Nakumbuka kumfahamu kwa mara ya kwanza kumfahamu Habibu Mhange ilikuwa mwaka 2010, alipokuja kutaka kugombea ubunge jimbo la Kibaha vijijni, baada ya kutangaza nia yake hiyo sisi kama wadau wa CHADEMA tulitaka kujua historia yake, Naye bila hiyana akatueleza kuwa yeye ni kijana mzaliwa wa jimbo hili na kwake ni kijiji cha Lupunga, ndipo tulipomshauri kuwa ni vyema twende mpaka kijijni kwao ili tukawasalimie wazazi wake na kuwatambua kwa kuwa jukumu analotaka kuomba ni zito sana.
Tukiwa safarini kuelekea huko aliposema ndio kwao aliongea mambo ikiwa na kuahidi kuwa tukirudi tu Mlandizi cha kwanza kufanya ni kulipa deni la pango la ofisi ya chama inayodaiwa na mwenye nyumba kiasi cha shilingi 15,0000.
Tulipofika ilipo shule ya kijijini hapo aliwaona wananchi wakijiandikisha katika daftari la kudumu la wapiga kura naye alisema kuwa hana kitambulisho cha mpiga kura na akaomba naye aandikishwe, lakini sisi kama watu makini tulianza kupata shaka na uzaliwa wa Mchange Kjijini hapo kwani hata wenyeji waliokuwepo hapo hawakuonyesha hata dalili ya kumjua ukiacha kumsahau, makalani wakataka kumwekea ngumu kumuandikisha lakini walizidiwa nguvu na mashinikizo yetu na hatimae Mchange akaandikishwa, baada ya hapo tukamuomba atupeleke kwenye nyumba yao, hapo napo tukapata mshtuko mwingine alipoanza kuuliza ilipo nyumba ya babu yake, na yule aliyemuuliza akatuelekeza, tukafika mpaka kwenye nyumba hiyo na kumkuta mzee mmoja na mkewe, walipotuona hawa kuonyesha kumfahamu hata mmoja wetu, ndipo baada ya kuwasalimia walitaka kutujua sisi ni akina nani, ndipo bwana Mchange alianza kujieleza na kuwa tambulisha wazee kuwa yeye ni nani.
Baada mabishano mafupi ndipo wale wazee walimkumbuka japo kwa shida, nao wakatufahamisha kuwa kijana mwenzetu tulioandamana naye (Mchange) ni mtu wa hovyo kwa kuwa aliondoka kijijin hapo akiwa mwenye miaka 15 na kuwa hajawahi kurudi tena hapo wao ni mjukuu wao.
Baada ya hali kutulia ndipo Mchange aliwaambia wazee nia yake, kwa hasira kali yule babu yake akaapa kuwa hatomuunga mkono katika suala hilo la kutaka ubunge kwa kuwa hana sifa, babu alimuhoji kama amemtekeza yeye na bibi yake itakuwaje kwa wananchi wengine? Huku kwa majonzi mzee alituonyesha kibanda chake wanacholala ambacho kimeinama tayari kwa kuwafunika, kwa mbinu za kisiasa na ulaghai alionao Mchange alimuahidi babu yake kuwa ndani ya wiki moja kutoka siku hiyo angemjengea nyumba, baada ya maongezi mafupi tuliwaaga yule bibi na babu, tulipofika Mlandizi tulimuweka kitimoto bwana Mchange kwa mambo kadhaa, alipokumbushiwa ahadi yake ya kulipa pango la ofisi akamaka kuwa hana pesa mpaka arudi Dar, mpaka sasa kimyaaa.
Kwa kuwa Kibaha vijijini kuna watu makini wakiongozwa na akina Majuto Ngozi, Mchechu Msisina, Mohamed Ngozi na wengineo ndani ya chadema tulimuweka wazi kuwa kwa nafasi hiyo yeye hatoshi, ndipo bwana Mchange alipokimbilia jimbo la Kibaha mjini nao bila kujuwa alimuamini na wakamfanya kuwa mgombea, na hakika alikubalika na watu walijitolea kwa hali na mali ili kuhakikisha anashinda, lakini alikuwa akiwalamba visogo wananchi na kukubaliwa kununulia kwa milioni 150 kutka kwa mgombea wa CCM ikumbukwe kuwa baada ya matokeo kutangazwa na mabomu kupigwa wananchi walijitolea kuchanga pesa ili kesi ya kupinga matokeo ifunguliwe.
Bwana Mchange aliichukuwa michango hiyo kupiga danana mpaka muda kwisha!
Hivyo basi kijana huyu hafai hata ujmbe wa nyumba kumi kwa kuwa hana radhi ya wazazi wake na laana ya watu wa Kibaha ipo juu yake