ICC justice is selective – Kagame

ICC justice is selective – Kagame

Mkama ni jina Takatifu na tunategemea mwenye nalo awe hivyo,Afande Kagame ni JEMBE hii inakwenda bila kupingwa wale watu wamejipanga, tunatumia fedha nyingi kwenda SINGAPORE kuona maendeleo yalivyo na tunarudi na perfume za wapendwa wetu tu ,wakati wenzetu walienda na matokeo yake yanaonekana.....tujipange......!!! EID MUBARAK.
 
Hana jipya, ni wale wale madikteta. Mwizi mkubwa huyo, arejeshe mali alizopora kwanza.
 
Kagame is like many strong and smart people, they are the engineers of their own demise

hakuna kiongozi kama yeye when it comes to setting goals, developing strategies and implement actions to achieve his goals, kila nilipopata bahati ya kukaa na watu wa international development na tukianza kuongea mambo ya Africa, he is next to none... governance, clients service, responsible and accountable government officers, contracts management, keeping his words, environment protection, urbanization, investment attraction, quick turn around you name it

However, his biggest challenge is to know his limit, and to to be patients

hats of his success, but a 'watch out dude" to his hasty decisions

(like)
 
Kagame ni Mwizi wa madini DRC na muuaji mkubwa !!!!
Sasa kama hana hatia kwa nini anaogopa Mahakama???
 
kama wewe sio mtuhumiwa kwa nn uogope mahakama ya icc viongozi wa africa acheni ubwege akuna kujito mtu hapo kagame yupo makinisana
 
Kapambana sana kuiweka Rwanda ilipo leo, japokua ana mikono michafu lakini amefanya juhudi kubwa sana kusaka maendeleo ya nchi yake
 
Hana jipya, ni wale wale madikteta. Mwizi mkubwa huyo, arejeshe mali alizopora kwanza.

Watanzania bana!Wakati mwingine tunaonekana kama vile mazuzu.Tunajifanya tuna uchungu na rasilimali za Wacongo wakati za kwetu wenyewe tunashindwa kuzilinda.Wakenya wanatupiga bao na Tanzanite zetu kule Arusha na tumeridhika tu wenyewe,Tembo wetu wanauawa kila siku,Wanyama wanatoroshwa Nchini kupitia Ndege lakini hatuonekani kujali utafikiri sisi sio Watanzania vile sasa huu uthubutu wa kuwa na uchungu na rasilimali za Wacongo tunautoa wapi tena?
 
Mahakama ya ICC idumu ili iwape funzo viongozi waroho wa madaraka.
 
hii sio njia sahihi ya kuchambua matendo ya kagame.ukiweka mada ya jinsi kagame anavyosimamia nchi ya Rwanda ikawa pamoja na jinsi kagame alivyoingia madarakani utakua na lengo la kumtetea zaidi.kiuchumi kagame amefanya makubwa na anaona mbali sana,ni kiongozi/mtawala anaemaanisha,lakini hilo halitoshi kumuondolea ubaya aliofanya.na ICC ni chombo kinachowashughulikia watawala wanaomwaga damu za watu,sasa kagame atasaini hapo?
 
hii sio njia sahihi ya kuchambua matendo ya kagame.ukiweka mada ya jinsi kagame anavyosimamia nchi ya Rwanda ikawa pamoja na jinsi kagame alivyoingia madarakani utakua na lengo la kumtetea zaidi.kiuchumi kagame amefanya makubwa na anaona mbali sana,ni kiongozi/mtawala anaemaanisha,lakini hilo halitoshi kumuondolea ubaya aliofanya.na ICC ni chombo kinachowashughulikia watawala wanaomwaga damu za watu,sasa kagame atasaini hapo?

Unajua tatizo letu kubwa ni kufuata mkumbo sasa sijui kwanini tunamchukia Kagame kwa anayowafanyia Raia wake wakati huo huo tunamtukuza Mchina ambaye kiutawala hana tofauti na Kagame.Ni nini hasa Watanzania tunachokisimamia ndo ambacho ninatamani kukifahamu.
 
Ile Arusha tribunal haikuwa inahusika na Rwanda genocide?
Je Arusha Tribunal haikuwa chini ya ICC???? kama hakusaini ICC ilikuwaje Rwanda ikahusishwa???
I SMELL THE RAT!!!!!
 
Kagame alionekana "DIKTETA" Kutoungamkono ICC leo nchi kibao zinataka kujitoa….. Naamini i[po siku kwahii issue ya congo pia Kagame Tutamuelewa tu..

Mahakama za kimataifa Kagame hazipendi sababu yeye mwenyewe alikuwa anatakiwa na mahakama ufaransa akasepa.Kwa hiyo kugomea ICC kunaeleweka aligoma akiogopa kuwa akisaini helikopta ingetua kigali kumbeba mzobemzobe hadi huko mahakamani

.Nchi nyingi za kiafrika kugomea ICC ni kwa sababu ya kutaka ku-harmonize sheria za ndani za nchi zao zinazowalinda na zile za kimataifa.Sheria Za ndani za nchi nyingi zinadai kiongozi hawezi shitakiwa akiwa madarakani kama mkuu wa nchi.Hivyo wamenogewa na hilo wanataka na ICC itamke hivyo hivyo.

