kisugujira
JF-Expert Member
- Aug 13, 2012
- 774
- 200
"Nchi yetu kwa muda mrefu imekuwa ni kisima cha amani na mfano wa kuigwa. Lakini sasa hivi kuna ufa umetokea nchini hakuna amani. Wakristo na waislamu wameishi kwa kuheshimiana na kwa upendo kwa muda mrefu. Hivi karibuni kumekuwepo na chokochoko za kidini. Makanisa yanachomwa moto, mapadri, wachungaji na waumini wanauawa.
Chama Cha Wananchi CUF kiliitwa ni chama cha kiislamu! Sasa hivi CHADEMA kinasemwa ni chama cha kikristo! Haya yote yanasemwa na serikali na wabunge wa CCM bungeni yakilenga kujenga hofu na kuleta chuki kwa wabunge wa upinzani na wananchi.''
Maneno hayo yalisemwa na Mh.Zito Kabwe wakati wa mjadala wa wizara ya mambo ya ndani baada ya tukio la kusikitisha na kutisha lililotokea Arusha. Aliomba liundwe azimio litakalokemea na kupinga kauli za chuki (hate speeches) toka kwa wabunge wa CCM kwenda kwa wabunge wa vyama vya upinzani bungeni.
Pia alipendekeza mihadhara ya kidini yenye kuleta na kuchochea chuki ipigwe marufuku nchini, huku akisisitiza upendo na umoja kwa kusema, "Sisi sote ni ndugu. Linapokuja swala linalohusu maslahi ya Taifa,tofauti za vyama, dini na ukabila yatupasa kuvitupilia mbali."
Leo hii azimio hilo na mambo mengine yenye manufaa kwa Taifa yamepigiwa kura na kuungwa mkono na wabunge wote bungeni Dodoma, huku Mh. Dr Augustino Lyatonga Mrema, akitoa siku saba za kukomesha mihadhara yote ya kidini hapa nchini.
Chama Cha Wananchi CUF kiliitwa ni chama cha kiislamu! Sasa hivi CHADEMA kinasemwa ni chama cha kikristo! Haya yote yanasemwa na serikali na wabunge wa CCM bungeni yakilenga kujenga hofu na kuleta chuki kwa wabunge wa upinzani na wananchi.''
Maneno hayo yalisemwa na Mh.Zito Kabwe wakati wa mjadala wa wizara ya mambo ya ndani baada ya tukio la kusikitisha na kutisha lililotokea Arusha. Aliomba liundwe azimio litakalokemea na kupinga kauli za chuki (hate speeches) toka kwa wabunge wa CCM kwenda kwa wabunge wa vyama vya upinzani bungeni.
Pia alipendekeza mihadhara ya kidini yenye kuleta na kuchochea chuki ipigwe marufuku nchini, huku akisisitiza upendo na umoja kwa kusema, "Sisi sote ni ndugu. Linapokuja swala linalohusu maslahi ya Taifa,tofauti za vyama, dini na ukabila yatupasa kuvitupilia mbali."
Leo hii azimio hilo na mambo mengine yenye manufaa kwa Taifa yamepigiwa kura na kuungwa mkono na wabunge wote bungeni Dodoma, huku Mh. Dr Augustino Lyatonga Mrema, akitoa siku saba za kukomesha mihadhara yote ya kidini hapa nchini.