Huyu mzee ananitakia mema kweli?

Huyu mzee ananitakia mema kweli?

Wewe hii simu ina edit keyboard sasa inaandika mali baada ya mahari sorry typing error

Kwa hiyo ikiandika mali nawe unaiacha hivyo hivyo kwa kuwa sisi tutaelewa si ndio? Halafu ni baada au badala??. Wewe una shida ya kujieleza na kujichabganya ndio maana huyo mkwe wako hataki maelezo mengi toka kwako yatakayompotezea muda..andaa sharehe uoe usitake mizunguuko usiyoimudu
 
Kwa hiyo ikiandika mali nawe unaiacha hivyo hivyo kwa kuwa sisi tutaelewa si ndio? Halafu ni baada au badala??. Wewe una shida ya kujieleza na kujichabganya ndio maana huyo mkwe wako hataki maelezo mengi toka kwako yatakayompotezea muda..andaa sharehe uoe usitake mizunguuko usiyoimudu
Mhhh kwanini unashindwa kuwa muungwana?
Hivi ukiongea bila kejeli unapungukiwa kitu au ujumbe hautafika?

Hata hunijui unaniletea dharau,
Hebu jirekebishe hatutafika kwa malumbano yasiyo na msingi.

Kama mtu timamu lazima ujue haya makosa ya kiuandishi ni kawaida. Sasa siwezi kukutolea maneno ya hovyo kwasababu sikujui na nakuheshimu.
Please maintain your dignity.
 
Mhhh kwanini unashindwa kuwa muungwana?
Hivi ukiongea bila kejeli unapungukiwa kitu au ujumbe hautafika?

Hata hunijui unaniletea dharau,
Hebu jirekebishe hatutafika kwa malumbano yasiyo na msingi.

Kama mtu timamu lazima ujue haya makosa ya kiuandishi ni kawaida. Sasa siwezi kukutolea maneno ya hovyo kwasababu sikujui na nakuheshimu.
Please maintain your dignity.

Basi yaishe ndugu ila uwe unapitia uandishi wako kabla ya kupost otherwise utaleta mkanganyiko usio wa lazima
 
Labda anahisi utamnyanyasa mwanae kwa kujiona "umemnunua"😀
 
Hivi jamani huyu baba mkwe mtarajiwa unampelekea Mahari anakataa anasema binti yake hauzwi, wewe andaa harusi tu.
Huyu Mchagga ananitakia mema Mimi na binti take kweli?

Hivi kwanini ukatae Mahari?
Mhhh huyu mzee kweli ana nia njema?
Au binti yake ni matatizo hadi akatae mali?
Siku huyu binti si anaweza anasema kwanza wewe hukunitolea Mahari niache niende kwetu?

Kuna maswali ukiyafikiria mweeeeh!
Jamani wadada hivi wewe ulipotolewa Mahari ulijisikiaje?

Tena Mahari ilipokuwa kubwa au ndogo moyoni ilikuwaje?

Tusaidiane tu maana hakuna namna!!!!!
Mahari ni zawadu kutoka kwa mumemtarajiwa kwa mkewe, mimi Wazazi wangu hawakutaka mahari Dad alimwambia mahari ni zawadi kutoka kwako kumpe mkeo mtarajiwa so chochote utakacho jaaliwa,muhimu nnachoomba kwako ni malezi mema kwa mtoto wangu masikilizano dogo maliza kubwa nilete,sijakuuzia bali ninnakuozesha mpango sijui wakumpiga
kumnyanyasa tutakosa,unahitaji msaada kwangu njoo 24/7 wewe sasa ni mwanangu. lakini hawakusema lete kilemba sijui kofia sijui kochi la kukalia mara kitanda na kabati la futi 5 ya wanaagiza vitu vya hatari hatari tuu,unaagiza kitanda halafu kinabaki kwa mke manake nini ? kua utaachwa urudi kwenu yani sielewi demand nyeingine lakini ni sawa kama wenyewe zinawaridhisha..
 
Umempunguzia mzigo atakuwa hana shukrani akipokea na hela!
 
Heshima yako mkuu Malcom, ukifikiria sana kudia mahari kuna mantiki gani hasa? Unamuhuza binti, je, unataka urudishiwe gharama za kumsomesha na kumtunza wakati ukijua wazi kwamba wewe kama mzazi huo ni wajibu wako bila kujali kama binti yako ataolewa au la.

Kwa wazazi wasomi hawapedi kabisa masuala ya mabinti zao kuonekana kama wananunuliwa vile, wanacho muomba Mungu ni binti yao hasipate ujauzito akiwa kwa wazazi wake basi, mengine kwao ni immaterial.

Binafsi nisingependa binti yangu atolewa mahari, cha muhimu akielewana na mwenza basi.

Sina shaka kinacho kusumbua wewe unafikiri wanakutega au hutakuwa na uhuru ni mkeo mtarajiwa kwa kuwa at back of your mind atakuwa anafikiria hujamtolea mahari hivyo huna uhuru nae hiyo si kweli Malcom.
 
Heshima yako mkuu Malcom, ukifikiria sana kutia mahari kuna mantiki gani hasa? Unamuhuza binti, je, unataka urudishiwe gharama za kumsomesha na kumtunza wakati ukujua wazi kwamba wewe kama mzazi huo ni wajibu wako bila kujali kama binti yako ataolewa au la.

Kwa wazazi wasomi hawapedi kabisa masuala ya mabinti zao kuonekana kama wananunuliwa vile, wanacho muomba Mungu ni binti yao hasipate ujauzito akiwa kwa wazazi wake basi, mengine kwao ni immaterial.

Binafsi nisingependa binti yangu atolewa mahari, cha muhimu akielewana na mwenza basi. Sina shaka kinacho kusumbua wewe unafikiri wanakutega au hutakuwa na uhuru ni mkeo mtarajiwa kwa kuwa at back of your mind atakuwa anafikiria hujamtolea mahari hivyo huna uhuru nae hiyo si kweli Malcom.

Mkuu naunga mkono hoja yako100/100. Nina binti na ni-wazo langu siku ikifika ntafanya the same kama mwanzisha thread alivyofanyiwa ukweni....
 
Tuliwahi kwenda kwa mkubwa mmoja kumchumbia mwanae mimi nikiwa mimemsindikiza mshenga. Ilipofika wakati wa kutajiwa mahari mzee akasema "ndugu zangu hapa hatufanyi biashara ya kuuziana bali tumekuwa familia moja.
Ningekuwa na uwezo hata senti tano msingetoa lakini kwa sababu ya mila kuna Shangazi, Wajomba, Bibi, kwa maana hiyo mtuletee Blanketi ya bibi na jembe pamoja na 100,000 watagawana mashangzi na wajomba, hiyo ndiyo mahari ninayoitaka.
Rafiki yangu hakuamini ukizingatia binti ni msomi (Daktari) alidhani atatajiwa mamilioni ya fedha.
 
Ni kawaida hiyo kwa baadhi ya familia....

Hata kwetu mahari sio kivile,kikubwa ni mzee anawatakia mkaishi vema
 
Makubaliano na wajomba, mzee anasema hiyo hela nimepanga itumiwe kwenye harusi. Sasa hapo ndipo sielewi kwa nini hiyo Mali asipokee tu?
Kwani kuna ugumu gani?
Hiyo ndio kashapokea na ndio maana anatoa maelekezo ya matumiz yake mjomba hausiki hapo labda kama unataka kuwapa rushwa
 
Back
Top Bottom