Ibada ya kweli kwa Muafrika ni tambiko

njundelekajo

JF-Expert Member
Dec 26, 2012
310
227
IBADA YA KWELI KWA MUAFRIKA NI TAMBIKO TU.

Tambiko ni ibada yenye asili ya Afrika.Katika tambiko muombaji hufikisha haja yake kwa mungu kupitia sadaka za kuchinja,kuteketeza mali na mengineyo.

Kwakua imani zote zimejenga dhana kwamba mungu ni wa kuogopwa na kuheshimika sana pasi kuruhusu mawasiliano ya moja kwa moja kati ya Mungu na binadamu,wamewekwa wajumbe wa kuyapokea na kuwasilisha maombi kwa Mungu.

Tambiko katika muktadha huu pia limeweka mjumbe anayeitwa Mzimu kama daraja la mawasiliano kati ya Mungu na binadamu.

MZIMU NI NANI?

Mzimu ni mtu aliyekufa. kwenye ukoo au familia ambaye jamii husika inaamini katika uhai wake aliishi maisha ya kumpendeza Mungu.Kinyume cha mzimu ni Kizuka.

Kwakua inaaminika mtu mwema anapokufa hukaa kwa Mungu ndivyo ndani ya tambiko inaaminika hivyo.Hivyo ni sahihi kuomba kupitia mzimu ili maombi yafikishwe kwa Mungu.

Hivyo ,kuna tofauti ndogo kati ya Mzimu na mtakatifu anayetajwa kwenye ukatoliki.Tofauti yenyewe ni mchakato unafanya huyu aitwe mtakatifu na huyu mwingine Mzimu.Ingawa wote wawili wanafanana katika msingi wa maisha yao kabla ya kufa.

Ndio maana ndani ya ukatoliki kuna watakatifu wengi kama mizimu ilivyokua mingi.

Kwakua Yesu na Mohamed ni bindamu waliokufa katika dhana iliyoelezwa hapo juu ya kuzingatia maisha maisha yao enzi za uhai hawa ni mizimu

Historia kama maarifa Yesu na Mohmed ni wanaharakati waliokua wakifanya harakati zao huko mashariki ya kati karibu na mito Euphrates na Tigris ambapo inaaminika harakati hizi ndizo zilizozaa mtazamo wa kiimani uliopo sasa.

NINI KILITOKEA ?

Kwanza tukubaliane ujio wa ukoloni Afrika hakua na nia njema kwa muafrika mwenyewe.Kama hivyo sawa basi yote yalionzishwa ,kukuzwa na kuimarishwa nao hayawezi kuwa mazuri ikiwamo na dini.

Wakati ule wanafika Afrika kwa lengo la kutunyonya wakakutana na Tambiko.Kwakua ibada hiyo na imani nyingine za kiafrika hazikutoa nafasi ya kutimiza lengo lao,wakaamua kuliua Tambiko .Hvyo wakaanzisha Propaganda Tambiko ni uchawi na ushenzi.

Kwenye Tambiko sadaka hapewi mtu mmoja kama ni chakula kinaliwa na wote walioshiriki ama wote kuacha.Kama wangeacha Tambiko liendelee wangeshindwa timiza lengo lao la unyonyaji kupitia dini.

Hivyo wakaleta ibada ambazo mtu mmoja mwenye afya tele,nguvu na akili anapokea sadaka yote na kuzila au kuzitumia kwa niaba ya Mungu.

NINI MADHARA YA WAAFRIKA KULITUPA TAMBIKO.

Enzi za Tambiko kulikua na utaratibu uliowekwa kwa wote wanaotakiwa kishiriki kwenye ibada hiyo.Baadhi ya jamii watu waliofanya ngono kabla ya ndoa ,wezi,ambao wana ugomvi na wengine hawakuruhusiwa.

Hivyo si tu ilipunguza mmonyoko wa maadili lakini pia magonjwa kama ukimwi,kisonono na mengine hayakuwepo licha ya kutokuwapo kinga kama kondomu.

