Huyu mwanaume mimi namwacha

Huyu mwanaume mimi namwacha

naomba nipm nikupe mbinu sahihi ya kumfanya asiwe na wivu kupindukia
 
Temana nae huyo! Sio kabisa. Usipomwacha sasahivi utakuja kumwacha ukiwa umechelewa!
 
naomba na miye leo nifunguke.

nina mwanaume tumekuwa kwenye uhusiano kimapenzi (namaanisha kimapenzi) kwa takriban mwaka mmoja sasa. lakini tulijuana miaka mitatu iliyopita akiwa kama rafiki mwema kwangu.

Ni kijana mwenye sifa nizipendazo, yaani ni mtaratibu, mwerevu, mwelewa, mwenye malengo na pia mcha mungu.
nilikutana na huyu kijana wakati wa tamasha la mwakakogwa huko makunduchi, basi kuanzia hapo tukawa marafiki. Aliwahi kunitamkia kuhusu kuwa na urafiki wa kimapenzi,lakini sikumkubalia kwa sababu nilikuwa na uhusiano na mwanaume mwingine ambaye tulikuwa na malengo ya kufunga ndoa.

Kusema kweli nilivutiwa na huyu kijana ila nilishindwa kukubali kuwa na uhusiano naye wa kimapenzi kwa sababu nilishaji commit kwa mwanaume mwingine, na miye ni binti niliyelelewa katika maadili kwa hiyo sikuwa tayari kumpaka mafuta huyu kijana wa watu kwa nyuma ya chupa, yaani kuwa mnafiki na ndumilakuwili wa kutaka huku na kule.

Urafiki wetu na huyu kijana ulikuwa ni wakawaida tu na mara chache tulikuwa tunakutana kwa mazungumzo ya hapa na pale katika kubadilishana mawazo.
katika kipindi ambacho huyu mwanaume niliyekuwa naye nilipomfumania na shogangu wa kupika na kupakua wakiwa kitandani wakifanya tendo, nilimsimulia huyu kijana kama rafiki mwema ili kupata ushauri na pia kufarijiwa kwa sababu tulishakuwa marafiki kwa muda mrefu.

alinishawishi sana nisivunje uhusiano na mpenzi wangu, akinisihi nimsamehe kwani ni ibilisitu alimpitia, lakini kutokana na kuumizwa na usaliti niliofanyiwa na mpenzi wangu niliyemuamini sana nilikata shauri niuvunje uhusiano na kushika hamsini zangu.
nilikaa kwa muda wa miezi sita bila kuwa na uhusiano, lakini pia nilisita kuwa karibu na huyu rafiki yangu kwa muda wote huo nikitaka kutafakari kilichonitokea nikiwa peke yangu.

Yule kijana wala hakufanya makeke ya kunitafuta, na yeye alikata mawasiliano. Baada ya hiyo miezi sita ya kuachana na mpenzi wangu, nikarudisha mawasiliano na huyu rafiki yangu baada ya kukutana kwenye mkesha wa maulid ya kuzaliwa mtume. Baada ya kurudisha mawasiliano ndipo akanitaka tuanzishe uhusiano wa kimapenzi akiniahidi kwamba tutaoana iwapo kila mmoja ataridhika na tabia za mwenzake.


tukaanzisha uhusiano wa kimapenzi na nilijenga imani kwamba, huyu atakuwa mume mwema kwa sababu anazo zifa zote nizitakazo, na tulishafahamiana kwa takriban miaka miwili nyuma kama marafiki na kila mmoja alikuwa anafahamu kuhusu mahusiano ya mwenzake.

