BRN
JF-Expert Member
- Nov 18, 2013
- 5,379
- 6,890
Yaani Mkuu ufahamu yote hayo uliyoyaeleza ushindwe hili? Kweliiiii?
Hilo bado sijalipata
Hilo bado sijalipata
Kasomi kajinga tena! Nadhani utakumbuka namaanisha nini. Umenichekesha kwa jibu lako hili la bado la ukwe hujalipata. Umenikumbusha bwana mmoja alimtambulisha jamaa mmoja kwangu. Akisema ni rafiki yake wa siku nyingi. Jamaa alipoondoka nikamuuliza mwenyeji wetu jina la huyo rafiki yake. Huwezi amini jibu alonipa. Hamfahamu jina! Rafiki yake sana?Hilo bado sijalipata
huu uzi umekaa ki chawa chawa saaana🙄🙄Huyu Ndiye Mohamed O. Mchengelwa
Teuzi Mpya za Baraza la la Mawaziri zimemuibua kijana Mzalendo na Mchapakazi.
Mohamed Omar Mchengelwa.
Mh.Mchengelwa ni Mbunge wa Rufiji toka 2015 akichukua nafasi ya
ya aliyekuwa Waziri wa Afya wakati wa Mzee JK Dr Seif Rashid.
Mh.Mchengelwa ni Mwanasheria msomi na bobezi katika eneo la Mahakama alikofanya kazi kabla ya kuwa Mbunge.
Mchengelwa Ni Mwanafunzi wa Shahada ya Tatu (PhD) katika Siasa na Mahusiano ya Kimataifa katika Chuo Kikuu Cha "Girne America University" nchini Cyprus.
Ukiacha hayo amekuwa Msaidizi wa Jaji Mkuu wa Tanzania kwa miaka sita(2009-2015).
Bungeni kwa muda mrefu amekuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Katiba na Sheria mpaka wakati huu Mh.Raisi anamteuwa kuwa Waziri.
Mh.Mchengelwa ni miongoni mwa Wabunge wenye kujenga hoja zenye maslahi makubwa kwa wananchi ya Jimbo la Rufiji na Tanzania kwa Ujumla.
Mfano hoja yake kwa nini tozo ya huduma inayopaswa kulipwa na Kampuni za kigeni zinazojenga Mradi wa Umeme wa Mwl Nyerere ilipwe halmashauri ya Wilaya ya Kinondoni badala ya Rufiji kwenye Mradi imepelekea wilaya Rufiji kupokea mabilioni ya pesa kutoka kwenye makampuni hayo na kuchangia kwa kiasi kikubwa maendelo ya wilaya hiyo kongwe, (Rufiji ni Wilaya toka Mkoloni).
Michango yake Bungeni imechangia kiasi kikubwa kuanza kwa Mradi wa Umeme wa Mwalimu Nyerere uliokwama kwa zaidi ya miaka 60(Rejea Ansad Bungeni)
Wakati fulani aliamshra fulaha Bungeni alipokumbusha ahadi ya Mwalimu Nyerere ya kujenga Barabara Tarafa ya Mkongo wilayani Rufiji aliyoitoa 1955 wakati wa Kikao Cha Halmashauri kuu ya Tanu kikichofanyika Tarafa ya Mkongo Rufiji.
Kwa Jitihada zake Mh Mchengelwa, halmashauri sasa wanajenga Shule ya Upili Tarafa ya Mkongo yenye jina la Muaaisi na Mpigani Uhuru wa Nchi hii Bibi Titi Mohamed.
Kwa Jimbo lake hakika ni Mwanasisa wa kupigiwa Mfano na kwa wanaojua siasa za Rufiji huwa ni ngumu Sana kwa Mbunge kupenya awamu ya pili lakini kwake haikuwa kazi ngumu sana kutokana na aliyoyafanya ndani ya awamu yake ya kwanza.
Kuanzia katika Utatuzi wa migogoro ya wakulima na wafugaji,Changamoto za maji,Barabara na Umeme.
