Huyu mwanaume mimi namwacha

Huyu mwanaume mimi namwacha

kwenye mapenz kikubwa ni uvumilivu ipo siku ataacha tabia hizo chamsing mvumilie tuu.
 
1) wewe hujalelewa kwenye maadili, umelelewa kwe sampuli ya maadili. weye maadili awaggedani kabla ya ndoa
2) ana kila haki ya kuwa na wasiwasi na hao male frends wako becoz yeye mwenyewe alikupata mkiwa frends (another reason why u should never trust a lady saying he is just a frend)
3) anashika simu yako becoz he has every ryt to do so. kama haupo tayari kwa serious relationship basi usiingie kwenye relationship. relationship is about forgoing the i and believing in the we. kama upo clean basi hamna shida ya kulalamika yeye kushika simu yako
4) a decent woman doesnt discuss bedroom affairs in public....its just unlady like.
5) yeye kukuuliza wewe kama anakugegeda vizuri kuliko ex wako ni consequence ya wewe kugegedwa kabla ya ndoa....u shuld deal with it becoz its a choice u made and the price u pay. tatizo mwanadamu ana tabia ya kujidai yeye anajua kuliko Mungu.
6) last but not least u need to do a self evaluation, clearly ur selection of the husband material man needs polish. yule wa kwanza ulisema uliona atakuwa future husband huyu nae future husband but all have fallen short. it could be kuwa kweli hao wanaume bogus but sometyms u need to be careful with ur selection.

Mweh! na wewe unaongea sana bwana!
Haya ndiyo hivyo nishaamua kuachia ngazi nawapisha wengine.
 
inaonyesha jamaa atakua hana hela angekuanazo vituko vyote ungevumilia tu cc lara 1 LMAO

Ha ha ha ha ha haaaaa, huku kwetu visiwani si sawa na huko kwenu Bara, mapenzi ya pesa hayana thamani, ni upendo pekee ndiyo una nafasi
 
pole sana,,,,awali ni awali hakuna awali mbovu,halafu nimeona hapo jamaa alivotamani akupate kirahisi japo ktk mahusiano hutokea mengi kipindi cha kuachana na mwenza wako wa kwanza ukakimbilia chap kwa huyo dah sikukushaur kabisa hvi we hukosei halafu ukiachana na huyo utatafuta tena mwingine kwa style hiyo utadate na wangapi?? hvi ukimwacha ndo utakua umepata suluhu?


ukisha jibu hayo ntaja na mengine
 
Naomba na miye leo nifunguke.

Nina mwanaume tumekuwa kwenye uhusiano kimapenzi (namaanisha kimapenzi) kwa takriban mwaka mmoja sasa. Lakini tulijuana miaka mitatu iliyopita akiwa kama rafiki mwema kwangu.

Ni kijana mwenye sifa nizipendazo, yaani ni mtaratibu, mwerevu, mwelewa, mwenye malengo na pia mcha Mungu.
Nilikutana na huyu kijana wakati wa tamasha la Mwakakogwa huko Makunduchi, basi kuanzia hapo tukawa marafiki. Aliwahi kunitamkia kuhusu kuwa na urafiki wa kimapenzi,lakini sikumkubalia kwa sababu nilikuwa na uhusiano na mwanaume mwingine ambaye tulikuwa na malengo ya kufunga ndoa.

Kusema kweli nilivutiwa na huyu kijana ila nilishindwa kukubali kuwa na uhusiano naye wa kimapenzi kwa sababu nilishaji commit kwa mwanaume mwingine, na miye ni binti niliyelelewa katika maadili kwa hiyo sikuwa tayari kumpaka mafuta huyu kijana wa watu kwa nyuma ya chupa, yaani kuwa mnafiki na ndumilakuwili wa kutaka huku na kule.

Urafiki wetu na huyu kijana ulikuwa ni wakawaida tu na mara chache tulikuwa tunakutana kwa mazungumzo ya hapa na pale katika kubadilishana mawazo.
Katika kipindi ambacho huyu mwanaume niliyekuwa naye nilipomfumania na shogangu wa kupika na kupakua wakiwa kitandani wakifanya tendo, nilimsimulia huyu kijana kama rafiki mwema ili kupata ushauri na pia kufarijiwa kwa sababu tulishakuwa marafiki kwa muda mrefu.

Alinishawishi sana nisivunje uhusiano na mpenzi wangu, akinisihi nimsamehe kwani ni ibilisitu alimpitia, lakini kutokana na kuumizwa na usaliti niliofanyiwa na mpenzi wangu niliyemuamini sana nilikata shauri niuvunje uhusiano na kushika hamsini zangu.
Nilikaa kwa muda wa miezi sita bila kuwa na uhusiano, lakini pia nilisita kuwa karibu na huyu rafiki yangu kwa muda wote huo nikitaka kutafakari kilichonitokea nikiwa peke yangu.

