Huyu ndiye FIRAUNI/FARAO na maajabu ya maiti yake kutokuoza

NIMEFANYA uamuzi wa kuandika makala hii baada ya hivi karibuni kuwa na mada juu ya Mfalme wa Misri ya kale (Pharaoh), aliyefahamika kwa jina la Ramesses II. Katika mada hiyo iliyojipambanua katika mfumo wa maswali na majibu, nilikutana na maswali mengi yenye utata hasa katika dhana za kidini katika imani za Kiislamu, Ukristo na Kiyahudi.

Mivutano ilikuwa ni mipana sana juu ya mada hiyo nikaona ni vyema kueleza hilo kwa upana hasa katika mitazamo ya kihistoria.

Hivyo nimeona angalau kwa uchache wake tufahamu nadharia hii ya wanakale (anthologist), juu ya dhana yao ambayo kimsingi hupishana na mafundisho ya kiimani. Ni vyema tukajifunza pia.
Mnayemuita Firauni yani yule kiongozi wa Misri ya kale aliyeishi zama moja na Mussa anayetajwa katika Bibilia na Quran, alikuwa mtu wa asili ya Afrika.

Alikuwa ni mweusi tii! Jina lake aliitwa Mkuu Ramesses wa II (Great Ramesses) au Sese. Nimekuwa nikiona habari kutoka kwa watu kuwa mwili wa Ramesses ll huwa ukizikwa unarudi juu kesho yake, jambo hili limekuwa likipingwa vikali na wanasayansi na wanahistoria wa mambo ya kale ya Misri.
Kimsingi wanakale wamekuwa wakidai kuwa jambo hilo ni propaganda na uvumi tu usio na ukweli wowote mmoja wa wasomi ni Prof Maurice, amekuwa akieleza mara kadhaa juu ya upembuzi wa usanifu juu ya maisha ya mapharaoh hao wa Misri juu ya historia zao na jinsi walivyohifadhiwa kwa teknolojia za kale.

Labda sasa turudi kwenye mada yetu ya leo juu ya Great Ramesses ll kuwa alizikwaje? Kimsingi huyu Pharaoh mwanzo alizikwa kwenye kaburi lilopewa jina la KV7 katika Bonde la Wafalme, lakini kwa sababu ya uporaji wa vitu vya thamani alivyokuwa amevishwa, makuhani walihamisha mwili kutoka eneo hilo na kuupeleka ndani ya kaburi la malkia Inhapy.

Miaka mingi baadaye waliuhamishia tena mwili kwenye kaburi la kuhani mkuu Pinudjem II. Yote hii ni sababu ya kumbukumbu katika Hieroglyphics. Kutokana na matetemeko yaliyoikumba Jiji la Giza miaka kati ya miaka 1000 AD hadi 1500 AD, vitu vingi vilipotea huku baadhi ya masanamu mengi yakiharibiwa vibaya na matetemeko hayo na baadhi ya makaburi, majumba na makumbusho mengine kupotea kabisa. Huku mwili wa Great Ramesses ll nao ukipotea katika matetemeko hayo. Hapa sasa ndio mkanganyiko unapoanza sasa.

Mwanzoni mwa miaka ya 1800, mwili huu ulipatikana tena pembezoni kidogo mwa bahari ya Red sea. Hapa sasa Prof Maurice anadai kuwa Ramesses ll, hakufa kwenye Gharika la Mussa kama watu wanavyodai, mwili wake hadi sasa unathibitisha kuwa alikufa akiwa mzee, zaidi ya miaka 80 kwa maradhi ya kawaida. Pia si mwili wa Ramesses ll tu uliopo kwenye makumbusho ya Misri pale mjini Cairo, ni miili mingi ya Mapharao tofauti na baadhi ya watu walioishi kwenye Egypt ya kale.

