Jidu La Mabambasi
JF-Expert Member
- Oct 20, 2014
- 18,135
- 29,792
Tunaendelea kushangaa matamshi ya huyu jamaa, Mzanzibari, eti Makamu wa Rais Nchimbi ni Yuda na msaliti.
Haya ni matamshi mazito kwa kiwango chochote.
Kwanza, sijui kama swala la usaliti, Bungeni ni mahali pake.
Pili, hatukuwahi kumsikia huyu Simai akilaani mauaji ya Oktoba 29, ambayo yalitekelewa kwa ushikiano na vikosi vya Zanzibar.
Tatu, ni ukosefu wa heshima na utovu wa nidhamu kwa matamshi haya ya ndugu Simai.
Nne na si mwisho, kila mtu ajajiuliza kuwa katumwa na nani?
Na je, hii ni ajenda ya Wazanzibari?