Habari ndugu wanajamvi!
Kagame, amseveni, Kenyatta, Mugabe, Albashiri ndio wanaoonekana vinara wa mpango huu, sasa tujiulize kuna nini nyuma ya pazia la utawala wao?
''Kagame, Museveni, Kenyatta, Mugabe, Albashiri.''
Kagame the killer without any doubt, ndiye aliitungua ndege ya rais na kusababisha mauaji ya kikatili nchini mwake, anaiba utajiri wa congo kwa kushirikiana na Museveni ambaye anamwachia madaraka mtoto wake, jiulize tangu lini rais anataka kumwachia madaraka mwanae. Huyu huyu Museveni ameshindwa kuwakabili Waganda wenzake ambao wako msituni wanapigana naye tangu aingie madarakani kuna sehemu hatii mguu. Ndiye huyu huyu Museveni aliyekuwa anataka kupigana vita na kenya kuhusu kisiwa kwenye lake victoria .... .. jiepushe na hili jini .... .... ..
Kenyatta inajulikana mauaji yaliyotokea kwenye uchaguzi uliopita sio huu alioshinda kinyemela kama nkwere.
Mugabe baada ya kupigwa ban na wazungu kwenda kufanya shopping za nguvu kila mwezi kwa pesa za walipa kodi na kujinufaisha binafsi, kujenga hekalu pale nje kidogo ya Harare kwa pesa za walipa kodi .... .. hata nkwere anajenga kule nsoga kwa njia kama hiyo. Kuua wapinzani kwa njia za ujambazi, raia kupotea bila kujulikana walipo nk the guy is a killer from the word go ..... .... remember jinsi alivyopanga mauaji ya Tongogara kule Mozambique under the nose of Samora.
Bashir kuua raia weusi wa South Sudan kwa kutumia ndege za kivita .... ..... raia wasiokuwa na any type of defence.
Viongozi wa Afrika wanaiogopa ICC kwa sababu ICC hawawezi kuhongwa kama majaji wa hizi nchi ambao kwanza wanapewa vyeo hivyo sio kwa merit bali kwa kuhongwa. Come on ICC flush these dictactors.
Hapo kwenye BLUE ndugu mbona huyu huyu Museven ndio ameteuliwa kuwa msuluishi wa Mgogoro wa DRC je waliomteua hawayajui haya uliyoyaandika? au ni propaganda tu ambazo hazina ukweli.
Viongozi wa kiafrika pamoja na kufuta tongotongo lakini bado hawana tofauti yoyote na ma chief wa makabila yetu miaka ile ya giza.
Kitendo cha wao kukubaliana na kusaini mkataba wa Roma na kisha baadae kuanza kulalamika na kutaka kujitoa ni kitendo ambacho hakina tofauti yoyote na mikataba aliyokuwa anaingia chief Mangungo wa Msowero!
Kama viongozi wetu wa kiafrika wangekuwa na akili nzuri wangekuwa wanajadiliana na kushauriana namna ya kuimarisha demokrasia na utawala bora katika nchi zao badala ya kwenda kupanga mipango miovu dhidi ya wananchi wao kisha wanabaki kulialia mara tu wanaposhtakiwa ICC kwa ufedhuli wao.
Hapo kwenye BLUE ndugu mbona huyu huyu Museven ndio ameteuliwa kuwa msuluishi wa Mgogoro wa DRC je waliomteua hawayajui haya uliyoyaandika? au ni propaganda tu ambazo hazina ukweli.
Utadharaulika na nani mkuu? Tatizo hii mahakama inabagua mataifa na nchi za kufuatilia. Waende Uingereza na Marekani wakafanye hivyo hivyo hakuna hata mtu atakayewaonyeshea kidole
ICC ni ukoloni mambo leo
Utadharaulika na nani mkuu? Tatizo hii mahakama inabagua mataifa na nchi za kufuatilia. Waende Uingereza na Marekani wakafanye hivyo hivyo hakuna hata mtu atakayewaonyeshea kidole
Ukweli wakati wanasaini huu mkataba niliwapinga nikiamini ni ukoloni mamboleo,lakini kwa vile AFRIKA KAMA AFRIKA mpaka leo imeshindwa kuunda chombo chake imara cha kusimamia viongozi wake ambao wengi wao wana chembechembe za kidictator na ukatili kwa UMMA na 'iachwe ICC ifanye yake'.