Historia yake kwa ufupi
Ramesses II, au kwa jina jingine Sese alikuwa ni mfalme wa pili wa uzao wa 19 wa familia ya kifalme (19TH dynasty). Alikuja kuwa miongoni mwa mapharao wenye nguvu kuwahi kuwepo Misri, ndio yeye aliyeifanya Misri kuwa dola kuu na Serikali kuu yenye nguvu (the world Super- Omnipotence) katika dunia ya zama hizo katika miaka ya 1269 BC. Ramesses II alipewa kiti cha ufalme mapema kwenye umri wa miaka 20 na akaongoza (kati ya mwaka 1279 BC) hadi alipofariki miaka 67 baadaye (1213 BC) kwa maradhi ya mishipa na ini. Aliongoza Misri kwa miaka 67 akiwa ni wa pili kuongoza kwa kipindi kirefu zaidi katika historia ya mapharao.

Mbali na vita, Ramses II anakumbukwa katika juhudi za utunzaji wa historia ya Misri katika mahekalu ya Ramesseum pamoja na Abu Simbel.

Kwa kumbukumbu nyingi muhimu zilizomo katika mahekalu haya kama sanamu, zana za kale, michoro na maandishi zinamfanya Ramsess kuwa mmoja wa mapharao muhimu wa Misri ya kale. Jeshi la Rammeses lilisaidia kulinda mipaka ya Misri kutoka kwa wavamizi na majambazi katika Meditrenian na Libya pia kutoka Hittites na Nubians. Pia alifanya kampeni za kurudisha ardhi iliyokuwa imeporwa na wavamizi kwa kusaini mikataba ya amani kabla ya kutumia nguvu kuwapiga.

Katika historia Ramesses alishindwa vita moja tu. Vita inayokumbukwa sana ni ile iliyofanyika Kadesh (Syria) ambayo ilifanyika mwaka 1274 BC dhidi Wahiti. Ilikuwa ni vita kubwa iliyotumia zana za kisasa zaidi wakati huo katika historia ya vita za kale. Rameses alifanya makosa kwa kugawa vibaya vikosi vyake kitu kilichofanya moja ya kikosi kufyekwa chote! Hatimaye mpinzani akajitangazia ushindi na Ramesses ikampasa arudi nyuma sababu ya kujiandaa kubaya na matatizo ya vifaa.

Dhana iliyozushwa juu ya kifo chake (kwa mujibu wa Prof Maurice), vitabu kadhaa vya dini kama vile Biblia na Quran vimekuwa vikizungumzia kifo chake katika hali ya kushangaza. Wao hudai kuwa Ramesses au Sese alifia kwenye maji wakati akiwafukuza Waisrael.

Wamisri wa kale wakipinga kabisa madai hayo na kudai Sese alifariki akiwa na miaka zaidi ya 87 kutokana na maradhi ya kibinadamu. Moja ya ushahidi ni wa mwili wake ambao unaonekana wazi kuwa mtu huyo alifariki akiwa mzee kabisa kwa mujibu wa utafiti wa wanasayansi wa mambo ya kale ulioongozwa na Prof Maurice.

Pia jambo jingine la kujiuliza ni kuwa kina Musa wakati wakimkimbia Ramesses II na kuwa wameshafanikiwa kuvuka bahari huku nyuma waliwezaje kumuona Ramesses katikati ya kikosi cha askari wa Misri akifa maji? Hayo ni mambo yanayowatatiza wengi huku wengine wakienda mbali zaidi kuwa Ramesses mwili wake huwa hautaki kuzikwa.
Huyu ndio Great Ramesses II au Sese mmoja wa mapharao muhimu zaidi Eghypt ya kale na leo katika historia.View attachment 1170766
Kichwa cha habari na hbari yenyewe haviendani, umeshindwa kueleza kama mwiliwake hauozi au unaoza na hali ya huo mwil kwa sasa, umeishia kutiririka porojo za maprofesa type ya Lipumba
 
Wazee wa C&P
Muwe mna toa na credit mnapo hamisha kazi za watu


Uzi OG uko hapa
 
Wazee wa C&P
Muwe mna toa na credit mnapo hamisha kazi za watu


Uzi OG uko hapa
 
Wana historia wa kisecular huwa wana vituko sana,wakiona jambo limewazidi ukubwa na maarifa basi wana hoji kitoto sana,hii si hoja bali ni wasi wasi tu.