Hatma ya hekari elfu hamsini zilizotengwa kando ya Mto Rufiji baada ya kukamilika ujenzi wa mradi Mwalimu Nyerere.
Kutowajibika ipasavyo kwa Mamlaka ya uendelezaji wa bonde la mto Rufiji/Rubada(Kwa mujibu wa tafiti kilimo Cha mpunga katika bonde hili kinaweza kulisha nchi mzima ya Tanzania)
Mara Kadhaa akijenga hoja bungeni kuwa ufumbuzi wa tatizo la sukari Tanzania utapatikana katika Bonde la Mto Rufiji(Kuna wawekezaji zaidi ya watatu wa viwanda vya Sukari Rufiji)
Ndio kusema
Mh.Mchengelwa ni Mbunge wa kuwasemea Watanzania.
Hakusita kuwa Mkali na Kusimamia alichokiamini wakati fulani alihoji Bungeni kwa lugha Kali kidogo ni Kwa nini Kampuni ya Sukari ya Kagera kukopa mabilioni ya Pesa na Kwenda kuwekeza DRC wakati nchi inashida kubwa ya Sukari,hayo na mengine mengi yenye Maslahi ya Tanzania yamekuwa ndio Kilio chake.
Jimboni kwake amefanya mengi huwezi kuweka yote hapa ila mawili yatakayomfanya akumbukwe na wana Rufiji ni Kuhakikisha kila Tarafa inakuwa na Shule ya A level(Mkongo,Ikwiriri na Shule pekee ya mabinti Mohoro)
Kutekeleza kwa asilimia 100% agizo la Serikali kuu kujenga madarasa mapya kuchukua wanafunzi waliokwama kuingia kidato cha kwanza(Madarsa 13 ya kisasa ndani ya Mwezi mmoja) na kufanya kuwa miongoni mwa halmashauri zilizofanya vyema katika zoezi hilo nchini.
Michango yake bungeni pia imepelekea Rufiji kutengewa fungu na Tamisemi kujenga jengo jipya halmashauri ili kuondokana na Boma wanalolitumia sasa lililorithiwa toka kwa Mjerumani.
Bila kusahau hoja yake Bungeni kwa nini Mradi wa Umeme wa Mwl Nyerere Rufiji utakaotoa ajira ya zaidi 6000 na serikali kuwekeza zaidi ya trilioni 6.5 unafanyika katika wilaya ambayo haina benki ya Serikali na hata binafsi imepelekea serikali kupeleka benki katika wilaya hio Kongwe.
Ndio kusema Mh.Mchengelwa anawasemea watu wake na taifa kwa Ujumla.
Ushauri wetu kwake aendelee kusemea wananchi wake na taifa bila kusahau Kilio chake cha muda mrefu juu ya ujenzi wa Barabara ya Kibiti Mloka kiwango cha lami
Kwani asilimia kubwa Malighafi za mradi ya Mradi wa Umeme Mwl Nyerere hupita kwenye barabar hii ambayo haiko kwenye hali nzuri hasa kipindi Cha Mvua.
Pia asimamie ahadi na Ilani ya Chama Cha mapinduzi ujenzi wa barabara Nyamwage Utete ambapo wabunge kabla yake hawakufanikiwa kufanya hivyo.
Kwa uzalendo wako na uchapakazi tunaamini utatumikia taifa ipasavyo katika jukumu lako jipya la Waziri ofisi ya Raisi utumishi na Utawala Bora na Kumsaidia Mh. Rais katika kazi yake ya kuijenga Tanzania Tuitakayo.
Promo za kutosha, ngoja tusubiri utekelezajiHuyu Ndiye Mohamed O. Mchengelwa
Teuzi Mpya za Baraza la la Mawaziri zimemuibua kijana Mzalendo na Mchapakazi.
Mohamed Omar Mchengelwa.
Mh.Mchengelwa ni Mbunge wa Rufiji toka 2015 akichukua nafasi ya
ya aliyekuwa Waziri wa Afya wakati wa Mzee JK Dr Seif Rashid.