Kwa upande wake, yeye aliwahi kunisimulia kwamba alikuwa na mpenzi wake ambaye alikuwa hajatulia, na hawaendani na hivyo aliamua kuvunja uhusiano huo.

lakini baada ya miezi kadhaa tangu kuanzisha uhusiano na huyu kijana, na yeye akaanza vibweka. Kwanza ana wivu kupindukia, na anapenda sana kuzungumzia mahusiano yangu ya nyuma kwa namna ya kuniumiza kihisia. Wakati mwingine tukiwa kitandani anataka kujua ni nani mzuri zaidi kati yake na huyo bwanangu wa zamani katika swala zima la kitandani.


hata nimsifie, lakini anahisi kama namnafiki tu na anapenda sana kusifiwa sifiwa na kudekezwa na kunithibiti nisiwasiliane na marafiki zangu. Hamuanini mtu yeyote wa jinsia ya kiume kuwa karibu na mimi, na hivi sasa anataka kuingilia mawasiliano yangu ya simu akitaka kujua nawasiliana na nani na kwa nini.

Kuna wakati aliwahi kufuta namba zote za wanaume niliowasevu kwenye simu yangu ambao wote ni jamaa zangu ambao nina nasaba nao.


nimeshindwamiye, bora yeshe, mwanaume gani huyu asiyejiamini, hivi tu ni wapenzi akijanioa si atanigeuza mdoli wa kuniweka hapo asubuhi na akirudi jioni anikute hapohapo.


nimeshindwa miye.

[atta 1411113940714.jpg 1411113940714.jpg ch]186393[/attach]
 
Pole sana bibie,wivu nao ukizid bana sio inshu
 
inaonyesha jamaa atakua hana hela angekuanazo vituko vyote ungevumilia tu cc lara 1 LMAO
 
Last edited by a moderator:
Na yeye anafikiria wewe hujatulia anataka akuache. Unatakiwa umwelewe la sivyo utakuwa na mahusiano na wanaume kibao mpaka utachoka.
 
mmmhh huyo kama unakazi basi utafukuzwa kazi kwa huo wivu wake au utakosa marafiki au washikaji ambao unashirikiana nae kibiashara...

Kubali yaishe...Kwanza ktika mahusiano wapenzi mnachotakiwa ni kuacha yalopita na kuganga yajayo..Ukiona mwanaume ambaye anapenda kukutamkia tamkia maudhi ya nyuma yaliyopita huyo atapenda kukuumiza kila mara...na kukusimanga...

Tafuta ustaarabu taaratiibu kama unanyata vileee





Bora yesheee shost.........huyo hafai........
 
Pole kwa masaibu yaliyo kupata, wanaume ndio hao hao utaachana na huyu ukimbie kwa mwingine lakini bado tatizo halitakuwa solved.


Visa vya huyu current ni vya kawaida kwa mtu anaetaka security ya penzi tena kwa mrembo design yako. Ni swala kuwa na effective communication, mpaka sasa hajajua mapungufu yake ambayo kwako ni kero.


Mpe guide line katika mazungumzo yenu ni nini hupendi kitamkwe kila mara wakati mlishaongea.


Kutafuta uhakika wa ukitaji, wala usimlaumu sana, si umesema aliwahi kuwa na mahusiano kabla? Alishakueleza ilikuwaje wakaachana na mwenzi wa awali.


Muulize na yeye kati yako na yule wa mwanzo nani zaidi, angalau aupate ujumbe wako kwa njia ile ile inayokukera. Akianza malalamiko mweleze wewe pia hupendi maswali ya namna hiyo.


Tulia ingea na mwenzio, mtapata suluhu.

Utahangaika kumsaka Mr. RIGHT kumbe wanatengenezwa.
 
Kweli ni tabu tupu. Wivu ukizidi nao ni tatizo. Ukipenda sana nalo tatizo. Usipoonyesha upendo nalo tatizo. Ukiishi bila wivu nalo tatizo..
sasa tufanyeje hizi tabu ziishe??
 
kweli ni tabu tupu. Wivu ukizidi nao ni tatizo. Ukipenda sana nalo tatizo. Usipoonyesha upendo nalo tatizo. Ukiishi bila wivu nalo tatizo..

mkuu mbona umetuacha hewani? Hujasema wazi the way forward.
 