Firauni alizama katika katika kuhaha kwake alisikia akizungunza maneno na huo ndio ushahidi tosha ya kuwa Firauni alikufa na Allah aliye juu aka ahidi ya kuwa ata uhifadhi mwili wa firauni ili watakao fata waone na wapate kujifunza. Lakini swali lina kuja je walio kusudiwa kuuona huo mwili ni kina nani na je ni kweli mwili wa Firauni upo kweli mpaka leo ? Ukweli uko kinyume.

Allah aliye juu anasema katika surat Yunus :

90. Tukawavusha bahari Wana wa Israili, na Firauni na askari wake wakawafuatia kwa dhulma na uadui. Hata Firauni alipo kuwa anataka kuzama akasema: Naamini kuwa hapana mungu ila yule waliye muamini Wana wa Israili, na mimi ni miongoni mwa walio nyenyekea!
91. Ala! Sasa? Na hali uliasi kabla yake na ukawa miongoni mwa mafisadi!
92. Leo, basi, tutakuokoa kwa mwili wako, ili uwe Ishara kwa ajili ya walio nyuma yako. Na hakika watu wengi wameghafilika na Ishara zetu. (Yunus : 90 - 92 )

Nipo ......
kwa akili tu ya kawaida, kama kweli firauni alisema hayo maneno ni nani aliyeyasikia na kuja kuyasimulia ? hivi kwa mfano mimi ningekuwa ni abiria wa meli iliyozama baharini kabla sijafa niseme maneno fulani alafu nife na abiria wenzangu, nyie huku jamiiforums mtayajuaje hayo maneno ?
 
Wazee wa C&P
Muwe mna toa na credit mnapo hamisha kazi za watu


Uzi OG uko hapa
Hata mimi nimemwambia.
 
kwa akili tu ya kawaida, kama kweli firauni alisema hayo maneno ni nani aliyeyasikia na kuja kuyasimulia ? hivi kwa mfano mimi ningekuwa ni abiria wa meli iliyozama baharini kabla sijafa niseme maneno fulani alafu nife na abiria wenzangu, nyie huku jamiiforums mtayajuaje hayo maneno ?

Tatizo uliposema hukufikiria na kama ulifikiria ulifikiria kwa upande mmoja,tukio linatokea mtume Musa na wafuasi waligeuka wakawa wana waangalia Farao na watu wake walivyokuwa wanaingia mpaka mpaka njia ikajifunga na wakawa wanazama na kufa.

Habari hiyo imekuja kupitia ufunuo,ufunuo ambao unatoka kwa Mola wetu mlezi,na sisi tuna uamini sababu umetoka kwa yule muweza wa wote.

Kama una swali lingine uliza,na mimi naomba nikuache na swali,huwa una amini vipi habari za kale yaani unaujuaje ukweli wa habari za kale ?
 
Hujajibu swali,nimesoma sijaona ndio uniambie sasa,Firauni alikuwa muislamu kivipi ? Nithibitishie hilo.

Usiwe na papara,unachotakiwa hapa kile unachokiongea a kukiandika uwe na elimu nacho na uweze kukijengea hoja,nasubiri uthibitisho ya kuwa Firauni alikuwa Muislamu.
Nenda Misri uone walivyo muhifadhi msikitini na wakisema alikuwa muislam. Wewe hata misri hujafika unabishana na waliokaribu na Wanaomtunza
 
Tatizo uliposema hukufikiria na kama ulifikiria ulifikiria kwa upande mmoja,tukio linatokea mtume Musa na wafuasi waligeuka wakawa wana waangalia Farao na watu wake walivyokuwa wanaingia mpaka mpaka njia ikajifunga na wakawa wanazama na kufa.

Habari hiyo imekuja kupitia ufunuo,ufunuo ambao unatoka kwa Mola wetu mlezi,na sisi tuna uamini sababu umetoka kwa yule muweza wa wote.

Kama una swali lingine uliza,na mimi naomba nikuache na swali,huwa una amini vipi habari za kale yaani unaujuaje ukweli wa habari za kale ?
We jamaa huyo molawako mlezi ni muongo sana.
 
Back
Top Bottom