I have been scammed 1,100$ through Forex

brightoscar

JF-Expert Member
Dec 29, 2013
360
517
Basi Ndugu zangu naandika hii ili kuwapa umakini Na haya mambo ya Forex mwanzo nilifanya Forex kupitia Templer FX nikapoteza Pesa nyingi Na BoT ilivyoingilia ikabidi niachane nayo, then kwenye Instragram nikaona program inaitwa BINOMO nikaidownload kwenye IOS nikaanza kutrade nikawa napata na kukosa inadepend na prediction unazoweka if the price will be up or down then kuna siku nikapata USD 200 kila nikajaribu kutoa inadelay then inabaki kwenye system nikavutiwa kuendelea ikaliwa yote.

Ikabidi niandike complain kwenye page yao ya Instagram maana tangu nimeanza nimepoteza like 500$ then nikaona kuna account imeniadd ya dada inatumia @kelseysabrina1 akanifuata DM akaniambia wana platform yao ambayo unainvest then they trade for you after 7 days unapata profit yako so ukiweka 200$ after 7days u get 2000$ akanishawishi nikajaa nikamtumia 200$ through bitcoins akaniunganisha kwenye platform yao inaitwa 360fxpool nikaona kwenye account yangu trading inaendelea after 7days ikawa 1400$ nikamuuliza mbona sio 2000$ kama tulivyoongea akasema kuna tatizo kwenye system baada ya muda ikabadilika ikawa 2975$ inclusive bonus kwasababu ni end of the year.

Then akaniambia kwenye policy ya kampuni yao imepitishwa withdrawal fee ya 205$ for that amount inabidi ilipiwe before withdrawal kwasababu other customers sio waaminifu wakitoa hawatoi commission nikatuma tena through bitcoins I see alivyopokea akaniblock kila kona nikajua nimepigwa.

Then nikaona jamaa kwenye Instagram Ad anaitwa @Branson_Rodgers akitangaza kufanya trading through bitcoins with nice profit but within 2 days nilivyoona ni ads nikamuamini nikawasiliana nae nikamueleza what happened akasikitika sana na kuniambia hutakiwi kutuma hela kabla hujapata profit yako nikaona huyu ni legit akaniambia initial capital ni 500$ within 2 days unapata 50% profit then unamtumia commision yake 20% nikacheck website anayotumia fxbitcointrade.com nikaona ni legit nikamtumia 500$ baada ya kutuma akaniambia pending withdrawal yangu inaonyesha itakuwa 2,000$ kwahiyo ili aweze kutrade inabidi niongeze 200$.

Ikabidi niongeze katrade 1st day ikawa 854$ 2nd day ikafika 1,400$ 3rd day ikafika 2,550$ kimbembe kikafika wakati wakutoa jamaa anasema nitume 300$ withdrawal fee nikaona ndio yaleyale nikajua nishapigwa tena ikawa ishafika 1,100$ nikajua ni kutokana na kutotoa fungu la kumi nikapiga moyo konde na kuanza moja kuweni makini jamani hakuna easy money wala hakuna mtu atakufanyia trade au kukusaidie upate hela huyu jamaa bado yuko Instagram na anaweka ads angalia msiibiwe jamani.

IMG_6744.JPG


IMG_6641.JPG


IMG_6914.JPG


Adjustments.JPG


IMG_6703.JPG


IMG_6633.JPG


IMG_6923.JPG
 
Eti tuma withdrawal fee ya $ 2 000 ? Si wakate huko huko wanipe $ 1 700?

Lingine...eti mtu a -trade kwa ajili yangu.

Anisaidie nipate faida kisha nikajichukulie pesa niliyosaidiwa na mtu fulani kuitafuta.

Jiulize kwanini yeye asitrade mwenyewe? Anauhakika hiyo faida yako anaweza kuimake sasa kwanini atafute kidogo kutoka kwako wakati akifanya mwenyewe anapata kingi?

Trade mwenyewe.
 
1100$ ni kama 2.5 milion ungeweza kuanzisha hata mgahawa wako mdogo amboa ungepata 20000 kama faida kwa siku

Kwa mwaka ungeweza kutengeneza milion 7.2

Vijana tubuni miradi pesa haiji hivi hivi.

Mimi uwa nawekeza kwenye vitu vidago vidogo na napiga pesa kweli nahakikisha hata kama niko kwenye majukumu mengine miradi inajiendesha yenyewe kwa simu.

Ukiwa na mighawa 5, saloon za kiume 5 pikipiki 5 na bajaji 5 kwa siku unatengeneza pesa kama laki3
 
Internet scams kama hizi ni common sana, yaani unajuwa kabisa huu ni utapeli kama zile
"mimi ni mtoto wa mwanasiasa flani mkubwa, baba yangu kafa kaacha pesa nyingi nje,sijuwi alikuwa uhamishoni, natakiwa nitume pesa flani ya kulipia bima na mengineyo nitumiwe pesa yangu, Sasa naomba uwatumie pesa kiasi hicho hao jamaa kisha watakuingizia pesa hii kwako tutagawana, nitakulipa riba kubwa au tutagawana 50/50".

Ukituma ndio ishakula kwako.
 
Back
Top Bottom