Mh.Mchengelwa ni Mwanasheria msomi na bobezi katika eneo la Mahakama alikofanya kazi kabla ya kuwa Mbunge.
Mchengelwa Ni Mwanafunzi wa Shahada ya Tatu (PhD) katika Siasa na Mahusiano ya Kimataifa katika Chuo Kikuu Cha "Girne America University" nchini Cyprus.
Ukiacha hayo amekuwa Msaidizi wa Jaji Mkuu wa Tanzania kwa miaka sita(2009-2015).
Bungeni kwa muda mrefu amekuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Katiba na Sheria mpaka wakati huu Mh.Raisi anamteuwa kuwa Waziri.
Mh.Mchengelwa ni miongoni mwa Wabunge wenye kujenga hoja zenye maslahi makubwa kwa wananchi ya Jimbo la Rufiji na Tanzania kwa Ujumla.
Mfano hoja yake kwa nini tozo ya huduma inayopaswa kulipwa na Kampuni za kigeni zinazojenga Mradi wa Umeme wa Mwl Nyerere ilipwe halmashauri ya Wilaya ya Kinondoni badala ya Rufiji kwenye Mradi imepelekea wilaya Rufiji kupokea mabilioni ya pesa kutoka kwenye makampuni hayo na kuchangia kwa kiasi kikubwa maendelo ya wilaya hiyo kongwe, (Rufiji ni Wilaya toka Mkoloni).
Michango yake Bungeni imechangia kiasi kikubwa kuanza kwa Mradi wa Umeme wa Mwalimu Nyerere uliokwama kwa zaidi ya miaka 60(Rejea Ansad Bungeni)
Wakati fulani aliamshra fulaha Bungeni alipokumbusha ahadi ya Mwalimu Nyerere ya kujenga Barabara Tarafa ya Mkongo wilayani Rufiji aliyoitoa 1955 wakati wa Kikao Cha Halmashauri kuu ya Tanu kikichofanyika Tarafa ya Mkongo Rufiji.
Kwa Jitihada zake Mh Mchengelwa, halmashauri sasa wanajenga Shule ya Upili Tarafa ya Mkongo yenye jina la Muaaisi na Mpigani Uhuru wa Nchi hii Bibi Titi Mohamed.
Kwa Jimbo lake hakika ni Mwanasisa wa kupigiwa Mfano na kwa wanaojua siasa za Rufiji huwa ni ngumu Sana kwa Mbunge kupenya awamu ya pili lakini kwake haikuwa kazi ngumu sana kutokana na aliyoyafanya ndani ya awamu yake ya kwanza.
Kuanzia katika Utatuzi wa migogoro ya wakulima na wafugaji,Changamoto za maji,Barabara na Umeme.
Hatma ya hekari elfu hamsini zilizotengwa kando ya Mto Rufiji baada ya kukamilika ujenzi wa mradi Mwalimu Nyerere.
Kutowajibika ipasavyo kwa Mamlaka ya uendelezaji wa bonde la mto Rufiji/Rubada(Kwa mujibu wa tafiti kilimo Cha mpunga katika bonde hili kinaweza kulisha nchi mzima ya Tanzania)
Mara Kadhaa akijenga hoja bungeni kuwa ufumbuzi wa tatizo la sukari Tanzania utapatikana katika Bonde la Mto Rufiji(Kuna wawekezaji zaidi ya watatu wa viwanda vya Sukari Rufiji)
Ndio kusema
Mh.Mchengelwa ni Mbunge wa kuwasemea Watanzania.
Hakusita kuwa Mkali na Kusimamia alichokiamini wakati fulani alihoji Bungeni kwa lugha Kali kidogo ni Kwa nini Kampuni ya Sukari ya Kagera kukopa mabilioni ya Pesa na Kwenda kuwekeza DRC wakati nchi inashida kubwa ya Sukari,hayo na mengine mengi yenye Maslahi ya Tanzania yamekuwa ndio Kilio chake.