Yule kijana wala hakufanya makeke ya kunitafuta, na yeye alikata mawasiliano. Baada ya hiyo miezi sita ya kuachana na mpenzi wangu, nikarudisha mawasiliano na huyu rafiki yangu baada ya kukutana kwenye mkesha wa Maulid ya kuzaliwa Mtume. Baada ya kurudisha mawasiliano ndipo akanitaka tuanzishe uhusiano wa kimapenzi akiniahidi kwamba tutaoana iwapo kila mmoja ataridhika na tabia za mwenzake.


Tukaanzisha uhusiano wa kimapenzi na nilijenga imani kwamba, huyu atakuwa mume mwema kwa sababu anazo zifa zote nizitakazo, na tulishafahamiana kwa takriban miaka miwili nyuma kama marafiki na kila mmoja alikuwa anafahamu kuhusu mahusiano ya mwenzake.

Kwa upande wake, yeye aliwahi kunisimulia kwamba alikuwa na mpenzi wake ambaye alikuwa hajatulia, na hawaendani na hivyo aliamua kuvunja uhusiano huo.

Lakini baada ya miezi kadhaa tangu kuanzisha uhusiano na huyu kijana, na yeye akaanza vibweka. Kwanza ana wivu kupindukia, na anapenda sana kuzungumzia mahusiano yangu ya nyuma kwa namna ya kuniumiza kihisia. Wakati mwingine tukiwa kitandani anataka kujua ni nani mzuri zaidi kati yake na huyo bwanangu wa zamani katika swala zima la kitandani.


Hata nimsifie, lakini anahisi kama namnafiki tu na anapenda sana kusifiwa sifiwa na kudekezwa na kunithibiti nisiwasiliane na marafiki zangu. Hamuanini mtu yeyote wa jinsia ya kiume kuwa karibu na mimi, na hivi sasa anataka kuingilia mawasiliano yangu ya simu akitaka kujua nawasiliana na nani na kwa nini.

Kuna wakati aliwahi kufuta namba zote za wanaume niliowasevu kwenye simu yangu ambao wote ni jamaa zangu ambao nina nasaba nao.


Nimeshindwamiye, bora yeshe, mwanaume gani huyu asiyejiamini, hivi tu ni wapenzi akijanioa si atanigeuza mdoli wa kuniweka hapo asubuhi na akirudi jioni anikute hapohapo.


Nimeshindwa miye.

kwa kweli mpendwa huyo si mwanaume, ukiingia kwenye ndoa unaweza usimalize mwaka ukatoka loh
 
alafu huwa najiuliza sana kwanini wanaume wengi ambao huwa marafiki wa kawaida kwa wadada wanapoanza mahusiano ya mapenzi hugeuke the worse bf ever? yani nimeshasikia wadada wengi sana wanalia na mahusiano ya aina hyo
 
mapenzi kizunguzungu

Dunia inayomambo, mambo yenye kuzidia,
Mambo kujaa vijambo, utaijua dunia,
Bora 'sifate mkumbo, mambo huleta udhia,
Mola naomba hekima, nikabili haya mambo.

Mola naomba hekima, ili niweze tulia,
Nifunze yaliyo mema, na si mtu kumwonea,
Mdomo usije sema, jambo sijafikiria,
Mola naomba hekima, nikabili haya mambo.

Mola naomba busara, iweze nitangulia,
Nisiifanye papara, mambo yanayonijia,
Unepushie hasira, kichwa kipate tulia,
Mola naomba hekima, nikabili haya mambo.

 
Jiweke pembeni kuepusha msongamano mwaya... Zinduna
 
Last edited by a moderator:
Zinduna....yako yanafanana na yangu....halafu jamaa wa huko huko Zenji...

Aise nimenyanyua mikono juu...kama ndo kupendwa ule upendo umenizidi umri....!
 
Zinduna,

Mpenzi wako wa kwanza sababu za msingi za kuwachana zilikuwepo, pole sana.

Ila huyu sioni sababu ya msingi hapo, Mwambie usiyoyapenda na unayoyapenda, kwa upande wako kuwa muwazi kwenye mawasiliano yako na simu, inaonekana kuna vitu haelewi kwenye mawasiliano yako na friends zako wa kiume na ukumbuke na yeye alikuwa rafiki yako wa kawaida pia na mawasiliano ndio yamewafikisha hapo!! unatarajia yeye ataamini kirahisi tu?

Hatutarajii wivu usiwepo kwenye mapenzi kabisa lakini swala la imani kwa mpenzi inategemea anavyo behave.
 
Back
Top Bottom