8) Epuka kutukana, kushambulia au kukwaza wengine: Maandiko ya chuki na yenye mrengo wa kuwashambulia watu hayatovumiliwa na JamiiForums. Wachukulie (waheshimu) wengine kama ambavyo wewe unataka uchukuliwe (uheshimiwe). Hivyo, kuleta andiko ambalo litachochea muitikio hasi kwa watu wengine inashauriwa kuepukwa.
Jiepushe kutuma kitu chochote ambacho ni kichafu, chukizo au cha kudhalilisha ambacho kinaweza kuvunja haki miliki ya mtu au haki yake ya faragha (privacy). Ikiwa unajiuliza mwenyewe kama jambo fulani linafaa, yawezekana halifai.