Matola;10641723]Kumbe na kwenye hizi maulid za mtume Mwamedi huwa mnatongozana?

MHHHHHHHH!
 
Kwanza ana wivu kupindukia, na . Wakati mwingine tukiwa kitandani anataka kujua ni nani mzuri zaidi kati yake na huyo bwanangu wa zamani katika swala zima la kitandani.

Hata nimsifie, lakini anahisi kama namnafiki tu na anapenda sana kusifiwa sifiwa na kudekezwa na kunithibiti nisiwasiliane na marafiki zangu. Hamuanini mtu yeyote wa jinsia ya kiume kuwa karibu na mimi, na hivi sasa anataka kuingilia mawasiliano yangu ya simu akitaka kujua nawasiliana na nani na kwa nini.

=
lack of confidence , heri utoke Ndukiiii kero zao huwa haziishi hao
 
sasa tufanyeje hizi tabu ziishe??

ichana nimeuliza swali hilo lakini sijajibiwa. Mie bibi yangu miaka mingi iliyopita alinitonya kuwa wivu ni chachu na ndio mpango mzima ktk penzi. Kwangu mie sina hata chembe ya wivu hata nikikuta jamaa amekuatamia ntakupa big up tu na maisha yataendelea.
 
charty huyu mwanaume habebeki na ni janga ka Boko Haram
Nishajisemesha mpaka basi. Ni mwepesi kuomba radhi, lakini habailiki.

Nitasubiri kama hatatokea mwanaume mwingine mwenye sifa angalau asilimia hamsini, bora nisiolewe

Zinduna nilijichanganya, kumbe ulikuwa unatupatia taarifa. Sawa move on...mwanzo si nikadhani unahitaji mawazo ya wengine.

Kweli bora usiolewe full stop.
 
Last edited by a moderator:
Naomba na miye leo nifunguke.

Nina mwanaume tumekuwa kwenye uhusiano kimapenzi (namaanisha kimapenzi) kwa takriban mwaka mmoja sasa. Lakini tulijuana miaka mitatu iliyopita akiwa kama rafiki mwema kwangu.

Ni kijana mwenye sifa nizipendazo, yaani ni mtaratibu, mwerevu, mwelewa, mwenye malengo na pia mcha Mungu.
Nilikutana na huyu kijana wakati wa tamasha la Mwakakogwa huko Makunduchi, basi kuanzia hapo tukawa marafiki. Aliwahi kunitamkia kuhusu kuwa na urafiki wa kimapenzi,lakini sikumkubalia kwa sababu nilikuwa na uhusiano na mwanaume mwingine ambaye tulikuwa na malengo ya kufunga ndoa.

Kusema kweli nilivutiwa na huyu kijana ila nilishindwa kukubali kuwa na uhusiano naye wa kimapenzi kwa sababu nilishaji commit kwa mwanaume mwingine, na miye ni binti niliyelelewa katika maadili kwa hiyo sikuwa tayari kumpaka mafuta huyu kijana wa watu kwa nyuma ya chupa, yaani kuwa mnafiki na ndumilakuwili wa kutaka huku na kule.

Urafiki wetu na huyu kijana ulikuwa ni wakawaida tu na mara chache tulikuwa tunakutana kwa mazungumzo ya hapa na pale katika kubadilishana mawazo.
Katika kipindi ambacho huyu mwanaume niliyekuwa naye nilipomfumania na shogangu wa kupika na kupakua wakiwa kitandani wakifanya tendo, nilimsimulia huyu kijana kama rafiki mwema ili kupata ushauri na pia kufarijiwa kwa sababu tulishakuwa marafiki kwa muda mrefu.

Alinishawishi sana nisivunje uhusiano na mpenzi wangu, akinisihi nimsamehe kwani ni ibilisitu alimpitia, lakini kutokana na kuumizwa na usaliti niliofanyiwa na mpenzi wangu niliyemuamini sana nilikata shauri niuvunje uhusiano na kushika hamsini zangu.
Nilikaa kwa muda wa miezi sita bila kuwa na uhusiano, lakini pia nilisita kuwa karibu na huyu rafiki yangu kwa muda wote huo nikitaka kutafakari kilichonitokea nikiwa peke yangu.

