Kwa hayo machache uliyoyaorodhesha hapa....haihitaji hata kuwa na degree kujua kuwa huyo mpenzi wako ni mtu wa aina gani......kimsingi ni kuwa huyo hawara yako ameshakiuka misingi na nguzo za upendo ambazo ni kujaliana, kuthaminiana na kusaidiana miongoni mwa wapendanao....kwa maana hiyo amepoteza sifa za kuwa mpenzi wako...na nitakuwa sijakosea kama nikisema kuwa huyo bwana hakupendi na haupo kwenye mipango yake isipokuwa amekufanya kama KIPOZEO....ninachokushauri ni kwamba usitoe hukumu ya upande mmoja huyu nae ni binaadamu huenda labda ana mambo yamemtinga so ndio maana yupo hivyo...tafuta muda muongelee hili swala mpaka mfikie muafaka....Vile vile inawezekana ikawa wewe pia bila kujijua ukawa ni sehemu au ni moja ya sababu ya yeye kuwa hivyo nakushauri pia na wewe ujiangalie vizuri pamoja na historia ya mahusiano yenu kwamba hiyo tabia imezuka tu hivi karibuni au ilikuwapo kabla na uliwezaje kuvumilia mpaka leo uje uone kuwa ni kero....maana kukaa kwenye uhawara kwa miaka mitatu ni mingi sana.....vile vile kumbuka muda ni bidhaa adimu sana ambayo ikishauzwa huwa hairudishwi kwa hiyo huna budi kuwa nao makini sana.....usipende kukaa na jambo muda mrefu bila kulitafutia ufumbuzi kwa huo muda unaoupoteza hautaupata tena....THINK BIG ,TAKE ACTION..........WELCOME JF........