Naomba
na miye leo nifunguke.
Nina mwanaume tumekuwa kwenye
uhusiano kimapenzi (namaanisha kimapenzi) kwa takriban mwaka mmoja sasa.
Lakini
tulijuana miaka mitatu iliyopita akiwa kama rafiki mwema kwangu.
Ni kijana mwenye sifa nizipendazo, yaani ni mtaratibu, mwerevu, mwelewa,
mwenye malengo na pia mcha
Mungu.Nilikutana
na huyu kijana wakati wa tamasha la Mwakakogwa huko Makunduchi, basi
kuanzia hapo tukawa marafiki. Aliwahi kunitamkia kuhusu kuwa na
urafiki wa kimapenzi,lakini sikumkubalia kwa sababu nilikuwa na uhusiano
na mwanaume mwingine ambaye tulikuwa na malengo ya kufunga ndoa.
Kusema kweli nilivutiwa na huyu kijana ila nilishindwa kukubali kuwa na
uhusiano naye wa kimapenzi kwa sababu nilishaji commit kwa mwanaume
mwingine, na miye ni binti niliyelelewa katika maadili kwa hiyo sikuwa
tayari kumpaka mafuta huyu kijana wa watu kwa nyuma ya chupa, yaani kuwa
mnafiki na ndumilakuwili wa kutaka huku na kule.
Urafiki wetu na huyu kijana ulikuwa ni wakawaida tu na mara chache
tulikuwa tunakutana kwa mazungumzo ya hapa na pale katika kubadilishana
mawazo. Katika
kipindi ambacho huyu mwanaume niliyekuwa naye nilipomfumania na
shogangu wa kupika na kupakua wakiwa kitandani wakifanya tendo,
nilimsimulia huyu kijana kama rafiki mwema ili kupata ushauri na pia
kufarijiwa kwa sababu tulishakuwa marafiki kwa muda mrefu.
Alinishawishi sana nisivunje uhusiano na mpenzi wangu, akinisihi
nimsamehe kwani ni ibilisitu alimpitia, lakini kutokana na kuumizwa na
usaliti niliofanyiwa na mpenzi wangu niliyemuamini sana nilikata shauri
niuvunje uhusiano na kushika hamsini zangu.
Nilikaa kwa
muda wa miezi sita bila kuwa na uhusiano, lakini pia nilisita kuwa
karibu na huyu rafiki yangu kwa muda wote huo nikitaka kutafakari
kilichonitokea nikiwa peke yangu.
Yule kijana wala hakufanya makeke ya kunitafuta, na yeye alikata
mawasiliano. Baada ya hiyo miezi sita ya kuachana na mpenzi wangu,
nikarudisha mawasiliano na huyu rafiki yangu baada ya kukutana kwenye
mkesha wa Maulid ya kuzaliwa Mtume. Baada ya kurudisha mawasiliano ndipo
akanitaka tuanzishe uhusiano wa kimapenzi akiniahidi kwamba tutaoana
iwapo kila mmoja ataridhika na tabia za
mwenzake.
Tukaanzisha uhusiano wa kimapenzi na nilijenga imani kwamba, huyu
atakuwa mume mwema kwa sababu anazo zifa zote nizitakazo, na
tulishafahamiana kwa takriban miaka miwili nyuma kama marafiki na kila
mmoja alikuwa anafahamu kuhusu mahusiano ya mwenzake.
Kwa upande wake, yeye aliwahi kunisimulia kwamba alikuwa na mpenzi wake
ambaye alikuwa hajatulia, na hawaendani na hivyo aliamua kuvunja
uhusiano huo.
Lakini baada ya miezi kadhaa tangu kuanzisha uhusiano na huyu kijana, na
yeye akaanza vibweka. Kwanza ana wivu kupindukia, na anapenda sana
kuzungumzia mahusiano yangu ya nyuma kwa namna ya kuniumiza kihisia.
Wakati mwingine tukiwa kitandani anataka kujua ni nani mzuri zaidi kati
yake na huyo bwanangu wa zamani katika swala zima la
kitandani.
Hata nimsifie, lakini anahisi kama namnafiki tu na anapenda sana
kusifiwa sifiwa na kudekezwa na kunithibiti nisiwasiliane na marafiki
zangu. Hamuanini mtu yeyote wa jinsia ya kiume kuwa karibu na mimi, na
hivi sasa anataka kuingilia mawasiliano yangu ya simu akitaka kujua
nawasiliana na nani na kwa nini.
Kuna wakati aliwahi kufuta namba zote za wanaume niliowasevu kwenye simu
yangu ambao wote ni jamaa zangu ambao nina nasaba
nao.
Nimeshindwamiye, bora yeshe, mwanaume gani huyu asiyejiamini, hivi tu ni
wapenzi akijanioa si atanigeuza mdoli wa kuniweka hapo asubuhi na
akirudi jioni anikute hapohapo.
Nimeshindwa
miye.