Agresive
JF-Expert Member
- Feb 18, 2018
- 889
- 1,226
Nawasalimu kwa JMT.
Katika miaka 5 iliyopita hakuna rangi ambayo hatujaona.
Ni kipindi wafanyabiashara walihama nchi.
Kodi ilikusanywa kibabe na akaunti kufungwa.
Kesi za kubambikiziwa uhujumu uchumi zilitamalaki.
Wahitimu wa vyuo walisahau kabisa kuhusu ajira.
Watumishi waliambia sitaongeza mshahara wala kupanda daraja,
Tulilazimishwa kupiga makofi na vigelegele kwa jambo zuri au baya.
Wanasiasa wa upinzani waliota joto la jiwe.
Katika yote hayo mtendaji mkuu master akijiita mtetezi wa wanyonge, wakati wanyonge wakilala njaa na kuambiwa maneno kuwa barabara zinajengwa,ndege kununuliwa vitu vyote hivyo vinawahusu.
Mungu hana kamati akafanya maamuzi,magumu sana.
Awamu ya 6 ikaja na maneno mapya kabisa ya kutia moyo.
1. Sitaki kodi ya dhuluma
2. Vyombo vya habari vifunguliwe
3. Sitaki uongozi wa kunyanyasa watu isipokuwa haki itendeke.
4. Wafanyabiashara na wawekezaji watengenezewe mazingira rafiki.
5. Mahusiano mema na nchi jilani na jumuiya ya kimataifa.
NAENDELEA KUJIULIZA KATIKA YOTE HAYA JE
Huyu ndiyo tuliyemtarajia mkombozi wetu au tuendelee kusubiri!!!
Katika miaka 5 iliyopita hakuna rangi ambayo hatujaona.
Ni kipindi wafanyabiashara walihama nchi.
Kodi ilikusanywa kibabe na akaunti kufungwa.
Kesi za kubambikiziwa uhujumu uchumi zilitamalaki.
Wahitimu wa vyuo walisahau kabisa kuhusu ajira.
Watumishi waliambia sitaongeza mshahara wala kupanda daraja,
Tulilazimishwa kupiga makofi na vigelegele kwa jambo zuri au baya.
Wanasiasa wa upinzani waliota joto la jiwe.
Katika yote hayo mtendaji mkuu master akijiita mtetezi wa wanyonge, wakati wanyonge wakilala njaa na kuambiwa maneno kuwa barabara zinajengwa,ndege kununuliwa vitu vyote hivyo vinawahusu.
Mungu hana kamati akafanya maamuzi,magumu sana.
Awamu ya 6 ikaja na maneno mapya kabisa ya kutia moyo.
1. Sitaki kodi ya dhuluma
2. Vyombo vya habari vifunguliwe
3. Sitaki uongozi wa kunyanyasa watu isipokuwa haki itendeke.
4. Wafanyabiashara na wawekezaji watengenezewe mazingira rafiki.
5. Mahusiano mema na nchi jilani na jumuiya ya kimataifa.
NAENDELEA KUJIULIZA KATIKA YOTE HAYA JE
Huyu ndiyo tuliyemtarajia mkombozi wetu au tuendelee kusubiri!!!