Huyu msichana ninayemtongoza ananipenda au ananizingua?

Huyu msichana ninayemtongoza ananipenda au ananizingua?

Noble Moh

Member
Joined
Feb 7, 2018
Posts
9
Reaction score
12
Jamani wana jamvi ,mimi kuna demu mmoja hivi ninamtongoza yapata wiki mbili hivi mpaka sasa ,lakini jibu lake ni moja tu" anasema kwa sasa hataki kuwa na mpenzi kwa sababu anataka kumpumzika "

Ila kinachonishangaza ni kwamba kila nikikutana nae na kumuomba nimkumbatie huwa anakubali na nikimuomba tupige story huwa anakubali na nampiga mpaka mabusu la ni kitu kimoja tu ambacho hakipendi '"Nikimuita baby au mpenzi huwa anachukia sana.

Juzi nimemtumia meseji na kumuomba nikutane nae lakini kanijibu shit sana, "Sitaki kukutana nawe tena na kama vipi unipotezee tu maana sitaki usumbufu mimi nikamjibu poa kama vip futa na namba yangu kabisa lakini hakunijibu chochote.

Sasa leo hii nimekaa pande za home mida ya mchana,ghafla meseji iliingia kwenye simu yangu ,nilipocheck nikakuta meseji ya yule demu ninayemtongoza ikisema hivi"mmh mbona upo kimya sana" Me sikumjibu chochote maana nilishamtoa akilini mwangu ,

Ninaomba ushauri wenu wadau maana sielewi kama ananipenda au ananizingua tu .
 
Angalia Usije Ingia Mtegoni ukaja Lia baadae... Huyo akikukubali ujue haijatoka Moyoni ila Amekukubali Kisa Yup9 Lonely.. keshatendwa Huko
 
Mungu nisaidie nisichangie Uzi huu naweza kukufuru.

R.I.P aquilina
 
Punguza utoto bhasiii twende na wakati jiongeze bhasi uingie kwenye Kundi la Wanaume
 
Kuna ulazima wa kujisumbua kuwa nae? Yeye mwenyew ameshakwambia kuwa hataki mapenz.. move on. Ukibembeleza anakuona boya
 
Nilivoona tu umeweka X badala ya S nikajua tu wew ni mtu wa aina gani,
So ttzo liko kwako
 
Ingekuwa enzi ujana unanisumbua hapo nishafuta namba kitambo wapo wengi hao kata mti panda mti.
 
Back
Top Bottom