Ila kuhusu suala la kumtetea Kenyatta na Rutto wamechemka.Kenyatta na Rutto walianza kushtakiwa wakiwa si maraisi.Kesi ile ilikuwa ni kesi endelea.Sasa wakisema wasiende the HAGUE si sahihi.VIONGOZI WA AFRICAN UNION KWA HILO WAMECHEMKA.

Pia kusema ICC inashtaki viongozi wa afrika tu si kweli ICC inashtaki wahalifu iwe waafrika au wazungu.Haishtaki waafrika.Ile ni mahakama inayoshughulika na wahalifu sio waafrika au wazungu.Kusema haibebi wazungu wanataka kusemaje kama wazungu haiwabebi kwa hiyo wahalifu waafrika waendelee na uhalifu wao? Mahakama lazima iwe na pa kuanzia tunashukuru imeanza na wahalifu wa huku kwetu Na CHARLES TAYLOR kala miaka yake 50 JELA.

Wananchi tungependa ICC iendelee kukamata viongozi wahalifu wa kivita hasa Afrika.Kama ni kipau mbele cha kamata kamata nawaomba ICC ipeni kipaumbele Afrika kuna bado viongozi wahuni na wahalifu sana huku na wengi wanajificha kwenye visheria walivyojitungia vya kutoshitakiwa wakiwa madarakani.Kesi za KENYATTA na RUTTO naomba endeleeni na kesi zao hadi kieleweke ilianza kabla hawajawa viongozi ICC endeleeni nayo hadi kieleweke.ICC HOYEE
 
The thread is trying to diverge attention and the facts of who is who in criminal world!!!
Regardless of how ......
 
Watanzania bana!Wakati mwingine tunaonekana kama vile mazuzu.Tunajifanya tuna uchungu na rasilimali za Wacongo wakati za kwetu wenyewe tunashindwa kuzilinda.Wakenya wanatupiga bao na Tanzanite zetu kule Arusha na tumeridhika tu wenyewe,Tembo wetu wanauawa kila siku,Wanyama wanatoroshwa Nchini kupitia Ndege lakini hatuonekani kujali utafikiri sisi sio Watanzania vile sasa huu uthubutu wa kuwa na uchungu na rasilimali za Wacongo tunautoa wapi tena?


Inapofikia suala la Kagame huwa sikuelewi kabisa ndugu, hivi kusema mtu fulani ni mwizi lazima awe amekuibia wewe?Mdau kasema huyo Kagame anaiba dhahabu ya Congo unasema anajidai anauchungu nayo wakati Tanzania pia wanaiba viongozi wetu, kwani hao viongozi wetu kama Kinana na mzee wa Ndovu hatuwasemi? Yaani hata kama ni mwizi asisemwe kisa anaiba nje ya Tanzania?

Kumsema Kagame kuwa anaiba Congo ni kuwa na uchungu na Congo?
 
Hivi Kaka yupi Bora kati ya hawa Wawili??
1.tajiri sana kutokana na mali nyingi ya urithi waliyoachiwa (yeye na wadogo zake)na marehem baba yao...Ni mbinafsi mno kiasi kwamba amejikuta AKIWADHULUMU wadogo zake kwa kuuza mali karibu yooote kwa kuendekeza anasa akiamini naye atafariki siku yoyote huku wadogo zake wakishindia mihogo kila siku...Mind you MALI inakaribia kuisha

2.Huyu nae ana wadogo zake,bahati mbaya baba yao kafariki na hakuwa na MALI yoyote ya kuwaachia Urithi...Anawapenda sana wadogo zake,amefikia hatua ya kwenda KUDHULUMU mali ya jirani yake ambayo ni kama SHAMBA LA BIBI na kuhamishia kwao akiamini nae siku yoyote atafariki anahitaji kuwaachia mali na misingi bora wadogo zake...Mind you MALI imekua nyingi na inaendelezwa na kusimamiwa vizuri
 
Hivi Kaka yupi Bora kati ya hawa Wawili??
1.tajiri sana kutokana na mali nyingi ya urithi waliyoachiwa (yeye na wadogo zake)na marehem baba yao...Ni mbinafsi mno kiasi kwamba amejikuta AKIWADHULUMU wadogo zake kwa kuuza mali karibu yooote kwa kuendekeza anasa akiamini naye atafariki siku yoyote huku wadogo zake wakishindia mihogo kila siku...Mind you MALI inakaribia kuisha

2.Huyu nae ana wadogo zake,bahati mbaya baba yao kafariki na hakuwa na MALI yoyote ya kuwaachia Urithi...Anawapenda sana wadogo zake,amefikia hatua ya kwenda KUDHULUMU mali ya jirani yake ambayo ni kama SHAMBA LA BIBI na kuhamishia kwao akiamini nae siku yoyote atafariki anahitaji kuwaachia mali na misingi bora wadogo zake...Mind you MALI imekua nyingi na inaendelezwa na kusimamiwa vizuri



Hapo kwenye Bold fanya hivi, huyu mtu baba yake alikuwa na wake wawili na tumbo lake wamezaliwa wawili yeye na mdogo wake na mama mwingine anawatoto watatu au wa4. Kaka huyu anakwenda kuiba/kudhulumu vya jirani na kumnufaisha zaidi mdogo wake wa kuzaliwa naye mmoja na kutowajali wale watatu kisa tu mama zao walikuwa na bifu la siku nyingi kipindi cha uhai wao ambapo bitu hilo ndilo lilipelekea wakauana.
 
Back
Top Bottom