Yule kijana wala hakufanya makeke ya kunitafuta, na yeye alikata mawasiliano. Baada ya hiyo miezi sita ya kuachana na mpenzi wangu, nikarudisha mawasiliano na huyu rafiki yangu baada ya kukutana kwenye mkesha wa Maulid ya kuzaliwa Mtume. Baada ya kurudisha mawasiliano ndipo akanitaka tuanzishe uhusiano wa kimapenzi akiniahidi kwamba tutaoana iwapo kila mmoja ataridhika na tabia za mwenzake.


Tukaanzisha uhusiano wa kimapenzi na nilijenga imani kwamba, huyu atakuwa mume mwema kwa sababu anazo zifa zote nizitakazo, na tulishafahamiana kwa takriban miaka miwili nyuma kama marafiki na kila mmoja alikuwa anafahamu kuhusu mahusiano ya mwenzake.

Kwa upande wake, yeye aliwahi kunisimulia kwamba alikuwa na mpenzi wake ambaye alikuwa hajatulia, na hawaendani na hivyo aliamua kuvunja uhusiano huo.

Lakini baada ya miezi kadhaa tangu kuanzisha uhusiano na huyu kijana, na yeye akaanza vibweka. Kwanza ana wivu kupindukia, na anapenda sana kuzungumzia mahusiano yangu ya nyuma kwa namna ya kuniumiza kihisia. Wakati mwingine tukiwa kitandani anataka kujua ni nani mzuri zaidi kati yake na huyo bwanangu wa zamani katika swala zima la kitandani.


Hata nimsifie, lakini anahisi kama namnafiki tu na anapenda sana kusifiwa sifiwa na kudekezwa na kunithibiti nisiwasiliane na marafiki zangu. Hamuanini mtu yeyote wa jinsia ya kiume kuwa karibu na mimi, na hivi sasa anataka kuingilia mawasiliano yangu ya simu akitaka kujua nawasiliana na nani na kwa nini.

Kuna wakati aliwahi kufuta namba zote za wanaume niliowasevu kwenye simu yangu ambao wote ni jamaa zangu ambao nina nasaba nao.


Nimeshindwamiye, bora yeshe, mwanaume gani huyu asiyejiamini, hivi tu ni wapenzi akijanioa si atanigeuza mdoli wa kuniweka hapo asubuhi na akirudi jioni anikute hapohapo.


Nimeshindwa miye.

1) wewe hujalelewa kwenye maadili, umelelewa kwe sampuli ya maadili. weye maadili awaggedani kabla ya ndoa
2) ana kila haki ya kuwa na wasiwasi na hao male frends wako becoz yeye mwenyewe alikupata mkiwa frends (another reason why u should never trust a lady saying he is just a frend)
3) anashika simu yako becoz he has every ryt to do so. kama haupo tayari kwa serious relationship basi usiingie kwenye relationship. relationship is about forgoing the i and believing in the we. kama upo clean basi hamna shida ya kulalamika yeye kushika simu yako
4) a decent woman doesnt discuss bedroom affairs in public....its just unlady like.
5) yeye kukuuliza wewe kama anakugegeda vizuri kuliko ex wako ni consequence ya wewe kugegedwa kabla ya ndoa....u shuld deal with it becoz its a choice u made and the price u pay. tatizo mwanadamu ana tabia ya kujidai yeye anajua kuliko Mungu.
6) last but not least u need to do a self evaluation, clearly ur selection of the husband material man needs polish. yule wa kwanza ulisema uliona atakuwa future husband huyu nae future husband but all have fallen short. it could be kuwa kweli hao wanaume bogus but sometyms u need to be careful with ur selection.
 
Back
Top Bottom