Huyu mwanaume jamani!

Huyu mwanaume jamani!

Usihamie arusha akapate hgal WA bure. Muambie unaenda kwenu, otherwise ndoa. Utatendewa vile unavyoruhusu. Set the pace mapemaaa kabla hakujakuchwa mama.
 
Hapa kuna sababu. Sio bure. Jichunguze. Hii ni story ya upande mmoja. Ulimzingua. Kuna kitu kikubwa umemfanyia na akajua akakausha au alikuambia usubiri ukalazimisha. Sema kweli yako ulifanya nini hata akakimbia mji?
 
pole sana Jacky.
U knw what..haya ni maisha yako na ni afya yako,,wewe ndio unafeel kila kitu na sio that idiot..sory but yes he is.
Me nngekuwa wewe..
Ningeenda kwetu niwashhirikishe ndugu zangu wenye akili,then ndugu zake wajue pia. .i mean ninge either force or shawishi hadi kieleweke.
Come on girl we ungekuwa ndo yeye ungemfanyia hivyo yeye?
Then hizo tarehe za ndoa em weka tag , cos nmemsoma kama mtu ambaye hayupo tayari kukuoa ama anakitu anaficha.
Even if he is a nice and perfect for you but honey u gotta raise ur eyebrows and think HARD with ur brain.
Kwa situation kama yako na reactions zake hmmmm. Pliiizz

Tofautisha kuoa na harusi.! Yawezekana huyu Dada ni wale ving'ang'anizi wa harusi ndo maana Jamaa katupiemo kitenesi. Huyu ameshaolewa na mahali kwao wameahakula, sioni anachosubiri kuhamia kwa Jamaa na mimba ameshapewa. Aafu bado kuna kazi unafukuzwa ukiwa mgonjwa?? Yawezekana huyu Dada ndio wale vijana wa kibongo typical! Story nyingi, ruhusa kila siku production zero. Kama ni hard worker hakuna bosi atakufukuza kisa mimba inakusumbua!!!
 
Kumfwata arusha naona itakuwa hatari zaidi kama utakutana na kitu cha ajabu na hiyo hali uliyonayo ni mbaya zaidi....mim naona rudi nyumbani kwenu...kaongee na shangazi yako...mwambie hali halisi...shangazi ataongea na wazazi wako afu watajadili nin cha kufanya....ila kuendelea kukaa mwanza ni kama unajichimbia kaburi....
 
Mimba inatakiwa kulelewa na watu wawili..,mfate hukohuko Arusha, msalimie na mwambie aache kukwepa majukumu..
 
Huyo si mume wewe ni janga tu hilo!! Mfate ama urudi kwenu ! Isitoshe mwenzio keshaoa huyo huko! Loh!

inawezekana ikawa kweli usemayo Munkari maana kama wanataka kuoana kwanini afiche ujauzito na wakati ameshatoa mpaka mahari kwanini hataki wazazi wajue huyu mwanaume kuna kitu kikubwa anaficha
 
Last edited by a moderator:
Hii harusi haikuwa inafahamika kwa watu?
Maana inaahirishwa vipi kirahisi namna hiyo bila sababu ambazo hata wewe muhusika mkuu huelewi?
Nahisi mtoto akizaliwa atakwambia mkapime DNA.
 
tarehe alipanga nwez wa tano baadae wazazi waksema hawana hela wajipange mpaka wa saba sasa yeye anasema itakua aibu sana sababu huo mwez wa saba tayar mimba itakua inamiezi 7 kwa hiyo itajulikana na kwao baba yake ni Askofu hivyo kukwepa aibu.
 
wazazi walidai hawana pesa wajipange mpaka mwez wa saba sasa akakataa anasema wasaba mimba itakua kubwa itaoneka bora nitoe au nisubiri nijifungue ndo tungendoa
 
Eeee makubwaa kama haelewek chomoa faster
 
wazazi walidai hawana pesa wajipange mpaka mwez wa saba sasa akakataa anasema wasaba mimba itakua kubwa itaoneka bora nitoe au nisubiri nijifungue ndo tungendoa

Hana akili utoe mimba wakati ana mpango wa kukuoaa hebu niambie anafikiri kwa kutumia nini?badala afurahi we kubeba mimba,tena mngefunga ndoa bado mimba ndogo,keshapata mchepuko umekuzidu mbinu utashangaa unaachwaa solembaa stuka mapemaa
 
Eeee makubwaa kama haelewek chomoa faster

Usitoe hiyo mimba dada, uenda mungu kakupa huyo mtoto 1, kwa sasa hiyo mimba yako ni bora zaidi ya ndoa. Maana jamaa anaweza kukutolea nje lakini ukabaki na mtoto wako. Kumbuka mtoto ni zawadi pekee kutoka kwa mungu ukiitoa unaeza kuijutia kipindi chote cha maisha yako.
 
kanipa mimba hataki kueleweka, katoa mahali nyumban harusi ilikua mwez wa 5tangu nimemwambia ninamimba anarusha miez mara wa 7 mara wa 10 sasa kasema mwaka kesho...., wazazi wa pande mbili hataki wajue kama ninamimba mm naishi kwangu mwanza nlikua nafanya kazi sasa nimeachishwa sababu ya kuumwa umwa kutokana na ujauzito ananiambia nikae hukuhuku nyumbani wasijue chochote mpaka nijifungue ndo mipango ya harusi iendelee... sasa nishaulini nitakaaje huku sina ndugu sina kazi nitaishije na huu ujauzito kumbuka ni mimba ya kwanza nikipata matatizo hakuna wa kunisaidia na yeye yupo arusha...nifanyeje?

Kwanza pole.
Pili huyo mwanaume amekudanganya atakuwa alishaoa ana mke na watoto, na hao wazazi kama alikutambulisha watakuwa feki. Hiyo mahari uliolipiwa alikuja na watu feki hamna hata mmoja ambae ni ndugu yake ndo mana hataki uende kwao coz walikuwa ndugu feki. Amka chukua hatua ukiamua kuzaa huyo mtoto ni wako mwenyewe usitegemee kama atakusaidia kulea ndo ushatelekezwa hivoo. Mtu kikwambia sitaki ndugu zangu wajue ujue manyoya hapo umetapeliwa.
Mwisho inaweza kuwa ni kweli ndugu zake walikuja kutoa mahari na wanakujua ila kapata mwingine anambana na kumchanganya hivo ukienda na miba yako uamharibia starehe na raha anazopata kwa huyo mpya.
Amua kujilipua uende kinguvu kwake ujue mbichi na mbivu mapema au urafute jinsi yako ya kuishi na mwanao.
Pole tena na kila la kheri, looh wanaume nyinyi!! Ngachoka kabsa kiruuu!!
 
Usitoe hiyo mimba dada, uenda mungu kakupa huyo mtoto 1, kwa sasa hiyo mimba yako ni bora zaidi ya ndoa. Maana jamaa anaweza kukutolea nje lakini ukabaki na mtoto wako. Kumbuka mtoto ni zawadi pekee kutoka kwa mungu ukiitoa unaeza kuijutia kipindi chote cha maisha yako.

asante nimekuelewa
 
Back
Top Bottom