani zikilenga zaidi Blue states za Democrats kisiasa.

lkn bado sielewi kuna shida gani kama ukiulizwa kitambulisho na mamlaka iliyoko kisheria na kuwaonyesha na kisha kuendelea na mambo yako? ...
 
asante kwa maelezo mazuri kwa hiyo wako kwa mujibu wa sheria za USA sasa tatizo liko wapi, kwa nini wanwazuiwa wasifanya kazi zao kwa maandamano na fujo za kila aina wakati wako kwa mujibu wa sheria na wanafwata sheria? ...
Tatizo liko kwenye "weaponizasition of law/lawfare" kama vile uhamiaji na TRA bongo ambavyo hurukia wakosoaji wa serikali ya CCM kwa kigezo cha kufuata sheria tu lakini wakiwa na malengo mengine tofauti kabisa.
 
Democrats wanaunga mkono uhamiaji haramu,hawa watu mwishowe wanapata uraia,watoto zao wanakuwa raia.

Kisha wanakuwa wanapigia kura democrats kwenye uchaguzi, republican party hawataki hizi mambo. Wana enforce immigration rules. Wakati wa Biden karibia wahamiaji milioni 10 waliingia Marekani kinyume cha sheria.
Democrats na mashabiki wao ndiyo wanaleta hizo fujo dhidi ya Ice. Kama unapata habari kupitia CNN, BBC,the guardian nk basi lazima urahisi ice ndiyo wakorofi. Maana hivyo ni vyombo vya habari vya mlengo wa kushoto.
 
lkn bado sielewi kuna shida gani kama ukiulizwa kitambulisho na mamlaka iliyoko kisheria na kuwaonyesha na kisha kuendelea na mambo yako? ...
Kuna mamilioni ya raia wa Marekani hawana vitambulisho.
 
lkn bado sielewi kuna shida gani kama ukiulizwa kitambulisho na mamlaka iliyoko kisheria na kuwaonyesha na kisha kuendelea na mambo yako? ...
Hawapewi due process.

Kabla hujaondolewa lazima upewe nafasi ya kusikilizwa kesi yako mahakamani kwasababu kuna njia nyingi za kupata uraia, kila mtu ana kesi yake.

Hata haki ya kutumia mwanasheria hawapewi. Kwahiyo ni changamoto.
 
asante kwa maelezo mazuri kwa hiyo wako kwa mujibu wa sheria za USA sasa tatizo liko wapi, kwa nini wanwazuiwa wasifanya kazi zao kwa maandamano na fujo za kila aina wakati wako kwa mujibu wa sheria na wanafwata sheria? ...
Ndiyo mkuu wapo chini ya sheria kadhaa mojawapo ni Homeland Security Act, 2002, Immigration and Nationality Act (INA) (Hii INA ndio sheria kuu ya uhamiaji ya Marekani) nakadhalika!
 
Back
Top Bottom