Jimboni kwake amefanya mengi huwezi kuweka yote hapa ila mawili yatakayomfanya akumbukwe na wana Rufiji ni Kuhakikisha kila Tarafa inakuwa na Shule ya A level(Mkongo,Ikwiriri na Shule pekee ya mabinti Mohoro)
Kutekeleza kwa asilimia 100% agizo la Serikali kuu kujenga madarasa mapya kuchukua wanafunzi waliokwama kuingia kidato cha kwanza(Madarsa 13 ya kisasa ndani ya Mwezi mmoja) na kufanya kuwa miongoni mwa halmashauri zilizofanya vyema katika zoezi hilo nchini.
Michango yake bungeni pia imepelekea Rufiji kutengewa fungu na Tamisemi kujenga jengo jipya halmashauri ili kuondokana na Boma wanalolitumia sasa lililorithiwa toka kwa Mjerumani.
Bila kusahau hoja yake Bungeni kwa nini Mradi wa Umeme wa Mwl Nyerere Rufiji utakaotoa ajira ya zaidi 6000 na serikali kuwekeza zaidi ya trilioni 6.5 unafanyika katika wilaya ambayo haina benki ya Serikali na hata binafsi imepelekea serikali kupeleka benki katika wilaya hio Kongwe.
Ndio kusema Mh.Mchengelwa anawasemea watu wake na taifa kwa Ujumla.
Ushauri wetu kwake aendelee kusemea wananchi wake na taifa bila kusahau Kilio chake cha muda mrefu juu ya ujenzi wa Barabara ya Kibiti Mloka kiwango cha lami
Kwani asilimia kubwa Malighafi za mradi ya Mradi wa Umeme Mwl Nyerere hupita kwenye barabar hii ambayo haiko kwenye hali nzuri hasa kipindi Cha Mvua.
Pia asimamie ahadi na Ilani ya Chama Cha mapinduzi ujenzi wa barabara Nyamwage Utete ambapo wabunge kabla yake hawakufanikiwa kufanya hivyo.
Kwa uzalendo wako na uchapakazi tunaamini utatumikia taifa ipasavyo katika jukumu lako jipya la Waziri ofisi ya Raisi utumishi na Utawala Bora na Kumsaidia Mh. Rais katika kazi yake ya kuijenga Tanzania Tuitakayo.
Kweli kasomi kajinga. Shukurani mkuu kwa kunikumbusha hayo🙏🙏🙏Kasomi kajinga tena! Nadhani utakumbuka namaanisha nini. Umenichekesha kwa jibu lako hili la bado la ukwe hujalipata. Umenikumbusha bwana mmoja alimtambulisha jamaa mmoja kwangu. Akisema ni rafiki yake wa siku nyingi. Jamaa alipoondoka nikamuuliza mwenyeji wetu jina la huyo rafiki yake. Huwezi amini jibu alonipa. Hamfahamu jina! Rafiki yake sana?
Huyu Mchengelwa wako naona kama ni rafiki yako sana. Tena sana kiasi cha kutofahamu jina lake! Elimu yake ina utata. Hata hili la uanafunzi wa phD pia. Kazi alizofanya kabla ya uteuzi huu nazo majanga. Mara kiongozi wa TISS na sasa msaidizi wa jaji mkuu. Kazi kwelikweli.
Kila kitu alichofanya umeeleza bila kusahau kuweka chumvi. Imekolea. Sehemu zote Rufiji umezitendea haki. Muhoro tu imekataa. Nahisi typing error.
Mwaka jana hakuna aliyechaguliwa. Uchaguzi haukuwepo. Labda ungekuwepo asingepita. Muulize hiyo 2015 aliponaje. Hasira ya Rufiji ingeonekana 2020. Alinusurikaje mauaji ya MKIRU? Muulize alikuwa wapi. Siku moja ayasimulie bungeni kama somo la historia(mpya) ya Tanzania! Au nalo limefukiwa? Kasomi kajinga tena!
Huyu sio Yule 'Wa mtakatifu YOHANA Evening class'.Safi sana cv yake iko poa.
Hongera Mchengelwa.