Na kwakua yalikua maombi stahiki kwa muafrika sehemu kubwa ya maaombi hayo yalijibiwa na Mungu.

Waafrika walipoomba mvua walipata,walipoomba mavuno walipata.Sasa hivi haiwezekani kuomba mvua na ikanyesha kwa sababu mizimu tunayoiomba si ya Keri ni ya warabu na wazungu.Ndio maana warabu na wazungu wanafanikiwa sana kuliko sisi wa Afrika kutokana na usahihi wa kuitumia mizimu yao.

JE TURUDI KWENYE TAMBIKO?

Ndio ,tukirudi kwenye misingi ya Uafrika wetu kizazi chetu kitabaki salama kwenye maeneo mengine yote.

Kama tutairudisha imani yetu basi pia tutapata namna yetu ya kuwapata viongozi wetu kupitia demokrasia yetu wenyewe ambayo haitafanya tuchinjane kama hii.

Tukirudi kwenye tambiko basi tupata namna ya kiimani ya kuendesha mambo yetu pasipo kufuata principles na kanuni za kimgharibi.

Kwakua imani ni tiba ya mambo yote mara tukaporudisha Tambiko Afrika tutagundua pia utajiri wa Taifa la Tanzania ukiupima kwenye kanuni za wazungu hutouona.

Wao wanapima shughuli zifanyazwo na wananchi wanakwepa kwa makusudi kujumlisha milima,madini,,tembo nk kwa sababi wana hakika mtawaamini kama mkishawaamini hata katika namna ya kuabudu.

Noel Nguzo.R.

20/1/2019
 
hakika umesema mkuu.
Mi nimekuelewa vyema na huo ndo ukweli japo wengi hawaujui.
Ni vigumu sana mara baada ya mkoloni kutuvisha IMANI yake na imetukaa BARABARA leo kukubali ukweli huu.

Watu wengi wamekuwa waanga sana baada ya kupokea imani za wakoloni na kusahau kule walipotoka.

Hii imekuwa ni mojawapo ya propaganda za kalne zile tulizotawaliwa na hao jamaa na kufikia hatua hii tuliyo nayo leo.

Hata serikali zote duniani mara baada ya kupoteza dini za awali nazo zimekumbatia UZUNGU na UHARABU pamoja na kwamba serikali wanachotaka ni AMANI tu.

**Namkumbuka marehemu mzee kingunge ambaye yeye inasemekana hakuwa mfuasi wa imani za wakoloni.

NB.
Bado nafasi ipo kila mtu kuamua kuabudu anachoona ni sahihi ili mradi asivunje katiba ya nchi.
 
kuna babu yetu yeyote mwenye historia ya kufanya mambo aliyoyafanya yesu
kupaa
kufufua watu
kutembea juu ya maji
kulisha watu elfu 5
nk,nk.nk
 
IBADA YA KWELI KWA MUAFRIKA NI TAMBIKO TU.

Tambiko ni ibada yenye asili ya Afrika.Katika tambiko muombaji hufikisha haja yake kwa mungu kupitia sadaka za kuchinja,kuteketeza mali na mengineyo.

Kwakua imani zote zimejenga dhana kwamba mungu ni wa kuogopwa na kuheshimika sana pasi kuruhusu mawasiliano ya moja kwa moja kati ya Mungu na binadamu,wamewekwa wajumbe wa kuyapokea na kuwasilisha maombi kwa Mungu.

Tambiko katika muktadha huu pia limeweka mjumbe anayeitwa Mzimu kama daraja la mawasiliano kati ya Mungu na binadamu.

MZIMU NI NANI?

Mzimu ni mtu aliyekufa. kwenye ukoo au familia ambaye jamii husika inaamini katika uhai wake aliishi maisha ya kumpendeza Mungu.Kinyume cha mzimu ni Kizuka.

