ICC na watawala wa Afrika

Ukweli hawa manyang'au wa Africa wana-practice era ambayo nahisi ni ya nyuma kuliko hata ya ukoloni. Badala ya kukutana wajadili wanaisaidianaje wasababishe maujibarani Africa wao wanfanya mambo ya ajabu kabisa. Yaani kwa ufupi wana-Africa wote tunapaswakupinga hili kwa nguvu zote..........................
 
Wengi wao ni "WATEJA WATARAJIWA". Ndio maana wana tokwa povu kuhusu ICC. Hivi si ujiulize ni kwa nini JK anahaha kuPiga kelele kuhusu ICC? Si ni kwa sababu anajuwa tayari jina lake limesha kuwa NOTED, hadi kupelekea baadhi ya maafisa kuitembelea Tanganyika. Huku akijua wazi kwamba jamaa hawana haraka kwenye kufuatilia tuhuma.

Ukizingatia SEBENE la 2015 anaota "MARUWE RUWE" ya kutoka kwenye FASTJET na kuwa mbeba "MTONDOO" nyuma ya NONDO.
 
Bara la Afrika kwa sasa ndilo linaloongoza kwa kuzalisha marais wengi madikteta,sasa marais wa aina hiyo wanapoketi Addis Ababa na kutoa mwito kuwa wao wana uwezo wa kuendesha kesi hizo nchini mwao.

Hivi katika nchi za kidikteta zinaweza kuwa na mahakama zinazoweza kutenda haki kwa kutoa hukumu za haki kwa wale waliotenda makosa,bila kujali political power zao?!

Jibu la wazi ni kuwa hilo haliwezekani kabisa kwenye nchi zetu.

Hebu tuonyeshe mfano mmoja tu wa madaraka aliyopewa Waziri wetu wa habari wa kuchunguza,kushitaki, na kuhukumu yeye mwenyewe bila kutoa nafasi ya upande unaoshitakiwa kujitetea!!

Kwa mazingira hayo nawaomba ICC muendeleze uzi huo huo, wa kuwaburuza hawa viongozi wetu madikteta na kuwapeleka the Hague, ambako huko hakuna cha DPP, wala IGP, wala TISS wa kuweza kuzizima hizo kesi!!
 
Back
Top Bottom