Kwakua inaaminika mtu mwema anapokufa hukaa kwa Mungu ndivyo ndani ya tambiko inaaminika hivyo.Hivyo ni sahihi kuomba kupitia mzimu ili maombi yafikishwe kwa Mungu.

Hivyo ,kuna tofauti ndogo kati ya Mzimu na mtakatifu anayetajwa kwenye ukatoliki.Tofauti yenyewe ni mchakato unafanya huyu aitwe mtakatifu na huyu mwingine Mzimu.Ingawa wote wawili wanafanana katika msingi wa maisha yao kabla ya kufa.

Ndio maana ndani ya ukatoliki kuna watakatifu wengi kama mizimu ilivyokua mingi.

Kwakua Yesu na Mohamed ni bindamu waliokufa katika dhana iliyoelezwa hapo juu ya kuzingatia maisha maisha yao enzi za uhai hawa ni mizimu

Historia kama maarifa Yesu na Mohmed ni wanaharakati waliokua wakifanya harakati zao huko mashariki ya kati karibu na mito Euphrates na Tigris ambapo inaaminika harakati hizi ndizo zilizozaa mtazamo wa kiimani uliopo sasa.

NINI KILITOKEA ?

Kwanza tukubaliane ujio wa ukoloni Afrika hakua na nia njema kwa muafrika mwenyewe.Kama hivyo sawa basi yote yalionzishwa ,kukuzwa na kuimarishwa nao hayawezi kuwa mazuri ikiwamo na dini.

Wakati ule wanafika Afrika kwa lengo la kutunyonya wakakutana na Tambiko.Kwakua ibada hiyo na imani nyingine za kiafrika hazikutoa nafasi ya kutimiza lengo lao,wakaamua kuliua Tambiko .Hvyo wakaanzisha Propaganda Tambiko ni uchawi na ushenzi.

Kwenye Tambiko sadaka hapewi mtu mmoja kama ni chakula kinaliwa na wote walioshiriki ama wote kuacha.Kama wangeacha Tambiko liendelee wangeshindwa timiza lengo lao la unyonyaji kupitia dini.

Hivyo wakaleta ibada ambazo mtu mmoja mwenye afya tele,nguvu na akili anapokea sadaka yote na kuzila au kuzitumia kwa niaba ya Mungu.

NINI MADHARA YA WAAFRIKA KULITUPA TAMBIKO.

Enzi za Tambiko kulikua na utaratibu uliowekwa kwa wote wanaotakiwa kishiriki kwenye ibada hiyo.Baadhi ya jamii watu waliofanya ngono kabla ya ndoa ,wezi,ambao wana ugomvi na wengine hawakuruhusiwa.

Hivyo si tu ilipunguza mmonyoko wa maadili lakini pia magonjwa kama ukimwi,kisonono na mengine hayakuwepo licha ya kutokuwapo kinga kama kondomu.

Na kwakua yalikua maombi stahiki kwa muafrika sehemu kubwa ya maaombi hayo yalijibiwa na Mungu.

Waafrika walipoomba mvua walipata,walipoomba mavuno walipata.Sasa hivi haiwezekani kuomba mvua na ikanyesha kwa sababu mizimu tunayoiomba si ya Keri ni ya warabu na wazungu.Ndio maana warabu na wazungu wanafanikiwa sana kuliko sisi wa Afrika kutokana na usahihi wa kuitumia mizimu yao.

JE TURUDI KWENYE TAMBIKO?

Ndio ,tukirudi kwenye misingi ya Uafrika wetu kizazi chetu kitabaki salama kwenye maeneo mengine yote.

Kama tutairudisha imani yetu basi pia tutapata namna yetu ya kuwapata viongozi wetu kupitia demokrasia yetu wenyewe ambayo haitafanya tuchinjane kama hii.

Tukirudi kwenye tambiko basi tupata namna ya kiimani ya kuendesha mambo yetu pasipo kufuata principles na kanuni za kimgharibi.

Kwakua imani ni tiba ya mambo yote mara tukaporudisha Tambiko Afrika tutagundua pia utajiri wa Taifa la Tanzania ukiupima kwenye kanuni za wazungu hutouona.

Wao wanapima shughuli zifanyazwo na wananchi wanakwepa kwa makusudi kujumlisha milima,madini,,tembo nk kwa sababi wana hakika mtawaamini kama mkishawaamini hata katika namna ya kuabudu.

Noel Nguzo.R.

20/1/2019
Ushirikina kwenda mbele

Mitume na Manabii wa Mola,walikuwa hawana matambiko,kisha walikuwa na miujiza ya wazi katika kudhihirisha nguvu za Muumba

Tambiko halina nafasi kwa mwanaadam
Bali ni upotevu wa wazi

Halina mjumbe wala ustaarabu
Bali ni upuuzi na ujinga uliotawala
ndio maana Waafrika tukatawaliwa kwa Haraka
na kuuliwa ktk vita ya maji maji kwa dhana potofu


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hiyo Ilikuwa njia fyongo ya kumtafuta Mungu.

Bibilia Imekuja kuwaelekeza kwenye Tambiko halisi Kwa Mungu aliyehai sio maiti za mababu zao, na mashetani.

'' Kwa Maana Jinsi hii Mungu aliupenda Ulimwengu hata akamtoa mwanaye wa pekee ili kila amuaminiye asipotee bali awe na uzima wa milele'' Yohana 3:16.

Kuendelea kukumbatia Giza wakati mwanga upo, ni ujinga.
 
HiyoVipi ukiomba mvua Ilikuwa njia fyongo ya kumtafuta Mungu.

Bibilia Imekuja kuwaelekeza kwenye Tambiko halisi Kwa Mungu aliyehai sio maiti za mababu zao, na mashetani.

'' Kwa Maana Jinsi hii Mungu aliupenda Ulimwengu hata akamtoa mwanaye wa pekee ili kila amuaminiye asipotee bali awe na uzima wa milele'' Yohana 3:16.

Kuendelea kukumbatia Giza wakati mwanga upo, ni ujinga.
 
kuna babu yetu yeyote mwenye historia ya kufanya mambo aliyoyafanya yesu
kupaa
kufufua watu
kutembea juu ya maji
kulisha watu elfu 5
nk,nk.nk
Mwanamalundi wa usukumani aliweka maziwa yakakaa miaka bila kuganda akiwa kifungoni kisiwani, aliukausha mti mkubwa sana kama ishara yake ya mwisho wakati akikamatwa na askari wa kikoloni, soma historia ya utamaduni wako ndugu usiishie kwenye sunday school tu na madrasa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Inashangaza mno na bado hatujakua kiakili, Mleta mada mie nimekupongeza sana, hili mada jana tumeliongea na mzee moja hapa kwetu ,nanukuu usemi wake " mjukuu wangu mwafrika hawezi kugundua kitu chochote tuliaambiwa na mjerumani mmoja hata kiberiti hatuwezi kukitengeneza"
 
Kabla ya uislamu waarabu nao walikuwa wanafuata imani za mababu zao za kama kuabudu masanamu,na ndio maana huwa inasemwa ulitumika upanga kueneza huo uislamu kwa sababu watu walikuwa hawataki kuacha imani za mababu zao na kuachia dini ya muhammad kuenea na kuondoa imani zao za asili.

Leo hii uislamu unaonekana ndio imani asili ya waarabu na hatuoni waarabu kulalamika uislamu kuwa umeondoa imani asili za mababu zao,na hii sio kwa uislamu na waarabu tu bali hata ukristo na jamii zengine kama wazungu nao walikuwa na imani zao hapo kabla ila ajabu waafrika tu ndio tunalilia imani za mababu zetu na kuona hatufanikiwi kisa tumeacha imani za mababu.
 
Back
Top Bottom